< Hesabu 28 >
1 BWANA akanena na Musa akamwambia,
Yahvé habló a Moisés, diciendo:
2 “Waamuru wana wa Isrseli uwaambie, 'Mtanitolea sadaka kwa wakati uliopangwa, chakula cha sadaka yangu kilichotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa ajili yangu.
“Ordena a los hijos de Israel y diles: ‘Procuren presentar mi ofrenda, mi alimento para mis ofrendas encendidas, como aroma agradable para mí, a su debido tiempo’.
3 Pia uwaambie, 'Hii ni sadaka iliyotengenezwa kwa moto ambayo mtaitoa kwa BWANA- mwanakondoo dume wa mwaka mmoja asiyekuwa na waa, wawili kila siku kuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku.
Les dirás: ‘Esta es la ofrenda encendida que ofrecerás a Yahvé: corderos machos de un año sin defecto, dos al día, para un holocausto continuo.
4 Mwanakodoo mmoja atatolewa sadaka asubuhi, na mwingine atatolewa sadaka jioni.
Ofrecerás un cordero por la mañana, y ofrecerás el otro cordero al atardecer,
5 Mtatoa sadaka ya sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa.
con la décima parte de un efa de harina fina como ofrenda, mezclada con la cuarta parte de un hin de aceite batido.
6 Hii ni sadaka ya ya kuteketezwa ya kila siku iliyoamriwa mlima Sinai ili kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili ya BWANA.
Es un holocausto continuo que fue ordenado en el monte Sinaí como aroma agradable, una ofrenda hecha por fuego a Yahvé.
7 Pamoja na robo ya hini ya sadaka ya kinywaji kwa mmoja wa hao wanakondoo. Utaimimina mahali patakatifu hiyo sadaka ya kinywaji kwa BWANA.
Su libación será la cuarta parte de un hin por cada cordero. Derramarás una libación de bebida fuerte a Yahvé en el lugar santo.
8 Yule mwanakondoo mwingine utamtoa sadaka jioni pamoja na sadaka ya unga kama kama yule wa asubuhi alivyotolewa. Pia utatoa tena sadaka ya kinywaji pamoja naye, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA.
El otro cordero lo ofrecerás al atardecer. Como la ofrenda de la mañana, y como su libación, lo ofrecerás, ofrenda encendida, como aroma agradable a Yahvé.
9 Katika siku ya Sabato utatoa wanakondoo dume wawili, wa umri wa mwaka mmoja kila mmoja wasiokuwa na dosari, na sehemu ya kumi mbili ya efa ya unga mwembamba kwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, pamoja na sadaka ya kinywaji.
“‘En el día de reposo, ofrecerás dos corderos machos de un año sin defecto, y dos décimas de efa de harina fina como ofrenda mezclada con aceite, y su libación:
10 Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa kila siku ya Sabato, kama nyongeza ya ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya kinywaji.
Este es el holocausto de cada sábado, además del holocausto continuo y su libación.
11 Kila mwanzo wa mwezi, mtatoa sadaka za kuteketezwa kwa BWANA. Utatoa sadaka ya fahari wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari.
“‘En los comienzos de tus meses, ofrecerás un holocausto a Yahvé dos novillos, un carnero, siete corderos machos de un año sin defecto,
12 Pia mtatoa sehemu ya kumi tatu ya efa unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari, na sehemu za kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa yule kondoo mume mmoja.
y tres décimas de un efa de harina fina para un holocausto mezclado con aceite, para cada toro; y dos décimas de harina fina para un holocausto mezclado con aceite, para el único carnero;
13 Pia mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga kwa kila mwanakondoo. Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa, ya kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajilI ya BWANA.
y una décima de harina fina mezclada con aceite para un holocausto a cada cordero, como ofrenda quemada de aroma agradable, ofrenda hecha por fuego a Yahvé.
14 Sadaka ya kinywaji ya watu itakuwa nusu ya hini ya divai ya yule fahari, sehemu ya tatu ya hini ya kondoo dume, na robo ya hini ya mwanakondoo. Hii ndiyo itakuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi kwa miezi yote ya mwaka.
Sus libaciones serán la mitad de un hin de vino para el becerro, la tercera parte de un hin para el carnero y la cuarta parte de un hin para el becerro. Este es el holocausto de cada mes durante todos los meses del año.
15 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kwa BWANA. Hii itakuwa nyongeza kwa ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya viinywaji.
También se ofrecerá un macho cabrío como ofrenda por el pecado a Yahvé, además del holocausto continuo y su libación.
16 Katika siku kumi na nne, ya mwezi wa kwanza itakuwa Pasaka ya BWANA.
“‘En el primer mes, el día catorce del mes, es la Pascua de Yahvé.
17 Katika sku ya kumi na tano ya mwezi huu kutakuwa na sikukuu. Mtakuka mikate isiyo na chachu kwa siku saba.
El decimoquinto día de este mes habrá una fiesta. Se comerá pan sin levadura durante siete días.
18 Katika siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA. Katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku
En el primer día habrá una santa convocación. No harás ningún trabajo regular,
19 Hata hivyo, mtatoa sadaka iliyotengenezwa kwa moto, sadaka ya kuteketezwa kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari wawili, kondoo dume mmoja, na kondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wakamilifu.
sino que ofrecerás una ofrenda encendida, un holocausto a Yahvé: dos novillos, un carnero y siete corderos de un año. Serán sin defecto,
20 Pamoja na yule fahari, mtatoa sadaka sehemu za tatu efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, pamoja na yule kondoo mume sehemu za pili za kumi.
con su ofrenda de harina, harina fina mezclada con aceite. Ofrecerás tres décimas por el becerro, y dos décimas por el carnero.
21 Kwa kila wale wanakondoo saba, mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta,
Ofrecerás una décima por cada cordero de los siete corderos;
22 na beberu mmoja kuwa sdaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
y un macho cabrío como ofrenda por el pecado, para hacer expiación por ti.
23 Mtotoa hivi vitu kama sadaka ya nyongeza katika ile sadaka ya kila siku inayotakiwa kila asubuhi.
Los ofrecerás además del holocausto de la mañana, que es un holocausto continuo.
24 Kama ilivyofafanuliwa hapa, mtatoa sadaka hizi kila siku, kwa zile siku saba za Pasaka, kile chakula cha sadaka kilichotengenezwa kwa moto kuwa harufu nzuri kwa BWANA. Hiki kitatolewa kuwa sadaka ya nyongeza ya ile sadaka ya kuteketezwa na pamoja na ile sadaka ya vinywaji.
Así ofrecerás cada día, durante siete días, el alimento de la ofrenda encendida, de aroma agradable para Yahvé. Se ofrecerá además del holocausto continuo y su libación.
25 Siku ya saba mtakuwa na kusanyiko takatifu ili kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye zile kazi zenu zakila siku.
El séptimo día tendréis una santa convocación. No harás ningún trabajo regular.
26 Pia katika siku ya malimbuko, mtakapokuwa mnatoa sadaka ya unga mpya katika sikukuu zenu za Majuma, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku.
“‘También en el día de las primicias, cuando ofrezcas una nueva ofrenda a Yahvé en tu fiesta de las semanas, tendrás una santa convocación. No harás ningún trabajo regular;
27 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari wawili wachanga, kondoo mume mmoja, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja.
sino que ofrecerás un holocausto como aroma agradable a Yahvé: dos novillos, un carnero, siete corderos macho de un año;
28 Pamoja na hiyo mtatoa sadaka ya unga: unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari na sehemu kumi mbili za yule kondoo mume.
y su ofrenda de harina fina mezclada con aceite, tres décimas por cada becerro, dos décimas por el único carnero,
29 Toeni sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila wale wanakondoo saba,
una décima por cada cordero de los siete corderos;
30 na beberu mmoja ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
y un macho cabrío, para hacer expiación por ti.
31 Mtakapotoa hao wanyama wasio na dosari, pamoja na sadaka zake za vinywaji, hii itakuwa sadaka ya nyongeza katika zile sadaka za kila siku na pamoja na zile sadaka za unga.'”
Además del holocausto continuo y su ofrenda de comida, los ofrecerás junto con sus libaciones. Procura que sean sin defecto.