< Hesabu 2 >
1 BWANA akasema na Musa na Haruni tena. Akamwambia,
Then spake Yahweh onto Moses and onto Aaron saying:
2 Kila mtu atapanga kulingana na mahali pake, pamoja na mabango ya baba zao. Watapanga kuzunguka hema ya kukutania kila upande.
Every man—near his standard with the ensigns belonging to their ancestral houses, shall the sons of Israel encamp, —at a distance round about the tent of meeting, shall they encamp.
3 Wale watakaopanga mashariki mwa hema ya kukutania, mahali ambapo juu huonekana wakati wa jua kuchomoza, ni makambi ya Yuda nao watakuwa katika kundi lao. Nashoni mwana wa Aminadabu ni kiongozi wa watu wa Yuda.
And they who encamp eastwards towards sunrise, shall be the standard of the camp of Judah by their hosts, —even the prince of the sons of Judah, Nashon, son of Amminadab;
4 Idadi ya watu wa Yuda ni 74, 600.
and his host, even they who are numbered of them, —seventy-four thousand and six hundred,
5 Kabila la Isakari litapanga mbele ya Yuda. Nethaneli mwana wa Zuari ataliongoza jeshi la Isakari.
Then they who encamp by him the tribe of Issachar, —even the prince of the sons of Issachar, Nethanel, son of Zuar;
6 Idadi ya kikosi chake ni wanaume 54, 000.
and his host even they who are numbered of them, —fifty-four thousand and four hundred.
7 Kabila la Zabuloni litapanga mbele ya Isakari. Eliabu mwana wa Heloni ndiye atakayeliongoza jeshi la Zabuloni.
The tribe of Zebulun, even the prince of the sons of Zebulun, Eliab, son of Helon;
8 Idadi ya kikosi chake ni 57, 400.
and his host, even they who are numbered of him, fifty-seven thousand and four hundred.
9 Idadi yote ya kambi y a Yuda ni 186, 400. Watakuwa wa kwanza kuondoka.
All they who are num-bered to the camp of Judah. a hundred and eighty-six thousand four hundred, by their hosts, shall first set forward.
10 Upande wa kusini kutakuwa na kambi ya Reubeni katika kundi lao. Kiongozi wa kundi la Reubeni ni Elizuri mwana wa Shedeuri.
The standard of the camp of Reuben southwards, by their hosts, —even the prince of the sons of Reuben, Elizur son of Shedeur;
11 Idadi ya kikosi chake ni 46, 500.
and his host, even they who are numbered of him, —forty-six thousand, and five hundred.
12 Simeoni atapanga mbele ya Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Zurishadai.
Then they who encamp by him, the tribe of Simeon, —even the prince of the sons of Simeon, Shelumiel son of Zurishaddai;
13 Waliohesabiwa kwenye kikosi chake ni 59, 300.
and his host, even they who are numbered of them, —fifty-nine thousand and three hundred.
14 Kabila la Gadi litafuatia. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deuli.
Then the tribe of Gad, even the prince of the sons of Gad, Eliasaph son of Reuel;
15 Idadi ya kikosi chake ni 45, 650.
and his host, even they who are numbered of them, —forty-five thousand, and six hundred and fifty.
16 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Reubeni, kulingana na kikosi chake, ni 151, 450. Watakuwa wa pili kuondoka.
All they who are num-bered to the camp of Reuben, —a hundred and fifty-one thousand and four hundred and fifty, by their hosts, and they in the second rank, shall set forward.
17 Kifuatacho, ni hema la kukutania kuondoka kambini pamoja na Walawi likiwa katikati ya kambi zote. Lazima waondoke hapo kambini kwa mpangilio huo kama walivyoingia kwenye kambi. Kila mwanamume lazima awe mahali pake kwa kufuata bango lake.
Then shall set forward the tent of meeting—the camp of the Levites in the midst of the camps, —as they encamp, so, shall they set forward, every man at the side thereof by their standards.
18 Migawanyiko ya kambi y Efraimu kufuata mahali pake. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
the standard of the camp of Ephraim, by their hosts westwards, —even the prince of the sons of Ephraim, Elishama son of Ammihud;
19 Hesabu ya kikosi hiki ni 40, 500.
and his host, even they who are numbered of them, —forty thousand, and five hundred.
20 Baada ya hao lilifuata kabila la Manase. Kiongozi wa Manase ni Gamaliel mwana wa Pedazuri.
Then by him, the tribe of Manasseh, even the prince of the sons of Manasseh, Gamaliel, son of Pedahzur;
21 Hesabu ya kikosi hiki ni 32, 200.
and his host, even they who are numbered of them, —thirty-two thousand and two hundred.
22 Kabila litakalofuata ni la Benjamini. Kiongozi wa Benjamini n Abidani mwana wa Gidioni.
Then the tribe of Benjamin, even the prince of the sons of Benjamin, Abidan, son of Gideoni;
23 Hesabu ya kikosi hiki ni 35, 000
and his host, even they who are numbered of them, —thirty-five thousand and four hundred.
24 Wote waliohesabiwa katika kambi ya Efraimu ni 108, 100. Watakuwa wa tatu kuondoka.
All they who are numbered to the camp of Ephraim a hundred and eight thousand and one hundred by their hosts, and they in the third rank, shall set forward.
25 Upande wa kaskazini kutakuwa na kambi ya kikosi cha Dani. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
the standard of the camp of Dan, north-wards by their hosts, even the prince of the sons of Dan, Ahiezer, son of Ammishaddai:
26 Hesabu ya kikosi hiki ni 62, 700.
and his host, even they who are numbered of them, —sixty-two thousand and seven hundred.
27 Watu wa kabila ya Asheri watapanga mbele ya Dani. Kiongozi wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okirani.
Then they who encamp by him the tribe of Asher, —even the prince of the sons of Asher, Pagiel, son of Ochran;
28 Hesabu ya Kikosi hiki ni 41, 500.
and his host, even they who are numbered of them, —forty-one thousand and five hundred.
29 Kabila la Naftali ndilo litakalofuatia. Kiongozi wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
Then the tribe of Naphtali, —even the prince of the sons of Naphtali, Ahira, son of Enan;
30 Hesabu ya kikosi hiki ni 53, 400.
and his host, even they who are numbered of them, —fifty-three thousand and four hundred,
31 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Dani ni 157, 600. Hawa watakuwa wa mwisho kuondoka kambini, wakifuata bango lao.
All they who are numbered to the camp of Dan, a hundred and fifty-seven thousand and six hundred, in the hindmost rank, shall they set forward, by their standards.
32 Hawa ndio Waisraeli, waliohesabiwa kufuata familia zao. Wote waliohesabiwa kwenye kambi zao, kwa kufuata vikosi vyao ni 603, 550.
These, are they who were numbered of the sons of Israel by their ancestral houses, —all they who were numbered of the camps by their hosts were six hundred and three thousand and five hundred and fifty.
33 Lakini Musa na Haruni hawakujumuisha Walawi kwenye Hesabu ya Waisrael. Ilikuwa kama BWANA alivyokuwa amemwagiza Musa.
But the Levites, were not numbered in the midst of the sons of Israel, —As Yahweh commanded Moses.
34 Watu wa Israel walifanya yote ambayo BWANA alimwagiza Musa. Walipanga kwa kufuata mabango yao. Walisafiri kutoka kambini kwa kufuata jamaa zao, kwa mpangilio wa familia za koo zao.
Thus did the sons of Israel, —according to all that Yahweh commanded Moses, so, did they encamp by their standards, and so, did they set forward, every one by his families near his ancestral house.