< Hesabu 4 >

1 BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
And the Lord spoke to Moses and Aaron, saying:
2 Fanya sensa ya uzao waume wa Kohathi kutoka kwa Walawi, kwa kufuata jamaa na na familia za koo.
“Take a total of the sons of Kohath from the midst of the Levites, by their houses and families,
3 Uwahesabu wanaume ambao wana umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Hawa wataungana na kundi linalotumika kutoa huduma kwenye hema ya kukutania.
from thirty years and above, even to the fiftieth year, of all who enter so as to stand and minister in the tabernacle of the covenant.
4 Uzao wa Kohathi watalinda vile vitu vitakatifu zaidi vilivyohifadhiwa kwa ajili yangu katika hema ya kukutania.
This is the service of the sons of Kohath: the tabernacle of the covenant and the Holy of holies.
5 Wakati kambi inapojiandaa kusonga mbele, Haruni na wanawe lazima waende hemani, kulishusha pazia linalotenganisha mahali patakatifu na kulifunika sanduku la ushuhuda kwa pazia hilo. Watalifunika hilo sanduku kwa ngozi za pomboo.
Aaron and his sons shall enter, when the camp is going to move, and they shall take down the veil, which hangs before the entrance, and they shall wrap the ark of the testimony in it,
6 Watatandika juu yake nguo za rangi ya samawi. Watachomeka hiyo miti ya kubebea.
and they shall cover it further with a veil of violet skins, and they shall extend over it a cloth made entirely of hyacinth, and they shall draw in the bars.
7 Watatandika nguo ya rangi ya samawi kwenye meza ya mikate ya wonyesho. Juu yake wataweka sahani, vijiko, mabakuli na vikombe vya kumiminia. Mikate itakuwepo daima mezani.
Likewise, they shall wrap the table of the presence in a cloth of hyacinth, and they shall place with it the censers and little mortars, the cups and bowls for pouring out libations; the bread shall be always on it.
8 Wataifunika na nguo ya rangi nyekundu na ngozi za pomboo. na kuweka miti ya kubebea.
And they shall extend over it a cloth of scarlet, which they shall further cover with a veil of violet skins, and they shall draw in the bars.
9 Watachukua nguo ya rangi ya samawi na kukifunika kinara, pamoja na taa zake, na koleo zake, na sahani zake na vikombe vyake vya kuwekea mafuta ya taa.
They shall take also a cloth of hyacinth, with which they shall cover the lampstand with the lamps, and its tongs, and the candle snuffers, and all the vessels of oil, which are necessary for the preparation of the lamps.
10 Wataweka kinara na vifaa vyake vikiwa vimefunikwa na ngozi ya pomboo, na wataweka kwenye miti ya kukibebea.
And over all this they shall place a covering of violet skins, and they shall draw in the bars.
11 Watafunika na nguo ya samawi katika madhabau ya dhahabu. Wataifunika na ngozi za pomboo, na kuweka ile miti ya kubebea.
And certainly they shall wrap the golden altar in a hyacinth garment, and they shall extend over it a covering of violet skins, and they shall draw in the bars.
12 Watavichukua vyombo vyote vya kazi takatifu na kuvizonga kwenye hiyo nguo ya rangi ya samawi. Watavifunika na ngozi za pomboo na kuviweka hivyo vyombo kwenye miti ya kubebea.
All the vessels with which they minister in the Sanctuary they shall wrap in a cloth of hyacinth, and they shall extend over it a covering of violet skins, and they shall draw in the bars.
13 Watayaondoa majivu kwenye madhabahu na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake.
Moreover, they shall cleanse the altar of ashes, and they shall wrap it in a purple garment,
14 Watavieka kwenye miti ya kubebea vyombo vyote wanavyovitumia kwa kazi ya madhabahuni. Vyombo hivi ni vyetezo, majembe, mabakuli na vitu vingine vya madhabahuni. Wataifuniks madhabahu na ngozi za pomboo na kuweka ile miti ya kubebea.
and they shall place it with all the vessels which they use in its ministry, that is, receptacles for fire, small hooks as well as forks, larger hooks and shovels. They shall cover all the vessels of the altar together with a veil of violet skins, and they shall draw in the bars.
15 Wakati Haruni na wanawe walipokuwa wamekamilisha kupafunika mahali patakatifu na vyombo vyote, na kambi itakapoanza kuendelea mbele, ndipo wana wa Kohathi watakapokuja kubeba vitu vya mahali patakatifu. Kama watagusa vyombo vitakatifu, lazima watakufa. Hii ni kazi ya wana wa uzao wa Kohathi, kubeba mapambo ya hema ya kukutania.
And when Aaron and his sons have wrapped the Sanctuary and its vessels at the dismantling of the camp, then the sons of Kohath shall enter, so as to carry what has been wrapped. And they shall not touch the vessels of the Sanctuary, lest they die. These are the burdens of the sons of Kohath concerning the tabernacle of the covenant.
16 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atalinda na kusimamia mafuta ya taa, ubani mzuri, sadaka za mara kwa mara na mafuta ya upako. Atasimamia ulinzi wa hema lote na vyote vilivyomo, mahali patakatifu na vyombo vyake.”
Over them shall be Eleazar, the son of Aaron the priest, to whom belongs the care of the oil to prepare the lamps, and the incense compound, and the sacrifice, which is offered continually, and the oil of unction, and whatever pertains to the service of the tabernacle, and all the vessels that are in the Sanctuary.”
17 BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
And the Lord spoke to Moses and Aaron, saying:
18 Usiruhusu kabila la Wakohathi kuondolewa kati ya Walawi.
“Do not be willing to lose the people of Kohath from the midst of the Levites.
19 Walinde waishi ili wasije wakafa, kwa kufanya hivi. Wanapokuwa wanasogelea
But do this for them, so that they may live, and so that they may not die by touching the Holies of holies. Aaron and his sons shall enter, and they shall assign the work of each one, and they shall determine what each one ought to carry.
20 wasije wakaingia ndani ili kuona eneo takatifu hata kwa kitambo, vinginevyo watakufa. Bali Haruni na wanawe wanaweza kuingia, ndipo Haruni na Wanawe watakapowapangia Wakohathi kazi maalumu ya kufanya, kwa kila mmoj.”
Let no others, out of curiosity, see the things that are in the Sanctuary before they are wrapped, otherwise they shall die.”
21 BWANA akanena na Musa tena, Akasema, “Fanya sensa kwa wana Gerishoni pia, kwa kufuata familia za mababu zao, koo zao.
And the Lord spoke to Moses, saying:
22 Uwahesabu wale wenye umri wa mika thelathini hadi miaka hamsini.
“Now also take a total of the sons of Gershon, by their houses and families and kinships,
23 Uwahesabu wote ili waje kuungana na wale wanaotumika katika hema ya kukutania.
from thirty years and above, even to fifty years. Number all those who enter and minister in the tabernacle of the covenant.
24 Hii ndiyo itakuwa kazi ya koo za Gerishoni, wanapotumikia na wanachobeba.
This is the duty of the family of the Gershonites:
25 Watabeba pazia la masikani, hema la kukutania, na vifunikio vyake, vifuniko vya ngozi ya pomboo ambvyo viko juu yake, na pazia kwenye lango la hema ya kukutania.
to carry the curtains of the tabernacle, and the roof of the covenant, the other covering, and the veil over everything, and the violet tent, which hangs at the entrance of the tabernacle of the covenant,
26 Watabeba pazia la ua, pazia la kwenye mlango wa ua, ambao uko karibu na maskani karibu na madhabahu, kamba zake na vifaa vyote vya utumishi wake. Chochote kinachotakiwa kufanywa kutokana na vitu hivi, wao ndio watakaofanya.
the curtains of the atrium, and the veil at the entrance, which is before tabernacle. Everything that pertains to the altar, the cords, and the vessels of the ministry
27 Haruni na wanawe ndio watakaongoza utumishi wa uzao wa Wagerishoni, kwa vitu vyote vile vya kusafirisha, na katika utumishi wao wote. Lazima uwagawie majukumu yao yote.
the sons of Gershon shall carry, under the orders of Aaron and his sons. And so shall each one know to which burden he ought to surrender.
28 Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa wana wa Wagerishoni katka hema ya kukutania. Ithamari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza katika utumishi.
This is the service of the family of the Gershonites, in the tabernacle of the covenant, and they shall be under the hand of Ithamar, the son of Aaron the priest.
29 Utawahesabu uzao wa Merari kwa koo zao, na uwapange katika familia za mabau zao,
Likewise, you shall take a census of the sons of Merari, by the families and houses of their fathers,
30 kuanzia wenye umri wa miaka thelatini hadi miaka hamsini. Umuhesabu kila atakayeungana na kundi lenye utumishi katika hema ya kukutania.
from thirty years and above, even to fifty years, of all who enter to the office of their ministry and to the service of the covenant of the testimony.
31 Huu ndio wajibu na kazi yao katika utumishi wao kwenye hema ya kukutania. Watazilinda mbao za maskani, mataluma yake, nguzo na makalishio yake,
These are their burdens: They shall carry the panels of the tabernacle and its bars, the columns and their bases,
32 pamoja na nguzo za ua zinazozunguka masikani, makalishio yake, vigingi na kamba zake, na vifaa vinginevya ujenzi. Waorodheshe kwa majina na majukumu yao.
also the columns surrounding the atrium, with their bases and tent pegs and cords. They shall accept by number all the vessels and articles, and so shall they carry them.
33 Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa Merari, ambao wanatakiwa kufanya katika hema ya kukutania, chini ya uongozi wa Ithmari mwana wa Haruni kuhani.”
This is the office of the family of the Merarites, and their ministry for the tabernacle of the covenant. And they shall be under the hand of Ithamar, the son of Aaron the priest.”
34 Musa na Haruni na viongozi wa watu waliwahesabu wana wa uzao wa Wakohathi kwa kufuata koo za familia za mababu zao.
Therefore, Moses and Aaron, and the leaders of the assembly, took a census of the sons of Kohath, by the kinships and houses of their fathers,
35 Waliwahesabu wale wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Walimhesabu kila mmoja aliyepaswa kuungana na kundi linalotoa huduma ya utumishi kwenye hema ya kukutania.
from thirty years and above, even to the fiftieth year, of all who enter to the ministry of the tabernacle of the covenant.
36 Waliwahesabu wanaume 2, 750 kwa kufuata koo zao.
And there were found two thousand seven hundred fifty.
37 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote kutoka koo na familia za Wakohathi ambao hutumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi kwa kumtii BWANA aliyewaagiza kupitia kwa Musa.
This is the number of the people of Kohath, who enter the tabernacle of the covenant. These Moses and Aaron numbered according to the word of the Lord by the hand of Moses.
38 Uzao wa Gerishoni walihesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao,
The sons of Gershon also were numbered by the kinships and houses of their fathers,
39 kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kwa kila mmoja aliyetakiwa kuungana na watu wanaotoa huduma kwenye hema ya kukutania.
from thirty years and above, even to the fiftieth year, all who enter so as to minister in the tabernacle of the covenant.
40 Wanaume wote waliohesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao walikuwa 2, 630.
And there were found two thousand six hundred thirty.
41 Musa na Haruni walizihesabu koo za uzao wa Gerishoni ambao watatumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi ili kutii ambacho BWANA aliwaamuru kufanya kuptia kwa Musa.
This is the people of the Gershonites, whom Moses and Aaron numbered according to the word of the Lord.
42 Uzao wa Merari walihesabiwa kwa koo kupitia familia za mababu zao,
The sons of Merari also were numbered by the kinships and houses of their fathers,
43 kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kila anayepaswa kuungana na watu wanaotumika kwenye hema ya kukutania.
from thirty years and above, even to the fiftieth year, all who enter to fulfill the rituals of the tabernacle of the covenant.
44 Wanaume wote waliohesabiwa kupitia koo za familia za mababu zao walikuwa 3. 200.
And there were found three thousand two hundred.
45 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume hawa, uzao wa Merari. Kw kufanya hivi walitii amri ya BWANA aliyowaaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
This is the number of the sons of Merari, whom Moses and Aaron counted according to the command of the Lord by the hand of Moses.
46 Kwa hiyo Musa na Haruni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kw kufuata koo na familia za mababu zao
All who were counted from the Levites, and whom, by name, Moses and Aaron, and the leaders of Israel, counted by the kinships and houses of their fathers,
47 kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. walimhesabu kila aliyepaswa kufanya kazi kwenye masikani, na kila aliyepaswa kubeba na kulinda vitu vya kwenye hema ya kukutania.
from thirty years and above, until the fiftieth year, entering for the ministry of the tabernacle and carrying the burdens,
48 Waliwahesabu wanaume 8, 580.
were together eight thousand five hundred eighty.
49 Kwa agizo la BWANA, Musa alimhesabu kila mwanamume na kutunza kumbukumbu ya kazi ambayo kila mmoja anaweza kufanya. Kwa hivyo, walitii kile ambacho BWANA alikuwa amewaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
Moses took a census of them, according to the word of the Lord, each one according to their office and their burdens, just as the Lord had instructed him.

< Hesabu 4 >