< Hesabu 5 >

1 BWANA alinena na Musa. Akasema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Waamuru wana wa Israel wawatoe watu wote wenye magonjwa ya ngozi yanayoambukiza, na kila mwenye mwenye vidonda vinavyotoa harufu, na ambaye amenajisika kwa kugusa maiti.
Command [the] people of Israel so they may send away from the camp any [one who] has a skin disease and any [one who] has a discharge and any [person] unclean to a corpse.
3 Awe mme au mke, umtoa kambini. Ili wasije wakaitia unajisi kambi, kwa sababu Mimi huishi ndani yake,”
From male unto female you will send away to from [the] outside of the camp you will send away them and not they will make unclean camps their which I [am] dwelling in midst of them.
4 Watu wa Israeli walifanya hivyo. Waliwatoa kambini, Kama BWANA alivyomwagiza Musa. Watu wa Israeli walimtii BWANA.
And they did so [the] people of Israel and they sent away them to from [the] outside of the camp just as he had spoken Yahweh to Moses so they did [the] people of Israel.
5 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
6 “Nena na wana wa Israeli. mtu mume na mtu mke akifanya dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana wao kwa wao, na mtu huyo akamwasi BWANA, mtu huyo atakuwa na hatia.
Speak to [the] people of Israel a man or a woman if they will do any of all [the] sins of humankind by acting unfaithfully unfaithfulness against Yahweh and it will be guilty the person that.
7 Ndipo huyo mtu ataungama hiyo dhambi aliyoifanya. Mtu huyo atarudisha malipo ya hatia yake na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi. Atamlipa huyo aliyemtendea makosa
And they will confess sin their which they have done and he will repay compensation its in sum its and fifth its let him add to it and he will give [it] to [the one] whom he was guilty to him.
8 Lakini kama huyo mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo, basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kuhani pamoja na kondoo dume kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.
And if not [belongs] to the person a kinsman-redeemer to repay the compensation to him the compensation which is repaid [belongs] to Yahweh for the priest besides [the] ram of atonement which he will make atonement by it on him.
9 Kila sadaka ya wana wa Israeli, vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli, vitakuwa vyake.
And every contribution to all [the] holy things of [the] people of Israel which they will bring near to the priest to him it will belong.
10 Sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake.”
And everyone holy things his to him they will belong everyone [that] which he will give to the priest to him it will belong.
11 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
12 “Nena na wana wa Israel. Uwaambie, 'kama mke wa mtu ataasi na kufanya dhambi dhidi ya mume wake.
Speak to [the] people of Israel and you will say to them a man a man if she will turn aside wife his and she will act unfaithfully against him unfaithfulness.
13 Halafu mtu mwingine akalala naye. Kwa sababu, hiyo atakuwa amenajisika. Na hata kama mume wake hakuona na hajui, hata kama hakuna mtu aliyemkamta akiwa katika tendo na hakuna mtu wa kushuhudia dhidi yake; hata hivyo ile roho ya wivu itaendele kumjulisha yule mume kuwa mke wake amenajisika.
And he will lie with a man with her a laying of seed and it will be hidden from [the] eyes of husband her and she will be undiscovered and she she has made herself unclean and [was] a witness there not against her and she not she was caught.
14 Ingawa, roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume wakati mke wake hajanajisika.
And it will pass over him a spirit of jealousy and he will be jealous of wife his and she she has made herself unclean or it has passed over him a spirit of jealousy and he will be jealous of wife his and she not she has made herself unclean.
15 Kwa mazingira hayo, yule mwanamume anapaswa kumpeleka mke wake kwa kuhani. Yule mwanamume anapaswa kutoa sadaka ya divai kwa ajili yake. Atapaswa kuleta sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Asitie mafuta juu yake wala asitie ubani juu yake maana ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho wa uovu.
And he will bring the man wife his to the priest and he will bring offering her on her tenth of ephah flour of barley not he will pour out on it oil and not he will put on it frankincense for [is] a grain offering of jealousi it a grain offering of remembrance [which] brings to remembrance iniquity.
16 Ndipo kuhani atasogeza karibu na kumweka mbele ya BWANA.
And he will bring near her the priest and he will make stand her before Yahweh.
17 Kuhani atachukua kikombe cha maji matakatifu na atachukua mavumbi ya kwenye masikani. Ataweka yale mavumbi kwenye maji.
And he will take the priest water holy in a vessel of earthenware and some of the dust which it will be on [the] floor of the tabernacle he will take the priest and he will put [it] into the water.
18 Kisha kuhani atamweka huyo mwanamke mbele za BWANA na atazifungua nywele kichwani kwa huyo mwanamke. Atamwekea mikononi mwake hiyo sadaka ya unga kwa ajili ya ukumbusho, ambayo ni sadaka ya unga kwa ajili ya wivu.
And he will make stand the priest the woman before Yahweh and he will let loose [the] head of the woman and he will put on hands her [the] grain offering of remembrance [is] a grain offering of jealousi it and in [the] hand of the priest they will be [the] waters of bitter [things] which bring a curse.
19 Kuhani atashikilia mikononi mwake maji machungu yanayoweza kuleta laana. Kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya kiapo na kumwambia. 'Kama haujafanya uzinzi na mwanaume mwingine, na kama hajakengeuka na kufanya uovu, basi utakuwa huru na maji haya yanayoweza kuleta laana.
And he will make swear her the priest and he will say to the woman if not he has lain with a man with you and if not you have turned aside uncleanness under husband your be free from [the] waters of bitter [things] which bring a curse these.
20 Lakini kama wewe, mwanamke uliye chini ya mume wako, umekengeuka, na kama umenajisika, na kama mwanamume mwingina amelala nawe,
And you if you have turned aside under husband your and if you have made yourself unclean and he has given a man in you copulation his from except husband your.
21 ndipo, (kuhani atamtaka huyo mwanamke aape kiapo kinachoweza kuleta laana kwake, na kwamba ataendelea kumwambia yule mwanamke) 'BWANA atakufanya wewe kuwa laana itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako. Hii itatokea pale BWANA atakapoyafanya mapaja yako kuoza na tumbo lako kuvimba.
And he will make swear the priest the woman with [the] oath of the curse and he will say the priest to the woman may he make Yahweh you into a curse and into a oath in among people your when makes Yahweh thigh your falling and belly your swollen.
22 Haya maji ambayo huleta laana yataingia tumboni mwako na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza,' mwanamke alitakiwa kujibu, 'Ndiyo, hayo yanipate kama mimi ni mwenye hatia.'
And they will go the waters which bring a curse these in inward parts your to make swell a belly and to make fall a thigh and she will say the woman amen - amen.
23 Naye kuhani ataziandika laana hizi kwenye kitabu, na kisha kuzifuta laana zilizoandikwa kwa maji ya uchungu.
And he will write the curses these the priest on the scroll and he will wipe [them] off into [the] waters of bitter [things].
24 Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji machungu yaletayo laana. Yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu.
And he will make drink the woman [the] waters of bitter [things] which bring a curse and they will go in her the waters which bring a curse to bitter [things].
25 Kuhani ataitwaa ile sadaka ya unga ya wivu mikononi mwa yule mwanamke. Atailekeza ile sadaka ya unga mbele ya BWANA na kuileta madhabahuni.
And he will take the priest from [the] hand of the woman [the] grain offering of jealousi and he will wave the grain offering before Yahweh and he will bring near it to the altar.
26 Kuhani atachukua konzi ya sadaka ya unga mkononi mwake kama sadaka ya kuwakilisha, na kuiteketeza madhabahuni. Ndipo atakapompatia mwanamke yale maji machungu ili ayanywe.
And he will take a handful the priest of the grain offering memorial offering its and he will make [it] smoke the altar towards and after he will make drink the woman the waters.
27 Wakati wa kumpa yale maji ili anywe, kama amenajisika kwa sababu alifanya uovu dhidi ya mume wake, ndipo yale maji yaletayo laana yatamwingia na kuwa machungu. Tumbo lake litavimba na paja lake litaoza. Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake.
And he will make drink her the waters and she will be if she has made herself unclean and she has acted unfaithfully unfaithfulness against husband her and they will go in her the waters which bring a curse to bitter [things] and it will swell belly her and it will fall thigh her and she will become the woman a curse in [the] midst of people her.
28 Lakini kama yule mwanake hajanajisika na kama ni msafi, basi atakuwa huru. Tena ataweza kubeba uja uzito.
And if not she has made herself unclean the woman and [is] pure she and she will be free and she will be impregnated seed.
29 Hii ndiyo sheria ya wivu. Ni sheria ya mwanamke anayekengeuka kwa mumewe na kunajisika.
This [is] [the] law of jealousi that she will turn aside a wife under husband her and she will make herself unclean.
30 Ni sheria ya mwanamume mwenye roho ya wivu kwa mkewe. Atamleta mwanamke mbele ya BWANA, na kuhani atamfanyia huyo mwanamke kila kitu ambacho sheria ya wivu inamtaka kufanya.
Or a man whom it will pass over him a spirit of jealousy and he will be jealous of wife his and he will make stand the woman before Yahweh and he will do to her the priest all the law this.
31 Yule mwanamume atakuwa hana hatia kwa kumleta mke wake kwa kuhani. Na yule mwanmke atauchukua uovu wake.”
And he will be free the man from iniquity and the woman that she will bear iniquity her.

< Hesabu 5 >