< Hesabu 33 >
1 Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
These are the journeys of the Israelites when they came out of the land of Egypt by their divisions under the leadership of Moses and Aaron.
2 Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
At the LORD’s command, Moses recorded the stages of their journey. These are the stages listed by their starting points:
3 Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
On the fifteenth day of the first month, on the day after the Passover, the Israelites set out from Rameses. They marched out defiantly in full view of all the Egyptians,
4 Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
who were burying all their firstborn, whom the LORD had struck down among them; for the LORD had executed judgment against their gods.
5 Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
The Israelites set out from Rameses and camped at Succoth.
6 Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
They set out from Succoth and camped at Etham, on the edge of the wilderness.
7 Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
They set out from Etham and turned back to Pi-hahiroth, opposite Baal-zephon, and they camped near Migdol.
8 Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
They set out from Pi-hahiroth and crossed through the sea, into the wilderness, and they journeyed three days into the Wilderness of Etham and camped at Marah.
9 Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
They set out from Marah and came to Elim, where there were twelve springs and seventy palm trees, and they camped there.
10 Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
They set out from Elim and camped by the Red Sea.
11 Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
They set out from the Red Sea and camped in the Desert of Sin.
12 Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
They set out from the Desert of Sin and camped at Dophkah.
13 Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
They set out from Dophkah and camped at Alush.
14 Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
They set out from Alush and camped at Rephidim, where there was no water for the people to drink.
15 Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
They set out from Rephidim and camped in the Wilderness of Sinai.
16 Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
They set out from the Wilderness of Sinai and camped at Kibroth-hattaavah.
17 Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
They set out from Kibroth-hattaavah and camped at Hazeroth.
18 Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
They set out from Hazeroth and camped at Rithmah.
19 Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
They set out from Rithmah and camped at Rimmon-perez.
20 Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
They set out from Rimmon-perez and camped at Libnah.
21 Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
They set out from Libnah and camped at Rissah.
22 Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
They set out from Rissah and camped at Kehelathah.
23 Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
They set out from Kehelathah and camped at Mount Shepher.
24 Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
They set out from Mount Shepher and camped at Haradah.
25 Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
They set out from Haradah and camped at Makheloth.
26 Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
They set out from Makheloth and camped at Tahath.
27 Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
They set out from Tahath and camped at Terah.
28 Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
They set out from Terah and camped at Mithkah.
29 Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
They set out from Mithkah and camped at Hashmonah.
30 Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
They set out from Hashmonah and camped at Moseroth.
31 Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
They set out from Moseroth and camped at Bene-jaakan.
32 Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
They set out from Bene-jaakan and camped at Hor-haggidgad.
33 Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
They set out from Hor-haggidgad and camped at Jotbathah.
34 Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
They set out from Jotbathah and camped at Abronah.
35 Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
They set out from Abronah and camped at Ezion-geber.
36 Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
They set out from Ezion-geber and camped at Kadesh in the Wilderness of Zin.
37 Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
They set out from Kadesh and camped at Mount Hor, on the outskirts of the land of Edom.
38 Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
At the LORD’s command, Aaron the priest climbed Mount Hor and died there on the first day of the fifth month, in the fortieth year after the Israelites had come out of the land of Egypt.
39 Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
Aaron was 123 years old when he died on Mount Hor.
40 Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
Now the Canaanite king of Arad, who lived in the Negev in the land of Canaan, heard that the Israelites were coming.
41 Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
And the Israelites set out from Mount Hor and camped at Zalmonah.
42 Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
They set out from Zalmonah and camped at Punon.
43 Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
They set out from Punon and camped at Oboth.
44 Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
They set out from Oboth and camped at Iye-abarim on the border of Moab.
45 Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
They set out from Iyim and camped at Dibon-gad.
46 Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
They set out from Dibon-gad and camped at Almon-diblathaim.
47 Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
They set out from Almon-diblathaim and camped in the mountains of Abarim facing Nebo.
48 Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
They set out from the mountains of Abarim and camped on the plains of Moab by the Jordan across from Jericho.
49 Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
And there on the plains of Moab they camped by the Jordan, from Beth-jeshimoth to Abel-shittim.
50 Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
On the plains of Moab by the Jordan across from Jericho, the LORD said to Moses,
51 “Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
“Speak to the Israelites and tell them: When you cross the Jordan into the land of Canaan,
52 ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
you must drive out before you all the inhabitants of the land, destroy all their carved images and cast idols, and demolish all their high places.
53 Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
You are to take possession of the land and settle in it, for I have given you the land to possess.
54 Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
And you are to divide the land by lot according to your clans. Give a larger inheritance to a larger clan and a smaller inheritance to a smaller one. Whatever falls to each one by lot will be his. You will receive an inheritance according to the tribes of your fathers.
55 Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
But if you do not drive out the inhabitants of the land before you, those you allow to remain will become barbs in your eyes and thorns in your sides; they will harass you in the land where you settle.
56 Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”
And then I will do to you what I had planned to do to them.”