< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Bwana MUNGU asema hivi juu ya Edomu Tumesikia habari kutoka kwa Bwana, na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, akisema, Inukeni! Tuinuke dhidi yake kwa vita!”
[the] vision of Obadiah thus he says [the] Lord Yahweh of Edom a report we have heard from with Yahweh and an envoy among the nations he has been sent arise so let us arise on it for battle.
2 Tazama, nitawafanya wadogo kati ya mataifa, mutadharauliwa sana.
Here! small I will make you among the nations [will be] despised you exceedingly.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya wewe, wewe ambaye unishi katika makaburi ya miamba, katika nyumba yako ya juu; asemaye moyoni mwako, 'Ni nani atakayenishusha mimi chini?'
[the] presumption of Heart your it has deceived you O dweller in clefts of rock [the] height of dwelling his [who] says in heart his who? will he bring down me [the] ground.
4 Ingawa unasimama juu kama tai na ingawa kiota chako huwekwa kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko, asema Yahweh.
If you will make high like eagle and if between [the] stars [will be] set nest your from there I will bring down you [the] utterance of Yahweh.
5 Kama wezi walikuja kwako, ikiwa wanyang'anyi wangekujilia usiku (jinsi ungekatilwa mbali!), Wasingeweza kuiba vya kuwatosha? Ikiwa wakusanya zabibu wangekujilia, wasingeacha mavuno?
If thieves they came to you if destroyers of night how! you will be destroyed ¿ not will they steal sufficiency their if grape gatherers they came to you ¿ not will they leave gleanings.
6 Jinsi Esau amekwisha kupigwa, na hazina zake zilizofichwa zimewekwa nje!
How! they will be plundered Esau they will be searched out hidden treasures its.
7 Watu wote wa ushirikiano wako watakupeleka katika njiani ya hadi mpakani. Watu waliokuwa na amani pamoja nawe wamekudanganya, na kukushinda. Wale wanaokula mkate wako wameweka mtego chini yako. Hakuna uelewa ndani yake.
To the border they will send away you all [the] men of covenant your they will deceive you they will prevail to you [the] men of peace your food your they will set a trap under you there not [is] understanding in him.
8 Je! Sikuweza siku hiyo, asema Bwana, kuwaangamiza watu wenye hekima kutoka Edomu na kuelewa kutoka mlima wa Esau?
¿ Not on the day that ([the] utterance of *L(abh)*) Yahweh and I will destroy wise [people] from Edom and understanding from [the] mountain of Esau.
9 Mashujaa wako watafadhaika, Temani, ili kila mtu akatiliwe mbali kutoka mlima wa Esau kwa kuuawa.
And they will be dismayed warriors your O Teman so that he may be cut off everyone from [the] mountain of Esau from slaughter.
10 Kwa sababu ya ukatili uliofanywa kwa ndugu yako Yakobo, utafunikwa na aibu, nawe utakatiliwa mbali milele.
From [the] violence of brother your Jacob it will cover you shame and you will be cut off for ever.
11 Siku ile ulikuwa umesimama, siku wageni walichukua mali zake, na waliokuwa wageni katika malango yake, na kupiga kura kwa Yerusalemu, wewe ulikuwa kama mmoja wao.
On [the] day standing you from before on [the] day took captive strangers wealth his and foreigners they came (gates his *Q(K)*) and on Jerusalem they cast a lot also you [were] like one from them.
12 Lakini usifurahi siku ya ndugu yako, siku ya msiba wake, wala usifurahi juu ya watu wa Yuda siku ya uharibifu wao; msijisifu siku ya dhiki yao.
And may not you look on [the] day of brother your on [the] day of misfortune his and may not you rejoice to [the] people of Judah on [the] day perish they and may not you make big mouth your on [the] day of trouble.
13 Usiingie mlango wa watu wangu siku ya msiba wao; usifurahi juu ya taabu yao siku ya msiba wao, wala msipotee utajiri wao siku ya uharibifu wao.
May not you go in [the] gate of people my on [the] day of disaster their may not you look also you on calamity his on [the] day of disaster his and may not you stretch out on wealth his on [the] day of disaster his.
14 Usisimama kwenye njia panda, ili kuwakatilia mbali wakimbizi wake na usiwatoe waathirika wake katika siku ya dhiki.
And may not you stand at the parting of ways to cut off fugitives his and may not you deliver up survivors his on [the] day of trouble.
15 Kwa maana siku ya Bwana iko karibu na mataifa yote. Kama ulivyofanya, itafanyika kwako; matendo yako yatarudi juu ya kichwa chako mwenyewe.
For [is] near [the] day of Yahweh on all the nations just as you have done it will be done to you recompense your it will return on own head your.
16 Kwa vile mlivyokunywa katika mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote yatakavyo kunywa daima. Watakunywa na kumeza na itakuwa kana kwamba hawakuwepo kabisa.
For just as you have drunk on [the] mountain of holiness my they will drink all the nations continually and they will drink and they will swallow and they will be like not they had been.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwa na wale waliookoka na watakuwa watakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki miliki zao.
And on [the] mountain of Zion it will be deliverance and it will be a holy place and they will take possession of [the] house Jacob possessions their.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu ni mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaunguza, na kuwateketeza. Hakutakuwa na waathirika kwa nyumba ya Esau, kwa kuwa Bwana amesema.
And it will be [the] house of Jacob a fire and [the] house of Joseph [will be] a flame and [the] house of Esau [will become] stubble and they will burn them and they will consume them and not he will belong a survivor to [the] house of Esau for Yahweh he has spoken.
19 Wote kutoka Negebu watamiliki mlima wa Esau na wale wa Shepela watamiliki nchi ya Wafilisti. Wao wataimiliki nchi ya Efraimu na nchi ya Samaria; na Benyamini atamiliki Gileadi.
And they will take possession of the Negev [the] mountain of Esau and the Shephelah Philistines and they will take possession of [the] region of Ephraim and [the] region of Samaria and Benjamin Gilead.
20 Wahamiaji wa jeshi hili la watu wa Israeli watamiliki ardhi ya Kanaani mpaka Sarepta. Wahamiaji wa Yerusalemu, waliopo Sefaradi, wataimiliki miji ya Negebu.
And [the] exile[s] of the fortress this of [the] people of Israel who [will be] Canaanites to Zarephath and [the] exile[s] of Jerusalem who [are] in Sepharad they will take possession of [the] cities of the Negev.
21 Waokoaji watakwenda hadi juu ya Mlima Sayuni kutawala nchi ya vilima ya Esau, na ufalme utakuwa wa Bwana.
And they will go up deliverers on [the] mountain of Zion to rule [the] mountain of Esau and it will belong to Yahweh the kingship.

< Obadia 1 >