< Hesabu 4 >

1 BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
L’Éternel parla à Moïse et à Aaron, et dit:
2 Fanya sensa ya uzao waume wa Kohathi kutoka kwa Walawi, kwa kufuata jamaa na na familia za koo.
Compte les fils de Kehath parmi les enfants de Lévi, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères,
3 Uwahesabu wanaume ambao wana umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Hawa wataungana na kundi linalotumika kutoa huduma kwenye hema ya kukutania.
depuis l’âge de trente ans et au-dessus jusqu’à l’âge de cinquante ans, tous ceux qui sont propres à exercer quelque fonction dans la tente d’assignation.
4 Uzao wa Kohathi watalinda vile vitu vitakatifu zaidi vilivyohifadhiwa kwa ajili yangu katika hema ya kukutania.
Voici les fonctions des fils de Kehath, dans la tente d’assignation: elles concernent le lieu très saint.
5 Wakati kambi inapojiandaa kusonga mbele, Haruni na wanawe lazima waende hemani, kulishusha pazia linalotenganisha mahali patakatifu na kulifunika sanduku la ushuhuda kwa pazia hilo. Watalifunika hilo sanduku kwa ngozi za pomboo.
Au départ du camp, Aaron et ses fils viendront démonter le voile, et ils en couvriront l’arche du témoignage;
6 Watatandika juu yake nguo za rangi ya samawi. Watachomeka hiyo miti ya kubebea.
ils mettront dessus une couverture de peaux de dauphins, et ils étendront par-dessus un drap entièrement d’étoffe bleue; puis ils placeront les barres de l’arche.
7 Watatandika nguo ya rangi ya samawi kwenye meza ya mikate ya wonyesho. Juu yake wataweka sahani, vijiko, mabakuli na vikombe vya kumiminia. Mikate itakuwepo daima mezani.
Ils étendront un drap bleu sur la table des pains de proposition, et ils mettront dessus les plats, les coupes, les tasses et les calices pour les libations; le pain y sera toujours;
8 Wataifunika na nguo ya rangi nyekundu na ngozi za pomboo. na kuweka miti ya kubebea.
ils étendront sur ces choses un drap de cramoisi, et ils l’envelopperont d’une couverture de peaux de dauphins; puis ils placeront les barres de la table.
9 Watachukua nguo ya rangi ya samawi na kukifunika kinara, pamoja na taa zake, na koleo zake, na sahani zake na vikombe vyake vya kuwekea mafuta ya taa.
Ils prendront un drap bleu, et ils couvriront le chandelier, ses lampes, ses mouchettes, ses vases à cendre et tous ses vases à huile, destinés à son service;
10 Wataweka kinara na vifaa vyake vikiwa vimefunikwa na ngozi ya pomboo, na wataweka kwenye miti ya kukibebea.
ils le mettront, avec tous ses ustensiles, dans une couverture de peaux de dauphins; puis ils le placeront sur le brancard.
11 Watafunika na nguo ya samawi katika madhabau ya dhahabu. Wataifunika na ngozi za pomboo, na kuweka ile miti ya kubebea.
Ils étendront un drap bleu sur l’autel d’or, et ils l’envelopperont d’une couverture de peaux de dauphins; puis ils placeront les barres de l’autel.
12 Watavichukua vyombo vyote vya kazi takatifu na kuvizonga kwenye hiyo nguo ya rangi ya samawi. Watavifunika na ngozi za pomboo na kuviweka hivyo vyombo kwenye miti ya kubebea.
Ils prendront tous les ustensiles dont on se sert pour le service dans le sanctuaire, et ils les mettront dans un drap bleu, et ils les envelopperont d’une couverture de peaux de dauphins; puis ils les placeront sur le brancard.
13 Watayaondoa majivu kwenye madhabahu na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake.
Ils ôteront les cendres de l’autel, et ils étendront sur l’autel un drap de pourpre;
14 Watavieka kwenye miti ya kubebea vyombo vyote wanavyovitumia kwa kazi ya madhabahuni. Vyombo hivi ni vyetezo, majembe, mabakuli na vitu vingine vya madhabahuni. Wataifuniks madhabahu na ngozi za pomboo na kuweka ile miti ya kubebea.
ils mettront dessus tous les ustensiles destinés à son service, les brasiers, les fourchettes, les pelles, les bassins, tous les ustensiles de l’autel, et ils étendront par-dessus une couverture de peaux de dauphins; puis ils placeront les barres de l’autel.
15 Wakati Haruni na wanawe walipokuwa wamekamilisha kupafunika mahali patakatifu na vyombo vyote, na kambi itakapoanza kuendelea mbele, ndipo wana wa Kohathi watakapokuja kubeba vitu vya mahali patakatifu. Kama watagusa vyombo vitakatifu, lazima watakufa. Hii ni kazi ya wana wa uzao wa Kohathi, kubeba mapambo ya hema ya kukutania.
Après qu’Aaron et ses fils auront achevé de couvrir le sanctuaire et tous les ustensiles du sanctuaire, les fils de Kehath viendront, au départ du camp, pour les porter; mais ils ne toucheront point les choses saintes, de peur qu’ils ne meurent. Telles sont les fonctions de porteurs, imposées aux fils de Kehath dans la tente d’assignation.
16 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atalinda na kusimamia mafuta ya taa, ubani mzuri, sadaka za mara kwa mara na mafuta ya upako. Atasimamia ulinzi wa hema lote na vyote vilivyomo, mahali patakatifu na vyombo vyake.”
Éléazar, fils du sacrificateur Aaron, aura sous sa surveillance l’huile du chandelier, le parfum odoriférant, l’offrande perpétuelle et l’huile d’onction; il aura sous sa surveillance tout le tabernacle et tout ce qu’il contient, le sanctuaire et ses ustensiles.
17 BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
L’Éternel parla à Moïse et à Aaron, et dit:
18 Usiruhusu kabila la Wakohathi kuondolewa kati ya Walawi.
N’exposez point la race des familles des Kehathites à être retranchée du milieu des Lévites.
19 Walinde waishi ili wasije wakafa, kwa kufanya hivi. Wanapokuwa wanasogelea
Faites ceci pour eux, afin qu’ils vivent et qu’ils ne meurent point, quand ils s’approcheront du lieu très saint: Aaron et ses fils viendront, et ils placeront chacun d’eux à son service et à sa charge.
20 wasije wakaingia ndani ili kuona eneo takatifu hata kwa kitambo, vinginevyo watakufa. Bali Haruni na wanawe wanaweza kuingia, ndipo Haruni na Wanawe watakapowapangia Wakohathi kazi maalumu ya kufanya, kwa kila mmoj.”
Ils n’entreront point pour voir envelopper les choses saintes, de peur qu’ils ne meurent.
21 BWANA akanena na Musa tena, Akasema, “Fanya sensa kwa wana Gerishoni pia, kwa kufuata familia za mababu zao, koo zao.
L’Éternel parla à Moïse, et dit:
22 Uwahesabu wale wenye umri wa mika thelathini hadi miaka hamsini.
Compte aussi les fils de Guerschon, selon les maisons de leurs pères, selon leurs familles;
23 Uwahesabu wote ili waje kuungana na wale wanaotumika katika hema ya kukutania.
tu feras le dénombrement, depuis l’âge de trente ans et au-dessus jusqu’à l’âge de cinquante ans, de tous ceux qui sont propres à exercer quelque fonction dans la tente d’assignation.
24 Hii ndiyo itakuwa kazi ya koo za Gerishoni, wanapotumikia na wanachobeba.
Voici les fonctions des familles des Guerschonites, le service qu’ils devront faire et ce qu’ils devront porter.
25 Watabeba pazia la masikani, hema la kukutania, na vifunikio vyake, vifuniko vya ngozi ya pomboo ambvyo viko juu yake, na pazia kwenye lango la hema ya kukutania.
Ils porteront les tapis du tabernacle et la tente d’assignation, sa couverture et la couverture de peaux de dauphins qui se met par-dessus, le rideau qui est à l’entrée de la tente d’assignation;
26 Watabeba pazia la ua, pazia la kwenye mlango wa ua, ambao uko karibu na maskani karibu na madhabahu, kamba zake na vifaa vyote vya utumishi wake. Chochote kinachotakiwa kufanywa kutokana na vitu hivi, wao ndio watakaofanya.
les toiles du parvis et le rideau de l’entrée de la porte du parvis, tout autour du tabernacle et de l’autel, leurs cordages et tous les ustensiles qui en dépendent. Et ils feront tout le service qui s’y rapporte.
27 Haruni na wanawe ndio watakaongoza utumishi wa uzao wa Wagerishoni, kwa vitu vyote vile vya kusafirisha, na katika utumishi wao wote. Lazima uwagawie majukumu yao yote.
Dans leurs fonctions, les fils des Guerschonites seront sous les ordres d’Aaron et de ses fils, pour tout ce qu’ils porteront et pour tout le service qu’ils devront faire; vous remettrez à leurs soins tout ce qu’ils ont à porter.
28 Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa wana wa Wagerishoni katka hema ya kukutania. Ithamari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza katika utumishi.
Telles sont les fonctions des familles des fils des Guerschonites dans la tente d’assignation, et ce qu’ils ont à garder sous la direction d’Ithamar, fils du sacrificateur Aaron.
29 Utawahesabu uzao wa Merari kwa koo zao, na uwapange katika familia za mabau zao,
Tu feras le dénombrement des fils de Merari, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères;
30 kuanzia wenye umri wa miaka thelatini hadi miaka hamsini. Umuhesabu kila atakayeungana na kundi lenye utumishi katika hema ya kukutania.
tu feras le dénombrement, depuis l’âge de trente ans et au-dessus jusqu’à l’âge de cinquante ans, de tous ceux qui sont propres à exercer quelque fonction dans la tente d’assignation.
31 Huu ndio wajibu na kazi yao katika utumishi wao kwenye hema ya kukutania. Watazilinda mbao za maskani, mataluma yake, nguzo na makalishio yake,
Voici ce qui est remis à leurs soins et ce qu’ils ont à porter, pour toutes leurs fonctions dans la tente d’assignation: les planches du tabernacle, ses barres, ses colonnes, ses bases,
32 pamoja na nguzo za ua zinazozunguka masikani, makalishio yake, vigingi na kamba zake, na vifaa vinginevya ujenzi. Waorodheshe kwa majina na majukumu yao.
les colonnes du parvis formant l’enceinte, leurs bases, leurs pieux, leurs cordages, tous les ustensiles qui en dépendent et tout ce qui est destiné à leur service. Vous désignerez par leurs noms les objets qui sont remis à leurs soins et qu’ils ont à porter.
33 Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa Merari, ambao wanatakiwa kufanya katika hema ya kukutania, chini ya uongozi wa Ithmari mwana wa Haruni kuhani.”
Telles sont les fonctions des familles des fils de Merari, toutes leurs fonctions dans la tente d’assignation, sous la direction d’Ithamar, fils du sacrificateur Aaron.
34 Musa na Haruni na viongozi wa watu waliwahesabu wana wa uzao wa Wakohathi kwa kufuata koo za familia za mababu zao.
Moïse, Aaron et les princes de l’assemblée firent le dénombrement des fils des Kehathites, selon leurs familles et selon les maisons de leurs pères,
35 Waliwahesabu wale wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Walimhesabu kila mmoja aliyepaswa kuungana na kundi linalotoa huduma ya utumishi kwenye hema ya kukutania.
de tous ceux qui, depuis l’âge de trente ans et au-dessus jusqu’à l’âge de cinquante ans, étaient propres à exercer quelque fonction dans la tente d’assignation.
36 Waliwahesabu wanaume 2, 750 kwa kufuata koo zao.
Ceux dont ils firent le dénombrement, selon leurs familles, furent deux mille sept cent cinquante.
37 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote kutoka koo na familia za Wakohathi ambao hutumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi kwa kumtii BWANA aliyewaagiza kupitia kwa Musa.
Tels sont ceux des familles des Kehathites dont on fit le dénombrement, tous ceux qui exerçaient des fonctions dans la tente d’assignation; Moïse et Aaron en firent le dénombrement sur l’ordre de l’Éternel par Moïse.
38 Uzao wa Gerishoni walihesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao,
Les fils de Guerschon dont on fit le dénombrement, selon leurs familles et selon les maisons de leurs pères,
39 kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kwa kila mmoja aliyetakiwa kuungana na watu wanaotoa huduma kwenye hema ya kukutania.
depuis l’âge de trente ans et au-dessus jusqu’à l’âge de cinquante ans, tous ceux qui étaient propres à exercer quelque fonction dans la tente d’assignation,
40 Wanaume wote waliohesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao walikuwa 2, 630.
ceux dont on fit le dénombrement, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères, furent deux mille six cent trente.
41 Musa na Haruni walizihesabu koo za uzao wa Gerishoni ambao watatumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi ili kutii ambacho BWANA aliwaamuru kufanya kuptia kwa Musa.
Tels sont ceux des familles des fils de Guerschon dont on fit le dénombrement, tous ceux qui exerçaient des fonctions dans la tente d’assignation; Moïse et Aaron en firent le dénombrement sur l’ordre de l’Éternel.
42 Uzao wa Merari walihesabiwa kwa koo kupitia familia za mababu zao,
Ceux des familles des fils de Merari dont on fit le dénombrement, selon leurs familles, selon les maisons de leurs pères,
43 kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kila anayepaswa kuungana na watu wanaotumika kwenye hema ya kukutania.
depuis l’âge de trente ans et au-dessus jusqu’à l’âge de cinquante ans, tous ceux qui étaient propres à exercer quelque fonction dans la tente d’assignation,
44 Wanaume wote waliohesabiwa kupitia koo za familia za mababu zao walikuwa 3. 200.
ceux dont on fit le dénombrement, selon leurs familles, furent trois mille deux cents.
45 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume hawa, uzao wa Merari. Kw kufanya hivi walitii amri ya BWANA aliyowaaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
Tels sont ceux des familles des fils de Merari dont on fit le dénombrement; Moïse et Aaron en firent le dénombrement sur l’ordre de l’Éternel par Moïse.
46 Kwa hiyo Musa na Haruni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kw kufuata koo na familia za mababu zao
Tous ceux des Lévites dont Moïse, Aaron et les princes d’Israël firent le dénombrement, selon leurs familles et selon les maisons de leurs pères,
47 kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. walimhesabu kila aliyepaswa kufanya kazi kwenye masikani, na kila aliyepaswa kubeba na kulinda vitu vya kwenye hema ya kukutania.
depuis l’âge de trente ans et au-dessus jusqu’à l’âge de cinquante ans, tous ceux qui étaient propres à exercer quelque fonction et à servir de porteurs dans la tente d’assignation,
48 Waliwahesabu wanaume 8, 580.
tous ceux dont on fit le dénombrement furent huit mille cinq cent quatre-vingts.
49 Kwa agizo la BWANA, Musa alimhesabu kila mwanamume na kutunza kumbukumbu ya kazi ambayo kila mmoja anaweza kufanya. Kwa hivyo, walitii kile ambacho BWANA alikuwa amewaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
On en fit le dénombrement sur l’ordre de l’Éternel par Moïse, en indiquant à chacun le service qu’il devait faire et ce qu’il devait porter; on en fit le dénombrement selon l’ordre que l’Éternel avait donné à Moïse.

< Hesabu 4 >