< Hesabu 36 >

1 Kisha wale viongozi wa nyumba za mababa wa ukoo wa Gileadi mwana wa Machiri (ambaye alikuwa mwana wa Manase), ambao walikuwa wa ukoo wa uzao wa Yusufu, walikuja wakasema mbele za Musa na mbele za vionigozi wa familia za mababa wa watu wa Israeli.
And the heads of the fathers of the family of the sons of Gilead, the son of Machir, the son of Manasseh, of the families of the sons of Joseph, came near, and spoke before Moses, and before the rulers, the heads of the fathers of the sons of Israel.
2 Wakasema, “BWANA alikuamuru, wewe bwana wetu, kutupa mgawo wa ardhi kwa kura kwa wana wa Israeli. Uliamuriwa na BWANA kutoa mgawo wa Zerofehadi kaka yetu kwa binti zake.
And they said, Jehovah commanded my lord to give the land for inheritance by lot to the sons of Israel. And my lord was commanded by Jehovah to give the inheritance of Zelophehad our brother to his daughters.
3 Lakini hawa binti wameolewa na wanaume toka kabila zingine za wana wa Israeli, basi mgawo wao wa ardhi utaondolewa kutoka kwenye mgawo wa mababa zao. Utaongezwa kwenye mgawo wa makabila ambayo wao wanaungana nao. Kwa sababu hiyo, Utaondolewa kwenye mgawo uliopangwa kwenye urithi wetu.
And if they be married to any of the sons of the other tribes of the sons of Israel, then their inheritance will be taken away from the inheritance of our fathers, and will be added to the inheritance of the tribe to which they shall belong. So it will be taken away from the lot of our inheritance.
4 Kwa sababu hiyo, wakati wa mwaka wa yubilee ya wana wa Israeli utakapofika, mgawo wao utaunganishwa na kabila ile waliyoungana nao. Kwa sababu hii mgawo wao utaondolewa kwenye mgawo wa mababa zetu.”
And when the jubilee of the sons of Israel shall be, then their inheritance will be added to the inheritance of the tribe to which they shall belong. So their inheritance will be taken away from the inheritance of the tribe of our fathers.
5 Basi Musa akawapa amri wana wa Israeli, kwa neno la BWANA. Akasema, “Kile wanachosema watu wa kabila la Yusufu kiko sahihi.
And Moses commanded the sons of Israel according to the word of Jehovah, saying, The tribe of the sons of Joseph speak right.
6 Hiki ndicho BWANA anaagiza kuhusu mabinti wa Zelofehadi. Anasema, 'Acha waolewa na wale ambao wao wanaofikri ni vizuri zaidi, lakini lazima waolewe ndani ya kabila ya baba yao.'
This is the thing which Jehovah commands concerning the daughters of Zelophehad, saying, Let them be married to whom they think best, only into the family of the tribe of their father shall they be married.
7 Hakuna mgawo wa watu utakaobadilika kutoka kabila moja kwenda jingine. Kila mtu wa Israeli ataendelea na mgawo wa kabila ya baba y ake.
So no inheritance of the sons of Israel shall remove from tribe to tribe, for the sons of Israel shall cling each one to the inheritance of the tribe of his fathers.
8 Kila mwanamke wa watu wa Israeli aliye na mgao kwenye kabila lake lazima aolewe na mtu wa ukoo unaotoka kwenye kabila la baba yake. Hii itafanyika hivyo ili kila mtu wa wana wa Israeli aweze kuwa na urithi kutoka kwa mababa zake.
And every daughter, who possesses an inheritance in any tribe of the sons of Israel, shall be wife to one of the family of the tribe of her father, that the sons of Israel may possess every man the inheritance of his fathers.
9 Hakuna mgawo utakaobadilika kutoka kabila nyingine kwenda kabila nyingine. Kila mtu wa kabila za watu wa Israeli atalinda urithi wake.”
So no inheritance shall move from one tribe to another tribe, for the tribes of the sons of Israel shall cling each one to his own inheritance.
10 Kwa hiyo wale binti wa Zelofehadi walifanya kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa. Mahila, Tiriza, Hogila, Milika, na Noha, binti za
Even as Jehovah commanded Moses, so did the daughters of Zelophehad,
11 Zelofehadi, waliolewa na wana wa uzao wa Manase.
for Mahlah, Tirzah, and Hoglah, and Milcah, and Noah, the daughters of Zelophedad, were married to their father's brothers' sons.
12 Waliolewa katika koo za uzao wa Manase mwana wa Yusufu. Kwa sababu hii, urithi wao ulibaki kwenye kabila la ukoo ambalo baba yao alikuwa anatoka.
They were married into the families of the sons of Manasseh the son of Joseph, and their inheritance remained in the tribe of the family of their father.
13 Hizi ndizo amri na maagizo ambayo BWANAaliyatoa kupitia Musa kwa wana wa Israeli katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
These are the commandments and the ordinances which Jehovah commanded by Moses to the sons of Israel in the plains of Moab by the Jordan at Jericho.

< Hesabu 36 >