< Hesabu 26 >

1 Ilitokea baada ya tauni ambayo BWANA alimwambia Musa na Eliazari mwana wa Haruni kuhani, Alisema,
After the plague was over, the Lord told Moses and Eleazar son of Aaron the priest,
2 Wahesabu watu wote wa Israeli, kuanzia miaka ishirini na zaidi, kwa jamaa ya familia zao wote ambao wanaweza kwenda kwenye vita kwa ajili ya Israeli.”
“Census all the Israelites by family—all those twenty years of age or older who are eligible for military service in the army of Israel.”
3 Kwa hiyo Musa na Eliazari kuhani wakawaambia katika uwanda wa Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko na kusema,
There on the plains of Moab beside the Jordan opposite Jericho, Moses and Eleazar the priest gave the order,
4 Wahesabuni watu, kuanzi umri wa miaka ishirini na zaidi kama BWANA alivyomwamuru Musa na watu wa Israeli walitoka katika nchi ya Misri.”
“Census the men twenty years of age or older, following the instructions the Lord gave to Moses.” The following is the genealogical record of those who left the land of Egypt.
5 Reubeni ndiye aliyekuwa wa kwanza, Kutoka kwa mwana wake Hanoki ulitokea ukoo wa Wahanoki. Kutoka kwa Palu ulitokea ukoo wa Wapalu.
These were the descendants of Reuben, Israel's firstborn: Hanoch, ancestor of the Hanochite family; Pallu, ancestor of the Palluite family;
6 Kutoka Hezroni. ulitokea ukoo wa Wahezroni. Kutoka kwa Kami ulitokea ukoo wa Wakami.
Hezron, ancestor of the Hezronite family; and Carmi, ancestor of the Carmite family.
7 Hizi ndizo zilikuwa koo za uzao wa Reubeni, ambzo idadi yao ilikuwa wanaume 43, 730.
These were the families descended from Reuben and they numbered 43,730.
8 Eliabu alikuwa mwana wa Palu.
Pallu's son was Eliab,
9 Wana wa Eliabu walikuwa ni Nemueli, Dathani. na Abiramu. Hawa ni walewale Dathani na Abiramu waliomfuata Kora waliompinga Musa na Haruni na kumpinga BWANA.
and Eliab's sons were Nemuel, Dathan, and Abiram. (It was Dathan and Abiram, leaders chosen by the Israelites, who joined the rebellion against Moses and Aaron with the followers of Korah when they rebelled against the Lord.
10 Pale ambapo dunia ilifungua kinywa na kuwameza pamoja na Kora wakati ambapo wafuasi wa Kora walikufa. Wakati ule, moto uliteketeza wanaume 250, amboa wlikuwa ishara ya onyo.
The earth opened up and swallowed them down, along with Korah. His followers died when the fire burned up 250 men. What happened to them was a warning to the Israelites.
11 Lakini uzao wa Kora haukufa.
But Korah's sons didn't die.)
12 Ukoo wa uzao wa Simeoni walikuwa hawa wafuatao: Kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli, kwa Jamini, ukoo wa Wajamini, kwa Jakini, ukoo wa Wajakini,
These were the descendants of Simeon by family: Nemuel, ancestor of the Nemuelite family; Jamin, ancestor of the Jaminite family; Jachin, ancestor of the Jachinite family;
13 kwa Zera, ukoo wa Wazera, kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
Zerah, ancestor of the Zerahite family; and Shaul, ancestor of the Shaulite family.
14 Hizi ndizo koo za uzao wa Simeoni, idadi yao ilikuwa wanaume 22, 200.
These were the families descended from Simeon and they numbered 22,200.
15 Koo za uzao wa Gadi zilikuwa hizi: Kwa Zefoni, Ukoo wa Wazefoni, kwa Hagi, ukoo wa Wahagi, kwa Shuni, ukoo wa Washuni,
These were the descendants of Gad by family: Zephon, ancestor of the Zephonite family; Haggi, ancestor of the Haggite family; Shuni, ancestor of the Shunite family;
16 kwa Ozini, ukoo wa Waozini, kwa Eri, ukoo wa Waeri,
Ozni, ancestor of the Oznite family; Eri, ancestor of the Erite family;
17 kwa Arodi, ukoo wa Waarodi, kwa Areli, ukoo wa Waareli.
Arod, ancestor of the Arodite family; Areli, ancestor of the Arelite family.
18 Hizi ndizo koo za uzao wa Gadi, idadi yao walikuwa wanaume 40, 500.
These were the families descended from Gad and they numbered 40,500.
19 Wana wa Yuda walikwa Er na Onani, lakini hawa walifia katika nchi ya Kanaani.
The sons of Judah who died in Canaan were Er and Onan. These were the descendants of Judah by family:
20 Koo zingine za uzao wa Yuda zilikuwa hizi: Kwa Shela, ukoo wa Washela, kwa Perezi, ukoo wa Waperezi, na kwa Zera, ukoo wa Wazera.
Shelah, ancestor of the Shelanite family; Perez, ancestor of the Perezite family; Zerah, ancestor of the Zerahite family.
21 Uzao wa Perezi walikuwa hawa: Kwa Hezroni, ukoo wa Wahezroni, kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
These were the descendants of Perez: Hezron, ancestor of the Hezronite family; and Hamul, ancestor of the Hamulite family.
22 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda, idadi yao ilikuwa wanaume 76, 500.
These were the families descended from Judah and they numbered 76,500.
23 Koo za uzao wa Isakari zilikuwa hizi: Kwa Tola, ukoo wa Watola, kwa Puva, ukoo wa Wapuva,
These were the descendants of Issachar by family: Tola, ancestor of the Tolaite family; Puvah, ancestor of the Punite family;
24 kwa Jashubu, ukoo wa Wajashubu, kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
Jashub, ancestor of the Jashubite family; and Shimron, ancestor of the Shimronite family.
25 Hizi ndizo zilikuwa koo za Isakari, Idadi yao ilikuwa wanaume 64, 300.
These were the families descended from Isaachar and they numbered 64,300.
26 Koo za uzao wa Zabuloni zilikuwa hizi: Kwa Seredi, ukoo wa Waseredi, kwa Eloni, ukoo wa Waeloni, kwa Jahaleeli, ukoo wa Wajahaleeli.
These were the descendants of Zebulun by family: Sered, ancestor of the Seredite family; Elon, ancestor of the Elonite family; and Jahleel, ancestor of the Jahleelite family.
27 Hizi ndizo zilikuwa koo za Zabuloni, idadi y ao ilikuwa wanaume 60, 500.
These were the families descended from Zebulun, and they numbered 60, 500.
28 Koo za uzao wa Ysufu zilikuwa Manase na Efraimu.
These were descendants of Joseph by family through Manasseh and Ephraim:
29 Huu ndio uliokuwa uzao wa Manase: Kwa Machiri, ukoo wa Wamachiri (Machiri ndiye aliyekuwa baba wa Giliedi), kwa Giliedi, ukoo wa Wagiliedi.
The descendants of Manasseh: Machir (he was the father of Gilead), ancestor of the Machirite family; and Gilead, ancestor of the Gileadite family.
30 Wazo wa Giliedi walikuwa hawa wfuatao: Kwa Lezeri, ukoo wa Walezeri, kwa Helweki, ukoo wa Waheleki, kwa Asrieli,
The descendants of Gilead: Izer, ancestor of the Iezerite family; Helek, ancestor of the Helekite family;
31 ukoo wa Asrieli wa Waasrieli, kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu,
Asriel, ancestor of the Asrielite family; Shechem, ancestor of the Shechemite family;
32 kwa Shemida, ukoo wa Washemida, kwa Hefa, ukoo wa Wahefa.
Shemida, ancestor of the Shemidaite family; and Hepher, ancestor of the Hepherite family.
33 Zelofehadi mwana wa Hefa hakuwa na watoto wa kiume bali alikuwa na mabinti. Majina ya binti zake yalikuwa Mahilahi, Noha, Hoglaha, Milika, na Tiriza.
(Zelophehad, son of Hepher, didn't have any sons, only daughters. Their names were Mahlah, Noah, Hoglah, Milcah, and Tirzah.)
34 Hizi ndizo koo za Manase, idadi yao ilikuwa wanaume 52, 700.
These were the families descended from Manasseh, and they numbered 52,700.
35 Koo za wana wa uzao wa Efraimu zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Shuthelaha, ukoo wa Washutheleha, kwa Becheri, ukoo wa Wabecheri, kwa Tahana, ukoo wa Watahana.
These were the descendants of Ephraim by family: Shuthelah, ancestor of the Shuthelahite family; Becher, ancestor of the Becherite family; and Tahan, ancestor of the Tahanite family.
36 Uzao wa Shuthelaha walikuwa, kwa Erani, ukoo wa Waerani.
The descendant of Shuthelah was Eran, ancestor of the Eranite family.
37 Hizi ndizo koo za uzao wa Efraimu, idadi yao ilikuwa wanaume 32, 500. Huu ndio uzao wa Yusufu, uliohesabiwa toka kila koo zao.
These were the families descended from Ephraim, and they numbered 32,500. These families were the descendants of Joseph.
38 Koo za uzao wa Benjamini zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Bela ukoo wa Wabela, kwa Ashibeli, ukoo wa Washibeli, kwa Ahiramu, ukoo wa Wahiramu,
These were the descendants of Benjamin by family: Bela, ancestor of the Belaite family; Ashbel, ancestor of the Ashbelite family; Ahiram, ancestor of the Ahiramite family;
39 kwa Shefufamu, ukoo wa Washefumamu, kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
Shupham, ancestor of the Shuphamite family; and Hupham, ancestor of the Huphamite family.
40 Wana wa Bela walikuwa ni Ardi na Naamani. Kutoka kwa Ardi ulijitokeza ukoo wa Waardi, na kutoka kwa Naamani ukajaitokeza ukoo wa Wanaamani.
The descendants of Bela were Ard, ancestor of the Ardite family; and Naaman, ancestor of the Naamite family.
41 Hizi ndizo koo za uzao wa Benjamini. Idadai yao ilikuwa wanaume 45, 600.
These were the families descended from Benjamin, and they numbered 45,600.
42 Kooo za uzao wa Dani zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo koo za uzao wa Dani.
These were the descendants of Dan by family: Shuham, ancestor of the Shuhamite families.
43 Idadi ya koo zote za Washuhamu ilikuwa wanaume 64, 400.
They were all Shuhamite families, and they numbered 64,400.
44 Koo za uzao wa Asheri zilikuwa zifuatazo: Kwa Imna, ukoo wa Waimna, kwa Ishvi, ukoo wa Waishivi, kwa Beria, ukoo wa Waberia.
These were the descendants of Asher by family: Imnah, ancestor of the Imnite family; Ishvi, ancestor of the Ishvite family; and Beriah, ancestor of the Beriite family.
45 Uzao wa Beria walikuwa hawa: Kwa Heberi, ukoo wa Waheberi, kwa Malikieli, ukoo wa Wamalikieli.
The descendants of Beriah were Heber, ancestor of the Heberite family; and Malchiel, ancestor of the Malchielite family.
46 Jina la binti wa Asheri lilikuwa Sera.
The name of Asher's daughter was Serah.
47 Hizi ndizo koo za uzao wa Asheri, idadi yao ilikuwa wanaume 53, 400.
These were the families descended from Asher, and they numbered 53,400.
48 Koo za uzao wa Naftali zilikuwa zifuatazo: Kwa Jahazeeli, ukoo wa Wajahazeel, kwa Guni, ukoo wa Waguni,
These were the descendants of Naphtali by family: Jahzeel, ancestor of the Jahzeelite family; Guni, ancestor of the Gunite family;
49 kwa Jezeri, ukoo wa Wajezeri, kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
Jezer, ancestor of the Jezerite family; and Shillem, ancestor of the Sheillemite family.
50 Hizi ndizo zilizokuwa koo za uzao wa Naftali, idadi yao walikuwa wanaume 45, 000.
These were the families descended from Naphtali, and they numbered 45,400.
51 Hii ndiyo iliyokuwa jumla kuu ya wanaume wa Israeli: 601, 730.
The total of all those counted was 601,730.
52 BWANA akanena na Musa akamwambia,
The Lord told Moses,
53 Ile ardhi itagawanywa kati ya wanaume hawa kama urithi wao kwa kufuata idadi ya majina yao.
“Divide the land that is to be owned based on the number of those censused.
54 Kwa zile koo kubwa utawagawia urithi mkubwa, na kwa koo ndogo ndogo utawagawia urithi kidogo. Kwa kila familia utawapa urithi kufuata idadi ya wanaume waliohesabiwa.
Give a larger area of land to large tribe, and a smaller area to a smaller tribe. Each tribe shall receive their allotment of land depending on their number counted in the census.
55 Lakini ardhi itagawiwa kwa kupigiwa kura. Watairithi nchi kama itakavyogawiwa kwa kufuata koo za mababu.
The land has to be divided up by casting lots. Everyone shall receive their allotted land based on the name of their ancestor's tribe.
56 Urithi huu utagiwiwa kufuata koo kubwa na ndogo, watagawiwa kwa kufuata kura zitakavyokuwa.
Every allocation of land is to be divided by casting lots among the tribes, whether large or small.”
57 Koo za Walawi, zilizohesabiwa kwa kufuata ukoo kwa ukoo, walikuwa hivi: Kwa Gerishoni, ukoo wa Wagerishoni, kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi, kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
These were the Levites censused by family: Gershon, ancestor of the Gershonite family; Kohath, ancestor of the Kohathite family; and Merari, ancestor of the Merarite family.
58 Koo za walawi zilikuwa hzi: ukoo wa Walibni, Ukoo wa Wahebroni, ukoo wa Wamahali, ukoo wa Wamushi, na ukoo wa Wakora. Kohathi alikuwa wa uzao wa Amramu.
The following were the families of the Levites: the Libnite family, the Hebronite family, the Mahlite family, the Mushite family, and the Korahite family. Kohath was the father of Amram,
59 Jina la mke wa Amramu lilikuwa Jokibed, wa ukoo wa Lawi, aliyekuwa amezaliwa kwa Walawi kule Misri. Alimzalia Amramu watoto wao, ambao walikuwa ni Haruni, Musa, na Miriamu dada yao.
and the name of Amram's wife was Jochebed. She was a descendant of Levi, born while the Levites were in Egypt. She had children with Amram: Aaron, Moses, and their sister Miriam.
60 Kwa Haruni alizaliwa Nadabu na Abihu, Eliazari na Ithamari.
Aaron's sons were Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar,
61 Nadabu na Abihu walikufa walipotoa sadaka kwa BWANA sadaka ya moto isiyokubalika.
but Nadab and Abihu died when they offered forbidden fire in the Lord's presence.
62 Waume walioheabaiwa miionigoni mwao walikuwa elfu ishirini na tatu, hawa nia wale wa umri wa mwezi mmoja na zaidi. Lakini hawakuhesabiwa kati ya wazawa wa Israeli kwa sababu hawakupewa urithi miongoni mwa wana wa Israeli.
The number of the Levites censused totaled 23,000. This included every male one month old or older. However, they were not counted with the other Israelites, because no land allotment was given to them with the other Israelites.
63 Hawa nadio wale walihesabiwa na Musa na Eliazari kuhani. Waliwahesabu watu wa Israeli katika uwanda wa Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko.
This is the record of those were censused by Moses and Eleazar the priest when they counted the Israelites on the plains of Moab beside the Jordan opposite Jericho.
64 Lakini miongoni mwa hawa hapakuwa na mwanamume aliyehasabiwa na Musa na Haruni kuhani wakati wana wa uzao wa Israeli walipohesabiwa katika jangwa la Sinai.
However, they did not include a single one who had previously been censused by Moses and Aaron the priest when they counted the Israelites in the Sinai Desert,
65 Kwa BWANA alikuwa amesema kuwa kwa hakika watu hao wote wangefia jangwani. Hapakuwa na mtu aliyebaki miongoni mwao, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Joshua mwana wa Nuni.
because the Lord had told them that they would all die in the desert. No one was left except Caleb, son of Jephunneh, and Joshua, son of Nun.

< Hesabu 26 >