< Hesabu 5 >
1 BWANA alinena na Musa. Akasema,
And the Lord spoke to Moses, saying:
2 “Waamuru wana wa Israel wawatoe watu wote wenye magonjwa ya ngozi yanayoambukiza, na kila mwenye mwenye vidonda vinavyotoa harufu, na ambaye amenajisika kwa kugusa maiti.
“Instruct the sons of Israel to cast out of the camp every leper, and those who have a flow of seed, and those who have been polluted because of the dead;
3 Awe mme au mke, umtoa kambini. Ili wasije wakaitia unajisi kambi, kwa sababu Mimi huishi ndani yake,”
cast out of the camp both male and female, lest they contaminate it while I am dwelling with you.”
4 Watu wa Israeli walifanya hivyo. Waliwatoa kambini, Kama BWANA alivyomwagiza Musa. Watu wa Israeli walimtii BWANA.
And the sons of Israel did so, and they cast them out, beyond the camp, just as the Lord had spoken to Moses.
5 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
And the Lord spoke to Moses, saying:
6 “Nena na wana wa Israeli. mtu mume na mtu mke akifanya dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana wao kwa wao, na mtu huyo akamwasi BWANA, mtu huyo atakuwa na hatia.
“Say to the sons of Israel: A man or a woman, when they have done anything out of all the sins that often befall men, or if, by negligence, they have transgressed the commandment of the Lord, and so have committed an offense,
7 Ndipo huyo mtu ataungama hiyo dhambi aliyoifanya. Mtu huyo atarudisha malipo ya hatia yake na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi. Atamlipa huyo aliyemtendea makosa
they shall confess their sin, and they shall restore the principle itself, plus a fifth part above it, to any against whom they have sinned.
8 Lakini kama huyo mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo, basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kuhani pamoja na kondoo dume kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.
But if there would be no one to receive it, they shall give it to the Lord, and it shall be for the priest, except for the ram, which is offered for expiation, in order to be a pleasing victim.
9 Kila sadaka ya wana wa Israeli, vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli, vitakuwa vyake.
Likewise, all the first-fruits, which the sons of Israel offer, belong to the priest,
10 Sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake.”
with whatever is offered by each one at the Sanctuary, and which is delivered into the hands of the priest; it shall be his.”
11 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
And the Lord spoke to Moses, saying:
12 “Nena na wana wa Israel. Uwaambie, 'kama mke wa mtu ataasi na kufanya dhambi dhidi ya mume wake.
“Speak to the sons of Israel, and you shall say to them: The man whose wife will have gone astray, and, disdaining her husband,
13 Halafu mtu mwingine akalala naye. Kwa sababu, hiyo atakuwa amenajisika. Na hata kama mume wake hakuona na hajui, hata kama hakuna mtu aliyemkamta akiwa katika tendo na hakuna mtu wa kushuhudia dhidi yake; hata hivyo ile roho ya wivu itaendele kumjulisha yule mume kuwa mke wake amenajisika.
will have slept with another man, and if her husband cannot discover it, but the adultery is secret, and if it cannot be proved by witnesses, because she was not caught in the shameful act,
14 Ingawa, roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume wakati mke wake hajanajisika.
if the spirit of jealousy stirs up the husband against his wife, who either has been polluted or is being assailed with a false suspicion,
15 Kwa mazingira hayo, yule mwanamume anapaswa kumpeleka mke wake kwa kuhani. Yule mwanamume anapaswa kutoa sadaka ya divai kwa ajili yake. Atapaswa kuleta sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Asitie mafuta juu yake wala asitie ubani juu yake maana ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho wa uovu.
he shall bring her to the priest, and he shall offer an oblation for her, a tenth part of native barley meal. He shall not pour oil over it, nor shall he place frankincense on it, because it is a sacrifice for jealousy, or an oblation investigating adultery.
16 Ndipo kuhani atasogeza karibu na kumweka mbele ya BWANA.
Therefore, the priest shall offer it, and he shall set it in the sight of the Lord.
17 Kuhani atachukua kikombe cha maji matakatifu na atachukua mavumbi ya kwenye masikani. Ataweka yale mavumbi kwenye maji.
And he shall take up holy water in an earthen vessel, and he shall cast a little earth from the pavement of the tabernacle into it.
18 Kisha kuhani atamweka huyo mwanamke mbele za BWANA na atazifungua nywele kichwani kwa huyo mwanamke. Atamwekea mikononi mwake hiyo sadaka ya unga kwa ajili ya ukumbusho, ambayo ni sadaka ya unga kwa ajili ya wivu.
And while the woman stands before the Lord, he shall uncover her head, and he shall place over her hands the sacrifice of recollection and oblation of jealousy. But he shall take hold of the most bitter waters, in which he has gathered curses with loathing.
19 Kuhani atashikilia mikononi mwake maji machungu yanayoweza kuleta laana. Kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya kiapo na kumwambia. 'Kama haujafanya uzinzi na mwanaume mwingine, na kama hajakengeuka na kufanya uovu, basi utakuwa huru na maji haya yanayoweza kuleta laana.
And he shall bind her by an oath, and he shall say: ‘If another man has not slept with you, and if you have not been polluted by forsaking the bed of your husband, these most bitter waters, into which I have gathered curses, shall not harm you.
20 Lakini kama wewe, mwanamke uliye chini ya mume wako, umekengeuka, na kama umenajisika, na kama mwanamume mwingina amelala nawe,
But if you have turned away from your husband, and also have been defiled, and have lain together with another man,
21 ndipo, (kuhani atamtaka huyo mwanamke aape kiapo kinachoweza kuleta laana kwake, na kwamba ataendelea kumwambia yule mwanamke) 'BWANA atakufanya wewe kuwa laana itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako. Hii itatokea pale BWANA atakapoyafanya mapaja yako kuoza na tumbo lako kuvimba.
these curses shall be thrown upon you: May the Lord turn you into a curse and an example among all his people. May he cause your thigh to rot, and may your abdomen swell up and burst out.
22 Haya maji ambayo huleta laana yataingia tumboni mwako na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza,' mwanamke alitakiwa kujibu, 'Ndiyo, hayo yanipate kama mimi ni mwenye hatia.'
May the cursed waters enter into your stomach, and may your womb swell and your thigh rot.’ And the woman shall respond: ‘Amen, amen.’
23 Naye kuhani ataziandika laana hizi kwenye kitabu, na kisha kuzifuta laana zilizoandikwa kwa maji ya uchungu.
And the priest shall write these curses in a little book, and then he shall erase them with the very bitter waters, into which he had gathered the curses,
24 Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji machungu yaletayo laana. Yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu.
and he shall give it to her to drink. And when she has emptied it,
25 Kuhani ataitwaa ile sadaka ya unga ya wivu mikononi mwa yule mwanamke. Atailekeza ile sadaka ya unga mbele ya BWANA na kuileta madhabahuni.
the priest shall take from her hand the sacrifice of jealousy, and he shall elevate it before the Lord, and he shall impose it upon the altar. Yet only after he first
26 Kuhani atachukua konzi ya sadaka ya unga mkononi mwake kama sadaka ya kuwakilisha, na kuiteketeza madhabahuni. Ndipo atakapompatia mwanamke yale maji machungu ili ayanywe.
takes a handful of the sacrifice from that which is offered, and burns it upon the altar, and then he may give the most bitter waters to the woman as a drink.
27 Wakati wa kumpa yale maji ili anywe, kama amenajisika kwa sababu alifanya uovu dhidi ya mume wake, ndipo yale maji yaletayo laana yatamwingia na kuwa machungu. Tumbo lake litavimba na paja lake litaoza. Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake.
And when she drinks it, if she has been defiled, and, having despised her husband, is guilty of adultery, the curse shall pass through her, and as her belly swells up, her thigh shall decay, and the woman shall become a curse and an example to all the people.
28 Lakini kama yule mwanake hajanajisika na kama ni msafi, basi atakuwa huru. Tena ataweza kubeba uja uzito.
But if she has not been defiled, she shall be unharmed and she shall bear children.
29 Hii ndiyo sheria ya wivu. Ni sheria ya mwanamke anayekengeuka kwa mumewe na kunajisika.
This is the law for jealousy. If a woman has turned aside from her husband, and if she has been polluted,
30 Ni sheria ya mwanamume mwenye roho ya wivu kwa mkewe. Atamleta mwanamke mbele ya BWANA, na kuhani atamfanyia huyo mwanamke kila kitu ambacho sheria ya wivu inamtaka kufanya.
and if the husband, being stirred up by the spirit of jealousy, has brought her before the sight of the Lord, and the priest has acted toward her according to all that has been written:
31 Yule mwanamume atakuwa hana hatia kwa kumleta mke wake kwa kuhani. Na yule mwanmke atauchukua uovu wake.”
then the husband shall be without guilt, and she shall bear her iniquity.”