< Hesabu 1 >

1 Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema,
And he spoke Yahweh to Moses in [the] wilderness of Sinai in [the] tent of meeting on [day] one of the month second in the year second of going out their from [the] land of Egypt saying.
2 'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume
Lift up [the] head of all [the] congregation of [the] people of Israel to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names of every male to heads their.
3 kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
From a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare in Israel you will enroll them to military groups their you and Aaron.
4 Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila.
And with you they will be a man a man to the tribe a man [is the] head of [the] house of ancestors his he.
5 Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri;
And these [are] [the] names of the men who they will stand with you for Reuben Elizur [the] son of Shedeur.
6 kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
For Simeon Shelumiel [the] son of Zurishaddai.
7 Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu;
For Judah Nahshon [the] son of Amminadab.
8 Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari;
For Issachar Nethanel [the] son of Zuar.
9 kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
For Zebulun Eliab [the] son of Helon.
10 kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri;
For [the] sons of Joseph for Ephraim Elishama [the] son of Ammihud for Manasseh Gamaliel [the] son of Pedahzur.
11 kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
For Benjamin Abidan [the] son of Gideoni.
12 Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai;
For Dan Ahiezer [the] son of Ammishaddai.
13 kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani;
For Asher Pagiel [the] son of Ocran.
14 kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli;
For Gad Eliasaph [the] son of Deuel.
15 na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani.”
For Naphtali Ahira [the] son of Enan.
16 Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
These ([were those] called *Q(K)*) [of] the congregation [the] leaders of [the] tribes of ancestors their [were] [the] heads of [the] families of Israel they.
17 Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina,
And he took Moses and Aaron the men these who they had been designated by names.
18 na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo.
And all the congregation they summoned on [day] one of the month second and they recorded their ancestry on clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards to heads their.
19 Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
Just as he had commanded Yahweh Moses and he enrolled them in [the] wilderness of Sinai.
20 Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia.
And they were [the] descendants of Reuben [the] firstborn of Israel genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names to heads their every male from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
21 Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Reuben [were] six and forty thousand and five hundred.
22 Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia.
Of [the] descendants of Simeon genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their enrolled [men] its by [the] number of names to heads their every male from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
23 Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Simeon [were] nine and fifty thousand and three hundred.
24 Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of [the] descendants of Gad genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
25 Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Gad [were] five and forty thousand and six hundred and fifty.
26 Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of [the] descendants of Judah genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
27 walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Judah [were] four and seventy thousand and six hundred.
28 Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of [the] descendants of Issachar genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
29 Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Issachar [were] four and fifty thousand and four hundred.
30 Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of [the] descendants of Zebulun genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
31 Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Zebulun [were] seven and fifty thousand and four hundred.
32 Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of [the] descendants of Joseph of [the] descendants of Ephraim genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
33 Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Ephraim [were] forty thousand and five hundred.
34 Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
Of [the] descendants of Manasseh genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
35 Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Manasseh [were] two and thirty thousand and two hundred.
36 Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of [the] descendants of Benjamin genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
37 Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Benjamin [were] five and thirty thousand and four hundred.
38 Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of [the] descendants of Dan genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
39 Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Dan [were] two and sixty thousand and seven hundred.
40 Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
Of [the] descendants of Asher genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
41 Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Asher [were] one and forty thousand and five hundred.
42 Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
[the] descendants of Naphtali genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
43 Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
Enrolled [men] their of [the] tribe of Naphtali [were] three and fifty thousand and four hundred.
44 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
These [were] the enrolled [men] whom he enrolled Moses and Aaron and [the] leaders of Israel two [plus] ten man a man one for [the] house of ancestors his they were.
45 Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao.
And they were all [those] enrolled of [the] people of Israel to [the] house of ancestors their from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare in Israel.
46 Walihesabu wanaume 603, 550.
And they were all those enrolled six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
47 Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa,
And the Levites to [the] tribe of ancestors their not they were enrolled in midst of them.
48 Kwa sababu BWANA alimwambia Musa,
And he had spoken Yahweh to Moses saying.
49 “usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
Only [the] tribe of Levi not you will enroll and head their not you will lift up in among [the] people of Israel.
50 Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
And you appoint the Levites over [the] tabernacle of the testimony and over all articles its and over all that [belongs] to it they they will carry the tabernacle and all articles its and they they will serve it and around the tabernacle they will encamp.
51 Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe.
And when sets out the tabernacle they will take down it the Levites and when encamps the tabernacle they will raise up it the Levites and the stranger approaching he will be put to death.
52 Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
And they will encamp [the] people of Israel everyone at camp his and everyone at standard his to military groups their.
53 Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano.”
And the Levites they will encamp around [the] tabernacle of the testimony and not it will be wrath towards [the] congregation of [the] people Israel and they will keep the Levites [the] duty of [the] tabernacle of the testimony.
54 Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.
And they did [the] people of Israel according to all that he had commanded Yahweh Moses so they did.

< Hesabu 1 >