< Hesabu 5 >

1 BWANA alinena na Musa. Akasema,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
2 “Waamuru wana wa Israel wawatoe watu wote wenye magonjwa ya ngozi yanayoambukiza, na kila mwenye mwenye vidonda vinavyotoa harufu, na ambaye amenajisika kwa kugusa maiti.
»Zapovej Izraelovim otrokom, da naj iz tabora odstranijo vsakega gobavca in vsakega, ki ima izliv in vsakogar, ki je omadeževan z mrtvim.
3 Awe mme au mke, umtoa kambini. Ili wasije wakaitia unajisi kambi, kwa sababu Mimi huishi ndani yake,”
Tako moškega in žensko boste poslali ven. Zunaj tabora jih boste poslali, da ne omadežujejo svojih taborov, v sredi katerih prebivam.«
4 Watu wa Israeli walifanya hivyo. Waliwatoa kambini, Kama BWANA alivyomwagiza Musa. Watu wa Israeli walimtii BWANA.
Izraelovi otroci so tako storili in jih poslali ven, zunaj tabora. Kakor je Gospod spregovoril Mojzesu, tako so Izraelovi otroci storili.
5 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
6 “Nena na wana wa Israeli. mtu mume na mtu mke akifanya dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana wao kwa wao, na mtu huyo akamwasi BWANA, mtu huyo atakuwa na hatia.
»Govori Izraelovim otrokom: ›Kadar bosta moški ali ženska zagrešila kakršenkoli greh, ki ga ljudje zagrešijo, da storita prestopek zoper Gospoda in da je oseba kriva,
7 Ndipo huyo mtu ataungama hiyo dhambi aliyoifanya. Mtu huyo atarudisha malipo ya hatia yake na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi. Atamlipa huyo aliyemtendea makosa
potem bosta priznala svoj greh, ki sta ga storila. In svoj prestopek bo poplačal z glavnico in ji dodal peti del od tega in to bo dal tistemu, zoper katerega je kršil.
8 Lakini kama huyo mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo, basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kuhani pamoja na kondoo dume kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.
Toda če človek nima nobenega sorodnika, da mu povrne prestopek, naj prestopek poplača Gospodu, celo duhovniku, poleg ovna sprave, s čimer bo zanj opravljena sprava.
9 Kila sadaka ya wana wa Israeli, vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli, vitakuwa vyake.
Vsaka daritev vseh svetih stvari Izraelovih otrok, ki jih prinesejo duhovniku, bo njegova.
10 Sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake.”
Vse človekove posvečene stvari bodo njegove; karkoli katerikoli človek daje duhovniku, to bo njegovo.‹«
11 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
12 “Nena na wana wa Israel. Uwaambie, 'kama mke wa mtu ataasi na kufanya dhambi dhidi ya mume wake.
»Govorite Izraelovim otrokom in jim recite: ›Če žena kateregakoli moškega zaide proč in zoper njega zagreši prestopek
13 Halafu mtu mwingine akalala naye. Kwa sababu, hiyo atakuwa amenajisika. Na hata kama mume wake hakuona na hajui, hata kama hakuna mtu aliyemkamta akiwa katika tendo na hakuna mtu wa kushuhudia dhidi yake; hata hivyo ile roho ya wivu itaendele kumjulisha yule mume kuwa mke wake amenajisika.
in moški z njo meseno leži in je to skrito pred očmi njenega soproga in je zadržano zaprto in je ona omadeževana in tam ni nobene priče zoper njo niti ona ni zasačena,
14 Ingawa, roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume wakati mke wake hajanajisika.
in pride nanj duh ljubosumnosti in je ljubosumen na svojo ženo in je ona omadeževana, ali če pride nanj duh ljubosumnosti in je ljubosumen na svojo ženo, pa ona ni omadeževana,
15 Kwa mazingira hayo, yule mwanamume anapaswa kumpeleka mke wake kwa kuhani. Yule mwanamume anapaswa kutoa sadaka ya divai kwa ajili yake. Atapaswa kuleta sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Asitie mafuta juu yake wala asitie ubani juu yake maana ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho wa uovu.
potem bo moški svojo ženo privedel k duhovniku in zanjo prinesel dar, desetino škafa ječmenove moke. Na to ne bo izlil olja niti nanj ne bo položil kadila, kajti to je daritev ljubosumnosti, daritev spominjanja, da bi v spomin privedla krivičnost.
16 Ndipo kuhani atasogeza karibu na kumweka mbele ya BWANA.
Duhovnik jo bo privedel bliže in jo postavil pred Gospoda.
17 Kuhani atachukua kikombe cha maji matakatifu na atachukua mavumbi ya kwenye masikani. Ataweka yale mavumbi kwenye maji.
Duhovnik bo vzel sveto vodo v lončeni posodi in od prahu, ki je na tleh šotorskega svetišča, bo duhovnik vzel in to dal v vodo.
18 Kisha kuhani atamweka huyo mwanamke mbele za BWANA na atazifungua nywele kichwani kwa huyo mwanamke. Atamwekea mikononi mwake hiyo sadaka ya unga kwa ajili ya ukumbusho, ambayo ni sadaka ya unga kwa ajili ya wivu.
Duhovnik bo žensko postavil pred Gospoda in odkril glavo ženske in v njene roke dal daritev spominjanja, kar je daritev ljubosumja. Duhovnik bo imel v svoji roki grenko vodo, ki povzroča prekletstvo,
19 Kuhani atashikilia mikononi mwake maji machungu yanayoweza kuleta laana. Kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya kiapo na kumwambia. 'Kama haujafanya uzinzi na mwanaume mwingine, na kama hajakengeuka na kufanya uovu, basi utakuwa huru na maji haya yanayoweza kuleta laana.
in duhovnik ji bo s prisego naročil ter ženski rekel: ›Če s teboj ni ležal noben moški in če nisi zašla v nečistost z drugim namesto svojega soproga, bodi čista pred to grenko vodo, ki povzroča prekletstvo.
20 Lakini kama wewe, mwanamke uliye chini ya mume wako, umekengeuka, na kama umenajisika, na kama mwanamume mwingina amelala nawe,
Toda če si zašla k drugemu namesto svojega soproga in če si omadeževana in je poleg tvojega soproga s teboj ležal nek moški,
21 ndipo, (kuhani atamtaka huyo mwanamke aape kiapo kinachoweza kuleta laana kwake, na kwamba ataendelea kumwambia yule mwanamke) 'BWANA atakufanya wewe kuwa laana itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako. Hii itatokea pale BWANA atakapoyafanya mapaja yako kuoza na tumbo lako kuvimba.
potem bo duhovnik žensko zaprisegel s prisego prekletstva in duhovnik bo ženski rekel: › Gospod naj te naredi za prekletstvo in prisego med tvojim ljudstvom, ko Gospod tvojemu stegnu stori, da zgnije in tvoj trebuh oteče,
22 Haya maji ambayo huleta laana yataingia tumboni mwako na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza,' mwanamke alitakiwa kujibu, 'Ndiyo, hayo yanipate kama mimi ni mwenye hatia.'
in ta voda, ki povzroča prekletstvo, bo šla v tvojo notranjost, da tvojemu trebuhu povzroči, da oteče in tvojemu stegnu, da zgnije.‹ In ženska naj reče: ›Amen, amen.‹
23 Naye kuhani ataziandika laana hizi kwenye kitabu, na kisha kuzifuta laana zilizoandikwa kwa maji ya uchungu.
Duhovnik bo ta prekletstva zapisal v knjigo in jih spral z grenko vodo.
24 Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji machungu yaletayo laana. Yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu.
Žensko bo primoral, da pije grenko vodo, ki povzroča prekletstvo in voda, ki povzroča prekletstvo, bo vstopila vanjo in postala grenka.
25 Kuhani ataitwaa ile sadaka ya unga ya wivu mikononi mwa yule mwanamke. Atailekeza ile sadaka ya unga mbele ya BWANA na kuileta madhabahuni.
Potem bo duhovnik vzel daritev ljubosumnosti iz roke ženske in daritev bo majal pred Gospodom in jo daroval na oltarju.
26 Kuhani atachukua konzi ya sadaka ya unga mkononi mwake kama sadaka ya kuwakilisha, na kuiteketeza madhabahuni. Ndipo atakapompatia mwanamke yale maji machungu ili ayanywe.
Duhovnik bo vzel prgišče daritve, torej njen spomin in to sežgal na oltarju in potem bo ženski povzročil, da spije vodo.
27 Wakati wa kumpa yale maji ili anywe, kama amenajisika kwa sababu alifanya uovu dhidi ya mume wake, ndipo yale maji yaletayo laana yatamwingia na kuwa machungu. Tumbo lake litavimba na paja lake litaoza. Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake.
Ko jo je primoral piti vodo, potem se bo zgodilo, da če je omadeževana in je storila prestopek zoper svojega soproga, da bo voda, ki povzroča prekletstvo, vstopila vanjo in postala grenka in njen trebuh bo otekel in njeno stegno bo zgnilo, in ženska bo prekletstvo med svojim ljudstvom.
28 Lakini kama yule mwanake hajanajisika na kama ni msafi, basi atakuwa huru. Tena ataweza kubeba uja uzito.
Če pa ženska ni omadeževana, temveč je čista, potem naj bo prosta in bo spočela seme.
29 Hii ndiyo sheria ya wivu. Ni sheria ya mwanamke anayekengeuka kwa mumewe na kunajisika.
To je postava ljubosumnosti, ko žena zaide k drugemu namesto svojega soproga in je omadeževana
30 Ni sheria ya mwanamume mwenye roho ya wivu kwa mkewe. Atamleta mwanamke mbele ya BWANA, na kuhani atamfanyia huyo mwanamke kila kitu ambacho sheria ya wivu inamtaka kufanya.
ali kadar pride nadenj duh ljubosumnosti in je ljubosumen na svojo ženo in bo ženo postavil pred Gospoda in bo duhovnik nad njo izvršil vso to postavo.
31 Yule mwanamume atakuwa hana hatia kwa kumleta mke wake kwa kuhani. Na yule mwanmke atauchukua uovu wake.”
Potem bo mož brez krivde pred krivičnostjo, ta ženska pa bo nosila svojo krivičnost.‹«

< Hesabu 5 >