< Hesabu 9 >

1 BWANA akanena na Musa katika katika jangwa la Sinai, mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya kutoka katika nci ya Misri. Akasema,
And Jehovah spoke to Moses in the wilderness of Sinai, in the first month of the second year after their departure from the land of Egypt, saying,
2 “Wana wa Israeli wataikumbuka Pasaka katika wakati wake kila mwaka.
Let the children of Israel also hold the passover at its set time;
3 Siku ya kumi na nne ya mwezi huu, muda wa jioni, utaikumbuka Pasaka kila mwaka kwa muda uliopanggwa. Lazima uikumbuke, fuata taratibu zake zote na utii sheria zake zote zinazohusiana na tukio hilo.
on the fourteenth day in this month between the two evenings, ye shall hold it at its set time; according to all the rites of it, and according to all the ordinances thereof shall ye hold it.
4 Kwa hiyo, Musa akawaambia wana wa Isareli kuwa wataishika sikukuu ya Pasaka.
And Moses spoke to the children of Israel, that they should hold the passover.
5 Kwa hiyo wakaishika sikuu ya Pasaka katika mwezi wa kwanza, wakati wa jioni wa siku ya kumi na nne ya mwezi katika jangwa la Sinai. Wana wa Israeli walitii kila kitu ambacho BWANA alimwamuru Musa kukifanya.
And they held the passover in the first [month] on the fourteenth day of the month, between the two evenings, in the wilderness of Sinai: according to all that Jehovah had commanded Moses, so did the children of Israel.
6 Kulikuwa na watu fulani walionajisika kwa sababu ya maiti ya mtu. Hawakuweza kuishika Pasaka siku hiyo. Kwa hiyo walikwenda kwa Musa na Haruni siku hiyohiyo.
And there were men, who were unclean through the dead body of a man, and could not hold the passover on that day; and they came before Moses and before Aaron on that day.
7 Wakamwambia Musa, “Sisi tumenajisika kwa sababu ya maiti ya mtu. Kwa nini basi unatutaka tuendelee kutoa sadaka kwa BWANA kwa wakati wa mwaka uliopangwa kwa wana wa Israeli?”
And those men said to him, We are unclean by reason of the dead body of a man: why are we kept back, that we may not present the offering of Jehovah at its set time among the children of Israel?
8 Naye Musa akawaambia, “Subirini nimsikilize BWANA ataniambia nini juu Yenu.”
And Moses said to them, Stay, and I will hear what Jehovah commands concerning you.
9 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
10 “Nena na wana wa Israeli, uwaambie, 'kama mmoja wenu au mwana wa uzao wenu amenajisika kwa sababu ya maiti, au ana safari ndefu, bado anaweza kuishika Pasaka ya BWANA.
Speak unto the children of Israel, saying, If any one of you or of your generations be unclean by reason of a dead body or be on a journey afar off, yet he shall hold the passover to Jehovah.
11 Wataishika Pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili wakati wa jioni. Wataila kwa mikate isyotiwa chahcu na mboga chungu.
In the second month, on the fourteenth day, between the two evenings, shall they hold it; with unleavened bread and bitter herbs shall they eat it.
12 Wasiiache mpaka jioni, au kuvunja mifupa yake. Watafuata taratibu zote za Pasaka.
They shall leave none of it until the morning, nor break a bone thereof: according to every ordinance of the passover shall they hold it.
13 Lakini mtu yeyote asiye najisi na hayuko safarini, na akashindwa kuishika Pasaka, huyo mtu lazima aondolewe kati ya watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ambayo BWANA huitaka kwa wakati wa mwaka uliopangwa. Huyo mtu lazima aibebe dhambi yake.
But a man that is clean, and is not on a journey, and forbeareth to hold the passover, that soul shall be cut off from among his peoples; because he presented not the offering of Jehovah at its set time: that man shall bear his sin.
14 Kama mtu mgeni anayeishi kati yenu na akaishika, Pasaka kwa heshima ya BWANA, ataishika na kufanya amri zote, na kutii taratibu zake. Utakuwa na sheria hizohizo kwa wageni na kwa wote waliaozaliwa katika nchi.
And if a stranger shall sojourn among you, and would hold the passover to Jehovah, according to the rite of the passover, and according to the ordinance thereof, so shall he do. Ye shall have one rite, both for the stranger and for him that is born in the land.
15 Na siku hiyo ambayo masikani iliposimamishwa, wingu lilifunika masikani, ile hema ya amari ya agano. Ilipokuwa jioni wingu lilkuwa juu ya masikani. Lilionekana kama moto mpaka asubuhi.
And on the day that the tabernacle was set up, the cloud covered the tabernacle of the tent of testimony; and at even it was upon the tabernacle as the appearance of fire, until the morning.
16 Liliendelea hivyohivyo. Lile wingu lilifunika masikani na kuonekana kama moto wakati wa usiku.
So it was continually: the cloud covered it, and at night it was as the appearance of fire.
17 Na kila wingu lilipochukuliwa kutoka kwenye hema, wana wa Isareli waliendelea na safari yao. Na kila wingu liliposimama, watu waliweka kambi.
And when the cloud rose from the tent, then the children of Israel journeyed; and at the place where the cloud stood still, there the children of Israel encamped.
18 Wana wa Israrli walisafiri kwa amri ya BWANA, na kwa amri yake waliweka kambi. Wakati wingu liliposimama juu ya masikani, nao walikaa kwenye kambi zao.
According to the commandment of Jehovah the children of Israel journeyed, and according to the commandment of Jehovah they [remained] encamped; all the days that the cloud dwelt upon the tabernacle they encamped.
19 Na wingu lilipobaki kwenye masikani kwa siku nyingi, wana wa Israeli walitakiwa kutii maelekezo ya BWANA na kusitisha safari yao.
And when the cloud was long upon the tabernacle many days, then the children of Israel kept the charge of Jehovah, and journeyed not.
20 Wakati mwingine wingu lilibaki kwa siku chache tu kwenye masikani. Kwa mazingira kama hayo walilazimika kutii amri ya BWANA - waliweka kambi na kisha kuendelea na safari tena kwa amri yake.
And if it were so that the cloud was a few days upon the tabernacle, according to the commandment of Jehovah they encamped, and according to the commandment of Jehovah they journeyed.
21 Wakati mwingine wingu lilikuwepo kambini kuanzia jioni mpaka asubuhi. Na wingu liliponyanyuliwa asubuhi, walisafiri. Kama liliendelea kwa mchana wote na kwa usiku wote, ni pale tu wingu liliponyanyuliwa ndipo walipoendelea na safari.
And if it were so that the cloud was there from the evening until the morning, and that the cloud was taken up in the morning, then they journeyed; or a day and a night, and the cloud was taken up, they journeyed;
22 Hata kama wingu lilibaki kwenye masikini kwa siku mbili, kwa mwezi mmoja, au kwa mwaka mmoja, ili mradi tu limebaki pale, wana wa Israeli walibaki kwenye kambi zao na kusitisha safari. Lakini pale wingu liliponyanyuliwa, walianza safari yao.
or two days, or a month, or many days, when the cloud was long upon the tabernacle, dwelling upon it, the children of Israel [remained] encamped, and journeyed not; but when it was taken up, they journeyed.
23 Walifanya kambi kwa amri ya BWANA, na walisafiri kwa amri yake. Walitii amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa
At the commandment of Jehovah they encamped, and at the commandment of Jehovah they journeyed: they kept the charge of Jehovah according to the commandment of Jehovah through Moses.

< Hesabu 9 >