< Hesabu 15 >

1 Kisha BWANA akanena na Musa, akasema,
And the Lord spoke to Moses, saying,
2 “Sema na wana wa Israeli uwaambie, 'Mtakapoingia katka nchi ambayo mtaishi, ambayo BWANA atawapa,
Speak to the children of Israel, and you shall say to them, When you are come into the land of your habitation, which I give to you,
3 mtatakiwa kuandaa sadaka kwa moto kwa BWANA, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kukamilisha kiapo au sadaka ya hiari, au sadaka katika sikukuu zenu, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA ya ng'ombe au ya kondoo.
and you will offer whole burnt offerings to the Lord, a whole burnt offering or a meat-offering to perform a vow, or a free-will offering, or to offer in your feasts a sacrifice of sweet savor to the Lord, whether of the herd or the flock:
4 Utamtolea BWANA sadaka ya kuteketezwa pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya sadaka ya unga mwembamba uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
then he that offers his gift to the Lord shall bring a meat-offering of fine flour, a tenth part of an ephah mingled with oil, even with the fourth part of a hin.
5 Na tena mtatoa pamoja na sadaka ya kuteketezwa, au kwa sadaka ya divai robo ya hini ya sadaka ya vinywaji kwa kila mwanakondoo.
And for a drink-offering you shall offer the fourth part of a hin on the whole burnt offering, or on the meat-offering: for every lamb you shall offer so much, as a sacrifice, a smell of sweet savor to the Lord.
6 Kama unatoa sadaka ya kondoo dume, utaandaa sadaka ya unga ya sehemu za kumi mbili za efa ya unga mwembamba uliochanganywa na sehemu ya tatu ya hini ya divai.
And for a ram, when you offer it as a whole burnt offering or as a sacrifice, you shall prepare as a meat-offering two tenths of fine flour mingled with oil, the third part of a hin.
7 Kwa sadaka ya kinywaji, mtatoa sehemu ya tatu ya hini ya divai ambayo itatoa harufu nzuri kwa BWANA.
And you shall offer for a smell of sweet savor to the Lord wine for a drink-offering, the third part of a hin.
8 Utakapoandaa fahari kwa ajiliy a sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo, au sadaka ya amani kwa BWANA,
And if you sacrifice [a bullock] from the herd for a whole burnt offering or for a sacrifice, to perform a vow or a peace-offering to the Lord,
9 Ndipo utakapotoa sadaka ya fahari pamoja na sadaka ya unga ya sehemu za kumi tatu za unga mwembamba uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
then [the worshipper] shall offer upon the calf a meat-offering, three tenth deals of fine flour mingled with oil, [even] the half of a hin.
10 Mtatoa sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai, sadaka iloyotengenezwa kwa moto ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
And wine for a drink-offering the half of a hin, a sacrifice for a smell of sweet savor to the Lord.
11 Itafanyika hivi kwa kila fahari, kwa kila kondoo dume, na kila mwanakondoo dume au mbuzi mchanga.
Thus shall you do to one calf or to one ram, or to one lamb of the sheep or kid of the goats.
12 Kila sdaka utakayoindaa na kuitoa itafanyika kama ilivyoanishwa hapa.
According to the number of what you shall offer, so shall you do to each one, according to their number.
13 Wazawa wote wa Israeli watafanya mambo haya kwa utaratibu huu, yeyote atakayeleta sadaka iliyotengenezwa kwa moto, ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
Every native of the country shall do thus to offer such things as sacrifices for a smell of sweet savor to the Lord.
14 Na kama kuna mgeni anayeishi kati yenu, au yeyote atakayeishi na watu wa vizazi vyenu vyote, lazima atengeneze sadaka iliytoengenezwa kwa moto, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Atafanya kama mnavyofanya.
And if there should be a stranger among you in your land, or one who should be born to you among your generations, and he will offer a sacrifice, a smell of sweet savor to the Lord—as you do, so the [whole] congregation shall offer to the Lord.
15 Kutakuwa na sheria hiyo hiyo kwa watu wote na kwa mgeni anayeishi kati yenu, sheria ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Ninyi mlivyo, ndivyo atakavyokuwa mgeni aliyeishi kati yenu. Atafanya kama mnavyofanya mbele ya BWANA.
There shall be one law for you and for the strangers dwelling among you, a perpetual law for your generations: as you [are], so shall the stranger be before the Lord.
16 Sheria na amri hiyohiyo ndiyo itakayotumika kwa mgeni anayeishi kati yenu.”
There shall be one law and one ordinance for you, and for the stranger that abides among you.
17 Tena BWANA akanena na Musa, akasema,
And the Lord spoke to Moses, saying,
18 “Nena wana wa Israeli uwaambie, 'mtakapofika katika nchi ninayowapeleka,
Speak to the sons of Israel, and you shall say to them, When you are entering into the land, into which I bring you,
19 mtakapokula chakula kinachozalishwa katika nchi hiyo, mtatoa sadaka ya kunipendeza mimi.
then it shall come to pass, when you shall eat of the bread of the land, you shall separate a wave-offering, a special offering to the Lord, the first fruits of your dough.
20 Kutoka kwenye mikate yenu ya kwanza mtatoa mkate wa kuinuliwa kama sadaka iliyoinuliwa kutoka mahali pa kupuria nafaka. Mtaiinua kwa jinsi hii.
You shall offer your bread a heave-offering: as a heave-offering from the threshing floor, so shall you separate it,
21 Watu wa uzao wako wote wtanitolea sadaka ya kuinuliwa kutoka kwenye unga wenu wa kwanza.
even the first fruits of your dough, and you shall give the Lord a heave-offering throughout your generations.
22 Wakati mwingine mtafanya dhambi pasipo kukusudia, Kama hamtatii amri zote hizi ambazo nimemwambia Musa
But whenever you shall transgress, and not perform all these commands, which the Lord spoke to Moses;
23 -kila kitu ambacho nimewaamuru kupitia Musa kuanzia siku ambayo nilianza kuwaamuru na kuendelea kwa watu wote wa uzao wako.
as the Lord appointed you by the hand of Moses, from the day which the Lord appointed you and forward throughout your generations,
24 Kwa swala la dhambi isiyokusudiwa ambayo watu wote hawaijui, basi watu wote watatoa fahari mchanga sadaka ya kuteketezwa ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Pamoja na haya yote, lazima itengenezwe sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji, kama ilivyoagaizwa katika amri, na beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
then it shall come to pass, if a trespass be committed unwillingly, unknown to the congregation, then shall all the congregation offer a calf of the herd without blemish for a whole burnt offering of sweet savor to the Lord, and its meat-offering and its drink-offering according to the ordinance, and one kid of the goats for a sin-offering.
25 Kuhani atafanya sadaka upatanisho kwa watu wote wa Israeli. Watasemehewa kwa sababu dhambi haikukusudiwa. Wametoa sadaka yao, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili yangu. Wameleta sadaka yao kwangu iliyotengenezwa kwa moto. Wameleta sadaka yao ya uovu mbele yangu kwa ajili ya kosa lao.
And the priest shall make atonement for all the congregation of the children of Israel, and [the trespass] shall be forgiven them, because it is involuntary; and they have brought their gift, a burnt offering to the Lord for their trespass before the Lord, even for their involuntary sins.
26 Ndipo watu wote wa Israeli watasamehewa, pia wageni wote wanaoishi kati yao, kwa sababu watu wote walitenda dhambi pasipo kukusudia.
And it shall be forgiven as respects all the congregation of the children of Israel, and the stranger that is dwelling among you, because [it is] involuntary to all the people.
27 Kama mtu atatenda dhambi bila kukusudia, atatoa mbuzi jike wa umri wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
And if one soul sin unwillingly, he shall bring one she-goat of a year old for a sin-offering.
28 Naye kuhani atafanya upatanisho kwa BWANA kwa ajili ya mtu yule aliyefanya dhambi pasipo kukusudia. Yule mtu atasamehewa baada ya upatanisho kufanyika.
And the priest shall make atonement for the soul that committed the trespass unwillingly, and that sinned unwillingly before the Lord, to make atonement for him.
29 Mtakuwa na sheria hiyohiyo kwa mtu yeyote anayefanya dhambi hiyo pasipo kukusudia, sheria hiyohiyo hata kwa mzawa wa Isreli na kwa wageni wanaoishi kati yao.
There shall be one law for the native among the children of Israel, and for the stranger that abides among them, whoever shall commit a trespass unwillingly.
30 Lakini mtu afanyaye chochote kwa KUkusudia, awe mzawa au mgeni, ananikufuru mimi. Huyo mtu ataondolewa kati ya watu wake.
And whatever soul either of the natives or of the strangers shall do any thing with a presumptuous hand, he will provoke God; that soul shall be cut off from his people,
31 Kwa sababu atakuwa amedharau neno langu na amevunja neno amri yangu, mtu huyo ataondolewa kabisa. Dhambi yake itakuwa juu yake.'”
for he has set at nothing the word of the Lord and broken his commands: that soul shall be utterly destroyed, his sin [is] upon him.
32 Wakati wana wa Israeli walipokuwa katika jangwa, wakamuona mwanamume akikusanya kuni sikiu ya Sabato.
And the children of Israel were in the wilderness, and they found a man gathering sticks on the sabbath-day.
33 Wale waliomwona wakamleta kwa Musa, Haruni na kwa watu wote.
And they who found him gathering sticks on the sabbath-day brought him to Moses and Aaron, and to all the congregation of the children of Israel.
34 Wakamweka kifungoni kwa sababu ilikuwa haijaamuliwa atakachotendewa.
And they placed him in custody, for they did not determine what they should do to him.
35 Kisha BWANA akanena na Musa, “Yule mwanamume lazima auawe. Watu wote lazima wampige kwa mawe nje ya kambi.”
And the Lord spoke to Moses, saying, Let the man be by all means put to death: [do you] all the congregation, stone him with stones.
36 Kwa hiyo watu wote wakamtoa nje ya kambi nao wakampiga kwa mawe mpaka akafa kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
And all the congregation brought him forth out of the camp; and all the congregation stoned him with stones outside the camp, as the Lord commanded Moses.
37 BWANA akanena na Musa tena, akasema,
And the Lord spoke to Moses, saying,
38 “Waambie wana wa Israeli na uwaamuru wajifanyie vishada wavining'inize katika mapindo ya mavazi yao, wavining'ineze katika ncha zote kwa nyuzi za rangi ya samawi. Watu wote watafanya hivi kwa watu wote wa kizazi chote.
Speak to the children of Israel, and you shall tell them; and let them make for themselves fringes upon the borders of their garments throughout their generations: and you shall put upon the fringes of the borders a lace of blue.
39 Huu utakuwa ukumbusho maalumu kwenu, kila mtakapovitazama, mtakumbuka amri zangu, na kuzishika ili kwamba msije mkatangatanga katika mioyo na macho yenu na kuwa waasherati wa hayo.
And it shall be on your fringes, and you shall look on them, and you shall remember all the commands of the Lord, and do them: and you shall not turn back after your imaginations, and after [the sight of your] eyes in the things after which you go a whoring;
40 Fanyeni hivi ili kwamba mweze kukumbuka na kutii amri zangu zote, na ili kwamba mpate kuwa watakatifu, waliotunzwa kwa ajili yangu, Mungu wenu.
that you may remember and perform all my commands, and you shall be holy to your God.
41 Mimi ndimi BWANA Mungu wenu niliyekutoa toka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
I [am] the Lord your God that brought you out of the land of Egypt, to be your God: I [am] the Lord your God.

< Hesabu 15 >