< Hesabu 28 >

1 BWANA akanena na Musa akamwambia,
Le Seigneur dit aussi à Moïse:
2 “Waamuru wana wa Isrseli uwaambie, 'Mtanitolea sadaka kwa wakati uliopangwa, chakula cha sadaka yangu kilichotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa ajili yangu.
Ordonne aux enfants d’Israël, et tu leur diras: Offrez en leurs temps mon oblation, les pains et le sacrifice consumé par le feu d’une odeur très suave.
3 Pia uwaambie, 'Hii ni sadaka iliyotengenezwa kwa moto ambayo mtaitoa kwa BWANA- mwanakondoo dume wa mwaka mmoja asiyekuwa na waa, wawili kila siku kuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku.
Voici les sacrifices que vous devez offrir: deux agneaux d’un an, sans tache, tous les jours, en holocauste perpétuel;
4 Mwanakodoo mmoja atatolewa sadaka asubuhi, na mwingine atatolewa sadaka jioni.
Vous en offrirez un le matin, et l’autre vers le soir:
5 Mtatoa sadaka ya sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa.
La dixième partie d’un éphi de fleur de farine, qui soit arrosée d’huile très pure, et de la quatrième partie du hin.
6 Hii ni sadaka ya ya kuteketezwa ya kila siku iliyoamriwa mlima Sinai ili kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili ya BWANA.
C’est l’holocauste perpétuel que vous avez offert sur la montagne de Sinaï, en odeur très suave d’un sacrifice au Seigneur, consumé par le feu.
7 Pamoja na robo ya hini ya sadaka ya kinywaji kwa mmoja wa hao wanakondoo. Utaimimina mahali patakatifu hiyo sadaka ya kinywaji kwa BWANA.
Et vous répandrez en libations la quatrième partie d’un hin de vin pour chaque agneau, dans le sanctuaire du Seigneur.
8 Yule mwanakondoo mwingine utamtoa sadaka jioni pamoja na sadaka ya unga kama kama yule wa asubuhi alivyotolewa. Pia utatoa tena sadaka ya kinywaji pamoja naye, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA.
Et l’autre agneau, vous l’offrirez de même vers le soir, selon tout le rite du sacrifice du matin, et de ses libations: oblation d’une très suave odeur pour le Seigneur.
9 Katika siku ya Sabato utatoa wanakondoo dume wawili, wa umri wa mwaka mmoja kila mmoja wasiokuwa na dosari, na sehemu ya kumi mbili ya efa ya unga mwembamba kwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, pamoja na sadaka ya kinywaji.
Mais au jour du sabbat, vous offrirez deux agneaux d’un an, sans tache, et deux décimes de fleur de farine, arrosée d’huile, pour le sacrifice, et les libations,
10 Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa kila siku ya Sabato, kama nyongeza ya ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya kinywaji.
Qui, selon les rites, sont répandues à chaque sabbat en holocauste perpétuel.
11 Kila mwanzo wa mwezi, mtatoa sadaka za kuteketezwa kwa BWANA. Utatoa sadaka ya fahari wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari.
Mais aux calendes, vous offrirez un holocauste au Seigneur: deux veaux pris d’un troupeau, un bélier, sept agneaux d’un an, sans tache,
12 Pia mtatoa sehemu ya kumi tatu ya efa unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari, na sehemu za kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa yule kondoo mume mmoja.
Et trois décimes de fleur de farine, arrosée d’huile, pour le sacrifice de chaque veau, et deux décimes de fleur de farine, arrosée d’huile, pour chaque bélier;
13 Pia mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga kwa kila mwanakondoo. Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa, ya kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajilI ya BWANA.
Et la décime d’une décime de fleur de farine avec de l’huile, pour le sacrifice de chaque agneau: holocauste d’une très suave odeur et d’un sacrifice au Seigneur consumé par le feu.
14 Sadaka ya kinywaji ya watu itakuwa nusu ya hini ya divai ya yule fahari, sehemu ya tatu ya hini ya kondoo dume, na robo ya hini ya mwanakondoo. Hii ndiyo itakuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi kwa miezi yote ya mwaka.
Quant aux libations de vin qui doivent être répandues pour chaque victime, les voici: la moitié du hin pour chaque veau, la troisième partie pour le bélier, la quatrième pour l’agneau: ce sera là un holocauste pour tous les mois qui se succèdent dans le cours de l’année.
15 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kwa BWANA. Hii itakuwa nyongeza kwa ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya viinywaji.
Un bouc aussi sera offert au Seigneur pour les péchés en holocauste perpétuel avec ses libations.
16 Katika siku kumi na nne, ya mwezi wa kwanza itakuwa Pasaka ya BWANA.
Mais au premier mois, au quatorzième jour du mois, sera la Pâque du Seigneur,
17 Katika sku ya kumi na tano ya mwezi huu kutakuwa na sikukuu. Mtakuka mikate isiyo na chachu kwa siku saba.
Et au quinzième jour, la solennité: pendant sept jours on mangera des azymes.
18 Katika siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA. Katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku
Le premier de ces jours sera vénérable et saint: vous ne ferez aucune œuvre servile en ce jour,
19 Hata hivyo, mtatoa sadaka iliyotengenezwa kwa moto, sadaka ya kuteketezwa kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari wawili, kondoo dume mmoja, na kondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wakamilifu.
Et vous offrirez un sacrifice holocauste au Seigneur: deux veaux pris d’un troupeau, un bélier, sept agneaux d’un an, sans tache;
20 Pamoja na yule fahari, mtatoa sadaka sehemu za tatu efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, pamoja na yule kondoo mume sehemu za pili za kumi.
Et les offrandes pour chacun, de fleur de farine qui soit arrosée d’huile, trois décimes pour chaque veau et deux décimes pour le bélier;
21 Kwa kila wale wanakondoo saba, mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta,
Et la décime d’une décime pour chaque agneau, c’est-à-dire, pour sept agneaux.
22 na beberu mmoja kuwa sdaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
Et un bouc pour le péché afin qu’il serve d’expiation pour vous;
23 Mtotoa hivi vitu kama sadaka ya nyongeza katika ile sadaka ya kila siku inayotakiwa kila asubuhi.
Outre l’holocauste du matin, que vous offrirez toujours.
24 Kama ilivyofafanuliwa hapa, mtatoa sadaka hizi kila siku, kwa zile siku saba za Pasaka, kile chakula cha sadaka kilichotengenezwa kwa moto kuwa harufu nzuri kwa BWANA. Hiki kitatolewa kuwa sadaka ya nyongeza ya ile sadaka ya kuteketezwa na pamoja na ile sadaka ya vinywaji.
C’est ainsi que vous ferez à chaque jour des sept jours pour l’entretien du feu, et en odeur très suave pour le Seigneur, laquelle s’élèvera de l’holocauste et des libations de chaque victime.
25 Siku ya saba mtakuwa na kusanyiko takatifu ili kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye zile kazi zenu zakila siku.
Le septième jour sera aussi très solennel et saint pour vous: vous ne ferez aucune œuvre servile en ce jour.
26 Pia katika siku ya malimbuko, mtakapokuwa mnatoa sadaka ya unga mpya katika sikukuu zenu za Majuma, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku.
De même, le jour des prémices, quand vous offrirez les nouveaux grains au Seigneur, les semaines étant accomplies, sera vénérable et saint: vous ne ferez aucune œuvre servile en ce jour.
27 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari wawili wachanga, kondoo mume mmoja, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja.
Et vous offrirez un holocauste en odeur très suave pour le Seigneur: deux veaux pris d’un troupeau, un bélier, et sept agneaux d’un an, sans tache;
28 Pamoja na hiyo mtatoa sadaka ya unga: unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari na sehemu kumi mbili za yule kondoo mume.
Et pour les oblations qui les accompagnent, trois décimes de fleur de farine, arrosée d’huile, pour chaque veau, deux pour les béliers,
29 Toeni sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila wale wanakondoo saba,
La décime d’une décime, pour les agneaux, qui font ensemble sept agneaux; et un bouc,
30 na beberu mmoja ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
Qui est immolé pour l’expiation, outre l’holocauste perpétuel et ses libations.
31 Mtakapotoa hao wanyama wasio na dosari, pamoja na sadaka zake za vinywaji, hii itakuwa sadaka ya nyongeza katika zile sadaka za kila siku na pamoja na zile sadaka za unga.'”
Vous offrirez sans tache toutes ces victimes avec leurs libations.

< Hesabu 28 >