< Hesabu 22 >

1 Watu wa Israeli wakasafiri mpaka wakaweka kambi kwenye uwanda wa Moabu karibu na Yeriko, kwenye upande mwingine wa mto Yorodani kutoka mji ule.
After, the children of Israel departed and pitched in the plaine of Moab on the other side of Iorden from Iericho.
2 Balaki mwana wa Zippori aliona yote ambayo Israeli aliwafanyia Waamori. Moabu aliogopa sana hao watu kwa sababu walikuwa wengi sana,
Now Balak the sonne of Zippor sawe all that Israel had done to the Amorites.
3 na Moabu alIwahofia wana wa Israeli.
And the Moabites were sore afraide of the people, because they were many, and Moab fretted against the children of Israel.
4 Mfalme wa Moabu akawaambia wazee wa Midiani, “Huu umati utakula kila kitu tulicho nacho na maksai hula nyasi za kondeni.” Sasa Balaki mwana wa Zippori alikuwa mfalme wa Moabu.
Therfore Moab said vnto the Elders of Midian, Nowe shall this multitude licke vp all that are round about vs, as an oxe licketh vp ye grasse of the fielde: and Balak the sonne of Zippor was King of the Moabites at that time.
5 Akatuma wajumbe kwenda kwa Balamu mwana wa Beori, kule Petho ambayo iko karibu na mto Frati, katika nchi ya taifa lake na watu wake. Akamwita na kumwambia, “Tazama, Kuna taifa ambalo wamekuja hapa tokea Misiri. Wanafunika uso wa dunia na sasa wananifuatia mimi.
Hee sent messengers therefore vnto Balaam the sonne of Beor to Pethor (which is by the riuer of the lande of the children of his folke) to call him, saying, Beholde, there is a people come out of Egypt, which couer the face of the earth, and lye ouer against me.
6 Tafadhali naomba uje unilaanie hili taifa, kwa sababu wana nguvu kuliko mimi. Labda nitaweza kuwavamia na kuwafukuza watoke katika nchi yangu. Najua kuwa yeyote unayembariki hubarikiwa na yeyote unayemlaani atalaaniwa.”
Come now therefore, I pray thee, and curse me this people (for they are stronger then I) so it may be that I shall be able to smite them, and to driue them out of the land: for I knowe that hee, whome thou blessest, is blessed, and he whom thou cursest, shall be cursed.
7 Kwa hiyo wazee wa Moabu na wale wa Midiani wakaondoka, pamoja nao wakachukua malipo ya uganga. Wakafika kwa Balaamu wakamwambia maneno ya Balaki.
And the Elders of Moab, and the Elders of Midian departed, hauing the reward of the soothsaying in their hande, and they came vnto Balaam, and tolde him the wordes of Balak.
8 Balaamu akawaambia, “Bakini hapa usiku wa leo. Kesho nitawaletea atakachoniambia BWANA.” Kwa hiyo wale viongozi wa Moabu wakabaki na Balaamu kwa usiku huo.
Who answered them, Tary here this night, and I will giue you an answere, as the Lord shall say vnto mee. So the princes of Moab abode with Balaam.
9 Mungu akaja kwa Balaamu na kumwambia, “Ni akina nani hawa waliokuja kwako?”
Then God came vnto Balaam, and sayde, What men are these with thee?
10 Balaamu akamjibu Mungu, “Balaki mwana wa Zippori, Mfalme wa Moabu amewatuma kwangu. Alisema,
And Baalam said vnto God, Balak ye sonne of Zippor, king of Moab hath set vnto me, saying,
11 'Tazama hawa watu waliotoka Misri wanafunika uso wa nchi yangu. Sasa naomba uje unilaanie hawa watu. Labada nitaweza kuwa kuwashinda na kuwafukuza.'”
Beholde, there is a people come out of Egypt and couereth the face of the earth: come nowe, curse them for my sake: so it may be that I shalbe able to ouercome them in battell, and to driue them out.
12 Mungu akamjiu Balaam, “Usiambatane na hao wanaume. Na usiwalaani hawa wana wa Israeli kwa sababu wamebarikiwa.”
And God said vnto Balaam, Go not thou with them, neither curse the people, for they are blessed.
13 Balaamu akaamka asubuhi na kuwaambia wale viongozi wa Balaki, “Rudini nchini kwenu kwa sababu BWANA amenikataza kuambatana nanyi.”
And Balaam rose vp in the morning, and sayde vnto ye princes of Balak, Returne vnto your land: for the Lord hath refused to giue me leaue to go with you.
14 Kwa hiyo wale viongozi wa Moabu wakaondoka na kurudi kwa Balaki. Wakamwambia, “Balaamu amekataa kuambatana nasi.”
So the princes of Moab rose vp, and went vnto Balak, and sayd, Balaam hath refused to come with vs.
15 Balaki akatuma viongozi wengine waliokuwa wanaheshimiwa zaidi kuliko kundi lile la awali.
Balak yet sent againe moe princes, and more honourable then they.
16 Wakaja kwa Balaamu na kumwambia, “Balaki mwana wa Zippori anasema hivi, 'Tafadhali hebu kitu chochote kisikuzuie kuja kwangu,
Who came to Balaam, and sayde to him, Thus saith Balak the sonne of Zippor, Bee not thou staied, I pray thee, from comming vnto me.
17 kwa sababu nitakulipa malipo mazuri sana na kukupa heshima kubwa, nami nitakufanyia chochote utakachoniambia. Tafadhali sana uje unilaanie hawa watu.'”
For I wil promote thee vnto great honour, and wil do whatsoeuer thou sayest vnto me: come therefore, I pray thee, curse me this people.
18 Balaamu akawajibu watu wa Balaki akawaambia, “Hata kama Balaki atanipa ikulu yake ikiwa imejaa fedha na dhahabu, sitaweza kufanya dhidi ya maneno ya BWANA, Mungu wangu na kufanya pungufu au zaidi ya kile anachoniambia.
And Balaam answered, and sayde vnto the seruants of Balak, If Balak woulde giue me his house full of siluer and golde, I can not goe beyonde the worde of the Lord my God, to doe lesse or more.
19 Sasa basi, tafadhali subirini hapa usiku wa leo pia, ili kwamba nipate kujifunza kitu zaidi ambacho BWANA ananiambia.”
But nowe, I pray you, tary here this night, that I may wit, what the Lord will say vnto mee more.
20 BWANA akaja kwa Balaamu usiku ule na kumwambia, “kwa kuwa hawa watu wamekuja kukuita, inuka uende nao. Lakini utafanya tu kile nitakachokuambia kufanya.”
And God came vnto Balaam by night, and sayd vnto him, If the men come to call thee, rise vp, and goe with them: but onely what thing I say vnto thee, that shalt thou doe.
21 Balaamu akainuka asubuhi, akatandika punda wake, akaenda pamoja na viongozi wa Moabu.
So Balaam rose vp early, and sadled his asse, and went with the princes of Moab.
22 Lakini kwa sababu alienda, hasira za Mungu zikawaka. Malaika wa BWANA akasimama barabarani kama adui wa Balaamu, aliyekuwa akimpanda yule punda. Watumishi wawili wa Balaamu walikuwa pamoja naye.
And ye wrath of God was kindled, because he went: and the Angel of the Lord stood in the way to be against him, as he rode vpon his asse, and his two seruants were with him.
23 Yule punda alimwona yule malaika wa BWANA akiwa amesimama barabarani akiwa na upanga mkononi mwake. Yule punda akageuka na kwenda shambani. Balaamu akampiga yule punda ili arudi barabarani.
And when the asse saw the Angel of the Lord stand in the way, and his sworde drawen in his hand, the asse turned out of the way and went into the field, but Balaam smote the asse, to turne her into the way.
24 Sasa malaika wa BWANA akasimama kwenye njia nyembamba katikati ya mashamba ya mizabibu, na kushoto kwake kulikuwa na ukuta.
Againe the Angel of the Lord stood in a path of the vineyardes, hauing a wall on the one side, and a wall on the other.
25 Yule punda akamwona yule malaika wa BWANA tena. Akasogea zaidi ukutani na kuubana mguu wa Balaamu ukutani. Balaamu akampiga tena yule punda.
And when the asse sawe the Angel of the Lord, she thrust her selfe vnto the wall, and dasht Balaams foote against the wall: wherefore hee smote her againe.
26 Yule malaika wa BWANA akasogea mbele zaidi kwenye eneo jingine jembamba zaidi ambalo haikuwezekana kugeuka upande mwingine.
Then the Angel of the Lord went further, and stoode in a narowe place, where was no way to turne, either to the right hand, or to the left.
27 Yule Punda akamwona tena yule malaika wa BWANA, akalala chini ya Balaamu. Hasira za Balaamu zikawaka, akampiga yule punda kwa fimbo yake.
And when the asse sawe the Angell of the Lord, she lay downe vnder Balaam: therefore Balaam was very wroth, and smote the asse with a staffe.
28 Kisha BWANA akafungua kinywa cha punda na akaongea. Akamwambia Balaamu, “Nimekukosea nini kiasi kwamba umenipiga mara tatu?”
Then the Lord opened the mouth of the asse, and she saide vnto Balaam, What haue I done vnto thee, that thou hast smitten me nowe three times?
29 Balaamu akamjibu yule punda, “Ni kwa sababu umenitendea kwa ujinga. Natamani kama ningekuwa na upanga mkononi mwangu, kama ningekuwa nao, sasa hivi ningekuwa nimekuua.”
And Balaam saide vnto the asse, Because thou hast mocked me: I woulde there were a sworde in mine hand, for nowe would I kill thee.
30 Yule punda akamwambia Balaamu, “Je, mimi si punda wako ambaye umenipanda maishani mwako mwote mpaka hivi sasa? Je, nimewahi kuwa na tabia ya kukufanyia hivi hapo awali?” Balaamu akasema “hapana.”
And the asse saide vnto Balaam, Am not I thine asse, which thou hast ridden vpon since thy first time vnto this day? haue I vsed at any time to doe thus vnto thee? Who said, Nay.
31 Basi BWANA akafungua macho ya Balaamu, na akamwona malaika wa BWANA amesimama barabarani akiwa na upanga mkononi mwake. Balaamu akainamisha kichwa chake chini.
And the Lord opened the eyes of Balaam, and he sawe the Angel of the Lord standing in the way with his sword drawen in his hande: then he bowed him selfe, and fell flat on his face.
32 Yule malaika wa BWANA akamwambia, “Kwa nini umempiga punda wako mara tatu? Tazama, Nimekuja kama adui yako kwa sababu matendo yako kwangu yamekuwa maovu.
And the Angel of the Lord said vnto him, Wherefore hast thou nowe smitten thine asse three times? beholde, I came out to withstande thee, because thy way is not straight before me.
33 Yule punda aliniona na akageuka kutoka kwangu mara tatu. Kama asingekuwa amegeuka kutoka kwangu, hakika ningekuwa nimekua na yeye kumwacha hai.
But the asse sawe me, and turned from me now three times: for els, if she had not turned from me, surely I had euen nowe slaine thee, and saued her aliue.
34 Balaamu akamwambia malaika wa BWANA, nimetenda dhambi. Sikujua kuwa ulisimama kinyume na mimi barabarani. Kwa hiyo sasa, kama haikupendezi, Nitageuka.”
Then Balaam saide vnto the Angel of the Lord, I haue sinned: for I wist not that thou stoodest in the way against me: now therefore if it displease thee, I will turne home againe.
35 Lakini yule malaika wa BWANA akamwambia Balaamu, “endelea na wale watu. Lakini utasema maneno nitakayokwambia tu.”Kwa hiyo Balaamu akaendelea na wale vioingozi wa Balaki.
But the Angel said vnto Balaam, Go with the men: but what I say vnto thee, that shalt thou speake. So Balaam went with ye princes of Balak.
36 Balaki aliposikia kuwa Balaamu alikuwa amekuja, alienda kukutana naye kule mjini Moabu pale Amoni, ambao uko mpakani.
And when Balak heard that Balaam came, he went out to meete him vnto a citie of Moab, which is in the border of Arnon, euen in the vtmost coast.
37 Balaki akamwambia Balaamu, “Je, mimi sikutuma watu kukuita? Basi kwa nini hukuja kwangu? Je, mimi sina uwezo wa kukufanya uheshimike?”
Then Balak saide vnto Balaam, Did I not sende for thee to call thee? Wherefore camest thou not vnto me? am I not able in deede to promote thee vnto honour?
38 Ndipo Balaamu alipomjibu Balaki, “Tazama, mimi nimekuja kwako. Je mimi sina mamlaka ya kusema chochote? Mimi ninaweza kusema maneno ambayo Mungu ameweka kinywani mwangu.”
And Balaam made answere vnto Balak, Lo, I am come vnto thee, and can I nowe say any thing at all? the worde that God putteth in my mouth, that shall I speake.
39 Balaamu akaenda na Balaki, na Wakafika Kiriathi Huzothi.
So Balaam went with Balak, and they came vnto the citie of Huzoth.
40 Kisha Balaki akatoa sadaka ya maksai na kondoo na kumpatia Balaamu baadhi ya hiyo nyama na wale viongozi waliokuwa pamoja naye.
Then Balak offred bullockes, and sheepe, and sent thereof to Balaam, and to the princes that were with him.
41 Kesho yake asubuhi, Balaki akampeleka Balaamu mpaka juu mahali pa Baali. Kule juu Balaamu aliweza kuona sehemu tu ya kambi za Waisraeli.
And on the morowe Balak tooke Balaam, and brought him vp into the hie places of Baal, that thence hee might see the vtmost part of the people.

< Hesabu 22 >