< Hesabu 34 >

1 BWANA akanena na Musa akasema,
Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
2 “Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
Ordonne aux enfants d’Israël, et tu leur diras: Lorsque vous serez entrés dans la terre de Chanaan, et qu’elle vous sera échue en possession par le sort, c’est par ces frontières qu’elle sera bornée:
3 Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
La partie méridionale commencera au désert de Sin, qui est près d’Edom; et elle aura pour frontière vers l’orient la mer très salée;
4 Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
Ces frontières environneront la partie australe par la montée du Scorpion, en sorte qu’elles passent à Senna, et qu’elles viennent depuis le midi jusqu’à Cadesbarné, d’où elles iront par les lieux limitrophes jusqu’au village du nom d’Adar, et s’étendront jusqu’à Asémona;
5 Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
Puis la limite ira en tournant d’Asémona jusqu’au torrent d’Egypte, et elle finira au rivage de la grande mer.
6 Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
Mais la partie occidentale commencera à la grande mer, et sera fermée par cette limite même.
7 Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
Or, vers la partie septentrionale, les limites commenceront à la grande mer, parvenant jusqu’à la très haute montagne,
8 kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
De laquelle elles viendront à Emath jusqu’aux confins de Sédada;
9 Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
Puis, elles iront par les lieux limitrophes jusqu’à Zéphrona, et au village d’Enan. Telles seront les limites dans la partie de l’aquilon.
10 Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
De là les frontières se mesureront contre la partie orientale, depuis le village d’Enan jusqu’à Séphama;
11 Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
Et de Séphama, les limites descendront à Rébla, contre la fontaine de Daphnim: de là elles parviendront contre l’orient à la mer de Cénéreth,
12 Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
S’étendront jusqu’au Jourdain, et enfin seront fermées par la mer très salée. C’est cette terre que vous aurez selon ses frontières dans son contour.
13 Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
Moïse ordonna donc aux enfants d’Israël, disant: Ce sera la terre que vous posséderez par le sort, et que le Seigneur a commandé qu’on donnât aux neuf tribus et à la demi-tribu.
14 Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
Car la tribu des enfants de Ruben, selon ses familles, et la tribu des enfants de Gad, selon le nombre de sa parenté, et aussi la demi-tribu de Manassé,
15 Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
C’est-à-dire deux tribus et demie, ont reçu leur part au-delà du Jourdain, contre Jéricho, à la partie orientale.
16 BWANA akanena na Musa akasema,
Le Seigneur dit aussi à Moïse:
17 “Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
Voici les noms des hommes qui vous partageront la terre: Eléazar, le prêtre, et Josué, fils de Nun,
18 Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
Et chaque prince de chaque tribu,
19 Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
Dont voici les noms: De la tribu de Juda, Caleb, fils de Jéphoné;
20 Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
De la tribu de Siméon, Samuel, fils d’Ammiud;
21 Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
De la tribu de Benjamin, Elidad, fils de Chasélon;
22 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
De la tribu des enfants de Dan, Bocci, fils de Jogli;
23 Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
Des enfants de Joseph: de la tribu de Manassé, Hanniel, fils d’Ephod;
24 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
De la tribu d’Ephraïm, Camuel, fils de Sephtan;
25 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
De la tribu de Zabulon, Elisaphan, fils de Pharnach;
26 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
De la tribu d’Issachar, le chef Phaltiel, fils d’Ozan;
27 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
De la tribu d’Aser, Ahiud, fils de Salomi:
28 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
De la tribu de Nephthali, Phédaël, fils d’Ammiud.
29 BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.
Tels sont ceux auxquels le Seigneur ordonna de partager aux enfants d’Israël la terre de Chanaan.

< Hesabu 34 >