< Hesabu 31 >

1 BWANA alinena na Musa na kumwambia,
Then the Lord said to Moses,
2 “Uwalipizie kisasi Wamidiani kwa kile walichowafanya Waisraeli. Baada ya kufanya hivyo utakufa na kukusanyika na watu wako.”
Give the Midianites punishment for the wrong they did to the children of Israel: and after that you will go to rest with your people.
3 Kwa hiyo Musa akawaambia watu. Akasema, “andaeni baadhi ya majeshi yenu kwa ajili ya vita ili kwamba wakawapige Wamidiani na kubeba kiapo cha BWANA.
So Moses said to the people, Let men from among you be armed for war to put into effect against Midian the Lord's punishment on them.
4 Kwa kila kabila la Israeli watatuma askari elfu moja kwa ajili ya vita.”
From every tribe of Israel send a thousand to the war.
5 Kwa hiyo kati ya wanaume maelfu elfu wa Israeli, wanaume elfu moja walitolewa kwa ajili ya vita, jumla ya wanaume elfu kumi na mbili.
So from the thousands of Israel a thousand were taken from every tribe, twelve thousand men armed for war.
6 Kisha Musa akawatuma kwenda vitani, elfu moja toka kila kabila pamoja na Finehasi mwana wa Eliazari kuhanai, wakiwa na vitu kutoka mahali patakatifu wakiwa na matarumbeta kwa ajili ya ishara za sauti.
And Moses sent them out to war, a thousand from every tribe, and with them Phinehas, the son of Eleazar the priest, taking in his hands the vessels of the holy place and the horns for sounding the note of war.
7 Wakapigana na Midiani, kama BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa. Wakamwua kila mwanaume.
And they made war on Midian, as the Lord gave orders to Moses; and they put to death every male.
8 Wakawaua wafalme wa Midiani pamoja na wengine waliowaua ni: Evi, Rekimu, Zuri, Huri, na Reba, hawa walaikuwa ndio waflme watano wa Midiani. pia walimwua Balaamu mwana wa Beori, kwa upanga.
They put the kings of Midian to death with the rest, Evi and Reken and Zur and Hur and Reba, the five kings of Midian: and Balaam, the son of Beor, they put to death with the sword.
9 Jeshi la Israeli likawachukua mateka wanawake wa Midiani, watoto wao, mifugo yao yote, kondoo wao na bidhaa zao zote. walivichukua hivi kama mateka.
The women of Midian with their little ones the children of Israel took prisoner; and all their cattle and flocks and all their goods they took for themselves;
10 Waliichoma moto miji yao yote walimoishi na kambi zao zote.
And after burning all their towns and all their tent-circles,
11 Walichukua vitu vyote na wafungwa, watu na wanyama.
They went away with the goods they had taken, man and beast.
12 Wakawaleta mateka, nyara, na wakakamata vitu wakavileta kwa Musa, na Eliazari kuhani, na kwa jamii ya watu wa Israeli. Wakavileta hivi vitu kambini katika uwanda wa Moabu, kule Yorodani karibu na Yeriko.
And the prisoners and the goods and everything they had taken, they took to Moses and Eleazar the priest and the people of Israel, to the tent-circle in the lowlands of Moab by the Jordan at Jericho.
13 Musa, Eliazari kuhani, pamoja na viongozi wa watu wakaenda kukutana nao nje ya kambi.
Then Moses and Eleazar the priest and the chiefs of the people went out to them before they had come into the tent-circle.
14 Lakini Musa alikuwa na hasira dhidi ya viongozi wa jeshi, Wale majemedari wa maelfu na maakida wa mamia, waliotoka kupigana.
And Moses was angry with the chiefs of the army, the captains of thousands and the captains of hundreds who had come back from the war.
15 Musa akawaambia, “Je, mmeawaacha wanawake wote kuishi?
And Moses said to them, Why have you kept all the women safe?
16 Tazama, wanawake hawa ndio waliosababisha watu wa Israeli, kwa kupitia ushauri wa Balaamu, kufanya dhambi dhidi ya BWANA huko Peori, wakati ile tauni iliposambaa kwa watu wa Mungu.
It was these who, moved by Balaam, were the cause of Israel's sin against the Lord in the question of Peor, because of which disease came on the people of the Lord.
17 Sasa basi, ueni kila mwanaume kuanzia wadogo, na ueni kila mwanamke aliyelala na mwanamume.
So now put every male child to death, and every woman who has had sex relations with a man.
18 Lakini chukueni wale mabinti wadogo ambao hawajalala na mwanamume.
But all the female children who have had no sex relations with men, you may keep for yourselves.
19 Mtaweka kambi nje na kambi za Israeli kwa muda wa siku saba. Ninyi wote ambao mmeua watu au ambao mmegusa maiti yeyote mtajitakasa wenyewe katika siku ya tatu na katika siku ya saba - ninyi na mateka wenu.
You yourselves will have to keep outside the tent-circle for seven days, anyone of you who has put any person to death or come near a dead body; and on the third day and on the seventh day make yourselves and your prisoners clean.
20 Na mtayatakasa mavazi yenu yote, na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi za wanyama, na manyoya ya mbuzi, na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao.”
And every bit of clothing, and anything made of leather or goats' hair or wood, you are to make clean.
21 Eliazarai kuahani akawaambia wale wanajeshi waliokuwa wameenda vitani, “Hii ni amri ya sheria ambayo BWANA alimpa Musa:
Then Eleazar the priest said to the men of war who had been to the fight, This is the rule of the law which the Lord has given to Moses:
22 Zile dhahabu, fedha, vyuma, bati, risasi,
But gold and silver and brass and iron and tin and lead,
23 na kila kitu knaweza kuhhimili moto, mtakiweka katka moto, navyo vitakuwa safi. Nakisha mtavitakasa vitu hivyo na maji ya farakano. Na vitu vyote ambavyo haviwezi kupita katika moto, mtavitakasa kwa maji hayo.
And anything which may be heated, is to go through the fire and be made clean; but in addition it is to be put in the water of cleaning: and anything which may not go through the fire is to be put in the water.
24 Na mtazifua nguao zenu katika siku ya saba, ndipo mtakapokuwa safi. Baada ya hapo mnaweza kurudi kwenye kambi za Israeli.”
And on the seventh day, after washing your clothing, you will be clean, and then you may come into the tent-circle.
25 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And the Lord said to Moses,
26 “Vihesabu vitu vyote vilivyochukuliwa nyara, wote watu na wanyama. Wewe, Eliazari kuhani, na viongozi wa watu kufuata koo
Get an account of everything which was taken in the war, of man and of beast, you and Eleazar the priest and the heads of families of the people:
27 watavigawa hivi vitu katika mkundi mawili. Mvigawe kwa wanajeshi walioenda kupigana na kwa watu wote.
And let division be made of it into two parts, one for the men of war who went out to the fight, and one for all the people:
28 Kisha toza kodi ambayo itatolewa kwangu kutoka kwa wanajeshi waliokuwa wameenda vitani. Hii kodi itakuwa moja kati ya mia tano, katika watu, ng'ombe, punda, kondoo, au mbuzi.
And from the men of war who went out let there be offered to the Lord one out of every five hundred, from the persons, and from the oxen and asses and sheep:
29 Uichukue hii kodi kutoka katika nusu yao na umpe Eliazari kuhani kwa ajili ya sadaka itakayotolewa kwangu.
Take this from their part and give it to Eleazar the priest as an offering to be lifted up to the Lord.
30 Pia kutoka katika nusu ya watu wa Israeli, utachukua moja kati ya hamsini -kutoka vitu, ng'ombe, punda, na mbuzi. Uvitoe hivi kwa Walawi wanaotumika katika masikani yangu.”
And from the part given to the children of Israel, take one out of every fifty, from the persons, and from the oxen and asses and sheep, and give it to the Levites who have the care of the House of the Lord.
31 Kwa hiyo Musa na Eliazari kuhani wakafanya kama BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
So Eleazar and Moses did as the Lord had given orders to Moses.
32 Sasa zile nyara zilizokuwa zimebaki ambazo wanajeshi walikuwa wameteka zilikuwa kondoo 675, 000,
Now the beasts taken, in addition to what the fighting-men took for themselves, were six hundred and seventy-five thousand sheep,
33 maksai elfu sabini na mbili,
And seventy-two thousand oxen,
34 punda elfu sitini na moja,
And sixty-one thousand asses;
35 na wanawake elfu thelathini na mbili ambao walikuwa hawajalala na mwanamume yeyote.
And thirty-two thousand persons, that is, women who had never had sex relations with a man.
36 Ile hesabu ya nusu iliyokuwa imetunzwa kwa ajili ya wanajeshi ilikuwa kondoo 337, 000. Ile sehemu ya
And the half given as their part to the men who went to the war, was three hundred and thirty-seven thousand, five hundred sheep,
37 BWANA ya kondoo ilikuwa kondoo 675.
Of which the Lord's part was six hundred and seventy-five.
38 Maksai walikuwa elfu thelathini na sita ambayo kodi ya BWANA ilikuwa sabini na mbili.
The number of oxen was thirty-six thousand, of which the Lord's part was seventy-two;
39 Punda walikuwa 30, 500 ambao sehemu ya BWANA ilikuwa sitini na moja.
The number of asses was thirty thousand, five hundred, of which the Lord's part was sixty-one.
40 Watu walikuwa wanawake elfu kumi na sita ambao kodi ya BWANA ilikuwa thelathini na mbili.
And the number of persons was sixteen thousand, of which the Lord's part was thirty-two persons.
41 Musa aliichukua ile kodi ambayo ilitakiwa kuwekwa sadaka kwa BWANA. Akampatia Eliazari kuhani, kama BWANA alivyomwamuru Musa.
And Moses gave the Lord's part, lifted up as an offering, to Eleazar the priest, as the Lord had given orders to Moses.
42 Ile nusu ya watu wa Israeli ambayo Musa alikuwa ameichukua toka kwa wanawjeshi waliokuwa wameenda vitani -
And from the half given to the children of Israel, which Moses had kept separate from that given to the fighting-men,
43 ile nusu y a watu ilikuwa kondoo 337, 500,
(Now the people's half was three hundred and thirty-seven thousand, five hundred sheep,
44 maksai elfu thelathini na sita,
And thirty-six thousand oxen,
45 punda 30, 500,
And thirty thousand, five hundred asses,
46 na wanawake elfu kumi na sita.
And sixteen thousand persons; )
47 Kutoka kwenye nusu ya watu wa Israeli, Musa alichukua moja katika hamsini, wote watu na wanyama. Aliwapa Walawi ambao huitumikia masikani ya BWANA, kama BWANA alivyokuwa amemwamuru kufanya.
Even from the children of Israel's half, Moses took one out of every fifty, men and beasts, and gave them to the Levites who had the care of the House of the Lord; as the Lord gave orders to Moses.
48 Kisha wale maakida wa jeshi, makamanda wa elfu na makapteni wa mamia, wakaja kwa Musa.
Then the men in authority over the thousands of the army, the captains of thousands and captains of hundreds, came to Moses,
49 Wakamwambia, “watumishi wako wamewahesabu wanajeshi ambao wako chini yetu, hakuna hata mmoja wao aliyekosa.
And said to him, Your servants have taken note of the number of all the fighting-men under our orders, and every one is present;
50 Tumemletea BWANA sadaka, ambayo kila mmoja amepata, vitu vya dhahabu, metali, timbi, pete za mhuri, vipini na vikuku, ili kujifanyia upatanisho kwa BWANA.”
And we have here an offering for the Lord from what every man took in the war, ornaments of gold, leg-chains and arm-rings, finger-rings, ear-rings, and neck-ornaments, to make our souls free from sin before the Lord.
51 Musa na Eliazari kuhani akapokea kutoka kwao dhahabu na vitu vyote vilivyotengenezwa kwa ufundi.
So Moses and Eleazar the priest took the gold from them, even all the worked ornaments.
52 Vitu vyote vya sadaka ya dhahabu ambavyo walimpa BWANA- sadaka toka kwa makamanda wa maelfu na kutoka kwa makepteni wa mamia - vilikuwa na uzito wa shekeli 16, 750.
And the gold which the captains of thousands and captains of hundreds gave, as an offering to be lifted up before the Lord, came to sixteen thousand, seven hundred and fifty shekels.
53 Kila mwanajeshi alikuwa ameteka nyara ya kila mtu kwa ajili yake.
(For every man of the army had taken goods for himself in the war.)
54 Musa na Eliazari kuhani wakazichukuazile dhahabu toka kwa makamanda wa maelfu na makepteni wa mamia. Wakavipeleka kwenye hema ya kukutania kama ukumbusho wa watu wa Israeli kwa BWANA.
Then Moses and Eleazar the priest took the gold given by the captains of thousands and captains of hundreds, and took it into the Tent of meeting, to be a sign in memory of the children of Israel before the Lord.

< Hesabu 31 >