< Hesabu 34 >
1 BWANA akanena na Musa akasema,
L’Éternel parla à Moïse en ces termes:
2 “Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
"Donne aux enfants d’Israël les instructions suivantes: Comme vous allez entrer dans ce pays de Canaan, voici quel territoire vous tombera en partage: le pays de Canaan selon ses limites.
3 Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
Vous aurez pour côté méridional le désert de Cîn, sur la lisière d’Edom; cette limite du midi commencera pour vous à la pointe orientale de la mer Salée.
4 Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
Puis la limite s’infléchira, par le midi, vers la montée d’Akrabbîm, atteindra Cîn et aboutira au midi de Kadêch-Barnéa; sortira vers Haçar-Addar, ira jusqu’à Açmôn;
5 Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
d’Açmôn, la ligne déviera vers le torrent d’Egypte, et se terminera à la mer.
6 Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
Pour la frontière occidentale, c’est la grande mer qui vous en tiendra lieu: telle sera pour vous la frontière occidentale.
7 Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
Voici quelles seront vos bornes au nord: vous tracerez une ligne de la grande mer à Hor-la-Montagne;
8 kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
de Hor-la-Montagne vous la continuerez jusqu’à Hémath, d’où la démarcation aboutira à Cedad;
9 Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
puis elle atteindra Zifrôn, et aura pour terme Haçar-Enân: telles seront vos bornes au nord.
10 Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
Pour vos bornes à l’orient, vous tirerez une ligne de Haçar-Hênân à Chefâm;
11 Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
de Chefâm, cette ligne descendra jusqu’à Ribla, en passant à l’orient d’Ayîn; puis, descendant encore, elle suivra le bord oriental de la mer de Kinnéreth,
12 Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
descendra encore le long du Jourdain, et viendra aboutir à la mer Salée. Tel sera votre territoire, quant aux limites qui doivent le circonscrire."
13 Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
Moïse transmit cet ordre aux enfants d’Israël, en disant: "C’Est là le territoire que vous vous partagerez au sort, et que l’Éternel a ordonné d’attribuer aux neuf tribus et demie.
14 Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
Car, pour la tribu des descendants de Ruben selon leurs familles paternelles, la tribu des descendants de Gad selon les leurs, et la demi-tribu de Manassé, elles ont déjà reçu leur lot:
15 Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
ces deux tribus et demie ont reçu leur lot sur la rive du Jourdain faisant face à Jéricho, du côté de l’orient."
16 BWANA akanena na Musa akasema,
L’Éternel parla à Moïse en ces termes:
17 “Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
"Voici les noms des hommes qui doivent prendre, pour vous, possession du pays: Eléazar le pontife, et Josué, fils de Noun;
18 Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
plus un chef, un chef par tribu, que vous chargerez de prendre possession du pays.
19 Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
Voici les noms de ces hommes: pour la tribu de Juda: Caleb, fils de Yefounné;
20 Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
pour la tribu des enfants de Siméon: Samuel, fils d’Ammihoud;
21 Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
pour la tribu de Benjamin: Elidad, fils de Kislôn;
22 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
pour la tribu des enfants de Dan, le chef sera Bouki, fils de Yogli;
23 Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
quant aux descendants de Joseph, la tribu des enfants de Manassé aura pour chef Hanniël, fils d’Efod,
24 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
et celles des enfants d’Ephraïm, Kemouêl, fils de Chiftân.
25 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
Chef pour la tribu des enfants de Zabulon: Eliçafân, fils de Parnakh;
26 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
chef pour la tribu des enfants d’Issachar: Paltïel, fils d’Azzân;
27 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
chef pour la tribu des enfants d’Aser: Ahihoud, fils de Chelomi;
28 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
et pour la tribu des enfants de Nephtali, le chef sera Pedahel, fils d’Ammihoud."
29 BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.
Tels sont ceux à qui l’Éternel donna mission de répartir entre les enfants d’Israël, le pays de Canaan.