< Hesabu 25 >
1 Israeli akakaa Shitimu, na wanaume wakaanza kufanya ukahaba na wanawake wa Moabu,
And it remained Israel in Shittim and it began the people to commit fornication into [the] daughters of Moab.
2 kwa kuwa Wamoabu waliwakaribishsa kutoa sadaka kwa miungu yao. Kwa hiyo watu wakala na kuisujudia miungu ya Moabu.
And they invited the people to [the] sacrifices of gods their and it ate the people and they bowed down to gods their.
3 Watu wa Israeli wakaungana kumwabudu Baali wa Peori, na hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya Israeli.
And it joined itself Israel to Baal Peor and it burned [the] anger of Yahweh on Israel.
4 BWANA akamwambia Musa, “Waue viongozi wote wa watu na uwanyonge mbele yangu ili waonekane wakati wa mchana, ili kwamba hasira yangu kali iondoke kwa Israeli.”
And he said Yahweh to Moses take all [the] leaders of the people and impale them to Yahweh before the sun so may it turn away [the] burning of [the] anger of Yahweh from Israel.
5 Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
And he said Moses to [the] judges of Israel kill everyone men his who have joined themselves to Baal Peor.
6 Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
And there! a man from [the] people of Israel [was] coming and he brought near to brothers his the Midianite [woman] to [the] eyes of Moses and to [the] eyes of all [the] congregation of [the] people of Israel and they [were] weeping [the] entrance of [the] tent of meeting.
7 Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
And he saw [it] Phinehas [the] son of Eleazar [the] son of Aaron the priest and he arose from among the congregation and he took a spear in hand his.
8 Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
And he went after [the] man of Israel into the tent and he pierced through both of them [the] man of Israel and the woman into belly her and it was restrained the plague from on [the] people of Israel.
9 Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
And they were those [who] died by the plague four and twenty thousand.
10 BWANA akanena na Musa, akasema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
11 “Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
Phinehas [the] son of Eleazar [the] son of Aaron the priest he has turned back rage my from against [the] people of Israel because was zealous he zeal my in midst of them and not I made an end of [the] people of Israel in zeal my.
12 Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.
Therefore say here I [am] about to give to him covenant my peace.
13 Kwake na kwa wana wake baada yake, litakuwa agano la kudumu la ukuhani kwa sababu alikuwa na wivu juu yangu, Mungu wake. Amewapatanisha wana wa Israeli.
And it will belong to him and to offspring his after him a covenant of priesthood of perpetuity because that he was zealous for God his and he made atonement on [the] people of Israel.
14 Sasa yule Muisraeli aliyeuwawa pamoja na Yule mwanamke Mmidiani alikuwa Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa familia ya uzao wa Simeoni.
And [the] name of [the] man of Israel who was struck down who he was struck down with the Midianite [woman] [was] Zimri [the] son of Salu a leader of a house of a father of the Simeonite[s].
15 Jina la yule Mmidiani aliyeuwawa lilikuwa Cozibi binti wa Zuri, ambaye alikuwa mkuu wa familia wa kabila huko Midiani.
And [the] name of the woman who was struck down the Midianite [woman] [was] Cozbi [the] daughter of Zur [was] a leader of tribes a house of a father in Midian he.
16 Kwa hiyo BWANA akanena na Musa na kusema,
And he spoke Yahweh to Moses say.
17 “Watendee Wamidiani kama maadui na uwaangamize, kwa kuwa waliwatendea kama maadui
oppose The Midianites and you will strike down them.
18 kwa kuwadanganya. Waliwaongoza katika uovu kwa swala la Peori na kwa swala la dada yao Cozibi, binti wa kiongozi wa Wamidiani, ambaye aliuawa siku ile ya tauni kwa swala la Peori.”
For [are] opposers they you by deceitfulness their which they have dealt deceptively to you on [the] matter of Peor and on [the] matter of Cozbi [the] daughter of [the] leader of Midian sister their who was struck down on [the] day of the plague on [the] matter of Peor.