< Hesabu 31 >

1 BWANA alinena na Musa na kumwambia,
And YHWH speaks to Moses, saying,
2 “Uwalipizie kisasi Wamidiani kwa kile walichowafanya Waisraeli. Baada ya kufanya hivyo utakufa na kukusanyika na watu wako.”
“Execute the vengeance of the sons of Israel against the Midianites—afterward you are gathered to your people.”
3 Kwa hiyo Musa akawaambia watu. Akasema, “andaeni baadhi ya majeshi yenu kwa ajili ya vita ili kwamba wakawapige Wamidiani na kubeba kiapo cha BWANA.
And Moses speaks to the people, saying, “Arm men from [among] you for the war, and they are against Midian, to put the vengeance of YHWH on Midian;
4 Kwa kila kabila la Israeli watatuma askari elfu moja kwa ajili ya vita.”
one thousand for a tribe—you send one thousand for a tribe, of all the tribes of Israel, to the war.”
5 Kwa hiyo kati ya wanaume maelfu elfu wa Israeli, wanaume elfu moja walitolewa kwa ajili ya vita, jumla ya wanaume elfu kumi na mbili.
And there are given out of the thousands of Israel one thousand for a tribe—twelve thousand armed ones [for] war;
6 Kisha Musa akawatuma kwenda vitani, elfu moja toka kila kabila pamoja na Finehasi mwana wa Eliazari kuhanai, wakiwa na vitu kutoka mahali patakatifu wakiwa na matarumbeta kwa ajili ya ishara za sauti.
and Moses sends them, one thousand for a tribe, to the war; [he sent] them and Phinehas son of Eleazar the priest to the war, with the holy vessels and the trumpets of shouting in his hand.
7 Wakapigana na Midiani, kama BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa. Wakamwua kila mwanaume.
And they war against Midian, as YHWH has commanded Moses, and slay every male;
8 Wakawaua wafalme wa Midiani pamoja na wengine waliowaua ni: Evi, Rekimu, Zuri, Huri, na Reba, hawa walaikuwa ndio waflme watano wa Midiani. pia walimwua Balaamu mwana wa Beori, kwa upanga.
and they have slain the kings of Midian besides their pierced ones: Evi, and Rekem, and Zur, and Hur, and Reba—five kings of Midian; and they have slain Balaam son of Beor with the sword.
9 Jeshi la Israeli likawachukua mateka wanawake wa Midiani, watoto wao, mifugo yao yote, kondoo wao na bidhaa zao zote. walivichukua hivi kama mateka.
And the sons of Israel take the women of Midian and their infants captive; and they have plundered all their livestock, and all their substance, and all their wealth;
10 Waliichoma moto miji yao yote walimoishi na kambi zao zote.
and they have burned all their cities, with their habitations, and all their towers, with fire.
11 Walichukua vitu vyote na wafungwa, watu na wanyama.
And they take all the spoil and all the prey, among man and among beast;
12 Wakawaleta mateka, nyara, na wakakamata vitu wakavileta kwa Musa, na Eliazari kuhani, na kwa jamii ya watu wa Israeli. Wakavileta hivi vitu kambini katika uwanda wa Moabu, kule Yorodani karibu na Yeriko.
and they bring in the captives, and the prey, and the spoil to Moses, and to Eleazar the priest, and to the congregation of the sons of Israel, to the camp, to the plains of Moab, which [are] by the Jordan, [near] Jericho.
13 Musa, Eliazari kuhani, pamoja na viongozi wa watu wakaenda kukutana nao nje ya kambi.
And Moses, and Eleazar the priest, and all the princes of the congregation, go out to meet them, to the outside of the camp,
14 Lakini Musa alikuwa na hasira dhidi ya viongozi wa jeshi, Wale majemedari wa maelfu na maakida wa mamia, waliotoka kupigana.
and Moses is angry against the inspectors of the force, chiefs of the thousands, and chiefs of the hundreds, who are coming in from the warfare of battle.
15 Musa akawaambia, “Je, mmeawaacha wanawake wote kuishi?
And Moses says to them, “Have you kept every female alive?
16 Tazama, wanawake hawa ndio waliosababisha watu wa Israeli, kwa kupitia ushauri wa Balaamu, kufanya dhambi dhidi ya BWANA huko Peori, wakati ile tauni iliposambaa kwa watu wa Mungu.
Behold, they have been to the sons of Israel, through the word of Balaam, to cause a trespass against YHWH in the matter of Peor, and the plague is in the congregation of YHWH.
17 Sasa basi, ueni kila mwanaume kuanzia wadogo, na ueni kila mwanamke aliyelala na mwanamume.
And now, slay every male among the infants, indeed, slay every woman knowing a man by the lying of a male;
18 Lakini chukueni wale mabinti wadogo ambao hawajalala na mwanamume.
and all the infants among the women who have not known the lying of a male you have kept alive for yourselves.
19 Mtaweka kambi nje na kambi za Israeli kwa muda wa siku saba. Ninyi wote ambao mmeua watu au ambao mmegusa maiti yeyote mtajitakasa wenyewe katika siku ya tatu na katika siku ya saba - ninyi na mateka wenu.
And you, encamp at the outside of the camp [for] seven days; any who has slain a person, and any who has come against a pierced one, cleanse yourselves on the third day and on the seventh day—you and your captives;
20 Na mtayatakasa mavazi yenu yote, na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi za wanyama, na manyoya ya mbuzi, na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao.”
and every garment, and every skin vessel, and every work of goats’ [hair], and every wooden vessel, you yourselves cleanse.”
21 Eliazarai kuahani akawaambia wale wanajeshi waliokuwa wameenda vitani, “Hii ni amri ya sheria ambayo BWANA alimpa Musa:
And Eleazar the priest says to the men of war who go to battle, “This [is] the statute of the law which YHWH has commanded Moses:
22 Zile dhahabu, fedha, vyuma, bati, risasi,
only the gold, and the silver, the bronze, the iron, the tin, and the lead,
23 na kila kitu knaweza kuhhimili moto, mtakiweka katka moto, navyo vitakuwa safi. Nakisha mtavitakasa vitu hivyo na maji ya farakano. Na vitu vyote ambavyo haviwezi kupita katika moto, mtavitakasa kwa maji hayo.
everything which may go into fire, you cause to pass over through fire, and it has been clean; it is surely cleansed with the water of separation; and all that may not go into fire, you cause to pass over through water;
24 Na mtazifua nguao zenu katika siku ya saba, ndipo mtakapokuwa safi. Baada ya hapo mnaweza kurudi kwenye kambi za Israeli.”
and you have washed your garments on the seventh day and have been clean, and afterward you come into the camp.”
25 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And YHWH speaks to Moses, saying,
26 “Vihesabu vitu vyote vilivyochukuliwa nyara, wote watu na wanyama. Wewe, Eliazari kuhani, na viongozi wa watu kufuata koo
“Take up the sum of the prey of the captives, among man and among beast, you, and Eleazar the priest, and the heads of the fathers of the congregation;
27 watavigawa hivi vitu katika mkundi mawili. Mvigawe kwa wanajeshi walioenda kupigana na kwa watu wote.
and you have halved the prey between those handling the battle, who go out to the war, and all the congregation;
28 Kisha toza kodi ambayo itatolewa kwangu kutoka kwa wanajeshi waliokuwa wameenda vitani. Hii kodi itakuwa moja kati ya mia tano, katika watu, ng'ombe, punda, kondoo, au mbuzi.
and you have raised a tribute to YHWH from the men of battle, who go out to the war, one body out of five hundred, of man, and of the herd, and of the donkeys, and of the flock;
29 Uichukue hii kodi kutoka katika nusu yao na umpe Eliazari kuhani kwa ajili ya sadaka itakayotolewa kwangu.
you take from their half and have given [it] to Eleazar the priest [as] a raised-offering of YHWH.
30 Pia kutoka katika nusu ya watu wa Israeli, utachukua moja kati ya hamsini -kutoka vitu, ng'ombe, punda, na mbuzi. Uvitoe hivi kwa Walawi wanaotumika katika masikani yangu.”
And from the sons of Israel’s half you take one possession out of fifty, of man, of the herd, of the donkeys, and of the flock, of all the livestock, and you have given them to the Levites keeping the charge of the Dwelling Place of YHWH.”
31 Kwa hiyo Musa na Eliazari kuhani wakafanya kama BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
And Moses does—Eleazar the priest also—as YHWH has commanded Moses.
32 Sasa zile nyara zilizokuwa zimebaki ambazo wanajeshi walikuwa wameteka zilikuwa kondoo 675, 000,
And the prey, the remainder of the spoil which the people of the host have spoiled, is six hundred thousand and seventy thousand and five thousand of the flock;
33 maksai elfu sabini na mbili,
and seventy-two thousand of the herd;
34 punda elfu sitini na moja,
and sixty-one thousand donkeys;
35 na wanawake elfu thelathini na mbili ambao walikuwa hawajalala na mwanamume yeyote.
and of mankind—of the women who have not known the lying of a male—all the persons [are] thirty-two thousand.
36 Ile hesabu ya nusu iliyokuwa imetunzwa kwa ajili ya wanajeshi ilikuwa kondoo 337, 000. Ile sehemu ya
And the half, the portion of those who go out into the war, is [in] number three hundred thousand and thirty thousand and seven thousand and five hundred of the flock.
37 BWANA ya kondoo ilikuwa kondoo 675.
And the tribute to YHWH of the sheep is six hundred seventy-five;
38 Maksai walikuwa elfu thelathini na sita ambayo kodi ya BWANA ilikuwa sabini na mbili.
and the herd [is] thirty-six thousand, and their tribute to YHWH [is] seventy-two;
39 Punda walikuwa 30, 500 ambao sehemu ya BWANA ilikuwa sitini na moja.
and the donkeys [are] thirty thousand and five hundred, and their tribute to YHWH [is] sixty-one;
40 Watu walikuwa wanawake elfu kumi na sita ambao kodi ya BWANA ilikuwa thelathini na mbili.
and of mankind [are] sixteen thousand, and their tribute to YHWH [is] thirty-two persons.
41 Musa aliichukua ile kodi ambayo ilitakiwa kuwekwa sadaka kwa BWANA. Akampatia Eliazari kuhani, kama BWANA alivyomwamuru Musa.
And Moses gives the tribute—YHWH’s raised-offering—to Eleazar the priest, as YHWH has commanded Moses.
42 Ile nusu ya watu wa Israeli ambayo Musa alikuwa ameichukua toka kwa wanawjeshi waliokuwa wameenda vitani -
And of the sons of Israel’s half, which Moses halved from the men who war—
43 ile nusu y a watu ilikuwa kondoo 337, 500,
and the congregation’s half is three hundred thousand and thirty thousand [and] seven thousand and five hundred of the flock;
44 maksai elfu thelathini na sita,
and thirty-six thousand of the herd;
45 punda 30, 500,
and thirty thousand and five hundred donkeys;
46 na wanawake elfu kumi na sita.
and sixteen thousand of mankind—
47 Kutoka kwenye nusu ya watu wa Israeli, Musa alichukua moja katika hamsini, wote watu na wanyama. Aliwapa Walawi ambao huitumikia masikani ya BWANA, kama BWANA alivyokuwa amemwamuru kufanya.
Moses takes from the sons of Israel’s half one possession from the fifty, of man and of beast, and gives them to the Levites keeping the charge of the Dwelling Place of YHWH, as YHWH has commanded Moses.
48 Kisha wale maakida wa jeshi, makamanda wa elfu na makapteni wa mamia, wakaja kwa Musa.
And the inspectors whom the thousands of the host have (heads of the thousands and heads of the hundreds), draw near to Moses,
49 Wakamwambia, “watumishi wako wamewahesabu wanajeshi ambao wako chini yetu, hakuna hata mmoja wao aliyekosa.
and they say to Moses, “Your servants have taken up the sum of the men of war who [are] with us, and not a man of us has been missed;
50 Tumemletea BWANA sadaka, ambayo kila mmoja amepata, vitu vya dhahabu, metali, timbi, pete za mhuri, vipini na vikuku, ili kujifanyia upatanisho kwa BWANA.”
and we bring YHWH’s offering near, each of that which he has found of vessels of gold—chain, and bracelet, seal-ring, [ear]-ring, and bead—to make atonement for ourselves before YHWH.”
51 Musa na Eliazari kuhani akapokea kutoka kwao dhahabu na vitu vyote vilivyotengenezwa kwa ufundi.
And Moses receives—Eleazar the priest also—the gold from them, every vessel of workmanship;
52 Vitu vyote vya sadaka ya dhahabu ambavyo walimpa BWANA- sadaka toka kwa makamanda wa maelfu na kutoka kwa makepteni wa mamia - vilikuwa na uzito wa shekeli 16, 750.
and all the gold of the raised-offering which they have lifted up to YHWH is sixteen thousand seven hundred and fifty shekels, from heads of the thousands and from heads of the hundreds;
53 Kila mwanajeshi alikuwa ameteka nyara ya kila mtu kwa ajili yake.
(the men of the host have each taken spoil for himself);
54 Musa na Eliazari kuhani wakazichukuazile dhahabu toka kwa makamanda wa maelfu na makepteni wa mamia. Wakavipeleka kwenye hema ya kukutania kama ukumbusho wa watu wa Israeli kwa BWANA.
and Moses takes—Eleazar the priest also—the gold from the heads of the thousands and of the hundreds, and they bring it into the Tent of Meeting [as] a memorial for the sons of Israel before YHWH.

< Hesabu 31 >