< Hesabu 18 >
1 BWANA akamwambia Haruni, “Wewe, wana wako, na uzao wa baba yako watawajibika kwa dhambi zote zilizotendwa mahali patakatifu. Lakini wewe na wana wako pekee mtawajibika kwa uovu uliofanywa na yeyote mahali patakatifu.
Yahvé dit à Aaron: « Toi, tes fils et la maison de tes pères avec toi, vous porterez l'iniquité du sanctuaire; toi et tes fils avec toi, vous porterez l'iniquité de votre sacerdoce.
2 Na ndugu zako nao wa kabila ya Lawi, kabila la ukoo wako, utawaleta pamoja na wewe ili kwamba waweze kuungana na wewe ili wakusaidie wakati wewe na wanao mnapokuwa mnatumikia mbele ya hema ya amri ya agano.
Fais aussi approcher de toi tes frères, la tribu de Lévi, la tribu de ton père, afin qu'ils soient associés à toi et qu'ils te servent; mais toi et tes fils avec toi, vous serez devant la tente du témoignage.
3 Watakutumikia wewe na hema yote. Hata hivyo, wasisogee karibu na chochote ndani ya mahali patakatifu au kitu chochote kilichounganishwa na madhabahu, vinginevyo wewe na wao mtakufa.
Ils observeront tes ordres et les devoirs de toute la tente; seulement, ils ne s'approcheront pas des ustensiles du sanctuaire ni de l'autel, afin qu'ils ne meurent pas, ni eux ni toi.
4 Wataungana na wewe na kuitunza hema ya kukutania, kwa kazi zote zinazohusiana na hema. Mtu mgeni asikusogelee.
Ils s'attacheront à toi et garderont la responsabilité de la Tente de la Rencontre, pour tout le service de la Tente. L'étranger ne s'approchera pas de toi.
5 Wewe utaajibika kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya madhabahu ili kwamba hasira yangu isiwajilie watu wa Israeli tena.
Vous accomplirez les fonctions du sanctuaire et de l'autel, afin qu'il n'y ait plus de colère contre les enfants d'Israël.
6 Tazama, Mmi mwenyewe nimewachagua ndugu zako wa kabila ya Walawi kutoka mioingoni mwa uzao wa Israeli. Wao ni zawadi kwako. walitolewa kwangu ili waifanye kazi inayohusiana na hema ya kukutania.
Voici, j'ai pris moi-même vos frères les Lévites parmi les enfants d'Israël. Ils te sont offerts, ils sont consacrés à l'Éternel, pour faire le service de la Tente de la Rencontre.
7 Lakini ni wewe pekee yako na wanao ndio mnaoruhusiwa kufanya kazi ya ukuhani kuhusiana na kila kitu kilichounganishwa na madhabahu na kitu chochote ndani ya lile pazia. Wewe mwenyewe lazima ukamilishe majukumu hayo. Mimi ninakupa ukuhani kama zawadi. Mgeni yeyote anayekaribia atauawa.”
Toi et tes fils avec toi, vous exercerez votre sacerdoce pour tout ce qui concerne l'autel et ce qui est en deçà du voile. Tu feras le service. Je vous fais don du service de la prêtrise. L'étranger qui s'approchera sera mis à mort. »
8 Kisha BWANA akamwambia Haruni, “Tazama, Nimekupa majukumu ya kusimamia sadaka za kuinuliwa kwangu, na sadaka zengine takatifu ambazo wana wa Israeli wanatoa kwangu. Nimekupa sadaka hizi wewe na wana wako kuwa haki yako milele.
Yahvé parla à Aaron: « Voici, je t'ai donné moi-même l'ordre d'offrir mes offrandes par agitation, toutes les choses saintes des enfants d'Israël. Je te les ai données, à cause de l'onction, ainsi qu'à tes fils, comme une part pour toujours.
9 Hivi ni vitu vitakatifu sana, amabavyo visiteketezwe kwa moto: kutoka kwenye sadaka zao-kila sadaka ya unga, kila sadaka ya dhambi, na kila sadaka ya hatia- ni vitu vitakatifu sana kwa ajili yako na wana wako.
Voici ce qui vous appartiendra parmi les choses très saintes du feu: toute offrande qu'ils m'offriront, toute offrande de farine, tout sacrifice pour le péché et tout sacrifice de culpabilité, sera très sainte pour vous et pour vos fils.
10 Sadaka hizi ni takatifu sana; kila mume lazima aile, kwa kuwa ni vitakatifu kwako.
Vous en mangerez comme des choses très saintes. Tout mâle en mangera. Ce sera pour vous une chose sainte.
11 Hizi ni sadaka ambazo zitakuwa zako: Sadaka zao, sadaka zote za kuinuliwa za wana wa Israeli. Nimekupa wewe, wana wako na binti zako kuwa gawio lako la milele. Kila mmoja ambaye ni msafi katika familia yako anaweza kula sadaka zozote katika hizi.
« Ceci est aussi à toi: l'offrande de leurs dons, toutes les offrandes des enfants d'Israël. Je te les ai données, à toi, à tes fils et à tes filles avec toi, comme une part pour toujours. Tous ceux qui sont purs dans ta maison en mangeront.
12 Mafuta yote mazuri, ile divai nzuri yote mpya na unga, malimbuko ambyo watu hutoa kwangu- vitu hivi vyote nimekupa wewe.
« Je te donne tout le meilleur de l'huile, tout le meilleur de la vendange et du blé, les prémices de ce qu'ils apportent à l'Éternel.
13 Mavuno ya kwanza yaliyoiva yaliyo katika ardhi yao ambayo wanaleta kwangu, yatakuwa yako. Kila mtu aliye msafi kwenye famila yako anaweza kula vitu hivi.
Les prémices de tout ce qui se trouve dans leur pays, qu'ils apporteront à l'Éternel, seront à toi. Tous ceux qui sont propres dans votre maison en mangeront.
14 Kila kitu kilichotolewa wakfu katika Israeli kitakuwa chako.
« Tout ce qui est consacré en Israël sera à toi.
15 Kila kitu kinachofungua tumbo, kila limbuko ambalo watu hutoa kwa BWANA, vyote vya watu na wanyama, vitakuwa vyako. Hata hivyo, watu lazima wawakomboe wazaliwa wa kwanza wa kiume, na watawakomboa wazaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi.
Tout ce qui ouvre le ventre, de toute chair qu'on offre à l'Éternel, tant des hommes que des animaux, sera à vous. Toutefois, vous rachèterez les premiers-nés des hommes et vous rachèterez les premiers-nés des animaux impurs.
16 Wale ambao wanahitaji kukombolewa na watu watakombolewa wakiwa na umri wa mwezi mmoja. Ndipo watu watawakomboa kwa bei ya shekeli tano, kwa kiwango cha shekeli za mahali patakatifu, ambacho ni sawa na gera ishirini.
Tu rachèteras ceux d'entre eux qui sont âgés d'un mois, selon ton estimation, pour cinq sicles d'argent, selon le sicle du sanctuaire, qui pèse vingt gérachs.
17 Lakini mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe, au mzaliwa wa kwana wa kondoo, au mzaliwa wa kwanza wa mbuzi-msiwakomboe hawa wanyama, wametengwa kwa ajili yangu. Utanyunyizia damu yake madhabahuni na kuteketeza mafuta yao kama sadaka ya moto, ambayo ni harufu nzuri ya kumpendeza BWANA.
« Mais tu ne rachèteras pas le premier-né d'une vache, ni le premier-né d'une brebis, ni le premier-né d'une chèvre. Ils sont saints. Tu feras l'aspersion de leur sang sur l'autel, et tu brûleras leur graisse en offrande consumée par le feu, comme une odeur agréable à Yahvé.
18 Nyama yao itakuwa yako. Kama kidali cha kuinuliwa na paja la kulia, nyama yao itakuwa yako.
Leur viande sera à toi, comme la poitrine offerte par onction et comme la cuisse droite, elle sera à toi.
19 Sadaka yote takatifu ambayo watu wa Israeli wanaitoa kwa BWANA, nimekupa wewe, na wana wako na binti zako walio pamoja nawe. Kama gawio la kudumu. Hili ni agano la milele la chumvi, agano linalofunga milele, mbele za BWANA kwako wewe na uzao wako walio pamoja na wewe.”
Toutes les offrandes par ondulation des choses saintes que les enfants d'Israël offrent à l'Éternel, je vous les donne, à vous, à vos fils et à vos filles avec vous, comme une part pour toujours. C'est une alliance de sel pour toujours devant l'Éternel, pour toi et pour ta descendance avec toi. »
20 BWANA akasema na Haruni. “hautakuwa na urithi katika ardhi ya watu, wala hautakuwa na gawio miongoni mwa watu. Mimi ndimi gawiio lenu na urithi wenu miongoni mwa watu wa Israeli.
Yahvé dit à Aaron: « Tu n'auras pas d'héritage dans leur pays, et tu n'auras pas de part au milieu d'eux. Je suis ta part et ton héritage parmi les enfants d'Israël.
21 Tazama, Nimewapatia uzao wa Lawi, zaka zote za Israeli kuwa urithi wao kwa sababu ya huduma wanayotoa katika hema ya kukutania.
« Aux fils de Lévi, voici, j'ai donné en héritage toute la dîme en Israël, en contrepartie du service qu'ils font, le service de la tente d'assignation.
22 Kuanzi a sasa, watu wa Israeli wasisogee karibu na hema ya kukutania, vinginevyo wataajibika kwa dhambi hii na kufa.
Désormais, les enfants d'Israël ne s'approcheront plus de la Tente de la Rencontre, de peur de porter le péché et de mourir.
23 Walawi wafanya kazi inayohusiana na hema ya kukutania. Wataajibika kwa dhambi inyohusiana na hema. Hii itakuwa sheri ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Na miongoni mwa watu wa Israeli hawa hawatakuwa na urithi.
Mais les Lévites feront le service de la Tente d'assignation, et ils porteront leur faute. Ce sera une loi pour toujours, de génération en génération. Ils n'auront pas d'héritage parmi les enfants d'Israël.
24 Kwa kuwa zaka za wana wa Israeli, wanazotoa kama mchango kwangu -ndivyo hivyo ambavyo nimewapa Walawi kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu ya kuwaambia, Kuwa hawatakuwa na urithi kati ya watu wa Israeli.
En revanche, j'ai donné en héritage aux Lévites la dîme des enfants d'Israël, qu'ils offrent en offrande à Yahvé. C'est pourquoi je leur ai dit: « Ils n'auront pas d'héritage parmi les enfants d'Israël. »
25 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
Yahvé parla à Moïse et dit:
26 “Inakupasa ukaseme na Walawi uwaambie, 'Mnapopokea zaka toka kwa watu ambayo BWANA amewapa kutoka kwao kuwa urithi, ndipo na nyie mtakapotoa sehemu ya kumi ya zaka hizo.
Tu parleras aux Lévites et tu leur diras: « Lorsque vous prélèverez sur les enfants d'Israël la dîme que je vous donne en héritage, vous en ferez une offrande pour Yahvé, la dîme de la dîme.
27 Zaka yenu itahesabika kama moja ya mapato ya sakafu ya kupuria nafaka ya mazao yenu au mazao ya vinu vya kukamulia zabibu.
Ton offrande ondulatoire te sera créditée comme le grain de l'aire et comme la plénitude de la cuve.
28 Kwa hiyo na ninyi lazima mtoe mchango wenu kwa BWANA kutokana na zaka mnazopata kutoka kwa watu wa Israeli. Kutokana na hizo mtatoa matoleo yenu kwa Haruni yule kuhani.
C'est ainsi que tu présenteras à l'Éternel une offrande par ondulation de toutes les dîmes que tu recevras des enfants d'Israël, et tu en donneras une au prêtre Aaron.
29 Kwa kila sadaka mnayopata, mtatoa matoleo yenu kwa BWANA. Mtafanya hivi kutokana na vitu vizuri na vitakatifu sana ambavyo mmepewa.
De toutes vos offrandes, vous présenterez à Yahvé chaque offrande par ondulation, dans toutes ses parties les meilleures, même la partie sainte.''
30 Kwa hiyo utawaambia, 'Mnapotoa hayo matoleo mazuri, ndipo itahesabika kwa Walawi kuwa ni mazao yao kutoka kwenye sakafu za kupuria na vinu vyao vya kukamulia.
Tu leur diras: « Lorsque vous en aurez récolté le meilleur, il sera porté au crédit des Lévites comme le produit de l'aire de battage et comme le produit du pressoir.
31 Ndipo matakapokula nafaka zote zinazobaki mahali popote, ninyi na famailia zenu kwa sababu ndiyo malipo yenu ya kazi y a kwenye hema ya kukutania.
Vous pourrez en manger partout, vous et vos familles, car c'est votre récompense pour votre service dans la Tente de la Rencontre.
32 Hamtakuwa na hatia yeyote kwa kuvila na kuvinywa, kama mtatoa kwa BWANA matoleo yenu mazuri mliyopokea. Lakini msizinajisi sadaka takatifu za wana wa Israeli, vinginevyo mtakufa.,”
Tu ne porteras pas de péché à cause d'elle, lorsque tu en auras tiré le meilleur. Tu ne profaneras pas les choses saintes des enfants d'Israël, afin de ne pas mourir.'"