< Hesabu 9 >

1 BWANA akanena na Musa katika katika jangwa la Sinai, mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya kutoka katika nci ya Misri. Akasema,
And Jehovah spoke to Moses in the wilderness of Sinai, in the first month of the second year after they came out of the land of Egypt, saying,
2 “Wana wa Israeli wataikumbuka Pasaka katika wakati wake kila mwaka.
Moreover let the sons of Israel keep the Passover in its appointed season.
3 Siku ya kumi na nne ya mwezi huu, muda wa jioni, utaikumbuka Pasaka kila mwaka kwa muda uliopanggwa. Lazima uikumbuke, fuata taratibu zake zote na utii sheria zake zote zinazohusiana na tukio hilo.
In the fourteenth day of this month, at evening, ye shall keep it in its appointed season. According to all the statutes of it, and according to all the ordinances of it, ye shall keep it.
4 Kwa hiyo, Musa akawaambia wana wa Isareli kuwa wataishika sikukuu ya Pasaka.
And Moses spoke to the sons of Israel, that they should keep the Passover.
5 Kwa hiyo wakaishika sikuu ya Pasaka katika mwezi wa kwanza, wakati wa jioni wa siku ya kumi na nne ya mwezi katika jangwa la Sinai. Wana wa Israeli walitii kila kitu ambacho BWANA alimwamuru Musa kukifanya.
And they kept the Passover in the first month, on the fourteenth day of the month, at evening, in the wilderness of Sinai. According to all that Jehovah commanded Moses, so did the sons of Israel.
6 Kulikuwa na watu fulani walionajisika kwa sababu ya maiti ya mtu. Hawakuweza kuishika Pasaka siku hiyo. Kwa hiyo walikwenda kwa Musa na Haruni siku hiyohiyo.
And there were certain men who were unclean by reason of the dead body of a man, so that they could not keep the Passover on that day. And they came before Moses and before Aaron on that day,
7 Wakamwambia Musa, “Sisi tumenajisika kwa sababu ya maiti ya mtu. Kwa nini basi unatutaka tuendelee kutoa sadaka kwa BWANA kwa wakati wa mwaka uliopangwa kwa wana wa Israeli?”
and those men said to him, We are unclean by reason of the dead body of a man. Why are we kept back, that we may not offer the oblation of Jehovah in its appointed season among the sons of Israel?
8 Naye Musa akawaambia, “Subirini nimsikilize BWANA ataniambia nini juu Yenu.”
And Moses said to them, Stay ye, that I may hear what Jehovah will command concerning you.
9 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
10 “Nena na wana wa Israeli, uwaambie, 'kama mmoja wenu au mwana wa uzao wenu amenajisika kwa sababu ya maiti, au ana safari ndefu, bado anaweza kuishika Pasaka ya BWANA.
Speak to the sons of Israel, saying, If any man of you or of your generations shall be unclean by reason of a dead body, or be on a journey afar off, yet he shall keep the Passover to Jehovah.
11 Wataishika Pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili wakati wa jioni. Wataila kwa mikate isyotiwa chahcu na mboga chungu.
In the second month on the fourteenth day at evening they shall keep it. They shall eat it with unleavened bread and bitter herbs.
12 Wasiiache mpaka jioni, au kuvunja mifupa yake. Watafuata taratibu zote za Pasaka.
They shall leave none of it to the morning, nor break a bone of it. According to all the statute of the Passover they shall keep it.
13 Lakini mtu yeyote asiye najisi na hayuko safarini, na akashindwa kuishika Pasaka, huyo mtu lazima aondolewe kati ya watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ambayo BWANA huitaka kwa wakati wa mwaka uliopangwa. Huyo mtu lazima aibebe dhambi yake.
But the man who is clean, and is not on a journey, and forbears to keep the Passover, that soul shall be cut off from his people, because he did not offer the oblation of Jehovah in its appointed season; that man shall bear his sin.
14 Kama mtu mgeni anayeishi kati yenu na akaishika, Pasaka kwa heshima ya BWANA, ataishika na kufanya amri zote, na kutii taratibu zake. Utakuwa na sheria hizohizo kwa wageni na kwa wote waliaozaliwa katika nchi.
And if a stranger shall sojourn among you, and will keep the Passover to Jehovah, according to the statute of the Passover, and according to the ordinance of it, so shall he do. Ye shall have one statute, both for the sojourner, and for him who is born in the land.
15 Na siku hiyo ambayo masikani iliposimamishwa, wingu lilifunika masikani, ile hema ya amari ya agano. Ilipokuwa jioni wingu lilkuwa juu ya masikani. Lilionekana kama moto mpaka asubuhi.
And on the day that the tabernacle was reared up the cloud covered the tabernacle, even the tent of the testimony, and at evening it was upon the tabernacle, as it were the appearance of fire, until morning.
16 Liliendelea hivyohivyo. Lile wingu lilifunika masikani na kuonekana kama moto wakati wa usiku.
So it was always: the cloud covered it, and the appearance of fire by night.
17 Na kila wingu lilipochukuliwa kutoka kwenye hema, wana wa Isareli waliendelea na safari yao. Na kila wingu liliposimama, watu waliweka kambi.
And whenever the cloud was taken up from over the tent, then after that the sons of Israel journeyed. And in the place where the cloud abode, there the sons of Israel encamped.
18 Wana wa Israrli walisafiri kwa amri ya BWANA, na kwa amri yake waliweka kambi. Wakati wingu liliposimama juu ya masikani, nao walikaa kwenye kambi zao.
At the commandment of Jehovah the sons of Israel journeyed, and at the commandment of Jehovah they encamped. As long as the cloud abode upon the tabernacle they remained encamped.
19 Na wingu lilipobaki kwenye masikani kwa siku nyingi, wana wa Israeli walitakiwa kutii maelekezo ya BWANA na kusitisha safari yao.
And when the cloud tarried upon the tabernacle many days, then the sons of Israel kept the charge of Jehovah, and did not journey.
20 Wakati mwingine wingu lilibaki kwa siku chache tu kwenye masikani. Kwa mazingira kama hayo walilazimika kutii amri ya BWANA - waliweka kambi na kisha kuendelea na safari tena kwa amri yake.
And sometimes the cloud was a few days upon the tabernacle, then according to the commandment of Jehovah they remained encamped, and according to the commandment of Jehovah they journeyed.
21 Wakati mwingine wingu lilikuwepo kambini kuanzia jioni mpaka asubuhi. Na wingu liliponyanyuliwa asubuhi, walisafiri. Kama liliendelea kwa mchana wote na kwa usiku wote, ni pale tu wingu liliponyanyuliwa ndipo walipoendelea na safari.
And sometimes the cloud was from evening until morning, and when the cloud was taken up in the morning, they journeyed, or if by day and by night, when the cloud was taken up, they journeyed.
22 Hata kama wingu lilibaki kwenye masikini kwa siku mbili, kwa mwezi mmoja, au kwa mwaka mmoja, ili mradi tu limebaki pale, wana wa Israeli walibaki kwenye kambi zao na kusitisha safari. Lakini pale wingu liliponyanyuliwa, walianza safari yao.
Whether it was two days, or a month, or a year, that the cloud tarried upon the tabernacle, abiding on it, the sons of Israel remained encamped, and did not journey, but when it was taken up, they journeyed.
23 Walifanya kambi kwa amri ya BWANA, na walisafiri kwa amri yake. Walitii amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa
At the commandment of Jehovah they encamped, and at the commandment of Jehovah they journeyed. They kept the charge of Jehovah, at the commandment of Jehovah by Moses.

< Hesabu 9 >