< Hesabu 25 >
1 Israeli akakaa Shitimu, na wanaume wakaanza kufanya ukahaba na wanawake wa Moabu,
Israel se quedó en Sitim, y el pueblo comenzó a prostituirse con las hijas de Moab;
2 kwa kuwa Wamoabu waliwakaribishsa kutoa sadaka kwa miungu yao. Kwa hiyo watu wakala na kuisujudia miungu ya Moabu.
pues llamaron al pueblo a los sacrificios de sus dioses. El pueblo comía y se inclinaba ante sus dioses.
3 Watu wa Israeli wakaungana kumwabudu Baali wa Peori, na hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya Israeli.
Israel se unió a Baal Peor, y la ira de Yahvé ardió contra Israel.
4 BWANA akamwambia Musa, “Waue viongozi wote wa watu na uwanyonge mbele yangu ili waonekane wakati wa mchana, ili kwamba hasira yangu kali iondoke kwa Israeli.”
Yahvé dijo a Moisés: reúne a todos los jefes del pueblo y ahórcalos delante de mí, “Toma a todos los jefes del pueblo a Yahvé ante el sol, para que el furor de Yahvé se aparte de Israel.”
5 Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
Moisés dijo a los jueces de Israel: “Maten todos a sus hombres que se han unido a Baal Peor”.
6 Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
He aquí que uno de los hijos de Israel vino y trajo a sus hermanos una mujer madianita a la vista de Moisés y de toda la congregación de los hijos de Israel, mientras lloraban a la puerta de la Tienda de Reunión.
7 Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
Cuando Finees, hijo de Eleazar, hijo del sacerdote Aarón, lo vio, se levantó de en medio de la congregación y tomó una lanza en su mano.
8 Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
Fue tras el hombre de Israel al pabellón, y los atravesó a ambos, al hombre de Israel y a la mujer por el cuerpo. Así se detuvo la plaga entre los hijos de Israel.
9 Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
Los que murieron por la plaga fueron veinticuatro mil.
10 BWANA akanena na Musa, akasema,
Yahvé habló a Moisés y le dijo:
11 “Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
“Finees, hijo de Eleazar, hijo del sacerdote Aarón, ha alejado mi ira de los hijos de Israel, ya que se puso celoso con mis celos entre ellos, para que yo no consumiera a los hijos de Israel en mis celos.
12 Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.
Por tanto, di: “He aquí que yo le doy mi pacto de paz.
13 Kwake na kwa wana wake baada yake, litakuwa agano la kudumu la ukuhani kwa sababu alikuwa na wivu juu yangu, Mungu wake. Amewapatanisha wana wa Israeli.
Será para él, y para su descendencia después de él, el pacto de un sacerdocio eterno, porque fue celoso por su Dios e hizo expiación por los hijos de Israel.’”
14 Sasa yule Muisraeli aliyeuwawa pamoja na Yule mwanamke Mmidiani alikuwa Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa familia ya uzao wa Simeoni.
El nombre del hombre de Israel que fue asesinado con la mujer madianita era Zimri, hijo de Salu, príncipe de una casa paterna entre los simeonitas.
15 Jina la yule Mmidiani aliyeuwawa lilikuwa Cozibi binti wa Zuri, ambaye alikuwa mkuu wa familia wa kabila huko Midiani.
El nombre de la mujer madianita que fue asesinada era Cozbi, hija de Zur. Era jefe de la gente de una casa paterna en Madián.
16 Kwa hiyo BWANA akanena na Musa na kusema,
Yahvé habló a Moisés, diciendo:
17 “Watendee Wamidiani kama maadui na uwaangamize, kwa kuwa waliwatendea kama maadui
“Acosa a los madianitas y atácalos;
18 kwa kuwadanganya. Waliwaongoza katika uovu kwa swala la Peori na kwa swala la dada yao Cozibi, binti wa kiongozi wa Wamidiani, ambaye aliuawa siku ile ya tauni kwa swala la Peori.”
porque te han acosado con sus artimañas, en las que te han engañado en el asunto de Peor, y en el incidente relativo a Cozbi, la hija del príncipe de Madián, su hermana, que fue asesinada el día de la plaga en el asunto de Peor.”