< Hesabu 3 >

1 Sasa hii ndiyo historia ya uzao wa Haruni na Musa wakati BWANA aliposema na Musa kwenye mlima Sinai.
These also were the generations of Aaron and Moses, in the day that the Lord spake with Moses in mount Sinai.
2 Majina ya watoto wa Haruni walikuwa Nadabu ambaye ndiyo mtoto wa kwanza, na Abihu, na Eliezeri, na Ithamari.
So these are the names of the sonnes of Aaron, Nadab the first borne, and Abihu, Eleazar, and Ithamar.
3 Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni, makuhani waliokuwa wamepakwa mafuta na kuwekwa wakfu kutumika kama makuhani.
These are the names of the sonnes of Aaron the anoynted Priests, whom Moses did consecrate to minister in the Priests office.
4 Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya BWANA walipomtolea moto usiokubalika walipokuwa katika nyika ya Sinai. Nadabu na Abihu hawakuwa na watoto, kwa hiyo Eliazari na Ithamari walitumika kama makuhani pamoja na baba yao.
And Nadab and Abihu died before the Lord, when they offred strange fire before the Lord in the wildernesse of Sinai, and had no children: but Eleazar and Ithamar serued in ye Priestes office in the sight of Aaron their father.
5 BWANA alinena na Musa, akamwambia,
Then the Lord spake vnto Moses, saying,
6 “Walete kabila ya Lawi na uwaweke kwa Haruni kuhani ili wamsaidie
Bring the tribe of Leui, and set the before Aaron the Priest that they may serue him,
7 Nao lazima wafanye majukumu badala ya Haruni na jumuiya yote mbele ya hema ya kukutania. Lazima watumike hemani.
And take the charge with him, euen the charge of the whole Congregation before the Tabernacle of the Congregation to doe the seruice of the Tabernacle.
8 Watayatunza mapambo ya hema ya kukutania, na watawatumikia makabila ya Israel kwa huduma ya hemani.
They shall also keepe all the instruments of the Tabernacle of the Congregation, and haue the charge of the children of Israel to doe the seruice of the Tabernacle.
9 Uwaweke Walawi kwa Haruni na watoto wake. Nimewatoa kikamilifu ili wamsaidie kuwatumikia watu wa Israel.
And thou shalt giue the Leuites vnto Aaron and to his sonnes: for they are giuen him freely from among the children of Israel.
10 Umchague Haruni na watoto wake kuwa makuhani, lakini mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe.”
And thou shalt appoint Aaron and his sonnes to execute their Priestes office: and the stranger that commeth neere, shalbe slayne.
11 BWANA alinena na Musa. akamwambia,
Also the Lord spake vnto Moses, saying,
12 “Tazama, nimewachagua Walawi katika watu wa Israel. Nimefanya hivyo badala ya kuchukua mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wana wa Israel. Hawa Walawi ni wangu.
Beholde, I haue euen taken the Leuites from among the childre of Israel: for al the first borne that openeth the matrice among the children of Israel, and the Leuites shalbe mine,
13 Na hata wazaliwa wa kwanza ni mali yangu. Katika siku ambyo niliwavamia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, Niliwatenga wazaliwa wa kwanza wa Israeli kwa ajili yangu, watu na wanyama pia. Ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.”
Because all the first borne are mine: for the same day, that I smote all the first borne in the land of Egypt, I sanctified vnto me all the first borne in Israel, both man and beast: mine they shalbe: I am the Lord.
14 BWANA alinena na Musa katika nyika ya Sinai. Akasema,
Moreouer, the Lord spake vnto Moses in the wildernesse of Sinai, saying,
15 “Wahesabu uzao wa Lawi katika kila familia, katika nyumba za koo zao. Hesabu kila mume kuanzia mwezi mmoja au zaidi.”
Nomber the children of Leui after the houses of their fathers, in their families: euery male from a moneth olde and aboue shalt thou nomber.
16 Musa aliwahesabu, kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.
Then Moses nombred them according to the word of the Lord, as he was commanded.
17 Majina ya watoto waLawi yalikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
And these are the sonnes of Leui by their names, Gershon, and Kohath, and Merari.
18 Ukoo uliotokana na watoto wa Gerishoni walikuwa ni Libni na Shimei.
Also these are the names of the sonnes of Gershon by their families: Libni and Shimei.
19 Ukoo uliotokana na watoto Kohathi walikuwa ni Amramu na, Izihari, Hebroni, na Uzieli.
The sonnes also of Kohath by their families: Amram, and Izehar, Hebron, and Vzziel.
20 Ukoo uliotokana na watoto wa Merari walikuwa ni Mahili na Mushi. Hizi ndizo koo za Walawi, zilizoorodheshwa ukoo kwa ukoo.
And the sonnes of Merari by their families: Mahli and Mushi. These are the families of Leui, according to the houses of their fathers.
21 Koo za Walibini na Washimei zilitokana na Wagerishoni. Hizi ndizo koo za Wagerishoni.
Of Gershon came the familie of the Libnites, and the familie of the Shimeites: these are the families of the Gershonites.
22 Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa na kufikia idadi ya 7, 500.
The summe whereof (after the nomber of all the males from a moneth olde and aboue) was counted seuen thousand and fiue hundreth.
23 Koo za Wagerishoni watapanga upande wa magharibi wa hema.
The families of the Gershonites shall pitch behind the Tabernacle westward.
24 Eliasafu mwana wa Laeli ataongoza koo za uzao wa Wagerishoni.
The captaine and auncient of the house of the Gershonites shalbe Eliasaph the sonne of Lael.
25 Familia ya Gerishoni watalilinda hema la kukutania pamoja na hiyo masikani. Watalilinda hema, kifuniko chake, na lile pazia la lango la hema ya kukutania.
And the charge of the sonnes of Gershon in the Tabernacle of the Congregation shall be the Tabernacle, and the pauilion, the couering thereof, and the vaile of the dore of the Tabernacle of the Congregation,
26 Wataulinda ua, lile pazia la kwenye lango—ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu. Watazilinda kamba za hema ya kukutania na vyote vilivyomo.
And the hanging of the court, and the vaile of the doore of the court, which is neere the Tabernacle, and neere ye Altar round about, and the cordes of it for all the seruice thereof.
27 Koo zifuatazo zinatokana na Kohathi: ukoo wa Waamrami, ukoo wa Waizihari ukoo wa Wahebroni, na ukoo wa Wauzieli. Koo hizi zinatokana na Wakohathi.
And of Kohath came the familie of the Amramites, and the familie of the Izeharites, and the familie of the Hebronites, and the familie of the Vzzielites: these are the families of the Kohathites.
28 Wanaume 8, 600 wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa ili kulinda vitu vya BWANA.
The nomber of all the males from a moneth olde and aboue was eight thousand and sixe hundreth, hauing the charge of the Sanctuarie.
29 Familia ya uzao wa Kohathi watapanga upande wa kusini wa Hema.
The families of the sonnes of Kohath shall pitch on the Southside of the Tabernacle.
30 Elizafani mwana wa Uzieli ndiye atakayeongoza ukoo wa Wakohathi.
The captaine and auncient of the house, and families of the Kohathites shall be Elizaphan the sonne of Vzziel:
31 Watalilinda sanduku, meza, vikalishio vya taa, madhabahu, vitu vitakatifu ambvyo hutumika katika huduma yao, pazia, na kazi zote zinazoambatana na hema.
And their charge shalbe the Arke, and the Table, and the Candlesticke, and the altars, and the instruments of the Sanctuarie that they minister with, and the vaile, and all that serueth thereto.
32 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza wanaume wanaowaongoza Walawi. Atawasimamia wanaume wanaongoza eneo takatifu.
And Eleazar the sonne of Aaron the Priest shalbe chiefe captaine of the Leuites, hauing the ouersight of them that haue the charge of the Sanctuarie.
33 Koo mbili zimetoka kwa Merari: Ukoo wa Mahili na ukoo wa Mushi. Koo hizi zimetokana na Merari,
Of Merari came the familie of the Mahlites, and the familie of the Mushites: these are the families of Merari.
34 Wanaume 6, 200 wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi walihesabiwa.
And the summe of them, according to the nomber of all the males, from a moneth olde and aboue was sixe thousand and two hundreth.
35 Zurieli mwana wa Abihaili ataongoza ukoo wa Merari. Hawa watapanga upande wa kaskazini mwa hema.
The captaine and the ancient of the house of the families of Merari shalbe Zuriel the sonne of Abihail: they shall pitche on the Northside of the Tabernacle.
36 Uzao wa Merari utatunza mbao za hema, mataruma, nguzo, makalishio, viifaa vya ujenzi na vitu vyote vinavyohusika,
And in ye charge and custodie of the sonnes of Merari shall be the boardes of the Tabernacle, and the barres thereof, and his pillars, and his sockets, and al the instruments therof, and al that serueth thereto,
37 na nguzo za ua zinazozunguka hema, makalishio, vigingi na kamba zake.
With the pillars of the court round about, with their sockets, and their pins and their coardes.
38 Musa na Haruni na watoto wake watapanga upande wa mashariki wa masikani, mbele ya hema ya kukutania kuelekea mawio ya jua. Wao wataajibika na majukumu ya mahali patakatifu na majukumu ya wana wa Israeli. Mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe.
Also on the forefront of the Tabernacle toward the East, before the Tabernacle, I say, of the Congregation Eastwarde shall Moses and Aaron and his sonnes pitch, hauing the charge of the Sanctuarie, and the charge of the children of Israel: but the stranger that commeth neere, shall be slayne.
39 Musa na Haruni wakawahesabu wanaume wote wa ukoo wa Walawi walikuwa na umri wa mwezi mmoja na zaidi, kama vile BWANA alivyokuwa ameagiza. Walihesabu wanaume ishirini na mbili elfu.
The wholesumme of ye Leuites, which Moses and Aaron nombred at the commandement of the Lord throughout their families, euen al the males from a moneth olde and aboue, was two and twentie thousand.
40 BWANA alisema na Musa, “Wahesabu wanaume wote ambo ni wazaliwa wa kwanza wa Israeli ambao wana umri wa mwezi mmoja na zaidi. Orodhesha majina yao.
And the Lord said vnto Moses, Nomber all the first borne that are Males among the children of Israel, from a moneth old and aboue, and take the nomber of their names.
41 Unitwalie walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli, Mimi ndimi BWANA. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa uzao wa Israeli,”
And thou shalt take ye Leuites to me for all the first borne of the children of Israel (I am the Lord) and the cattell of the Leuites for all the first borne of the cattell of the children of Israel.
42 Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli kama BWANA alivyomwagiza kufanya.
And Moses nombred, as the Lord commanded him, all the first borne of the children of Israel.
43 Aliwahesabu wazaliwa wote wa kwanza kwa mjina, wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi. Alihesabu wanaume 22, 273.
And all the first borne males rehearsed by name (from a moneth olde and aboue) according to their nomber were two and twentie thousand, two hundreth seuentie and three.
44 Tena BWANA alinena na Musa. Akasema,
And the Lord spake vnto Moses, saying,
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa wana wa Israeli. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wanyama wa Waisreli wengine. Walawi ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.
Take the Leuites for all the first borne of the children of Israel, and the cattell of the Leuites for their cattel, and the Leuites shalbe mine, (I am the Lord)
46 Unikusanyie shekeli tano za wokovu kwa kila hao 273 za hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli za hao wanaozidi idadi ya Walawi.
And for the redeeming of the two hundreth seuentie and three, (which are moe then the Leuites) of the first borne of the children of of Israel,
47 Utazitumia hizo shekeli tano kwa kipimo cha mahali patakatifu. Shekeli moja ni sawa na gera ishirini.
Thou shalt also take fiue shekels for euery person: after the weight of the Sanctuarie shalt thou take it: ye shekel conteineth twenty gerahs.
48 Utawalipa hizo shekeli za wokovu kwa Haruni na wanawe.”
And thou shalt giue the money, wherwith the odde nomber of them is redeemed, vnto Aaron and to his sonnes.
49 Kwa hiyo Musa akakusanya shakeli za wokovu kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliookolewa na Walawi.
Thus Moses tooke the redemption of the that were redeemed, being more then the Leuites:
50 Musa akakusanya zile fedha kutoka kwa hao wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli. Alikusanya jumla ya shekeli 1, 365, zenye kipimo sawa na mahali patakatifu. Musa akamlipa Haruni na wanawe hizo shekeli za wokovu.
Of the first borne of the children of Israel tooke he the mony: eue a thousand three hundreth three score and fiue shekels after the shekel of the Sanctuarie.
51 Musa akafanya kila kitu alichoagizwa na neno la BWANA kama BWANA alivyomwagiza.
And Moses gaue the money of them that were redeemed, vnto Aaron and to his sonnes according to the word of the Lord, as the Lord had commanded Moses.

< Hesabu 3 >