< Hesabu 20 >

1 Kwa hiyo wana wa Israeli, na jamii yote ya watu, wakaenda katika jangwa la Sini katika mwezi wa kwanza; wakaa Kadeshi. Hapo ndipo Miriamu alipofia na kuzikwa.
And the sons of Israel, and the entire multitude, went into the desert of Sin, in the first month. And the people stayed at Kadesh. And Miriam died there, and she was buried in the same place.
2 Huko hapakuwa na maji kwa ajili ya watu, kwa hiyo wakakusanyika kinyume na Musa na Haruni huko.
And when the people were in need of water, they came together against Moses and Aaron.
3 Watu wakamlalamikia Musa. Wakasema, “Ilikuwa ni bora kama tungelikufa wakati Waisraeli wenzetu walipokufa mbele za BWANA.
And as it turned into sedition, they said: “If only we had perished among our brothers in the sight of the Lord.
4 Kwa nini umewaleta watu wa BWANA kufia katika jangwa hili, sisi na wanyama wetu?
Why have you led away the Church of the Lord, into the wilderness, so that both we and our cattle would die?
5 Kwa nini ulitutoa Misri na kutuleta katika eneo hili baya? Hapa hakuna nafaka, wala mitini, wala mizabibu, wala makomamanga. Na hakuna maji ya kunywa.”
Why did you cause us to ascend from Egypt, and why have you led us into this most wretched place, which is not able to be sown, which does not produce figs, or vines, or pomegranates, and which, moreover, does not even have water to drink?”
6 Basi Musa na Haruni wakatoweka mbele ya mkutano huo. Wakaenda kwenye hema ya kukutania wakalala kifudifudi. Ndipo pale utukufu wa Busara wa BWANA ukaonekana kwao.
And Moses and Aaron, dismissing the multitude, entered the tabernacle of the covenant, and they fell prone on the ground, and they cried out to the Lord, and they said: “O Lord God, listen to the outcry of this people, and open for them, from your storehouse, a fountain of living water, so that, being satisfied, their murmuring may cease.” And the glory of the Lord appeared over them.
7 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And the Lord spoke to Moses, saying:
8 “Chukua fimbo yako na uwakusanye watu, wewe na Haruni ndugu yako. Uumbie huu mwamba mbele ya macho yao, na uumuru utoe maji. Nawe utawapa maji kutoka kwenye huu mwamba, nawe utawapa maji ya kunywa hao watu na wanyama wao.”
“Take the rod, and gather the people, you and your brother Aaron, and speak to the rock before them, and it shall bestow waters. And when you have brought forth water from the rock, the entire multitude and their cattle shall drink.”
9 Musa akachukua hiyo fimbo mbele ya BWANA, kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru kufanya.
Therefore, Moses took the rod, which was in the sight of the Lord, just as he had instructed him.
10 Kisha Musa na Haruni wakawakusanya watu pamoja mbele ya ule mwamba. Ndipo Musa akawaambia, “Sasa sikilizeni, enyi wapinzani. Lazima tuwape maji kutoka kwenye huu mwamba?”
And having gathered the multitude before the rock, he said to them: “Listen, you who are rebellious and unbelieving. Would we be able to cast out water from this rock?”
11 Ndipo Musa akanyosha mkono wake na kuupiga ule mwamba mara mbili kwa fimbo yake, na maji mengi yakatoka. Wale watu wakanywa pamoja na wanyama wao.
And when Moses had lifted up his hand, striking the stone twice with the rod, very great waters went forth, so much so that the people and their cattle were able to drink.
12 Kisha BWANA akamwambia Musa na Haruni, “Kwa kuwa hamkuniheshimu mimi na kuniamini mbele ya watu wa Israeli, hamtawaingiza hawa watu katika nchi niliyowaahidi.
And the Lord said to Moses and Aaron, “Because you did not believe me, so as to sanctify me before the sons of Israel, you shall not lead this people into the land, which I will give to them.”
13 Mahali hapa paliitwa maji ya Meriba kwa sababu wana wa Israeli walitofautiana na BWANA pale, na akajionyesha kwao kuwa mtakatifu.
This is the Water of Contradiction, where the sons of Israel were quarreling against the Lord, and he was sanctified in them.
14 Musa akatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwa mfalme wa Edom: Ndugu yako Israeli anasema hivi: “Wewe unajua magumu yote ambayo yametupata.
Meanwhile, Moses sent messengers from Kadesh to the king of Edom. They said: “Your brother Israel says this: You know of all the hardships which have overtaken us,
15 Na unajua kuwa babu zetu walienda Misri na waliishi Misri kwa muda mrefu. Wamisri walitutendea vibaya pamoja na babu zetu.
how our fathers descended into Egypt, and we lived there for a long time, and the Egyptians afflicted both us and our fathers,
16 Tulipomlilia BWANA, akatusikia na kututumia malaika ambaye alitutoa toka Misri. Tazama, sasa tuko Kadeshi, mji unaopakana na nchi yako.
and how we cried out to the Lord, and he heeded us and sent an Angel, who led us away from Egypt. Behold, we are situated in the city of Kadesh, which is at the extremity of your borders.
17 Tunakuomba uturuhusu kupita katika nchi yako. Hatutapita mashambani wala kwenye mashamba ya mizabibu, wala hatutakunywa maji ya visima vyako. Tutapita kwenye njia kuu ya mfalme. Hatutageuka upande wa kulia wala upande wa kushoto mpaka tutakapopita mpaka wako.”
And we beg you to permit us to cross through your land. We will not go through the fields, nor through the vineyards; we will not drink the waters of your wells, but we will travel by the public ways, neither turning aside to the right, nor to the left, until we have passed your borders.”
18 Lakini mfalme wa Edomu akamjibu, “Msipite hapa. Kama mtafanya hivyo, Nitakuja na upanga kukuvamia.”
Edom responded to them: “You shall not cross through me, otherwise, I will meet you armed.”
19 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia,”tutapitia njia kuu. Kama sisi au wanyama wetu watakunywa maji yako, basi tutalipa. Tunaomba uturuhusu tupite tukitembea kwa miguu yetu, bila kufanya jambo lolote lile.”
And the sons of Israel said: “We will travel by the well-trodden path. And if we or our cattle drink from your waters, we will give you what is just. There shall be no difficulty in the price, only let us cross through quickly.”
20 Lakini mfalme wa Edomu akajibu, “Usipite hapa.” Kwa hiyo nfalme wa Edomu akawa kinyume cha Israeli kwa mkono wenye nguvu pamoja na jeshi kubwa sana.
But he answered, “You shall not cross.” And immediately he went out to meet them with a countless multitude and a strong hand;
21 Mfame wa Edomu akawazuia wana wa Israeli kupita kwenye mipaka yake. Kwa sababu ya hili, Israeli akageuka kuiacha nchi ya Edomu.
neither was he willing to agree to their petition to concede passage through his borders. For this reason, Israel diverted away from him.
22 Kwa hiyo watu wakasafiri kutoka Kadeshi. Wana wa Israeli, watu wote, wakafika Mlima Hori.
And when they had moved the camp from Kadesh, they arrived at mount Hor, which is at the borders of the land of Edom,
23 BWANA akanena na Musa na Haruni hapo kwenye Mlima Hori, kwenye mpaka wa Edomu. Akasema,
where the Lord spoke to Moses:
24 “Sasa ni wakati wa Haruni kukusanyika na watu wake, hataingia katika nchi ile niliyowaahidi wana wa Israeli. Hii ni kwa sababu ninyi wawili hamkuitii sauti yangu pale kwenye maji ya Meriba.
“Let Aaron,” he said, “go to his people. For he shall not enter into the land which I have given to the sons of Israel, because he did not believe my mouth at the Waters of Contradiction.
25 Mchukue Haruni na Eliazari mwanaye, na uwalete juu ya Mlima Hori.
Take Aaron, and his son with him, and lead them on to mount Hor.
26 Umvulishi HarunI yale mavazi ya kikuhani na umvalishe Eliazari mwanaye. Haruni atakufa na kulazwa pamoja na watu wake.”
And when you have stripped the father of his vestments, you shall put them on Eleazar, his son. Aaron shall be gathered and shall die there.”
27 Musa akafanya kama BWANA alivyomwamuru. Wakaenda juu y a Mlima Hori na watu wote wakiona.
Moses did just as the Lord had instructed. And they ascended mount Hor, in the sight of the entire multitude.
28 Musa akamvulisha Haruni yale mavazi ya kikuhani na kumvalisha Mwanaye Eliazari. Haruni akafa pale juu ya Mlima Hori. Kisha Musa na Eliazari wakashuka.
And when he had despoiled Aaron of his vestments, he clothed his son Eleazar with them. And when Aaron had died at the top of the mountain, Moses came down with Eleazar.
29 Watu walipoona kuwa Haruni amekufa, taifa lote wakamlilia Haruni kwa siku arobaini.
And the entire multitude, seeing that Aaron lay dead, wept over him for thirty days, throughout all their families.

< Hesabu 20 >