< Hesabu 21 >

1 Aradi mfalme wa Wakanaani, aliyekuwa akiishi Negebu, aliposikia kuwa Israeli alikuwa akisafiri kwa kupitia barabara kuelekea Atharimu, akapigana dhidi ya Israeli na kujitwalia baadhi ya mateka.
The Canaanite [Descendant of Humbled], the king of Arad, who lived in the South, sh'ma ·heard obeyed· that Israel [God prevails] came by the way of Atharim. He fought against Israel [God prevails], and took some of them captive.
2 Israeli akaapa mbele ya BWANA akasema, “Kama utatupa ushindi dhidi ya hawa watu, ndipo tutakapoingamiza kabisa miji yao,”
Israel [God prevails] vowed a vow to Adonai, and said, “If you will indeed deliver this people into my hand, then I will utterly destroy their cities.”
3 BWANA akaisikia sautiya Israeli na kuwapa ushindi dhidi ya Wakanaani. Wakawaangamiza kabisa pamoja na miji yao. Mahali pale paliitwa Horima.
Adonai sh'ma ·heard obeyed· the voice of Israel [God prevails], and delivered up the Canaanites [Descendants of Humbled]; and they utterly destroyed them and their cities. The name of the place was called Hormah.
4 Wakasafiri kutoka Mlima Hori kwa barabara kuelekea bahari ya shamu wakiizunguka nchi ya Edomu. Watu walikufa moyo kwa njia hiyo.
They traveled from Mount Hor by the way to the Sea of Suf [Reed Sea], to go around the land of Edom [Red] The soul of the people was very discouraged because of the journey.
5 Watu wakamnung'unikia Mungu na Musa: “Kwa nini umetutoa Misiri ili tufa katika jangwa hili? Hapa hakuna mikate, wala maji, na chakula hiki dhaifu kimetukinai.”
The people spoke against God, and against Moses [Drawn out], “Why have you brought us up out of Egypt [Abode of slavery] to die in the wilderness? For there is no bread, and there is no water; and our soul loathes this light bread.”
6 Basi Mungu akatuma nyoka wa sumu kati yao. Wale nyoka wakawauma wale watu; watu wengi walikufa.
Adonai sent fiery serpents among the people, and they bit the people. Many people of Israel [God prevails] died.
7 Watu wakaenda kwa Musa wakamwambia, “Tumetenda dhambi kwa sababu tumemnung'unikia Mungu na wewe. Mwombe Mungu atuondolee hawa nyoka.” Kwa hiyo Musa akawaombea watu.
The people came to Moses [Drawn out], and said, “We have sinned, because we have spoken against Adonai, and against you. Pray to Adonai, that he take away the serpents from us.” Moses [Drawn out] prayed for the people.
8 BWANA akamwambia Musa, “Tengeneza nyoka na umweke kwenye nguzo. Na itakuwa kila anayeumwa, akimwangalia huyo nyoka atapona,”
Adonai said to Moses [Drawn out], “Make a fiery serpent, and set it up on a pole. It shall happen, that everyone who is bitten, when he sees it, shall live.”
9 Kwa hiyo Musa akatengeneza nyoka wa shaba naye akamweka juu ya nguzo. Na kila mtu alipoumwa na nyoka na kumwangalia huyo nyoka alipona.
Moses [Drawn out] made a serpent of bronze, and set it on the pole. If a serpent had bitten any man, when he looked at the serpent of bronze, he lived.
10 Kisha watu wa Israeli wakasafiri na kisha kuweka kambi Obothi.
The children of Israel [God prevails] traveled, and encamped in Oboth.
11 Kisha wakasafiri kutoka pale na kuweka kambi Iye Abarimu katika jangwa linalokabili Moabu kuelekea upande wa mashariki.
They traveled from Oboth, and encamped at Iyeabarim, in the wilderness which is before Moab [From father], toward the sunrise.
12 Kutoka pale wakasafiri na kuweka kambi katika bonde la Zeredi.
From there they traveled, and encamped in the valley of Zered.
13 Kutoka pale walisafiri na kuweka kambi kwenye upande mwingine wa mto Amoni, ambao ukubwa wake unaanzia kwenye mpaka wa Waamori. Mto wa Amoni ndio unaootengeneza mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
From there they traveled, and encamped on the other side of the Arnon, which is in the wilderness, that comes out of the border of the Amorites [Descendants of Talkers]: for the Arnon is the border of Moab [From father], between Moab [From father] and the Amorites [Descendants of Talkers].
14 Ndiyo maana imeandikwa katika gombo la Kitabu cha BWANA, “Wahebu katika Sufa, na bonde la Amoni,
Therefore it is said in the book of the Wars of Adonai, “Vaheb in Suphah, the valleys of the Arnon,
15 mtelemko wa bonde linaloelekea katika mji wa Ari na kuelekea kwenye mpaka wa Moabu,”
the slope of the valleys that incline toward the dwelling of Ar, leans on the border of Moab [From father].”
16 Kutoka pale wakasafiri mpaka Beeri, hapo ndipo palipo na kisima ambacho Bwana alimwambia Musa, “Wakusanye watu kwa ajili yangu ili uwape maji,”
From there they traveled to Beer; that is the well of which Adonai said to Moses [Drawn out], “Gather the people together, and I will give them water.”
17 Ndipo Israeli waipoimba wimbo huu: “enyi visima, yajazeni maji. Imbeni juu ya kisima hiki.
Then Israel [God prevails] sang this song: “Spring up, well! Sing to it,
18 Kisima ambacho viongozi wetu walichimba, kisima ambacho wenye hekima walichimba kwa fimbo ya kifalme na kwa fimbo ya kutembelea.” Kisha kutoka jangwani walitembea mpaka Matanaha.
the well, which the princes dug, which the nobles of the people dug, with the scepter, and with their poles.” From the wilderness they traveled to Mattanah;
19 Kutoka Matanaha walisafiri mpaka Nathalieli, na kutoka Nathalieli mpaka Bamothi,
and from Mattanah to Nahaliel; and from Nahaliel to Bamoth;
20 na kutoka Bamothi hadi kwenye bonde la Moabu. Hapo ndipo kilele cha Mlima Piska kinapoonekana jangwani.
and from Bamoth to the valley that is in the field of Moab [From father], to the top of Pisgah, which looks down on the desert.
21 Kisha Israeli akatuma wajumbe kwa Sihoni mfalme wa Waamori akisema,
Israel [God prevails] sent messengers to Sihon king of the Amorites [Descendants of Talkers], saying,
22 Tunaomba tupite katika nchi yako. hatutapita katika shamba au kwenye shamba la mizabibu. Hatutakunywa maji ya visima vyako. Tutapita katika njia kuu ya mfalme mpaka tutakapopita mpaka wako.”
“Let me pass through your land. We will not turn aside into field, or into vineyard. We will not drink of the water of the wells. We will go by the king’s highway, until we have passed your border.”
23 Lakini mfalme Sihoni hakumruhusu Israeli kupita kwenye mpaka wao. Badala yake, Sihoni akakusanya jeshi lake lote na kumvamia Isreli huko jangwani. Akaja kwa Jahazi, ambapo alipigana dhidi ya Israeli.
Sihon would not allow Israel [God prevails] to pass through his border, but Sihon gathered all his people together, and went out against Israel [God prevails] into the wilderness, and came to Jahaz. He fought against Israel [God prevails].
24 Israeli akalivamia jeshi la Sihoni na nchi ya upanga na kuchukua nchi yao kutoka Amon mpaka mto Jabboki, hadi kufikia nchi ya watu wa Amoni. Sasa mpaka wa watu wa Amoni ulikuwa umefungwa.
Israel [God prevails] struck him with the edge of the sword, and possessed his land from the Arnon to the Jabbok, even to the children of Ammon [Tribal people]; for the border of the children of Ammon [Tribal people] was strong.
25 Israeli akachukua miji yote ya Waamori na akaishi ndani yake, pamoja na Heshiboni na vijiji vyake wote.
Israel [God prevails] took all these cities. Israel [God prevails] lived in all the cities of the Amorites [Descendants of Talkers], in Heshbon, and in all its villages.
26 Heshiboni ulikuwa mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye hapo awali alipigana dhidi ya mfalme wa kwanza wa Moabu. Sihoni alikuwa ameteka ardhi yake yote toka mipaka yake mpaka mto wa Amoni.
For Heshbon was the city of Sihon the king of the Amorites [Descendants of Talkers], who had fought against the former king of Moab [From father], and taken all his land out of his hand, even to the Arnon.
27 Hiyo ndiyo sababu wala ambao huongea kwa Mitahali husema, “Njoni Heshboni. Mji wa Sihoni ujengwe na kuimarishwa tena.
Therefore those who speak in proverbs say, “Come to Heshbon. Let the city of Sihon be built and established;
28 Moto uliwaka toka Heshiboni, moto kutoka mji wa Sihoni ambao uliiteketeza Ari ya Moabu, na wenyeji wa miji ya juu ya Amoni.
for a fire has gone out of Heshbon, a flame from the city of Sihon. It has devoured Ar of Moab [From father], The lords of the high places of the Arnon.
29 Ole wako, Moabu! umepotea, enyi watu wa Chemoshi. Amewafanya watu wake kuwa wakimbizi na binti zake kuwa wafungwa wa Sihoni mfalme wa Waamori.
Woe to you, Moab [From father]! You are undone, people of Chemosh! He has given his sons as fugitives, and his daughters into captivity, to Sihon king of the Amorites [Descendants of Talkers].
30 Lakini tumempiga Sihoni. Tumeiangsmiza Heshibon mpaka Diboni. Tumewaharibu wote mpaka Nofa, ambayo inafika mpaka Madeba.”
We have shot at them. Heshbon has perished even to Dibon. We have laid waste even to Nophah, Which reaches to Medeba.”
31 Kwa hiyo Israeli akaanza kuishi katika nchi ya Waamori,
Thus Israel [God prevails] lived in the land of the Amorites [Descendants of Talkers].
32 Kisha Musa akatuma watu kwenda kuingalia Yaziri. Waliviteka vijiji vyake na kuwafukuza Waamori waliokuwa wakiishi humo.
Moses [Drawn out] sent to spy out Jazer. They took its villages, and drove out the Amorites [Descendants of Talkers] who were there.
33 Kisha wakageuka na kuelekea njia inayoelekea Bashani. Ogu mfalme wa Bashani akatofautiana nao, yeye na Jeshi lake lote, ili apigane nao kule Ederei.
They turned and went up by the way of Bashan. Og the king of Bashan went out against them, he and all his people, to battle at Edrei.
34 Kisha BWANA akasema na Musa, “Msimwogope, kwa sababu nimewapeni ushindi dhidi yake, Jeshi lake lote na nchi yake. Mfanyeni kama mlivyomfanya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekuwa akiishi Heshiboni.”
Adonai said to Moses [Drawn out], “Don’t fear him, for I have delivered him into your hand, with all his people, and his land. You shall do to him as you did to Sihon king of the Amorites [Descendants of Talkers], who lived at Heshbon.”
35 Kwa hiyo wakamuua, na wanawe, na jeshi lake lote, mpaka wote wakaishi na hakubaki hata mmoja aliyebaki hai. Kisha wakaichukua nchi yake.
So they struck him, with his sons and all his people, until there were no survivors; and they possessed his land.

< Hesabu 21 >