< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Bwana MUNGU asema hivi juu ya Edomu Tumesikia habari kutoka kwa Bwana, na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, akisema, Inukeni! Tuinuke dhidi yake kwa vita!”
The vision of Obadiah. The Lord Yahweh says this concerning Edom: We have heard a report from Yahweh and an ambassador has been sent among the nations, saying, “Rise up! Let us rise up against her for battle!”
2 Tazama, nitawafanya wadogo kati ya mataifa, mutadharauliwa sana.
Behold, I will make you small among the nations, you will be greatly despised.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya wewe, wewe ambaye unishi katika makaburi ya miamba, katika nyumba yako ya juu; asemaye moyoni mwako, 'Ni nani atakayenishusha mimi chini?'
The pride of your heart has deceived you, you who live in the clefts of the rock, in your lofty home; who say in your heart, “Who will bring me down to the ground?”
4 Ingawa unasimama juu kama tai na ingawa kiota chako huwekwa kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko, asema Yahweh.
Though you soar high like the eagle and though your nest is set among the stars, I will bring you down from there, says Yahweh.
5 Kama wezi walikuja kwako, ikiwa wanyang'anyi wangekujilia usiku (jinsi ungekatilwa mbali!), Wasingeweza kuiba vya kuwatosha? Ikiwa wakusanya zabibu wangekujilia, wasingeacha mavuno?
If thieves came to you, if robbers came by night—how you will be ruined!—would they not steal only as much as they needed? If grape gatherers came to you, would they not leave the gleanings?
6 Jinsi Esau amekwisha kupigwa, na hazina zake zilizofichwa zimewekwa nje!
How Esau has been ransacked, his hidden treasures will be searched out!
7 Watu wote wa ushirikiano wako watakupeleka katika njiani ya hadi mpakani. Watu waliokuwa na amani pamoja nawe wamekudanganya, na kukushinda. Wale wanaokula mkate wako wameweka mtego chini yako. Hakuna uelewa ndani yake.
All the men of your alliance will send you on your way to the border. The men who were at peace with you have deceived you, and prevailed against you. They who eat your bread have set a trap under you. There is no understanding in him.
8 Je! Sikuweza siku hiyo, asema Bwana, kuwaangamiza watu wenye hekima kutoka Edomu na kuelewa kutoka mlima wa Esau?
“Will I not on that day,” says Yahweh, “destroy the wise men from Edom and understanding out of the mountain of Esau?
9 Mashujaa wako watafadhaika, Temani, ili kila mtu akatiliwe mbali kutoka mlima wa Esau kwa kuuawa.
Your mighty men will be dismayed, Teman, so that every man may be cut off from the mountain of Esau by slaughter.
10 Kwa sababu ya ukatili uliofanywa kwa ndugu yako Yakobo, utafunikwa na aibu, nawe utakatiliwa mbali milele.
Because of the violence done to your brother Jacob, you will be covered with shame, and you will be cut off forever.
11 Siku ile ulikuwa umesimama, siku wageni walichukua mali zake, na waliokuwa wageni katika malango yake, na kupiga kura kwa Yerusalemu, wewe ulikuwa kama mmoja wao.
On the day you stood aloof, on the day strangers carried away his wealth, and foreigners entered into his gates, and cast lots for Jerusalem, you were like one of them.
12 Lakini usifurahi siku ya ndugu yako, siku ya msiba wake, wala usifurahi juu ya watu wa Yuda siku ya uharibifu wao; msijisifu siku ya dhiki yao.
But do not gloat over your brother's day, in the day of his misfortune, and do not rejoice over the people of Judah in the day of their destruction; do not boast in the day of their distress.
13 Usiingie mlango wa watu wangu siku ya msiba wao; usifurahi juu ya taabu yao siku ya msiba wao, wala msipotee utajiri wao siku ya uharibifu wao.
Do not enter my people's gate in the day of their calamity; do not gloat over their affliction in the day of their disaster, do not loot their wealth in the day of their ruin.
14 Usisimama kwenye njia panda, ili kuwakatilia mbali wakimbizi wake na usiwatoe waathirika wake katika siku ya dhiki.
Do not stand at the crossroads to cut down his fugitives, and do not deliver up his survivors in the day of distress.
15 Kwa maana siku ya Bwana iko karibu na mataifa yote. Kama ulivyofanya, itafanyika kwako; matendo yako yatarudi juu ya kichwa chako mwenyewe.
For the day of Yahweh is near upon all the nations. As you have done, it will be done to you; your deeds will return on your own head.
16 Kwa vile mlivyokunywa katika mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote yatakavyo kunywa daima. Watakunywa na kumeza na itakuwa kana kwamba hawakuwepo kabisa.
For as you have drunk on my holy mountain, so will all the nations drink continually. They will drink and swallow and it will be as though they had never existed.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwa na wale waliookoka na watakuwa watakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki miliki zao.
But in Mount Zion there will be those that escape and it will be holy; and the house of Jacob shall possess their own possessions.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu ni mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaunguza, na kuwateketeza. Hakutakuwa na waathirika kwa nyumba ya Esau, kwa kuwa Bwana amesema.
The house of Jacob will be a fire, and the house of Joseph a flame, and the house of Esau will be stubble, and they will burn them, and consume them. There will be no survivors to the house of Esau, for Yahweh has spoken it.”
19 Wote kutoka Negebu watamiliki mlima wa Esau na wale wa Shepela watamiliki nchi ya Wafilisti. Wao wataimiliki nchi ya Efraimu na nchi ya Samaria; na Benyamini atamiliki Gileadi.
Those from the Negev will possess the mount of Esau and those of the Shepelah will possess the land of the Philistines. They will possess the land of Ephraim and the land of Samaria; and Benjamin will possess Gilead.
20 Wahamiaji wa jeshi hili la watu wa Israeli watamiliki ardhi ya Kanaani mpaka Sarepta. Wahamiaji wa Yerusalemu, waliopo Sefaradi, wataimiliki miji ya Negebu.
The exiles of this host of the people of Israel will possess the land of Canaan as far as Zarephath. The exiles of Jerusalem, who are in Sepharad, will possess the cities of the Negev.
21 Waokoaji watakwenda hadi juu ya Mlima Sayuni kutawala nchi ya vilima ya Esau, na ufalme utakuwa wa Bwana.
Deliverers will go up to Mount Zion to rule over the hill country of Esau, and the kingdom will belong to Yahweh.

< Obadia 1 >