< Hesabu 2 >

1 BWANA akasema na Musa na Haruni tena. Akamwambia,
And the Lord said to Moses and Aaron,
2 Kila mtu atapanga kulingana na mahali pake, pamoja na mabango ya baba zao. Watapanga kuzunguka hema ya kukutania kila upande.
The children of Israel are to put up their tents in the order of their families, by the flags of their fathers' houses, facing the Tent of meeting on every side.
3 Wale watakaopanga mashariki mwa hema ya kukutania, mahali ambapo juu huonekana wakati wa jua kuchomoza, ni makambi ya Yuda nao watakuwa katika kundi lao. Nashoni mwana wa Aminadabu ni kiongozi wa watu wa Yuda.
Those whose tents are on the east side, looking to the dawn, will be round the flag of the children of Judah, with Nahshon, the son of Amminadab, as their chief.
4 Idadi ya watu wa Yuda ni 74, 600.
The number of his army was seventy-four thousand, six hundred.
5 Kabila la Isakari litapanga mbele ya Yuda. Nethaneli mwana wa Zuari ataliongoza jeshi la Isakari.
And nearest to him will be the tribe of Issachar, with Nethanel, the son of Zuar, as their chief.
6 Idadi ya kikosi chake ni wanaume 54, 000.
The number of his army was fifty-four thousand, four hundred.
7 Kabila la Zabuloni litapanga mbele ya Isakari. Eliabu mwana wa Heloni ndiye atakayeliongoza jeshi la Zabuloni.
After him, the tribe of Zebulun, with Eliab, the son of Helon, as their chief.
8 Idadi ya kikosi chake ni 57, 400.
The number of his army was fifty-seven thousand, four hundred.
9 Idadi yote ya kambi y a Yuda ni 186, 400. Watakuwa wa kwanza kuondoka.
The number of all the armies of Judah was a hundred and eighty-six thousand, four hundred. They go forward first.
10 Upande wa kusini kutakuwa na kambi ya Reubeni katika kundi lao. Kiongozi wa kundi la Reubeni ni Elizuri mwana wa Shedeuri.
On the south side is the flag of the children of Reuben, in the order of their armies, with Elizur, the son of Shedeur, as their chief.
11 Idadi ya kikosi chake ni 46, 500.
The number of his army was forty-six thousand, five hundred.
12 Simeoni atapanga mbele ya Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Zurishadai.
And nearest to him, the tribe of Simeon, with Shelumiel, the son of Zurishaddai, as their chief.
13 Waliohesabiwa kwenye kikosi chake ni 59, 300.
The number of his army was fifty-nine thousand, three hundred.
14 Kabila la Gadi litafuatia. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deuli.
Then the tribe of Gad, with Eliasaph, son of Reuel, as their chief.
15 Idadi ya kikosi chake ni 45, 650.
The number of his army was forty-five thousand, six hundred and fifty.
16 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Reubeni, kulingana na kikosi chake, ni 151, 450. Watakuwa wa pili kuondoka.
The number of all the armies of Reuben together came to a hundred and fifty-one thousand, four hundred and fifty. They go forward second.
17 Kifuatacho, ni hema la kukutania kuondoka kambini pamoja na Walawi likiwa katikati ya kambi zote. Lazima waondoke hapo kambini kwa mpangilio huo kama walivyoingia kwenye kambi. Kila mwanamume lazima awe mahali pake kwa kufuata bango lake.
Then the Tent of meeting is to go forward, with the tents of the Levites, in the middle of the armies; in the same order as their tents are placed, they are to go forward, every man under his flag.
18 Migawanyiko ya kambi y Efraimu kufuata mahali pake. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
On the west side will be the flag of the children of Ephraim, with Elishama, the son of Ammihud, as their chief.
19 Hesabu ya kikosi hiki ni 40, 500.
The number of his army was forty thousand, five hundred.
20 Baada ya hao lilifuata kabila la Manase. Kiongozi wa Manase ni Gamaliel mwana wa Pedazuri.
And by him the tribe of Manasseh with Gamaliel, the son of Pedahzur, as their chief.
21 Hesabu ya kikosi hiki ni 32, 200.
The number of his army was thirty-two thousand, two hundred.
22 Kabila litakalofuata ni la Benjamini. Kiongozi wa Benjamini n Abidani mwana wa Gidioni.
Then the tribe of Benjamin, with Abidan, the son of Gideoni, as their chief.
23 Hesabu ya kikosi hiki ni 35, 000
The number of his army was thirty-five thousand, four hundred.
24 Wote waliohesabiwa katika kambi ya Efraimu ni 108, 100. Watakuwa wa tatu kuondoka.
The number of all the armies of Ephraim was a hundred and eight thousand, one hundred. They go forward third.
25 Upande wa kaskazini kutakuwa na kambi ya kikosi cha Dani. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
On the north side will be the flag of the children of Dan, with Ahiezer, the son of Ammishaddai, as their chief.
26 Hesabu ya kikosi hiki ni 62, 700.
The number of his army was sixty-two thousand, seven hundred.
27 Watu wa kabila ya Asheri watapanga mbele ya Dani. Kiongozi wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okirani.
Nearest to him will be the tribe of Asher, with Pagiel, the son of Ochran, as their chief.
28 Hesabu ya Kikosi hiki ni 41, 500.
The number of his army was forty-one thousand, five hundred;
29 Kabila la Naftali ndilo litakalofuatia. Kiongozi wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
Then the tribe of Naphtali, with Ahira, the son of Enan, as their chief.
30 Hesabu ya kikosi hiki ni 53, 400.
The number of his army was fifty-three thousand, four hundred.
31 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Dani ni 157, 600. Hawa watakuwa wa mwisho kuondoka kambini, wakifuata bango lao.
The number of all the armies in the tents of Dan was a hundred and fifty-seven thousand, six hundred. They will go forward last, by their flags.
32 Hawa ndio Waisraeli, waliohesabiwa kufuata familia zao. Wote waliohesabiwa kwenye kambi zao, kwa kufuata vikosi vyao ni 603, 550.
These are all who were numbered of the children of Israel, in the order of their fathers' families: all the armies in their tents together came to six hundred and three thousand, five hundred and fifty.
33 Lakini Musa na Haruni hawakujumuisha Walawi kwenye Hesabu ya Waisrael. Ilikuwa kama BWANA alivyokuwa amemwagiza Musa.
But the Levites were not numbered among the children of Israel, as the Lord said to Moses.
34 Watu wa Israel walifanya yote ambayo BWANA alimwagiza Musa. Walipanga kwa kufuata mabango yao. Walisafiri kutoka kambini kwa kufuata jamaa zao, kwa mpangilio wa familia za koo zao.
So the children of Israel did as the Lord said to Moses, so they put up their tents by their flags, and they went forward in the same order, by their families, and by their fathers' houses.

< Hesabu 2 >