< Hesabu 5 >
1 BWANA alinena na Musa. Akasema,
И рече Господь к Моисею, глаголя:
2 “Waamuru wana wa Israel wawatoe watu wote wenye magonjwa ya ngozi yanayoambukiza, na kila mwenye mwenye vidonda vinavyotoa harufu, na ambaye amenajisika kwa kugusa maiti.
повели сыном Израилевым, и да изгонят из полка всякаго прокаженнаго, и всякаго проливающаго семя, и всякаго нечистаго душею:
3 Awe mme au mke, umtoa kambini. Ili wasije wakaitia unajisi kambi, kwa sababu Mimi huishi ndani yake,”
от мужеска полу до женска, изгоните вне полка, и да не осквернят полков своих, в нихже Аз пребываю.
4 Watu wa Israeli walifanya hivyo. Waliwatoa kambini, Kama BWANA alivyomwagiza Musa. Watu wa Israeli walimtii BWANA.
И сотвориша сынове Израилевы тако, и изгнаша их вне полка: якоже глагола Господь Моисею, тако сотвориша сынове Израилевы.
5 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
И рече Господь к Моисею, глаголя:
6 “Nena na wana wa Israeli. mtu mume na mtu mke akifanya dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana wao kwa wao, na mtu huyo akamwasi BWANA, mtu huyo atakuwa na hatia.
рцы сыном Израилевым, глаголя: муж или жена, иже аще сотворит от всех грехов человеческих и презирая презрит Господа, и преступит душа она:
7 Ndipo huyo mtu ataungama hiyo dhambi aliyoifanya. Mtu huyo atarudisha malipo ya hatia yake na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi. Atamlipa huyo aliyemtendea makosa
да исповесть грех, егоже сотвори, и да отдаст преступление истое, пятую часть его да приложит к тому, и да отдаст, емуже согреши.
8 Lakini kama huyo mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo, basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kuhani pamoja na kondoo dume kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.
Аще же несть человеку ужика, яко отдати ему преступление, преступление отдаемое Господу, жерцу да будет, кроме овна очищения, имже помолится о нем.
9 Kila sadaka ya wana wa Israeli, vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli, vitakuwa vyake.
И всяк начаток, и вся освящаемая в сынех Израилевых, елика аще приносят Господу, жерцу самому да будут:
10 Sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake.”
и коегождо освященая, тому да будут и муж аще даст жерцу, тому да будет.
11 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
И рече Господь к Моисею, глаголя:
12 “Nena na wana wa Israel. Uwaambie, 'kama mke wa mtu ataasi na kufanya dhambi dhidi ya mume wake.
глаголи сыном Израилевым и речеши к ним: мужа, мужа аще преступит жена его, и презирающи презрит его,
13 Halafu mtu mwingine akalala naye. Kwa sababu, hiyo atakuwa amenajisika. Na hata kama mume wake hakuona na hajui, hata kama hakuna mtu aliyemkamta akiwa katika tendo na hakuna mtu wa kushuhudia dhidi yake; hata hivyo ile roho ya wivu itaendele kumjulisha yule mume kuwa mke wake amenajisika.
и будет кто с нею ложем семене, и утаится от очию мужа ея, и укрыется, она же будет осквернена, и свидетеля не будет на ню и сия несть ята,
14 Ingawa, roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume wakati mke wake hajanajisika.
и приидет на него дух ревнования, и возревнует к жене своей, она же осквернена есть, или приидет ему дух ревнования, и возревнует к жене своей, она же не будет осквернена,
15 Kwa mazingira hayo, yule mwanamume anapaswa kumpeleka mke wake kwa kuhani. Yule mwanamume anapaswa kutoa sadaka ya divai kwa ajili yake. Atapaswa kuleta sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Asitie mafuta juu yake wala asitie ubani juu yake maana ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho wa uovu.
и да приведет муж жену свою к жерцу, и да принесет дар за ню, десятую часть меры ефи муки ячныя: да не возлиет на ню елеа, ниже да возложит на ню ливана: жертва бо ревнования есть, жертва памяти воспоминающая грех.
16 Ndipo kuhani atasogeza karibu na kumweka mbele ya BWANA.
И приведет ю жрец и поставит ю пред Господем:
17 Kuhani atachukua kikombe cha maji matakatifu na atachukua mavumbi ya kwenye masikani. Ataweka yale mavumbi kwenye maji.
и да возмет жрец воду живу чисту в сосуде глиняне, и от персти на земли сущия у скинии свидения, и взем жрец да всыплет в воду:
18 Kisha kuhani atamweka huyo mwanamke mbele za BWANA na atazifungua nywele kichwani kwa huyo mwanamke. Atamwekea mikononi mwake hiyo sadaka ya unga kwa ajili ya ukumbusho, ambayo ni sadaka ya unga kwa ajili ya wivu.
и да поставит жрец жену пред Господем, и да открыет главу жене, и да даст в руце ея жертву памяти, жертву ревнования: в руце же жерца да будет вода обличения клятвенная сия.
19 Kuhani atashikilia mikononi mwake maji machungu yanayoweza kuleta laana. Kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya kiapo na kumwambia. 'Kama haujafanya uzinzi na mwanaume mwingine, na kama hajakengeuka na kufanya uovu, basi utakuwa huru na maji haya yanayoweza kuleta laana.
И да закленет ю жрец и речет жене: аще никтоже бысть с тобою, и неси преступила осквернитися под мужем твоим, невинна буди от воды обличения клятвенныя сея:
20 Lakini kama wewe, mwanamke uliye chini ya mume wako, umekengeuka, na kama umenajisika, na kama mwanamume mwingina amelala nawe,
аще же преступила еси, мужата сущи, или осквернена еси, и даде кто тебе ложе свое, кроме мужа твоего.
21 ndipo, (kuhani atamtaka huyo mwanamke aape kiapo kinachoweza kuleta laana kwake, na kwamba ataendelea kumwambia yule mwanamke) 'BWANA atakufanya wewe kuwa laana itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako. Hii itatokea pale BWANA atakapoyafanya mapaja yako kuoza na tumbo lako kuvimba.
И закленет жрец жену клятвами клятвы сея, и речет жрец жене: да даст тя Господь в клятву и проклятие среди людий твоих, внегда дати Господу стегну твоему отпасти и чреву твоему разсестися:
22 Haya maji ambayo huleta laana yataingia tumboni mwako na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza,' mwanamke alitakiwa kujibu, 'Ndiyo, hayo yanipate kama mimi ni mwenye hatia.'
и внидет вода клятвенная сия во чрево твое, еже расторгнути утробу твою, и отпасти стегну твоему. И отвещает жена:
23 Naye kuhani ataziandika laana hizi kwenye kitabu, na kisha kuzifuta laana zilizoandikwa kwa maji ya uchungu.
и да напишет жрец клятвы сия в книзе, и изгладит в воде обличения клятвеннаго:
24 Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji machungu yaletayo laana. Yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu.
и напоит жену водою обличения клятвенною, и внидет в ню вода клятвенная обличения.
25 Kuhani ataitwaa ile sadaka ya unga ya wivu mikononi mwa yule mwanamke. Atailekeza ile sadaka ya unga mbele ya BWANA na kuileta madhabahuni.
И да возмет жрец от руки женски жертву ревнования, и да возложит жертву пред Господем, и да принесет ю ко олтарю:
26 Kuhani atachukua konzi ya sadaka ya unga mkononi mwake kama sadaka ya kuwakilisha, na kuiteketeza madhabahuni. Ndipo atakapompatia mwanamke yale maji machungu ili ayanywe.
и да возмет жрец горстию от жертвы память ея, и да принесет ю на олтарь, и по сем напоит водою жену.
27 Wakati wa kumpa yale maji ili anywe, kama amenajisika kwa sababu alifanya uovu dhidi ya mume wake, ndipo yale maji yaletayo laana yatamwingia na kuwa machungu. Tumbo lake litavimba na paja lake litaoza. Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake.
И будет аше есть осквернена, и аще утаением утаися от мужа своего, и внидет в ню вода клятвенная обличения, и надмет чрево ея, и отпадет стегно ея, и будет жена в проклятие в людех своих:
28 Lakini kama yule mwanake hajanajisika na kama ni msafi, basi atakuwa huru. Tena ataweza kubeba uja uzito.
аще же не будет осквернена жена, и чиста есть, и невинна будет, и плодствовати будет семя.
29 Hii ndiyo sheria ya wivu. Ni sheria ya mwanamke anayekengeuka kwa mumewe na kunajisika.
Сей закон ревнования, комулибо аще преступит жена, мужата сущи, и осквернится:
30 Ni sheria ya mwanamume mwenye roho ya wivu kwa mkewe. Atamleta mwanamke mbele ya BWANA, na kuhani atamfanyia huyo mwanamke kila kitu ambacho sheria ya wivu inamtaka kufanya.
или человек, емуже аще найдет нань дух ревнования, и возревнует к жене своей, и поставит жену свою пред Господем, и да сотворит ей жрец весь закон сей:
31 Yule mwanamume atakuwa hana hatia kwa kumleta mke wake kwa kuhani. Na yule mwanmke atauchukua uovu wake.”
и чист будет человек от греха, и жена та возмет грех свой.