< Hesabu 4 >

1 BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
Et l'Eternel parla à Moïse, et à Aaron, en disant:
2 Fanya sensa ya uzao waume wa Kohathi kutoka kwa Walawi, kwa kufuata jamaa na na familia za koo.
Faites le dénombrement des enfants de Kéhath d'entre les enfants de Lévi par leurs familles, [et] par les maisons de leurs pères,
3 Uwahesabu wanaume ambao wana umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Hawa wataungana na kundi linalotumika kutoa huduma kwenye hema ya kukutania.
Depuis l'âge de trente ans et au dessus, jusqu'à l'âge de cinquante ans, tous ceux qui entrent en rang, pour s'employer au Tabernacle d'assignation.
4 Uzao wa Kohathi watalinda vile vitu vitakatifu zaidi vilivyohifadhiwa kwa ajili yangu katika hema ya kukutania.
C'est ici le service des enfants de Kéhath au Tabernacle d'assignation, [c'est-à-dire], le lieu très-Saint.
5 Wakati kambi inapojiandaa kusonga mbele, Haruni na wanawe lazima waende hemani, kulishusha pazia linalotenganisha mahali patakatifu na kulifunika sanduku la ushuhuda kwa pazia hilo. Watalifunika hilo sanduku kwa ngozi za pomboo.
Quand le camp partira, Aaron et ses fils viendront, et ils détendront le voile de tapisserie, et en couvriront l'Arche du Témoignage.
6 Watatandika juu yake nguo za rangi ya samawi. Watachomeka hiyo miti ya kubebea.
Puis ils mettront au dessus une couverture de peaux de taissons, ils étendront par dessus un drap de pourpre, et ils y mettront ses barres.
7 Watatandika nguo ya rangi ya samawi kwenye meza ya mikate ya wonyesho. Juu yake wataweka sahani, vijiko, mabakuli na vikombe vya kumiminia. Mikate itakuwepo daima mezani.
Et ils étendront un drap de pourpre sur la Table [des pains] de proposition, et mettront sur elle les plats, les tasses, les bassins, et les gobelets d'aspersion. Le pain continuel sera sur elle.
8 Wataifunika na nguo ya rangi nyekundu na ngozi za pomboo. na kuweka miti ya kubebea.
Ils étendront au dessus un drap teint de cramoisi, ils le couvriront d'une couverture de peaux de taissons, et ils y mettront ses barres.
9 Watachukua nguo ya rangi ya samawi na kukifunika kinara, pamoja na taa zake, na koleo zake, na sahani zake na vikombe vyake vya kuwekea mafuta ya taa.
Et ils prendront un drap de pourpre, et en couvriront le chandelier du luminaire avec ses lampes, ses mouchettes, ses creuseaux, et tous les vaisseaux d'huile, desquels on se sert pour le chandelier;
10 Wataweka kinara na vifaa vyake vikiwa vimefunikwa na ngozi ya pomboo, na wataweka kwenye miti ya kukibebea.
Et ils le mettront avec tous ses vaisseaux dans une couverture de peaux de taissons, et le mettront sur des leviers.
11 Watafunika na nguo ya samawi katika madhabau ya dhahabu. Wataifunika na ngozi za pomboo, na kuweka ile miti ya kubebea.
Ils étendront sur l'autel d'or un drap de pourpre, ils le couvriront d'une couverture de peaux de taissons, et ils y mettront ses barres.
12 Watavichukua vyombo vyote vya kazi takatifu na kuvizonga kwenye hiyo nguo ya rangi ya samawi. Watavifunika na ngozi za pomboo na kuviweka hivyo vyombo kwenye miti ya kubebea.
Ils prendront aussi tous les ustensiles du service dont on se sert au Sanctuaire, ils [les] mettront dans un drap de pourpre, et ils les couvriront d'une couverture de peaux de taissons, et les mettront sur des leviers.
13 Watayaondoa majivu kwenye madhabahu na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake.
Ils ôteront les cendres de l'autel, et étendront dessus un drap d'écarlate.
14 Watavieka kwenye miti ya kubebea vyombo vyote wanavyovitumia kwa kazi ya madhabahuni. Vyombo hivi ni vyetezo, majembe, mabakuli na vitu vingine vya madhabahuni. Wataifuniks madhabahu na ngozi za pomboo na kuweka ile miti ya kubebea.
Et ils mettront dessus les ustensiles dont on se sert pour l'autel, les encensoirs, les crochets, les racloirs, les bassins, et tous les vaisseaux de l'autel; ils étendront dessus une couverture de peaux de taissons, et ils y mettront ses barres.
15 Wakati Haruni na wanawe walipokuwa wamekamilisha kupafunika mahali patakatifu na vyombo vyote, na kambi itakapoanza kuendelea mbele, ndipo wana wa Kohathi watakapokuja kubeba vitu vya mahali patakatifu. Kama watagusa vyombo vitakatifu, lazima watakufa. Hii ni kazi ya wana wa uzao wa Kohathi, kubeba mapambo ya hema ya kukutania.
Le camp partira après qu'Aaron et ses fils auront achevé de couvrir le Sanctuaire et tous ses vaisseaux, et après cela les enfants de Kéhath viendront pour le porter, et ils ne toucheront point les choses saintes, de peur qu'ils ne meurent; c'[est] là ce que les enfants de Kéhath porteront du Tabernacle d'assignation.
16 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atalinda na kusimamia mafuta ya taa, ubani mzuri, sadaka za mara kwa mara na mafuta ya upako. Atasimamia ulinzi wa hema lote na vyote vilivyomo, mahali patakatifu na vyombo vyake.”
Et Eléazar fils d'Aaron, Sacrificateur, aura la charge de l'huile du luminaire, du parfum de drogues, du gâteau continuel, et de l'huile de l'onction; la charge de tout le pavillon, et de toutes les choses qui sont dans le Sanctuaire, et de ses ustensiles.
17 BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
Et l'Eternel parla à Moïse et à Aaron, en disant:
18 Usiruhusu kabila la Wakohathi kuondolewa kati ya Walawi.
Ne donnez point occasion que la race des familles de Kéhath soit retranchée d'entre les Lévites.
19 Walinde waishi ili wasije wakafa, kwa kufanya hivi. Wanapokuwa wanasogelea
Mais faites ceci pour eux, afin qu'ils vivent et ne meurent point; c'est que quand ils approcheront des choses très-Saintes, Aaron et ses fils viendront, qui les rangeront chacun à son service, et à ce qu'il doit porter.
20 wasije wakaingia ndani ili kuona eneo takatifu hata kwa kitambo, vinginevyo watakufa. Bali Haruni na wanawe wanaweza kuingia, ndipo Haruni na Wanawe watakapowapangia Wakohathi kazi maalumu ya kufanya, kwa kila mmoj.”
Et ils n'entreront point pour regarder quand on enveloppera les choses saintes, afin qu'ils ne meurent point.
21 BWANA akanena na Musa tena, Akasema, “Fanya sensa kwa wana Gerishoni pia, kwa kufuata familia za mababu zao, koo zao.
L'Eternel parla aussi à Moïse, en disant:
22 Uwahesabu wale wenye umri wa mika thelathini hadi miaka hamsini.
Fais aussi le dénombrement des enfants de Guerson selon les maisons de leurs pères, [et] selon leurs familles;
23 Uwahesabu wote ili waje kuungana na wale wanaotumika katika hema ya kukutania.
Depuis l'âge de trente ans, et au dessus, jusqu'à l'âge de cinquante ans, dénombrant tous ceux qui entrent pour tenir leur rang, afin de s'employer à servir au Tabernacle d'assignation.
24 Hii ndiyo itakuwa kazi ya koo za Gerishoni, wanapotumikia na wanachobeba.
C'est ici le service des familles des Guersonites, en ce à quoi ils doivent servir, et en ce qu'ils doivent porter.
25 Watabeba pazia la masikani, hema la kukutania, na vifunikio vyake, vifuniko vya ngozi ya pomboo ambvyo viko juu yake, na pazia kwenye lango la hema ya kukutania.
Ils porteront donc les rouleaux du pavillon, et le Tabernacle d'assignation, sa couverture, la couverture de taissons qui est sur lui par dessus, et la tapisserie de l'entrée du Tabernacle d'assignation;
26 Watabeba pazia la ua, pazia la kwenye mlango wa ua, ambao uko karibu na maskani karibu na madhabahu, kamba zake na vifaa vyote vya utumishi wake. Chochote kinachotakiwa kufanywa kutokana na vitu hivi, wao ndio watakaofanya.
Les courtines du parvis, et la tapisserie de l'entrée de la porte du parvis, qui servent pour le pavillon et pour l'autel tout autour, leur cordage, et tous les ustensiles de leur service, et tout ce qui est fait pour eux; c'est ce en quoi ils serviront.
27 Haruni na wanawe ndio watakaongoza utumishi wa uzao wa Wagerishoni, kwa vitu vyote vile vya kusafirisha, na katika utumishi wao wote. Lazima uwagawie majukumu yao yote.
Tout le service des enfants de Guerson en tout ce qu'ils doivent porter, et en tout ce à quoi ils doivent servir, sera [réglé] par les ordres d'Aaron et de ses fils, et vous les chargerez d'observer tout ce qu'ils doivent porter.
28 Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa wana wa Wagerishoni katka hema ya kukutania. Ithamari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza katika utumishi.
C'est là le service des familles des enfants des Guersonites au Tabernacle d'assignation; et leur charge sera sous la conduite d'Ithamar, fils d'Aaron Sacrificateur.
29 Utawahesabu uzao wa Merari kwa koo zao, na uwapange katika familia za mabau zao,
Tu dénombreras aussi les enfants de Mérari selon leurs familles [et] selon les maisons de leurs pères.
30 kuanzia wenye umri wa miaka thelatini hadi miaka hamsini. Umuhesabu kila atakayeungana na kundi lenye utumishi katika hema ya kukutania.
Tu les dénombreras depuis l'âge de trente ans et au dessus, jusqu'à l'âge de cinquante ans; tous ceux qui entrent en rang pour s'employer au service du Tabernacle d'assignation.
31 Huu ndio wajibu na kazi yao katika utumishi wao kwenye hema ya kukutania. Watazilinda mbao za maskani, mataluma yake, nguzo na makalishio yake,
Or c'est ici la charge de ce qu'ils auront à porter, selon tout le service qu'ils auront à faire au Tabernacle d'assignation, [savoir] les ais du pavillon, ses barres, et ses piliers, avec ses soubassements;
32 pamoja na nguzo za ua zinazozunguka masikani, makalishio yake, vigingi na kamba zake, na vifaa vinginevya ujenzi. Waorodheshe kwa majina na majukumu yao.
Et les piliers du parvis tout autour, et leurs soubassements, leurs clous, leurs cordages, tous leurs ustensiles, et tout ce dont on se sert en ces choses-là, et vous leur compterez tous les ustensiles qu'ils auront charge de porter, pièce par pièce.
33 Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa Merari, ambao wanatakiwa kufanya katika hema ya kukutania, chini ya uongozi wa Ithmari mwana wa Haruni kuhani.”
C'est là le service des familles des enfants de Mérari, pour tout ce à quoi ils doivent servir au Tabernacle d'assignation, sous la conduite d'Ithamar, fils d'Aaron, Sacrificateur.
34 Musa na Haruni na viongozi wa watu waliwahesabu wana wa uzao wa Wakohathi kwa kufuata koo za familia za mababu zao.
Moïse donc et Aaron, et les principaux de l'assemblée dénombrèrent les enfants des Kéhathites, selon leurs familles, et selon les maisons de leurs pères.
35 Waliwahesabu wale wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Walimhesabu kila mmoja aliyepaswa kuungana na kundi linalotoa huduma ya utumishi kwenye hema ya kukutania.
Depuis l'âge de trente ans, et au dessus, jusqu'à l'âge de cinquante ans, tous ceux qui entraient en rang pour servir au Tabernacle d'assignation.
36 Waliwahesabu wanaume 2, 750 kwa kufuata koo zao.
Et ceux dont on fit le dénombrement selon leurs familles, étaient deux mille sept cent cinquante.
37 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote kutoka koo na familia za Wakohathi ambao hutumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi kwa kumtii BWANA aliyewaagiza kupitia kwa Musa.
Ce sont là les dénombrés des familles des Kéhathites, tous servant au Tabernacle d'assignation, lesquels Moïse et Aaron dénombrèrent semon le commandement que l'Eternel en avait fait par le moyen de Moïse.
38 Uzao wa Gerishoni walihesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao,
Or quant aux dénombrés des enfants de Guerson selon leurs familles, et selon les maisons de leurs pères,
39 kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kwa kila mmoja aliyetakiwa kuungana na watu wanaotoa huduma kwenye hema ya kukutania.
Depuis l'âge de trente ans, et au dessus, jusqu'à l'âge de cinquante ans, tous ceux qui entraient en rang pour servir au Tabernacle d'assignation,
40 Wanaume wote waliohesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao walikuwa 2, 630.
Ceux, [dis-je], qui en furent dénombrés selon leurs familles, et selon les maisons de leurs pères, étaient deux mille six cent trente.
41 Musa na Haruni walizihesabu koo za uzao wa Gerishoni ambao watatumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi ili kutii ambacho BWANA aliwaamuru kufanya kuptia kwa Musa.
Ce sont là les dénombrés des familles des enfants de Guerson, tous servant au Tabernacle d'assignation, lesquels Moïse et Aaron dénombrèrent selon le commandement de l'Eternel.
42 Uzao wa Merari walihesabiwa kwa koo kupitia familia za mababu zao,
Et quant aux dénombrés des familles des enfants de Mérari, selon leurs familles, [et] selon les maisons de leurs pères,
43 kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kila anayepaswa kuungana na watu wanaotumika kwenye hema ya kukutania.
Depuis l'âge de trente ans, et au dessus, jusqu'à l'âge de cinquante ans, tous ceux qui entraient en rang, pour servir au Tabernacle d'assignation;
44 Wanaume wote waliohesabiwa kupitia koo za familia za mababu zao walikuwa 3. 200.
Ceux, [dis-je], qui en furent dénombrés selon leurs familles, étaient trois mille deux cents.
45 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume hawa, uzao wa Merari. Kw kufanya hivi walitii amri ya BWANA aliyowaaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
Ce sont là les dénombrés des familles des enfants de Mérari, que Moïse et Aaron dénombrèrent selon le commandement que l'Eternel en avait fait par le moyen de Moïse.
46 Kwa hiyo Musa na Haruni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kw kufuata koo na familia za mababu zao
Ainsi tous ces dénombrés, que Moïse et Aaron et les principaux d'Israël dénombrèrent d'entre les Lévites, selon leurs familles, et selon les maisons de leurs pères;
47 kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. walimhesabu kila aliyepaswa kufanya kazi kwenye masikani, na kila aliyepaswa kubeba na kulinda vitu vya kwenye hema ya kukutania.
Depuis l'âge de trente ans, et au dessus, jusqu'à l'âge de cinquante ans, tous ceux qui entraient en service pour s'employer en ce à quoi il fallait servir, et à ce qu'il fallait porter du Tabernacle d'assignation.
48 Waliwahesabu wanaume 8, 580.
Tous ceux, [dis-je], qui en furent dénombrés, étaient huit mille cinq cent quatre-vingts.
49 Kwa agizo la BWANA, Musa alimhesabu kila mwanamume na kutunza kumbukumbu ya kazi ambayo kila mmoja anaweza kufanya. Kwa hivyo, walitii kile ambacho BWANA alikuwa amewaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
On les dénombra selon le commandement que l'Eternel en avait fait par le moyen de Moïse, chacun selon ce en quoi il avait à servir, et ce qu'il avait à porter, et la charge de chacun fut telle que l'Eternel l'avait commandé à Moïse.

< Hesabu 4 >