< Hesabu 15 >
1 Kisha BWANA akanena na Musa, akasema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Sema na wana wa Israeli uwaambie, 'Mtakapoingia katka nchi ambayo mtaishi, ambayo BWANA atawapa,
Speak to [the] people of Israel and you will say to them that you will go into [the] land of dwelling places your which I [am] about to give to you.
3 mtatakiwa kuandaa sadaka kwa moto kwa BWANA, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kukamilisha kiapo au sadaka ya hiari, au sadaka katika sikukuu zenu, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA ya ng'ombe au ya kondoo.
And you will make a fire offering to Yahweh a burnt offering or a sacrifice to fulfill a vow or a freewill offering or at appointed feasts your to make an odor of soothing to Yahweh from the herd or from the flock.
4 Utamtolea BWANA sadaka ya kuteketezwa pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya sadaka ya unga mwembamba uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
And he will bring near the [one who] brings near offering his to Yahweh a grain offering fine flour one tenth [of an ephah] mixed with [the] fourth of hin oil.
5 Na tena mtatoa pamoja na sadaka ya kuteketezwa, au kwa sadaka ya divai robo ya hini ya sadaka ya vinywaji kwa kila mwanakondoo.
And wine for the drink offering fourth of hin you will offer with the burnt offering or for the sacrifice for the lamb one.
6 Kama unatoa sadaka ya kondoo dume, utaandaa sadaka ya unga ya sehemu za kumi mbili za efa ya unga mwembamba uliochanganywa na sehemu ya tatu ya hini ya divai.
Or for the ram you will offer a grain offering fine flour two tenths [of an ephah] mixed with oil third of hin.
7 Kwa sadaka ya kinywaji, mtatoa sehemu ya tatu ya hini ya divai ambayo itatoa harufu nzuri kwa BWANA.
And wine for the drink offering third of hin you will bring near an odor of soothing to Yahweh.
8 Utakapoandaa fahari kwa ajiliy a sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo, au sadaka ya amani kwa BWANA,
And if you will offer a young one of cattle a burnt offering or a sacrifice to fulfill a vow or peace offerings to Yahweh.
9 Ndipo utakapotoa sadaka ya fahari pamoja na sadaka ya unga ya sehemu za kumi tatu za unga mwembamba uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
And he will bring near with [the] young one of cattle a grain offering fine flour three tenths [of an ephah] mixed with oil half of hin.
10 Mtatoa sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai, sadaka iloyotengenezwa kwa moto ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
And wine you will bring near for the drink offering half of hin a fire offering of an odor of soothing to Yahweh.
11 Itafanyika hivi kwa kila fahari, kwa kila kondoo dume, na kila mwanakondoo dume au mbuzi mchanga.
Thus it will be done for the bull one or for the ram one or for the small livestock among the lambs or among the kids.
12 Kila sdaka utakayoindaa na kuitoa itafanyika kama ilivyoanishwa hapa.
According to the number which you will offer thus you will do for the one according to number their.
13 Wazawa wote wa Israeli watafanya mambo haya kwa utaratibu huu, yeyote atakayeleta sadaka iliyotengenezwa kwa moto, ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
Every native-born he will do thus these [things] to bring near a fire offering of an odor of soothing to Yahweh.
14 Na kama kuna mgeni anayeishi kati yenu, au yeyote atakayeishi na watu wa vizazi vyenu vyote, lazima atengeneze sadaka iliytoengenezwa kwa moto, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Atafanya kama mnavyofanya.
And if he will sojourn with you a sojourner or [one] who [is] among midst of you to generations your and he will offer a fire offering of an odor of soothing to Yahweh just as you do so he will do.
15 Kutakuwa na sheria hiyo hiyo kwa watu wote na kwa mgeni anayeishi kati yenu, sheria ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Ninyi mlivyo, ndivyo atakavyokuwa mgeni aliyeishi kati yenu. Atafanya kama mnavyofanya mbele ya BWANA.
The assembly a statute one [will belong] to you and to the sojourner who sojourns a statute of perpetuity to generations your as you as the sojourner it will be before Yahweh.
16 Sheria na amri hiyohiyo ndiyo itakayotumika kwa mgeni anayeishi kati yenu.”
A law one and judgment one it will belong to you and to the sojourner who sojourns with you.
17 Tena BWANA akanena na Musa, akasema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
18 “Nena wana wa Israeli uwaambie, 'mtakapofika katika nchi ninayowapeleka,
Speak to [the] people of Israel and you will say to them when come you into the land where I [am] about to bring you there.
19 mtakapokula chakula kinachozalishwa katika nchi hiyo, mtatoa sadaka ya kunipendeza mimi.
And it will be when eat you from [the] food of the land you will offer up a contribution to Yahweh.
20 Kutoka kwenye mikate yenu ya kwanza mtatoa mkate wa kuinuliwa kama sadaka iliyoinuliwa kutoka mahali pa kupuria nafaka. Mtaiinua kwa jinsi hii.
[the] first of Dough your a cake you will offer up a contribution like a contribution of [the] threshing floor so you will offer up it.
21 Watu wa uzao wako wote wtanitolea sadaka ya kuinuliwa kutoka kwenye unga wenu wa kwanza.
Some of [the] first of dough your you will give to Yahweh a contribution to generations your.
22 Wakati mwingine mtafanya dhambi pasipo kukusudia, Kama hamtatii amri zote hizi ambazo nimemwambia Musa
And if you will err and not you will observe all the commandments these which he has spoken Yahweh to Moses.
23 -kila kitu ambacho nimewaamuru kupitia Musa kuanzia siku ambayo nilianza kuwaamuru na kuendelea kwa watu wote wa uzao wako.
All that he has commanded Yahweh to you by [the] hand of Moses from the day when he commanded Yahweh and onwards to generations your.
24 Kwa swala la dhambi isiyokusudiwa ambayo watu wote hawaijui, basi watu wote watatoa fahari mchanga sadaka ya kuteketezwa ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Pamoja na haya yote, lazima itengenezwe sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji, kama ilivyoagaizwa katika amri, na beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
And it will be if away from [the] eyes of the congregation it was done to inadvertence and they will offer all the congregation a young bull a young one of cattle one to a burnt offering to an odor of soothing to Yahweh and grain offering its and drink offering its according to the ordinance and a male goat of goats one to a sin offering.
25 Kuhani atafanya sadaka upatanisho kwa watu wote wa Israeli. Watasemehewa kwa sababu dhambi haikukusudiwa. Wametoa sadaka yao, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili yangu. Wameleta sadaka yao kwangu iliyotengenezwa kwa moto. Wameleta sadaka yao ya uovu mbele yangu kwa ajili ya kosa lao.
And he will make atonement the priest on all [the] congregation of [the] people of Israel and it will be forgiven to them for [was] inadvertence it and they they have brought offering their a fire offering to Yahweh and sin offering their before Yahweh on inadvertence their.
26 Ndipo watu wote wa Israeli watasamehewa, pia wageni wote wanaoishi kati yao, kwa sababu watu wote walitenda dhambi pasipo kukusudia.
And it will be forgiven to all [the] congregation of [the] people of Israel and to the sojourner who sojourns in midst of them for to all the people by inadvertence.
27 Kama mtu atatenda dhambi bila kukusudia, atatoa mbuzi jike wa umri wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
And if a person one it will sin by inadvertence and it will bring near a female goat a daughter of year its to a sin offering.
28 Naye kuhani atafanya upatanisho kwa BWANA kwa ajili ya mtu yule aliyefanya dhambi pasipo kukusudia. Yule mtu atasamehewa baada ya upatanisho kufanyika.
And he will make atonement the priest on the person who has gone astray by sin by inadvertence before Yahweh to make atonement on him and it will be forgiven to him.
29 Mtakuwa na sheria hiyohiyo kwa mtu yeyote anayefanya dhambi hiyo pasipo kukusudia, sheria hiyohiyo hata kwa mzawa wa Isreli na kwa wageni wanaoishi kati yao.
The native-born among [the] people of Israel and to the sojourner who sojourns in midst of them a law one it will belong to you for the [one who] acts by inadvertence.
30 Lakini mtu afanyaye chochote kwa KUkusudia, awe mzawa au mgeni, ananikufuru mimi. Huyo mtu ataondolewa kati ya watu wake.
And the person who it will act - with a hand raised one of the native-born and one of the sojourner[s] Yahweh he [is] blaspheming and it will be cut off the person that from [the] midst people its.
31 Kwa sababu atakuwa amedharau neno langu na amevunja neno amri yangu, mtu huyo ataondolewa kabisa. Dhambi yake itakuwa juu yake.'”
For [the] word of Yahweh he has despised and commandment his he has broken certainly - it will be cut off the person that iniquity its [will be] on it.
32 Wakati wana wa Israeli walipokuwa katika jangwa, wakamuona mwanamume akikusanya kuni sikiu ya Sabato.
And they were [the] people of Israel in the wilderness and they found a man gathering wood on [the] day of the sabbath.
33 Wale waliomwona wakamleta kwa Musa, Haruni na kwa watu wote.
And they brought near him the [ones who] found him gathering wood to Moses and to Aaron and to all the congregation.
34 Wakamweka kifungoni kwa sababu ilikuwa haijaamuliwa atakachotendewa.
And they left him in custody for not it had been decided what? will it be done to him.
35 Kisha BWANA akanena na Musa, “Yule mwanamume lazima auawe. Watu wote lazima wampige kwa mawe nje ya kambi.”
And he said Yahweh to Moses certainly he will be put to death the man it will stone him with stones all the congregation from [the] outside of the camp.
36 Kwa hiyo watu wote wakamtoa nje ya kambi nao wakampiga kwa mawe mpaka akafa kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
And they brought out him all the congregation to from [the] outside of the camp and they stoned him with stones and he died just as he had commanded Yahweh Moses.
37 BWANA akanena na Musa tena, akasema,
And he said Yahweh to Moses saying.
38 “Waambie wana wa Israeli na uwaamuru wajifanyie vishada wavining'inize katika mapindo ya mavazi yao, wavining'ineze katika ncha zote kwa nyuzi za rangi ya samawi. Watu wote watafanya hivi kwa watu wote wa kizazi chote.
Speak to [the] people of Israel and you will say to them and they will make for themselves tassel[s] on [the] corners of clothes their to generations their and they will put on [the] tassel[s] of the corner a cord of violet stuff.
39 Huu utakuwa ukumbusho maalumu kwenu, kila mtakapovitazama, mtakumbuka amri zangu, na kuzishika ili kwamba msije mkatangatanga katika mioyo na macho yenu na kuwa waasherati wa hayo.
And it will become for you tassel[s] and you will see it and you will remember all [the] commandments of Yahweh and you will observe them and not you will go about after own heart your and after own eyes your which you [are] acting as prostitutes after them.
40 Fanyeni hivi ili kwamba mweze kukumbuka na kutii amri zangu zote, na ili kwamba mpate kuwa watakatifu, waliotunzwa kwa ajili yangu, Mungu wenu.
So that you may remember and you will observe all commandments my and you will be holy to God your.
41 Mimi ndimi BWANA Mungu wenu niliyekutoa toka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
I [am] Yahweh God your who I brought out you from [the] land of Egypt to become for you God I [am] Yahweh God your.