< Hesabu 33 >

1 Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
Voici les demeures des enfants d’Israël, qui sont sortis de l’Egypte, selon leurs bandes, par l’entremise de Moïse et d’Aaron;
2 Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
Lesquels Moïse décrivit, selon les lieux de leurs campements qu’ils changeaient par le commandement du Seigneur.
3 Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
Partis donc de Ramessès, au premier mois, au quinzième jour du premier mois, le lendemain de la Pâque, les enfants d’Israël, par une main élevée, tous les Egyptiens le voyant,
4 Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
Et ensevelissant leurs premiers-nés qu’avait frappés le Seigneur (or, même sur leurs dieux il avait exercé sa vengeance),
5 Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
Campèrent à Soccoth,
6 Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
Et de Soccoth ils vinrent à Etham, qui est aux derniers confins du désert.
7 Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
Sortis donc de là, ils vinrent contre Phihahiroth, qui regarde Béelséphon, et ils campèrent devant Magdalum.
8 Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
Et partis de Phihahiroth, ils passèrent par le milieu de la mer dans le désert; et marchant durant trois jours par le désert d’Etham, ils campèrent à Mara.
9 Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
Or, partis de Mara, ils vinrent à Elim, où étaient douze sources d’eaux, et soixante-dix palmiers; et ils y campèrent.
10 Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
Mais étant encore sortis de là, ils plantèrent leurs tentes sur la mer Rouge. Et partis de la mer Rouge,
11 Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
Ils campèrent dans le désert de Sin;
12 Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
D’où étant sortis, ils vinrent à Daphca.
13 Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
Et partis de Daphca, ils campèrent à Alus.
14 Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
Or, sortis d’Alus, ils plantèrent leurs tentes à Raphidim, où l’eau pour boire manqua au peuple.
15 Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
Et partis de Raphidim, ils campèrent dans le désert de Sinaï.
16 Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
Mais, sortis aussi du désert de Sinaï, ils vinrent aux Sépulcres de la concupiscence.
17 Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
Et partis des Sépulcres de la concupiscence, ils campèrent à Haséroth.
18 Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
Or, de Haséroth, ils vinrent à Rethma.
19 Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
Et partis de Rethma, ils campèrent à Remmompharès;
20 Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
D’où étant sortis, ils vinrent à Lebna.
21 Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
De Lebna, ils campèrent à Ressa.
22 Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
Et sortis de Cessa, ils vinrent à Céélatha;
23 Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
D’où étant partis, ils campèrent à la montagne de Sépher.
24 Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
Sortis de la montagne de Sépher, ils vinrent à Arada.
25 Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
Partant delà, ils campèrent à Macéloth.
26 Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
Et étant partis de Macéloth, ils vinrent à Thahath.
27 Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
De Thahath, ils campèrent à Tharé;
28 Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
D’où étant sortis, ils plantèrent leurs tentes à Methca.
29 Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
Et de Methca, ils campèrent à Hesmona.
30 Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
Or, partis de Hesmona, ils vinrent à Moséroth.
31 Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
Et de Moséroth, ils campèrent à Bénéjaacan.
32 Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
Mais partis de Bénéjaacan, ils vinrent à la montagne de Gadgad;
33 Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
D’où étant partis ils campèrent à Jétébatha.
34 Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
Et de Jétébatha, ils vinrent à Hébrona.
35 Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
Et, sortis d’Hébrona, ils campèrent à Asiongaber
36 Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
Partis de là, ils vinrent au désert de Sin; c’est Cadès.
37 Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
Et, sortis de Cadès, ils campèrent à la montagne de Hor, aux derniers confins de la terre d’Edom.
38 Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
Or, Aaron, le prêtre, monta sur la montagne de Hor, le Seigneur l’ordonnant, et là il mourut, en l’année quarantième de la sortie des enfants d’Israël de l’Egypte, au cinquième mois, au premier jour du mois,
39 Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
Comme il avait cent vingt-trois ans.
40 Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
Cependant le roi d’Arad, Chananéen, qui habitait vers le midi, apprit que les enfants d’Israël étaient venus dans la terre de Chanaan.
41 Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
Or, partis de la montagne de Hor, ils campèrent à Salmona;
42 Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
D’où étant sortis, ils vinrent à Phunon.
43 Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
Et partis de Phunon, ils campèrent à Oboth.
44 Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
Et d’Oboth ils vinrent à Jiéabarim, qui est aux confins des Moabites.
45 Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
Puis, partis de Jiéabarim, ils plantèrent leurs tentes à Dibongad;
46 Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
D’où étant sortis, ils campèrent à Helmondéblathaïm.
47 Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
Et sortis de Helmondéblathaïm, ils vinrent aux montagnes d’Abarim, contre Nabo.
48 Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
Or, partis des montagnes d’Abarim, ils passèrent dans les plaines de Moab, sur le Jourdain, contre Jéricho.
49 Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
Et là ils campèrent, depuis Bethsimoth jusqu’à Abelsatim, dans les lieux les plus plats des Moabites,
50 Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
Où le Seigneur dit à Moïse:
51 “Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
Ordonne aux enfants d’Israël, et dis-leur: Quand vous aurez passé le Jourdain, entrant dans la terre de Chanaan,
52 ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
Détruisez tous les habitants de cette terre; brisez les monuments, mettez en pièces les statues, et ravagez tous les hauts lieux,
53 Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
Purifiant la terre, et y habitant; car c’est moi qui vous l’ai donnée en possession;
54 Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
Vous vous la partagerez par le sort. Au plus grand nombre, vous donnerez la partie la plus étendue, et au plus petit nombre, la partie la plus resserrée. Comme le sort sera échu à chacun, ainsi sera donné l’héritage. C’est par tribus et par familles que la possession sera partagée.
55 Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
Mais si vous ne voulez pas tuer les habitants de la terre, ceux qui resteront seront comme des clous dans vos yeux et des lances dans vos côtés, et ils vous seront contraires dans la terre de votre habitation;
56 Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”
Et ce que j’avais pensé à leur faire, c’est à vous que je le ferai.

< Hesabu 33 >