< Hesabu 23 >
1 Balaamu akamwabia Balaki, “Jenga madhabahu saba kwa ajili yangu na uandae mafahari saba na kondoo dume saba.”
And Balaam says to Balak, “Build seven altars for me in this [place], and prepare seven bullocks and seven rams for me in this [place].”
2 Kwa hiyo Balaki akafanya kama Balaamu alivyoomba. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume mmoja kwa kila madhabahu.
And Balak does as Balaam has spoken, and Balak—Balaam also—offers a bullock and a ram on the altar,
3 Ndipo Balaamu alipomwamiba Balaki, “Simama kwenye sadaka yako ya kuteketezwa na mimi nitaenda. Labda BWANA atakuja kukutana na mimi. Chochote atakachoniambia nitakuambia.” Kwa hiyo akaenda juu ya mlima usiokuwa na miti.
and Balaam says to Balak, “Station yourself by your burnt-offering and I go on, it may be YHWH comes to meet me, and the thing which He shows me I have declared to you”; and he goes [to] a high place.
4 Wakati bado akiwa juu ya mlima. Mungu akakutana naye, na Balaamu akamwambia, “Nimejenga madhabahu saba, na nimetoa sadaka ya fahari na kondoo dume kwa kila madhabahu.”
And God comes to Balaam, and he says to Him, “I have arranged the seven altars, and I offer a bullock and a ram on the altar”;
5 BWANA akaweka ujumbe kwenye kinywa cha Baalamu akasema, “Rudi kwa Balaki ukamwambie.”
and YHWH puts a word in the mouth of Balaam and says, “Return to Balak, and thus you speak.”
6 Kwa hiyo Balaamu akarudi kwa Balaki aliyekuwa amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, na viongozi wote wa Moabu walikuwa pamoja naye.
And he returns to him, and behold, he is standing by his burnt-offering, he and all the princes of Moab.
7 Ndipo Balaamu alipoanza kunena unabii wake akisema, “Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka katika milima ya mashariki, 'Njoo, nilaanie Yakobo kwa ajili yangu,' alisema, 'Njoo umtie unajisi Israeli,'
And he takes up his allegory and says: “Balak king of Moab leads me from Aram; From mountains of the east. Come—curse Jacob for me, And come—be indignant [with] Israel.
8 Nawezaje kuwalaani wale ambao Mungu hajawalaani? Nawezaje kuwapinga wale ambao Mungu hawapingi?
How do I pierce [when] God has not pierced? And how am I indignant [when] YHWH has not been indignant?
9 Kwa kuwa kutoka juu ya miamba Ninamwona; kutoka kwenye milima ninamtazama. Kuna watu wanaoishi pekee yao na hawajioni wenyewe kama ni taifa la kawaida.
For from the top of rocks I see him, And from heights I behold him; Behold a people! He dwells alone, And does not reckon himself among nations.
10 Nani awezaye kuyahesabu mavumbi ya Yakobo au kuhesabu hata robo ya Israeli? Naomba nife kifo cha mtu mwenye haki, na mwisho wa maisha yangu uwe kama wake!”
Who has counted the dust of Jacob, And the number of the fourth of Israel? Let me die the death of upright ones, And let my last end be like his!”
11 Balaki akamwambia Balaamu, “Umenifanyia nini? Nilikuleta ili uwalaani maadui wangu, lakini ona, umewabariki,”
And Balak says to Balaam, “What have you done to me? I have taken you to pierce my enemies, and behold, you have certainly blessed”;
12 Balaamu akajibu akasema, “Kwa nini nisiwe mwangalifu kusema kile ambacho BWANA anaweka kinywani mwangu?”
and he answers and says, “That which YHWH puts in my mouth—do I not take heed to speak it?”
13 Basi Balaki akamwambia, “Hebu uje nami kwenye eneo jingine ili uwaone. Utakaowaona ni wale wa karibu tu, huwezi kuwaona wote. Huko sasa unaweza kunilaania hawa watu.”
And Balak says to him, “Come! Come to another place with me, from where you see it—you see only its extremity, and you do not see all of it, and pierce it for me there”;
14 Kwa hiyo akampeleka Balaamu kwenye shamba la Zofimu, lililo juu ya Mlima Pisiga, na kule akajenga madhabau zingine saba. Akatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume kwa kila madhabahu.
and he takes him [to] the field of Zophim, to the top of Pisgah, and builds seven altars, and offers a bullock and a ram on the altar.
15 Kisha Balaamu akamwambia Balaki, “Simama hapa karibu na sadaka zako, wakati mimi naenda kukutana na BWANA kule.”
And he says to Balak, “Station yourself here by your burnt-offering, and I meet [Him] there”;
16 Kwa hiyo BWANA akakutana na Balaamu na kumwekea ujumbe kinywani mwake. Alimwambia, “Rudi kwa Balaki ukamwambie huu ujumbe toka kwangu.”
and YHWH comes to Balaam, and sets a word in his mouth, and says, “Return to Balak, and thus you speak.”
17 Balaamu akamrudia, na tazama, alikuwa amesimama karibu na sadaka zake za kuteketezwa, na vionigozi wa Moabu walikuwa pamoja naye. Balaki akamwuliza, “BWANA amekwambiaje?”
And he comes to him, and behold, he is standing by his burnt-offering, and the princes of Moab [are] with him, and Balak says to him: “What has YHWH spoken?”
18 Balaamu akaanza kutoa unabii. Akasema, “Inuka, Balaki na usikilize. Nisikilize mimi wewe mwana wa Zippori.
And he takes up his allegory and says: “Rise, Balak, and hear; Give ear to me, son of Zippor!
19 Mungu siyo mtu, kwamba umdanganye, au mwanadamu awezaye kubadili mawazo. Je, alishawahi kuahidi kitu pasipo kukitekeleza? Je, alishawahi kusema kuwa atafanya kitu bila kufanya kama alivyosema?
God [is] not a man—and lies, And a son of man—and relents! Has He said—and He does not do [it]? And spoken—and He does not confirm it?
20 Tazama, Mimi nimeamriwa kuwabariki. Mungu ametoa baraka, nami siwezi kuibadilisha.
Behold, I have received [only] to bless; Indeed, He blesses, and I cannot reverse it.
21 Hajawahi kuona magumu katika Yakobo au tabu katika Israeli. BWANA Mungu wao yuko pamoja nao, na kelele za wafalme wao ziko pamoja nao.
He has not beheld iniquity in Jacob, Nor has He seen perverseness in Israel; His God YHWH [is] with him, And a shout of a king [is] in him.
22 Mungu aliwatoa Misri kwa nguvu kama za nyati.
God is bringing them out from Egypt, As the swiftness of a wild ox for him;
23 Hakuna uganga utakaofanikiwa dhidi ya Yakobo, na hakuna uchawi utakaomwumiza Israeli. Badala yake, itasemwa juu ya Yakobo na Israeli, 'Tazama kile ambacho Mungu amefanya!'
For no enchantment [is] against Jacob, Nor divination against Israel; At the time it is said of Jacob and Israel, O what God has worked!
24 Tazama, watu wanainuka kama simba jike, kama vile simba ainukavyo na kuvamia. Halali chini mpaka ale windo lake na kunywa damu ya windo lake,”
Behold, the people rises as a lioness, And he lifts himself up as a lion; He does not lie down until he eats prey, And drinks blood of pierced ones.”
25 Kisha Balaki akamwambia Balaamu, “Kamwe usiwalaani wala kuwabariki.”
And Balak says to Balaam, “Neither pierce it at all, nor bless it at all”;
26 Lakini Balaamu akamjibu Balaki, “Sijakuambia kuwa nitasema yote ambayo BWANA ananiambia kusema?
and Balaam answers and says to Balak, “Have I not spoken to you, saying, All that YHWH speaks—I do it?”
27 Balaki akamwambia Balaamu, “Njoo sasa, Nami nitakupeleka mahali pengine. Labda kule itampendeza Mungu kunilaania hawa hawa watu.”
And Balak says to Balaam, “Please come, I take you to another place; it may be it is right in the eyes of God to pierce it for me from there.”
28 Kwa hiyo Balaki akampeleka Balaamu juu ya Mlima Peori, ambao unalitazama chini lile jangwa,
And Balak takes Balaam to the top of Peor, which is looking on the front of the wilderness,
29 Balaamu akamwambia Balaki, “Nijengee madhabahu saba hapa na uniandalie mafahari saba na kondoo duume saba.
and Balaam says to Balak, “Build seven altars for me in this [place], and prepare seven bullocks and seven rams for me in this [place]”;
30 “Kwa hiyo Balaki akafanya kama alivyoambiwa; akatoa sadaka ya fahari na kondoo mume kwenye kila madhabahu.
and Balak does as Balaam said, and he offers a bullock and a ram on an altar.