< Hesabu 29 >

1 Katika siku ya kwanza, ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA. Katika siku hiyo hamtafanya kazi zenu za kila siku. Itakuwa siku ya kupiga matarumbeta.
“And in the seventh month, on the first of the month, you have a holy convocation; you do no servile work; it is a day of shouting to you;
2 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ya kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari mchanga, kondoo dume mmoja na wanakondoo dume saba wa mwaka mmoja, kila mmoja mkamilifu.
and you have prepared a burnt-offering for refreshing fragrance to YHWH: one bullock, a son of the herd, one ram, seven lambs, sons of a year, perfect ones;
3 Pamoja na hao mtatoa sadaka ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa ajili ya huyo fahari, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya huyo kondoo mume,
and their present of flour mixed with oil: three-tenth parts for the bullock, two-tenth parts for the ram,
4 na sehemu ya kumi ya kila hao wanakondoo waume saba.
and one-tenth part for one lamb, for the seven lambs;
5 Na mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
and one kid of the goats [for] a sin-offering, to make atonement for you;
6 Toeni hizo sadaka katika mwezi wa saba kama nyongeza ya sadaka mtakazotoa kila mwanzo wa kila mwezi: pamoja na sadaka maalumu za kuteketezwa na sadaka za unga. Hizi zitakuwa nyongeza za sadaka za kuteketezwa za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji. Utakapokuwa ukiendelea na sadaka hizi, utakuwa ukitii kile kilichoamriwa kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa BWANA.
apart from the burnt-offering of the month and its present, and the continual burnt-offering and its present, and their drink-offerings, according to their ordinance, for refreshing fragrance, a fire-offering to YHWH.
7 Siku ya kumi ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA. Mtajinyeneyekeza na hamtafanya kazi.
And on the tenth of this seventh month you have a holy convocation, and you have humbled your souls; you do no work;
8 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari mmoja mchanga ili kutoa harufu nzuri, kondoo mmoja mume, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja. Wote wakamilifu.
and you have brought a burnt-offering near to YHWH, a refreshing fragrance: one bullock, a son of the herd, one ram, seven lambs, sons of a year; they are perfect ones for you;
9 Pamoja na sadaka hizo utatoa sadaka ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa ajili ya fahari, sehemu mbili za kumi za kondoo dume mmoja,
and their present of flour mixed with oil: three-tenth parts for the bullock, two-tenth parts for one ram,
10 na sehemu ya kumi ya efa moja kwa kila mwanakondoo wale saba.
a tenth—a tenth part for one lamb, for the seven lambs,
11 Mtatatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya upatanisho. Hii itakuwa sadaka ya nyongeza ya upatanisho, ya sadaka ya kila siku ya kuteketezwa, pamoja na sadaka za unga, na sadaka zake za vinywaji.
one kid of the goats [for] a sin-offering, apart from the sin-offering of the atonements, and the continual burnt-offering and its present, and their drink-offerings.
12 Siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu lakumwabudu BWANA. Siku hiyo hamtafanya kazi za kila siku, na mtazitunza hizo sikukuu kwa muda wa siku saba kwa ajili ya BWANA.
And on the fifteenth day of the seventh month you have a holy convocation; you do no servile work; and you have celebrated a festival to YHWH [for] seven days,
13 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ilikutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa mafahari wachanga kumi na tatu, kondoo waume wawili, na wanakondoo waume kumi na nne wa mwaka mmoja. Wote wakamilifu.
and have brought a burnt-offering near, a fire-offering of refreshing fragrance, to YHWH: thirteen bullocks, sons of the herd, two rams, fourteen lambs, sons of a year; they are perfect ones;
14 Pamoja na hao mtatoa sadaka ya unga, unga mwembaba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa kila fahari katika hao kumi na tatu, sehemu mbili za kumi kwa kila hao kondoo dume wawili,
and their present of flour mixed with oil: three-tenth parts for one bullock, for the thirteen bullocks, two-tenth parts for one ram, for the two rams,
15 na sehemu ya kumi ya efa ya hao wanakondoo kumi na nne.
and a tenth—a tenth part for one lamb, for the fourteen lambs;
16 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kuteketezwa, sadaka yake ya unga, pamoja na sadaka za vinywaji.
and one kid of the goats [for] a sin-offering, apart from the continual burnt-offering, its present, and its drink-offering.
17 Siku ya pili ya kusanyiko, mtatoa mafahari kumi na mbili, kondoo dume wawili na wanakondoo dume kumi na mbili wa umri wa mwaka mmoja, wote wakamilifu.
And on the second day: twelve bullocks, sons of the herd, two rams, fourteen lambs, sons of a year, perfect ones;
18 Pamoja nao mtatoa sadaka ya unga, na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, kondoo dume, na kwa ajili ya wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilvyoamriwa.
and their present and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the sheep, in their number, according to the ordinance;
19 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kuwa nyongeza ya sadaka za kila siku, sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji.
and one kid of the goats [for] a sin-offering, apart from the continual burnt-offering, and its present, and their drink-offerings.
20 Siku ya tatu ya kusanyiko, mtatoa sadaka mafahari kumi na moja, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa umri wa mwaka mmoja, wakamilifu.
And on the third day: eleven bullocks, two rams, fourteen lambs, sons of a year, perfect ones;
21 Pamoja na hizo sadaka mtatoa sadaka ya unga na sdaka ya vinywaji kwa wale mafahari, kwa wale kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, utoe sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
and their present and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, in their number, according to the ordinance;
22 Mtatoa sadaka beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya zile sadaka za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
and one goat [for] a sin-offering, apart from the continual burnt-offering, and its present, and its drink-offering.
23 Siku ya nne ya kusanyiko, mtatoa mafahari kumi, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
And on the fourth day: ten bullocks, two rams, fourteen lambs, sons of a year, perfect ones;
24 Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga na sdaka za vinywaji kwa wale mafahari, na kwa wale kondoo dume na kwa wale wanakodoo, mtatoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
their present and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, in their number, according to the ordinance;
25 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kuwa nyongeza ya sadaka za kuteketezwa za kila siku, sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji
and one kid of the goats [for] a sin-offering, apart from the continual burnt-offering, its present, and its drink-offering.
26 Siku ya tano ya kusanyiko, mtatoa mafahari tisa, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
And on the fifth day: nine bullocks, two rams, fourteen lambs, sons of a year, perfect ones;
27 Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, kondoo dume, na wale wanakondoo, mkitoa sdaka nyingi kama ilivyoamriwa.
and their present and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, in their number, according to the ordinance;
28 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kuteketezwa za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka za vinywaji.
and one goat [for] a sin-offering, apart from the continual burnt-offering, and its present, and its drink-offering.
29 Siku ya sita ya kusanyiko, mtatoa mafahari wanane, kondoo dume wawili, na wanakondoo kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
And on the sixth day: eight bullocks, two rams, fourteen lambs, sons of a year, perfect ones;
30 Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga nasadaka za vinywaji kwa wale mafahari, kondoo wa dume na wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
and their present and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, in their number, according to the ordinance;
31 Mtatoa beberu kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kila siku za kuteketezwa, sadaka zadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
and one goat [for] a sin-offering, apart from the continual burnt-offering, its present, and its drink-offering.
32 Siku ya saba ya kusanyiko, mtatoa mafahari saba, kondoo dume saba, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
And on the seventh day: seven bullocks, two rams, fourteen lambs, sons of a year, perfect ones;
33 Pamoja nao mtataengeneza sadaka ya unga na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, na kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
and their present and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, in their number, according to the ordinance;
34 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka ya kuteketezwa ya kila siku, na sadaka yake ya unga, na sadaka yake ya vinywaji.
and one goat [for] a sin-offering, apart from the continual burnt-offering, its present, and its drink-offering.
35 Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko lingine makini. Hamtafanya kazi zenu za kila siku.
On the eighth day you have a restraint; you do no servile work;
36 Mtafanya sadaka za kuteketezwa, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari mmoja, kondoo mmoja dume, na wanakondoo saba dume wa umri wa mwaka mmoja, wakamilifu.
and you have brought a burnt-offering near, a fire-offering of refreshing fragrance, to YHWH: one bullock, one ram, seven lambs, sons of a year, perfect ones;
37 Mtatoa sadaka zake za unga na sadaka zake za vinywaji kwa ajili ya yule fahari, kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, mkifanya sadaka nyingi kadri ilivyoamriwa.
their present and their drink-offerings for the bullock, for the ram, and for the lambs, in their number, according to the ordinance;
38 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
and one goat [for] a sin-offering, apart from the continual burnt-offering, and its present, and its drink-offering.
39 Hivi ndivyo utakavyotoa sadaka kwa BWANA katika sikukuu zenu za kila mwaka. Hivi vitakuwa nyongeza ya viapo vyenu na sadaka zenu za hiari. Mtavitoa hivi kama sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za unga, sadaka za vinywaji, na sadaka za amani.”
You prepare these to YHWH in your appointed times—apart from your vows and your free-will offerings—for your burnt-offerings, and for your presents, and for your drink-offerings, and for your peace-offerings.”
40 Musa aliwaambia wana wa Israeli kila kitu ambacho BWANA alikuwa amemwamuru kusema.
And Moses speaks to the sons of Israel according to all that YHWH has commanded Moses.

< Hesabu 29 >