< Hesabu 18 >

1 BWANA akamwambia Haruni, “Wewe, wana wako, na uzao wa baba yako watawajibika kwa dhambi zote zilizotendwa mahali patakatifu. Lakini wewe na wana wako pekee mtawajibika kwa uovu uliofanywa na yeyote mahali patakatifu.
And the Lord said unto Aaron, Thou and thy sons and thy father's house with thee shall bear the iniquity of the sanctuary; and thou and thy sons with thee shall bear the iniquity of your priesthood.
2 Na ndugu zako nao wa kabila ya Lawi, kabila la ukoo wako, utawaleta pamoja na wewe ili kwamba waweze kuungana na wewe ili wakusaidie wakati wewe na wanao mnapokuwa mnatumikia mbele ya hema ya amri ya agano.
And also thy brethren, the tribe of Levi, the tribe of thy father, bring thou near with thee, that they may be joined with thee, and minister unto thee; while thou and thy sons with thee shall be before the tabernacle of the testimony.
3 Watakutumikia wewe na hema yote. Hata hivyo, wasisogee karibu na chochote ndani ya mahali patakatifu au kitu chochote kilichounganishwa na madhabahu, vinginevyo wewe na wao mtakufa.
And they shall keep thy charge, and the charge of all the tabernacle: only unto the vessels of the sanctuary and unto the altar shall they not come near, that they may not die, either they or you.
4 Wataungana na wewe na kuitunza hema ya kukutania, kwa kazi zote zinazohusiana na hema. Mtu mgeni asikusogelee.
And they shall be joined unto thee, and keep the charge of the tabernacle of the congregation, respecting all the service of the tabernacle: and a stranger shall not come nigh unto you.
5 Wewe utaajibika kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya madhabahu ili kwamba hasira yangu isiwajilie watu wa Israeli tena.
And ye shall keep the charge of the sanctuary, and the charge of the altar; that there be not any more wrath upon the children of Israel.
6 Tazama, Mmi mwenyewe nimewachagua ndugu zako wa kabila ya Walawi kutoka mioingoni mwa uzao wa Israeli. Wao ni zawadi kwako. walitolewa kwangu ili waifanye kazi inayohusiana na hema ya kukutania.
And I, behold, I have taken your brethren the Levites from the midst of the children of Israel; unto you are they given as a gift for the Lord, to perform the service of the tabernacle of the congregation.
7 Lakini ni wewe pekee yako na wanao ndio mnaoruhusiwa kufanya kazi ya ukuhani kuhusiana na kila kitu kilichounganishwa na madhabahu na kitu chochote ndani ya lile pazia. Wewe mwenyewe lazima ukamilishe majukumu hayo. Mimi ninakupa ukuhani kama zawadi. Mgeni yeyote anayekaribia atauawa.”
And thou and thy sons with thee shall keep your priesthood concerning every matter of the altar, and for that within the vail, where ye shall serve: as a service of gift do I give you your priesthood; and the stranger that cometh nigh shall be put to death.
8 Kisha BWANA akamwambia Haruni, “Tazama, Nimekupa majukumu ya kusimamia sadaka za kuinuliwa kwangu, na sadaka zengine takatifu ambazo wana wa Israeli wanatoa kwangu. Nimekupa sadaka hizi wewe na wana wako kuwa haki yako milele.
And the Lord spoke unto Aaron, And I, behold, I give thee the charge of my heave-offerings; of all the hallowed things of the children of Israel, unto thee have I given them as an official portion, and to thy sons, as a fixed right for ever.
9 Hivi ni vitu vitakatifu sana, amabavyo visiteketezwe kwa moto: kutoka kwenye sadaka zao-kila sadaka ya unga, kila sadaka ya dhambi, na kila sadaka ya hatia- ni vitu vitakatifu sana kwa ajili yako na wana wako.
This shall belong to thee of the most holy things, from the fire-[offerings]: every oblation of theirs, namely, every meat-offering of theirs, and every sin-offering of theirs, and every, trespass-offering of theirs, which they shall render unto me, shall, as most holy things, belong to thee and to thy sons.
10 Sadaka hizi ni takatifu sana; kila mume lazima aile, kwa kuwa ni vitakatifu kwako.
In a most holy place shalt thou eat it: every male shall eat it; holy shall it be unto thee.
11 Hizi ni sadaka ambazo zitakuwa zako: Sadaka zao, sadaka zote za kuinuliwa za wana wa Israeli. Nimekupa wewe, wana wako na binti zako kuwa gawio lako la milele. Kila mmoja ambaye ni msafi katika familia yako anaweza kula sadaka zozote katika hizi.
And this shall be thine, as the heave-offering of their gift, of all the wave-offerings of the children of Israel; unto thee have I given them, and to thy sons and to thy daughters with thee, as a fixed portion for ever: every one that is clean in thy house may eat thereof.
12 Mafuta yote mazuri, ile divai nzuri yote mpya na unga, malimbuko ambyo watu hutoa kwangu- vitu hivi vyote nimekupa wewe.
All the best of oil, and all the best of wine, and of corn, the first-fruits thereof which they shall offer unto the Lord, to thee have I given them.
13 Mavuno ya kwanza yaliyoiva yaliyo katika ardhi yao ambayo wanaleta kwangu, yatakuwa yako. Kila mtu aliye msafi kwenye famila yako anaweza kula vitu hivi.
The first ripe fruit of whatsoever is in their land, which they may bring unto the Lord, shall be thine: every one that is clean in thy house may eat thereof.
14 Kila kitu kilichotolewa wakfu katika Israeli kitakuwa chako.
Every thing devoted in Israel shall be thine.
15 Kila kitu kinachofungua tumbo, kila limbuko ambalo watu hutoa kwa BWANA, vyote vya watu na wanyama, vitakuwa vyako. Hata hivyo, watu lazima wawakomboe wazaliwa wa kwanza wa kiume, na watawakomboa wazaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi.
Whatever openeth the womb of all flesh, which they bring unto the Lord, be it of men or of cattle, shall be thine: nevertheless thou shalt redeem the first-born of man, and the firstling of the unclean cattle shalt thou redeem.
16 Wale ambao wanahitaji kukombolewa na watu watakombolewa wakiwa na umri wa mwezi mmoja. Ndipo watu watawakomboa kwa bei ya shekeli tano, kwa kiwango cha shekeli za mahali patakatifu, ambacho ni sawa na gera ishirini.
And those that are to be redeemed from a month old shalt thou redeem, according to the usual estimation of five shekels of silver, after the shekel of the sanctuary, which is twenty gerahs.
17 Lakini mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe, au mzaliwa wa kwana wa kondoo, au mzaliwa wa kwanza wa mbuzi-msiwakomboe hawa wanyama, wametengwa kwa ajili yangu. Utanyunyizia damu yake madhabahuni na kuteketeza mafuta yao kama sadaka ya moto, ambayo ni harufu nzuri ya kumpendeza BWANA.
But the firstling of an ox, or the firstling of a sheep, or the firstling of a goat, thou shalt not redeem; they are holy: their blood shalt thou sprinkle upon the altar, and their fat shalt thou burn as a fire-offering, for a sweet savor unto the Lord.
18 Nyama yao itakuwa yako. Kama kidali cha kuinuliwa na paja la kulia, nyama yao itakuwa yako.
And their flesh shall be thine: as the breast that is waved and as the right shoulder shall it be thine.
19 Sadaka yote takatifu ambayo watu wa Israeli wanaitoa kwa BWANA, nimekupa wewe, na wana wako na binti zako walio pamoja nawe. Kama gawio la kudumu. Hili ni agano la milele la chumvi, agano linalofunga milele, mbele za BWANA kwako wewe na uzao wako walio pamoja na wewe.”
All the heave-offerings of the holy things, which the children of Israel set apart unto the Lord, I have given to thee, and to thy sons and to thy daughters with thee, as a fixed portion for ever: it is a covenant of salt for ever before the Lord for thee and for thy seed with thee.
20 BWANA akasema na Haruni. “hautakuwa na urithi katika ardhi ya watu, wala hautakuwa na gawio miongoni mwa watu. Mimi ndimi gawiio lenu na urithi wenu miongoni mwa watu wa Israeli.
And the Lord said unto Aaron, In their land shalt thou have no inheritance, and any portion shalt thou not have among them: I am thy portion and thy inheritance among the children of Israel.
21 Tazama, Nimewapatia uzao wa Lawi, zaka zote za Israeli kuwa urithi wao kwa sababu ya huduma wanayotoa katika hema ya kukutania.
And to the children of Levi, behold, I have given every tithe in Israel, for an inheritance, in lieu of their service which they render, the service of the tabernacle of the congregation.
22 Kuanzi a sasa, watu wa Israeli wasisogee karibu na hema ya kukutania, vinginevyo wataajibika kwa dhambi hii na kufa.
And the children of Israel shall not henceforth come nigh unto the tabernacle of the congregation, to bear sin, to die thereby.
23 Walawi wafanya kazi inayohusiana na hema ya kukutania. Wataajibika kwa dhambi inyohusiana na hema. Hii itakuwa sheri ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Na miongoni mwa watu wa Israeli hawa hawatakuwa na urithi.
But they of the tribe of Levi themselves shall perform the service of the tabernacle of the congregation, and they shall bear their iniquity: a statute for ever shall it be throughout your generations; and among the children of Israel shall they not possess any inheritance.
24 Kwa kuwa zaka za wana wa Israeli, wanazotoa kama mchango kwangu -ndivyo hivyo ambavyo nimewapa Walawi kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu ya kuwaambia, Kuwa hawatakuwa na urithi kati ya watu wa Israeli.
But the tithes of the children of Israel, which they offer as a heave-offering unto the Lord, have I given to the Levites for an inheritance: therefore have I said unto them, Among the children of Israel shall they obtain no inheritance.
25 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
26 “Inakupasa ukaseme na Walawi uwaambie, 'Mnapopokea zaka toka kwa watu ambayo BWANA amewapa kutoka kwao kuwa urithi, ndipo na nyie mtakapotoa sehemu ya kumi ya zaka hizo.
And unto the Levites shalt thou speak, and say unto them, When ye take from the children of Israel the tithes which I have given you from them for your inheritance: then shall ye separate therefrom a heave-offering of the Lord, the tenth part of the tithe.
27 Zaka yenu itahesabika kama moja ya mapato ya sakafu ya kupuria nafaka ya mazao yenu au mazao ya vinu vya kukamulia zabibu.
And your heave-offering shall be reckoned unto you, like the corn of the threshing-floor, and as the fulness of the wine-press.
28 Kwa hiyo na ninyi lazima mtoe mchango wenu kwa BWANA kutokana na zaka mnazopata kutoka kwa watu wa Israeli. Kutokana na hizo mtatoa matoleo yenu kwa Haruni yule kuhani.
Thus shall ye also offer a heave-offering unto the Lord from all your tithes, which ye may receive from the children of Israel; and ye shall give thereof the heave-offering of the Lord to Aaron the priest.
29 Kwa kila sadaka mnayopata, mtatoa matoleo yenu kwa BWANA. Mtafanya hivi kutokana na vitu vizuri na vitakatifu sana ambavyo mmepewa.
From all your gifts shall ye set apart every heave-offering of the Lord, from every best part thereof, its hallowed portion therefrom.
30 Kwa hiyo utawaambia, 'Mnapotoa hayo matoleo mazuri, ndipo itahesabika kwa Walawi kuwa ni mazao yao kutoka kwenye sakafu za kupuria na vinu vyao vya kukamulia.
And thou shalt say unto them, When ye have separated the best thereof from it: then shall [the remainder] be counted unto the Levites as the produce of the threshing-floor, and as the produce of the wine-press.
31 Ndipo matakapokula nafaka zote zinazobaki mahali popote, ninyi na famailia zenu kwa sababu ndiyo malipo yenu ya kazi y a kwenye hema ya kukutania.
And ye may eat it in every place, ye and your households; for it is your reward in lieu of your service at the tabernacle of the congregation.
32 Hamtakuwa na hatia yeyote kwa kuvila na kuvinywa, kama mtatoa kwa BWANA matoleo yenu mazuri mliyopokea. Lakini msizinajisi sadaka takatifu za wana wa Israeli, vinginevyo mtakufa.,”
And ye shall not bear any sin by reason of it, when ye have separated its best part from it: and the holy things of the children of Israel shall ye not profane, lest ye die.

< Hesabu 18 >