< Hesabu 25 >

1 Israeli akakaa Shitimu, na wanaume wakaanza kufanya ukahaba na wanawake wa Moabu,
When the Israelites were staying at Shittim the men started to have sex with Moabite women
2 kwa kuwa Wamoabu waliwakaribishsa kutoa sadaka kwa miungu yao. Kwa hiyo watu wakala na kuisujudia miungu ya Moabu.
who invited them to the sacrifices made to their gods. The Israelites ate the pagan meals and bowed down before these gods.
3 Watu wa Israeli wakaungana kumwabudu Baali wa Peori, na hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya Israeli.
In this way the Israelites devoted themselves in worship to Baal of Peor, and the Lord was angry with them.
4 BWANA akamwambia Musa, “Waue viongozi wote wa watu na uwanyonge mbele yangu ili waonekane wakati wa mchana, ili kwamba hasira yangu kali iondoke kwa Israeli.”
The Lord told Moses, “Arrest all the Israelite leaders and kill them before the Lord where everyone can see in order to turn the Lord's furious anger away from the people.”
5 Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
So Moses instructed Israel's judges, “Each of you has to kill all of your men who have devoted themselves to worshiping Baal of Peor.”
6 Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
Right then an Israelite man brought a Midianite woman to his family tent in full view of Moses and all the Israelites as they were crying at the entrance to the Tent of Meeting.
7 Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
When he saw this, Phinehas, son of Eleazar, the son of Aaron the priest, left the assembly, grabbed a spear
8 Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
and followed the man into his tent. There Phinehas drove the spear through both of them, through the Israelite and on into the woman's stomach. This action stopped the plague that had started to kill the Israelites,
9 Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
but 24,000 had already died.
10 BWANA akanena na Musa, akasema,
The Lord told Moses,
11 “Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
“Phinehas son of Eleazar, the son of Aaron the priest, has turned my anger away from the Israelites, because out of all of them he was passionately dedicated to me, so I did not destroy the Israelites in my passionate anger.
12 Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.
So make an announcement that I am granting him my peace agreement.
13 Kwake na kwa wana wake baada yake, litakuwa agano la kudumu la ukuhani kwa sababu alikuwa na wivu juu yangu, Mungu wake. Amewapatanisha wana wa Israeli.
It will be an agreement that ensures a permanent priesthood for him and his descendants, because he was passionately dedicated to his God and set the Israelites right.”
14 Sasa yule Muisraeli aliyeuwawa pamoja na Yule mwanamke Mmidiani alikuwa Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa familia ya uzao wa Simeoni.
The name of the Israelite who was killed with the Midianite woman was Zimri, son of Salu, a family leader of the tribe of Simeon.
15 Jina la yule Mmidiani aliyeuwawa lilikuwa Cozibi binti wa Zuri, ambaye alikuwa mkuu wa familia wa kabila huko Midiani.
The name of the Midianite woman who was killed was Cozbi, daughter of Zur, a family leader of a Midianite tribe.
16 Kwa hiyo BWANA akanena na Musa na kusema,
The Lord told Moses,
17 “Watendee Wamidiani kama maadui na uwaangamize, kwa kuwa waliwatendea kama maadui
“Attack the Midianites and kill them,
18 kwa kuwadanganya. Waliwaongoza katika uovu kwa swala la Peori na kwa swala la dada yao Cozibi, binti wa kiongozi wa Wamidiani, ambaye aliuawa siku ile ya tauni kwa swala la Peori.”
because they attacked you deceptively, leading you astray by using Peor and their woman Cozbi, the daughter of the Midianite leader—the woman who was killed on the day the plague came because of their devotion to Peor.”

< Hesabu 25 >