< Hesabu 32 >

1 Sasa wana wa uzao wa Reubeni na wa Gadi walikuwa na idadi kubwa ya wanyama. Waliiona ardhi ya Jazeri na Gileadi, kuwa ni ardhi nzuri kwa mifugo.
Now the children of Reuben and the children of Gad had a very great multitude of cattle; and when they saw the land of Jazer, and the land of Gilead, that, behold, the place was a place for cattle,
2 Kwa hiyo wana wa Gadi na wa Reubeni wakaja kumwambia Musa, na Eliazari kuhani, na viongozi wa watu. Wakasema,
the children of Gad and the children of Reuben came and spoke unto Moses, and to Eleazar the priest, and unto the princes of the congregation, saying:
3 “Hii ndiyo orodha ya maeneo ambayo tumeyatembelea: Diboni, Jazeri, Nimraha, Heshibonni, Ellealehi, Sebamu, Nebo, na Beoni.
'Ataroth, and Dibon, and Jazer, and Nimrah, and Heshbon, and Elealeh, and Sebam, and Nebo, and Beon,
4 Haya ni maeneo ambayo BWANA aliyachukua mbele ya watu wa Israeli, na maeneo mazuri kwa ajili ya mifugo. Sisi watumishi wako tuna mifugo mingi sana.
the land which the LORD smote before the congregation of Israel, is a land for cattle, and thy servants have cattle.'
5 Wakasema kuwa, “Kama tutapata kibali mbele ya macho yako, tunaomba ardhi hii tupewe, sisi watumishi wako, kuwa urithi. Usituvushe ng'ambo ya Yorodani.”
And they said: 'If we have found favour in thy sight, let this land be given unto thy servants for a possession; bring us not over the Jordan.'
6 Musa akawajibu wale wana wa auzao wa Gadi na Reubeni, “Je, mngependa ndugu zenu waende vitani wakati ninyi mkikaa hapa?
And Moses said unto the children of Gad and to the children of Reuben: 'Shall your brethren go to the war, and shall ye sit here?
7 Kwa nini kuwafish moyo watu wa Israeli wasivuke kwenda kwenye nchi ambayo BWANA amewapa?
And wherefore will ye turn away the heart of the children of Israel from going over into the land which the LORD hath given them?
8 Baba zenu walifanya hivyo nilipowatuma kutoka Kadeshi Banea kwenda kuipeleleza ile nchi.
Thus did your fathers, when I sent them from Kadesh-barnea to see the land.
9 Walienda mpaka kwenye bonde la Eskoli. Waliiona ile ardhi kisha wakawafisha moyo watu wa Israeli kwa hiyo wakagoma kuingia kwenye nchi ambayo BWANA alikuwa amewapa.
For when they went up unto the valley of Eshcol, and saw the land, they turned away the heart of the children of Israel, that they should not go into the land which the LORD had given them.
10 Siku hiyo hasira ya BWANA iliwaka. Akaapa akisema,
And the LORD'S anger was kindled in that day, and He swore, saying:
11 'Kwa hakika hakuna mtu aliyetoka Misri, kuanzia wa umri wa miaka ishirini na zaidi ambao wataiona nchi ambao niliwaapia Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, kwa sababu hawakunifuata mimi kwa ukamilifu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi, na Yoshua mwana wa Nuni.
Surely none of the men that came up out of Egypt, from twenty years old and upward, shall see the land which I swore unto Abraham, unto Isaac, and unto Jacob; because they have not wholly followed Me;
12 Ni Kalebu na Joshua tu ndio walionifuata kwa ukamilifu.'
save Caleb the son of Jephunneh the Kenizzite, and Joshua the son of Nun; because they have wholly followed the LORD.
13 Kwa hiyo hasira za BWANA ziliwaka juu ya Israei. Akawafanya wazunguke zunguke jangwani kwa miaka arobaini mpaka kile kizazi kilichofanya maovu mbele za macho yake kilipoteketea.
And the LORD'S anger was kindled against Israel, and He made them wander to and fro in the wilderness forty years, until all the generation, that had done evil in the sight of the LORD, was consumed.
14 Tazama, mmetokea katika nafasi za baba zenu, kama watu wengine wenye dhambi zaidi, ili kuongeza hasira ya BWANA kwa Israeli.
And, behold, ye are risen up in your fathers' stead, a brood of sinful men, to augment yet the fierce anger of the LORD toward Israel.
15 Kama hamtamfuata, ataiacha Israeli jangwani na mtakuwa mmewateketeza watu hawa wote.
For if ye turn away from after Him, He will yet again leave them in the wilderness; and so ye will destroy all this people.'
16 Kwa hiyo wakaja karibu na Musa wakamwambia, “Turuhusu tujenga hapa uzio kwa ajili ya ng'ombe zetu na miji hapa kwa ajili ya familia zetu.
And they came near unto him, and said: 'We will build sheepfolds here for our cattle, and cities for our little ones;
17 Hata hivyo, sisi wenyewe tutajipanga kijeshi kwenda na jeshi la Israeli mpaka tumewaongoza kupata maeneo yao. Lakini familia zetu zitakuwa kwenye miji ya maboma kwa ssbabu ya watu wengine ambao bado wanaishi katika nchi hii.
but we ourselves will be ready armed to go before the children of Israel, until we have brought them unto their place; and our little ones shall dwell in the fortified cities because of the inhabitants of the land.
18 Hatutarudi kwenye familia zetu mpaka kila mmoja watu wa Israeli apate urithi wake.
We will not return unto our houses, until the children of Israel have inherited every man his inheritance.
19 Sisi hatutachukua urithi wa ardhi pamoja nao kule ng'ambo ya Yorodani, kwa sababu urithi wetu uko hapa upande wa mashariki mwa Yorodani.”
For we will not inherit with them on the other side of the Jordan, and forward, because our inheritance is fallen to us on this side of the Jordan eastward.'
20 Kwa hiyo Musa akawajibu, “Kama mtafanya mnachokisema, kama mtajipanga wenyewe mbele za BWANA kwenda vitani,
And Moses said unto them: 'If ye will do this thing: if ye will arm yourselves to go before the LORD to the war,
21 basi kila mmoja wa wanajeshi wenu lazima avuke Yorodani mbele za BWANA, mpaka atakapowafukuza maadui zake kutoka mbele zake
and every armed man of you will pass over the Jordan before the LORD, until He hath driven out His enemies from before Him,
22 na nchi itawaliwe na Israeli mbele zake. Kisha mtaweza kurudi. Hamtakuwa na hatia mbele za BWANA na mbele ya Israeli. Hii nchi itakuwa miliki yenu mbele za BWANA.
and the land be subdued before the LORD, and ye return afterward; then ye shall be clear before the LORD, and before Israel, and this land shall be unto you for a possession before the LORD.
23 Bali kama hamtafnya hivyo, tazama, mtakuwa mmefanya dhambi mbele ya BWANA. Mwe na hakika kuwa dhambi yenu itaonekana
But if ye will not do so, behold, ye have sinned against the LORD; and know ye your sin which will find you.
24 wazi. Jengeni miji kwa ajili ya familia zenu na mazizi kwa ajili ya kondoo zenu; kisha fanyeni kile mlichokisema.”
Build you cities for your little ones, and folds for your sheep; and do that which hath proceeded out of your mouth.'
25 Wale wana wa Gadi na Reubeni wakamwambia Musa, wakisema, “Watumishi wako wtafanya kama vile wewe, bwana wetu, unavyotuamuru.
And the children of Gad and the children of Reuben spoke unto Moses, saying: 'Thy servants will do as my lord commandeth.
26 Watoto wetu, wake zetu, makundi yetu, na wanyama wetu wote watakaa huko kwenye miji ya Gileadi.
Our little ones, our wives, our flocks, and all our cattle, shall be there in the cities of Gilead;
27 Hata hivyo, sisi watumishi wako, tutavuka kwenda ng'ambo mbele za BWANA kupigana, kila mtu ambaye yuko tayari kwa vita, kama vile wewe, bwana wetu, unavyosema.”
but thy servants will pass over, every man that is armed for war, before the LORD to battle, as my lord saith.'
28 Kwa hiyo Musa akawapa maelekezo yayowahusu kwa Eliazari kuhani, kwa Joshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa koo kufuata jamaa zao katika makabila ya wana wa Israeli.
So Moses gave charge concerning them to Eleazar the priest, and to Joshua the son of Nun, and to the heads of the fathers' houses of the tribes of the children of Israel.
29 Musa akawaambia, “Kama uzao wa Reubeni na Gadi watavuka ng'ambo ya Yorodani pamoja nanyi, kila mwanamume anayetakiwa kuwa vitani mbele za BWANA, na kama nchi mtaitawala mbele zenu, ndipo mtakapowapa eneo la Gileadi kuwa miliki yao.
And Moses said unto them: 'If the children of Gad and the children of Reuben will pass with you over the Jordan, every man that is armed to battle, before the LORD, and the land shall be subdued before you, then ye shall give them the land of Gilead for a possession;
30 Lakini kama hawatavuka pamoja nanyi wakiwa na silaha zao, basi mtawapa urithi wao katika nchi ya Kanaani.”
but if they will not pass over with you armed, they shall have possessions among you in the land of Canaan.'
31 Kwas hiyo wana wa uzao wa Gadi na wa Reubeni wakamjibu wakisema, Kama vile BWANA alivyosema nasi, sisi watumwa wako, hiki ndicho tutakachokifanya.
And the children of Gad and the children of Reuben answered, saying: 'As the LORD hath said unto thy servants, so will we do.
32 Tutavuka tukiwa na silaha zetu mbele za BWANA kuingia katika nchi ya Kanaani, lakini urithi wetu utabaki utabaki upande huu wa Yorodani.”
We will pass over armed before the LORD into the land of Canaan, and the possession of our inheritance shall remain with us beyond the Jordan.'
33 Kwa hiyo uzao wa Gadi na Reubeni, na pia nusu ya kabila la Manase mwana wa Yusufu, Musa akawapa ufalme wa Sihoni, mfalme wa Waamori, na wa Ogi, mafalme wa Bashani, Aliwapa hiyo nchi, na kuwagawia miji yake yote pamoja na mipaka yake, miji yote ya nchi inayowazunguka.
And Moses gave unto them, even to the children of Gad, and to the children of Reuben, and unto the half-tribe of Manasseh the son of Joseph, the kingdom of Sihon king of the Amorites, and the kingdom of Og king of Bashan, the land, according to the cities thereof with their borders, even the cities of the land round about.
34 Wale wa uzao wa Gadi wakaijenga Diboni,
And the children of Gad built Dibon, and Ataroth, and Aroer;
35 Atarothi, Aroeri, Atrothi, Jazeri, Jogbehaha, Bethi Nimraha,
and Atroth-shophan, and Jazer, and Jogbehah;
36 na Bethi Harani kuwa miji iliyo na maboma na mazizi ya kondoo wao.
and Beth-nimrah, and Beth-haran; fortified cities, and folds for sheep.
37 Wale wa uzao wa Reubeni wakaijenga Heshiboni. Elealehi, Kiriathaimu,
And the children of Reuben built Heshbon, and Elealeh, and Kiriathaim;
38 Nebo, Baali Meoni - baadaye waliyabadili majina yao, na Sibimaha.
and Nebo, and Baal-meon — their names being changed — and Sibmah; and gave their names unto the cities which they builded.
39 Wale wa uzao wa Machiri mwana wa Manase walienda Gileadi na kuutwaa kutoka kwa Waamori waliokuwa wakiishi humo.
And the children of Machir the son of Manasseh went to Gilead, and took it, and dispossessed the Amorites that were therein.
40 Kisha Musa akaitoa Gileadi kwa Machiri mwana wa Manase, na watu wake wakaishi humo.
And Moses gave Gilead unto Machir the son of Manasseh; and he dwelt therein.
41 Jairi mwana wa Manase alienda kuiteka miji yake na kuiita Havothi Jairi.
And Jair the son of Manasseh went and took the villages thereof, and called them Havvoth-jair.
42 Nobaha alienda kuitieka Kenathi na vijiji vyake, na akauita kwa jina lake Nobaha.
And Nobah went and took Kenath, and the villages thereof, and called it Nobah, after his own name.

< Hesabu 32 >