< Hesabu 21 >

1 Aradi mfalme wa Wakanaani, aliyekuwa akiishi Negebu, aliposikia kuwa Israeli alikuwa akisafiri kwa kupitia barabara kuelekea Atharimu, akapigana dhidi ya Israeli na kujitwalia baadhi ya mateka.
And the Canaanite, king of Arad, dwelling in the south, hears that Israel has come the way of the Atharim, and he fights against Israel, and takes [some] of them captive.
2 Israeli akaapa mbele ya BWANA akasema, “Kama utatupa ushindi dhidi ya hawa watu, ndipo tutakapoingamiza kabisa miji yao,”
And Israel vows a vow to YHWH and says, “If You certainly give this people into my hand, then I have devoted their cities”;
3 BWANA akaisikia sautiya Israeli na kuwapa ushindi dhidi ya Wakanaani. Wakawaangamiza kabisa pamoja na miji yao. Mahali pale paliitwa Horima.
and YHWH listens to the voice of Israel and gives up the Canaanite, and he devotes them and their cities, and calls the name of the place Hormah.
4 Wakasafiri kutoka Mlima Hori kwa barabara kuelekea bahari ya shamu wakiizunguka nchi ya Edomu. Watu walikufa moyo kwa njia hiyo.
And they journey from Mount Hor, the way of the Red Sea, to go around the land of Edom, and the soul of the people is short in the way,
5 Watu wakamnung'unikia Mungu na Musa: “Kwa nini umetutoa Misiri ili tufa katika jangwa hili? Hapa hakuna mikate, wala maji, na chakula hiki dhaifu kimetukinai.”
and the people speak against God and against Moses, “Why have you brought us up out of Egypt to die in a wilderness? For there is no bread, and there is no water, and our soul has been weary of this light bread.”
6 Basi Mungu akatuma nyoka wa sumu kati yao. Wale nyoka wakawauma wale watu; watu wengi walikufa.
And YHWH sends the burning serpents among the people, and they bite the people, and many people of Israel die;
7 Watu wakaenda kwa Musa wakamwambia, “Tumetenda dhambi kwa sababu tumemnung'unikia Mungu na wewe. Mwombe Mungu atuondolee hawa nyoka.” Kwa hiyo Musa akawaombea watu.
and the people come to Moses and say, “We have sinned, for we have spoken against YHWH and against you; pray to YHWH that He turns the serpent aside from us”; and Moses prays in behalf of the people.
8 BWANA akamwambia Musa, “Tengeneza nyoka na umweke kwenye nguzo. Na itakuwa kila anayeumwa, akimwangalia huyo nyoka atapona,”
And YHWH says to Moses, “Make a burning [serpent] for yourself, and set it on an ensign; and it has been, everyone who is bitten and has seen it—he has lived.”
9 Kwa hiyo Musa akatengeneza nyoka wa shaba naye akamweka juu ya nguzo. Na kila mtu alipoumwa na nyoka na kumwangalia huyo nyoka alipona.
And Moses makes a serpent of bronze, and sets it on the ensign, and it has been, if the serpent has bitten any man, and he has looked expectingly to the serpent of bronze—he has lived.
10 Kisha watu wa Israeli wakasafiri na kisha kuweka kambi Obothi.
And the sons of Israel journey and encamp in Oboth.
11 Kisha wakasafiri kutoka pale na kuweka kambi Iye Abarimu katika jangwa linalokabili Moabu kuelekea upande wa mashariki.
And they journey from Oboth and encamp in Ije-Abarim, in the wilderness that [is] on the front of Moab, at the rising of the sun.
12 Kutoka pale wakasafiri na kuweka kambi katika bonde la Zeredi.
From there they have journeyed and encamp in the Valley of Zared.
13 Kutoka pale walisafiri na kuweka kambi kwenye upande mwingine wa mto Amoni, ambao ukubwa wake unaanzia kwenye mpaka wa Waamori. Mto wa Amoni ndio unaootengeneza mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
From there they have journeyed and encamp beyond Arnon, which [is] in the wilderness which is coming out of the border of the Amorite, for Arnon [is] the border of Moab, between Moab and the Amorite;
14 Ndiyo maana imeandikwa katika gombo la Kitabu cha BWANA, “Wahebu katika Sufa, na bonde la Amoni,
therefore it is said in [the] scroll of the Wars of YHWH: “Waheb in Suphah, And the brooks of Arnon;
15 mtelemko wa bonde linaloelekea katika mji wa Ari na kuelekea kwenye mpaka wa Moabu,”
And the spring of the brooks, Which turned aside to the dwelling of Ar, And has leaned to the border of Moab.”
16 Kutoka pale wakasafiri mpaka Beeri, hapo ndipo palipo na kisima ambacho Bwana alimwambia Musa, “Wakusanye watu kwa ajili yangu ili uwape maji,”
And from there [they journeyed] to Beer; it [is] the well [concerning] which YHWH said to Moses, “Gather the people, and I give water to them.”
17 Ndipo Israeli waipoimba wimbo huu: “enyi visima, yajazeni maji. Imbeni juu ya kisima hiki.
Then Israel sings this song: “Spring up, O well, Let all answer to it!
18 Kisima ambacho viongozi wetu walichimba, kisima ambacho wenye hekima walichimba kwa fimbo ya kifalme na kwa fimbo ya kutembelea.” Kisha kutoka jangwani walitembea mpaka Matanaha.
A well—princes have dug it, Nobles of the people have prepared it, With the lawgiver, with their staffs.” And from the wilderness [they journeyed] to Mattanah,
19 Kutoka Matanaha walisafiri mpaka Nathalieli, na kutoka Nathalieli mpaka Bamothi,
and from Mattanah to Nahaliel, and from Nahaliel to Bamoth,
20 na kutoka Bamothi hadi kwenye bonde la Moabu. Hapo ndipo kilele cha Mlima Piska kinapoonekana jangwani.
and from Bamoth, in the valley which [is] in the field of Moab, [to] the top of Pisgah, which has looked on the front of the wilderness.
21 Kisha Israeli akatuma wajumbe kwa Sihoni mfalme wa Waamori akisema,
And Israel sends messengers to Sihon king of the Amorite, saying,
22 Tunaomba tupite katika nchi yako. hatutapita katika shamba au kwenye shamba la mizabibu. Hatutakunywa maji ya visima vyako. Tutapita katika njia kuu ya mfalme mpaka tutakapopita mpaka wako.”
“Let me pass through your land, we do not turn aside into a field or into a vineyard; we do not drink waters of a well; we go in the king’s way until we pass over your border.”
23 Lakini mfalme Sihoni hakumruhusu Israeli kupita kwenye mpaka wao. Badala yake, Sihoni akakusanya jeshi lake lote na kumvamia Isreli huko jangwani. Akaja kwa Jahazi, ambapo alipigana dhidi ya Israeli.
And Sihon has not permitted Israel to pass through his border, and Sihon gathers all his people, and comes out to meet Israel in the wilderness, and comes to Jahaz, and fights against Israel.
24 Israeli akalivamia jeshi la Sihoni na nchi ya upanga na kuchukua nchi yao kutoka Amon mpaka mto Jabboki, hadi kufikia nchi ya watu wa Amoni. Sasa mpaka wa watu wa Amoni ulikuwa umefungwa.
And Israel strikes him by the mouth of the sword, and possesses his land from Arnon to Jabbok—to the sons of Ammon; for the border of the sons of Ammon [is] strong.
25 Israeli akachukua miji yote ya Waamori na akaishi ndani yake, pamoja na Heshiboni na vijiji vyake wote.
And Israel takes all these cities, and Israel dwells in all the cities of the Amorite, in Heshbon and in all its villages;
26 Heshiboni ulikuwa mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye hapo awali alipigana dhidi ya mfalme wa kwanza wa Moabu. Sihoni alikuwa ameteka ardhi yake yote toka mipaka yake mpaka mto wa Amoni.
for Heshbon is a city of Sihon king of the Amorite, and he has fought against the former king of Moab, and takes all his land out of his hand as far as Arnon;
27 Hiyo ndiyo sababu wala ambao huongea kwa Mitahali husema, “Njoni Heshboni. Mji wa Sihoni ujengwe na kuimarishwa tena.
therefore those using allegories say: “Enter Heshbon, Let the city of Sihon be built and ready,
28 Moto uliwaka toka Heshiboni, moto kutoka mji wa Sihoni ambao uliiteketeza Ari ya Moabu, na wenyeji wa miji ya juu ya Amoni.
For fire has gone out from Heshbon, A flame from the city of Sihon, It has consumed Ar of Moab, Owners of the high places of Arnon.
29 Ole wako, Moabu! umepotea, enyi watu wa Chemoshi. Amewafanya watu wake kuwa wakimbizi na binti zake kuwa wafungwa wa Sihoni mfalme wa Waamori.
Woe to you, O Moab, You have perished, O people of Chemosh! He has given his sons [as] fugitives, And his daughters into captivity, To Sihon king of the Amorite!
30 Lakini tumempiga Sihoni. Tumeiangsmiza Heshibon mpaka Diboni. Tumewaharibu wote mpaka Nofa, ambayo inafika mpaka Madeba.”
And we shoot them; Heshbon has perished as far as Dibon, And we make desolate as far as Nophah, Which [is] as far as Medeba.”
31 Kwa hiyo Israeli akaanza kuishi katika nchi ya Waamori,
And Israel dwells in the land of the Amorite,
32 Kisha Musa akatuma watu kwenda kuingalia Yaziri. Waliviteka vijiji vyake na kuwafukuza Waamori waliokuwa wakiishi humo.
and Moses sends to spy out Jaazer, and they capture its villages, and dispossess the Amorite who [is] there,
33 Kisha wakageuka na kuelekea njia inayoelekea Bashani. Ogu mfalme wa Bashani akatofautiana nao, yeye na Jeshi lake lote, ili apigane nao kule Ederei.
and turn and go up the way of Bashan, and Og king of Bashan comes out to meet them, he and all his people, to battle [at] Edrei.
34 Kisha BWANA akasema na Musa, “Msimwogope, kwa sababu nimewapeni ushindi dhidi yake, Jeshi lake lote na nchi yake. Mfanyeni kama mlivyomfanya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekuwa akiishi Heshiboni.”
And YHWH says to Moses, “Do not fear him, for into your hand I have given him, and all his people, and his land, and you have done to him as you have done to Sihon king of the Amorite, who is dwelling in Heshbon.”
35 Kwa hiyo wakamuua, na wanawe, na jeshi lake lote, mpaka wote wakaishi na hakubaki hata mmoja aliyebaki hai. Kisha wakaichukua nchi yake.
And they strike him, and his sons, and all his people, until he has no remnant left to him, and they possess his land.

< Hesabu 21 >