< Hesabu 25 >

1 Israeli akakaa Shitimu, na wanaume wakaanza kufanya ukahaba na wanawake wa Moabu,
Forsothe in that tyme Israel dwellide in Sechym; and the puple dide fornycacioun with the douytris of Moab;
2 kwa kuwa Wamoabu waliwakaribishsa kutoa sadaka kwa miungu yao. Kwa hiyo watu wakala na kuisujudia miungu ya Moabu.
whiche douytris clepiden hem to her sacrifices, and thei eten, and worschipiden the goddis of tho douytris;
3 Watu wa Israeli wakaungana kumwabudu Baali wa Peori, na hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya Israeli.
and Israel made sacrifice to Belphegor. And the Lord was wrooth,
4 BWANA akamwambia Musa, “Waue viongozi wote wa watu na uwanyonge mbele yangu ili waonekane wakati wa mchana, ili kwamba hasira yangu kali iondoke kwa Israeli.”
and seide to Moises, Take thou alle the princes of the puple, and hange hem ayens the sunne in iebatis, that my wodnesse, `that is stronge veniaunce, be turned awai fro Israel.
5 Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
And Moises seide to the iugis of Israel, Ech man sle his neiyboris, that maden sacrifice to Belphagor.
6 Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
And, lo! oon of the sones of Israel entride bifor his britheren to `an hoore of Madian, in the siyt of Moises, and al the cumpeny of the sones of Israel, whiche wepten bifor the yatis of the tabernacle.
7 Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
And whanne Phynees, the sone of Eleazar, sone of Aaron, preest, hadde seyn this, he roos fro the myddis of the multitude; and whanne he hadde take a swerd,
8 Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
he entride aftir the man of Israel in to the `hoore hows, and stikide thorou both togidere, that is, the man and the womman, in the places of gendryng. And the veniaunce ceesside fro the sones of Israel,
9 Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
and foure and twenti thousand of men weren slayn.
10 BWANA akanena na Musa, akasema,
And the Lord seide to Moises,
11 “Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
Fynees, the sone of Eleazar, sone of Aaron, preest, turnede away myn yre fro the sones of Israel; for he was stirid ayens hem bi my feruent loue, that Y my silf schulde not do awai the sones of Israel in my greet hete, `ether strong veniaunce.
12 Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.
Therfor speke thou to hym, Lo! Y yyue to hym the pees of my couenaunt,
13 Kwake na kwa wana wake baada yake, litakuwa agano la kudumu la ukuhani kwa sababu alikuwa na wivu juu yangu, Mungu wake. Amewapatanisha wana wa Israeli.
and it schal be an euerlastynge couenaunt of preesthod, as wel to hym silf as to his seed; for he louyde feruentli for his God, and he clenside the greet trespas of the sones of Israel.
14 Sasa yule Muisraeli aliyeuwawa pamoja na Yule mwanamke Mmidiani alikuwa Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa familia ya uzao wa Simeoni.
Forsothe the name of the man of Israel, that was slayn with the womman of Madian, was Zambri, the sone of Salu, duyk of the kynrede and lynage of Symeon.
15 Jina la yule Mmidiani aliyeuwawa lilikuwa Cozibi binti wa Zuri, ambaye alikuwa mkuu wa familia wa kabila huko Midiani.
Forsothe the womman of Madian that was slayn togidere, was clepid Cobri, the douyter of Sur, the nobleste prince of Madianytis.
16 Kwa hiyo BWANA akanena na Musa na kusema,
And the Lord spak to Moises and seide,
17 “Watendee Wamidiani kama maadui na uwaangamize, kwa kuwa waliwatendea kama maadui
`Madianytis feele you enemyes, and smyte ye hem;
18 kwa kuwadanganya. Waliwaongoza katika uovu kwa swala la Peori na kwa swala la dada yao Cozibi, binti wa kiongozi wa Wamidiani, ambaye aliuawa siku ile ya tauni kwa swala la Peori.”
for also thei diden enemyliche ayens you, and disseyueden thorow tresouns, bi the idol of Phegor, and bi `the douyter of Corbri, duyk of Madian, her sister, which douyter was sleyn in the dai of veniaunce, for the sacrilege of Phegor.

< Hesabu 25 >