< Hesabu 11 >

1 Sasa watu wakanung'unika juu ya matatizo yao wakati BWANA alipokuwa akiwasikiliza. BWANA akawasikia watu naye akakasirika. Moto kutoka kwa BWANA ukashuka na ukawaka kati yao na kuteketeza baadhi ya kambi kwenye pembe zake.
Le peuple affecta de se plaindre amèrement aux oreilles du Seigneur. Le Seigneur l’entendit et sa colère s’enflamma, le feu de l’Éternel sévit parmi eux, et déjà il dévorait les dernières lignes du camp.
2 Ndipo watu wakamwita Musa kwa nguvu, Naye Musa akamwomba BWANA, na ule moto ukazimika.
Mais le peuple implora Moïse; Moïse pria le Seigneur, et le feu s’affaissa.
3 Mahali pale paliitwa Tabera, kwa sababu moto wa BWANA uliwaka kati yao.
On nomma cet endroit Tabérah, parce que le feu de l’Éternel y avait sévi parmi eux.
4 Baadhi ya wageni wakaanza kuweka kambi zao pamoja na wana wa wa Israeli. Walitaka kula chakula kizuri. Kisha wana wa Israeli walipoanza kulia wakisema, “Ni nani atakayetupatia nyama za kula?
Or, le ramas d’étrangers qui était parmi eux fut pris de convoitise; et, à leur tour, les enfants d’Israël se remirent à pleurer et dirent: "Qui nous donnera de la viande à manger?
5 Tunakumbuka samaki tulizokula bure kule Misri, yale matango, na matikiti maji, na mboga na vitunguu na vitunguu saumu.
Il nous souvient du poisson que nous mangions pour rien en Egypte, des concombres et des melons, des poireaux, des oignons et de l’ail.
6 Na sasa hatuna hamu ya kula, kwa sababu tunaona mana tu.
Maintenant, nous sommes exténués, nous manquons de tout: point d’autre perspective que la manne!"
7 Mana ilifanana na punje ya mtama. ilionekana kama bedola.
(Or, la manne était comme de la graine de coriandre, et son aspect comme l’aspect du bdellium.
8 watu wakazunguka kisha wakakusanyika. Wakaisaga, wakaitwanga kwa vinu, wakaitokosa nyunguni, na kuitengeneza mikate. radha yake ilikuwa kama mafuta mapya ya mizeituni.
Le peuple se dispersait pour la recueillir, puis on l’écrasait sous la meule ou on la pilait au mortier; on la mettait cuire au pot, et l’on en faisait des gâteaux. Elle avait alors le goût d’une pâtisserie à l’huile.
9 Na umande ulipoanguka kambini usiku ule, na mana ilianguka pia.
Lorsque la rosée descendait sur le camp, la nuit, la manne y tombait avec elle).
10 Musa akawasikia watu wakilia katika familia zao, na kila mtu alikuwa kwenye lango la hema yake. BWANA alikasirika sana, na mbele ya macho ya Musa malalamiko yao yalikuwa mabaya.
Moïse entendit le peuple gémir, groupé par familles, chacun à l’entrée de sa tente. L’Éternel entra dans une grande colère; Moïse en fut contristé,
11 Musa akasema na BWANA, “Kwa nini umemtendea mtumishi wako vibaya namna hiyo? kwa nini hujapendezwa na mimi? unanifanya kubeba mizigo ya hawa watu.
et il dit à l’Éternel: "Pourquoi as-tu rendu ton serviteur malheureux? Pourquoi n’ai-je pas trouvé grâce à tes yeux, et m’as-tu imposé le fardeau de tout ce peuple?
12 Je, mimi ndiye niliyewatungia mimba hawa watu? Mimi ndiye niliyewazaa kiasi kwamba unaniambia, “wabebe kwa ukaribu vifuani mwako kama baba abebavyo mtoto wake? Je, nitawabeba mpaka kwenye nchi ambayo uliwaahidi mababu zao kuwapa?
Est-ce donc moi qui ai conçu tout ce peuple, moi qui l’ai enfanté, pour que tu me dises: Porte-le dans ton sein, comme le nourricier porte le nourrisson, jusqu’au pays que tu as promis par serment à ses pères?
13 Naweza kupata wapi nyama za kuwapa watu wote hawa? Wanalia mbele zangu na wanasema, 'tupe nyama tule.'
Où trouverai-je de la chair pour tout ce peuple, qui m’assaille de ses pleurs en disant: Donne-nous de la chair à manger!
14 Mimi peke yangu siwezi kuwabeba watu wote hawa. Ni wengi sana kwangu.
Je ne puis, moi seul, porter tout ce peuple: c’est un faix trop pesant pour moi.
15 Kwa vile unanitendea hivi, basi uniue, na kama wewe ni mpole kwangu, basi niondolee mzigo huu.”
Si tu me destines un tel sort, ah! Je te prie, fais-moi plutôt mourir, si j’ai trouvé grâce à tes yeux! Et que je n’aie plus cette misère en perspective!"
16 BWANA akamwambia Musa, “Niletee wazee sabini miongoni mwa Waisraeli. Hakikisha ni wazee na viongozi wa watu. Uwalete kwenye hema ya kukutania wasimame pamoja na wewe.
L’Éternel répondit à Moïse: "Assemble-moi soixante-dix hommes entre les anciens d’Israël, que tu connaisses pour être des anciens du peuple et ses magistrats; tu les amèneras devant la tente d’assignation, et là ils se rangeront près de toi.
17 Nami nitashuka niseme nawe mahali pale. Nitatoa sehemu ya roho iliyo ndani yako na kuwapatia wao. Nao watabeba mzigo wa watu pamoja nawe. na hautaubeba peke yako.
C’Est là que je viendrai te parler, et je retirerai une partie de l’esprit qui est sur toi pour la faire reposer sur eux: alors ils porteront avec toi la charge du peuple, et tu ne la porteras plus à toi seul.
18 Waambie watu, 'Jitakaseni ninyi wenyewe, kwa kuwa kesho mtakuala nyama, kwa kuwa mmelia na BWANA amesikia, “Mlipokuwa mkisema kuwa nani atakayetupa nyama tule? Kule Misri tulikula chakula kizuri!” Kwa hiyo BWANA atawapeni nyama, nanyi mtakula nyama.
Quant à ce peuple, tu lui diras: Tenez-vous prêts pour demain, vous mangerez de la chair, puisque vous avez sangloté aux oreilles de l’Éternel en disant: "Qui nous donnera de la viande à manger? Nous étions plus heureux en Egypte!" L’Éternel vous en donnera à manger, de la viande.
19 Hamtakula nyama kwa siku moja tu, au siku mbili, au siku tano, au siku kumi, au siku ishirini,
Ce n’est pas un jour ni deux que vous en mangerez; ce n’est pas cinq jours, ni dix jours, ni vingt jours,
20 Lakini mtakula nyama kwa mwezi mmoja mpaka zitakapowatokea puani. Mpaka zitawakinai kwa sababu mmemkataa BWANA ambaye yuko kati yenu. Mmelia mbele yake. mmesema, “Kwa nini tulitoka Misri?””
mais un mois entier, tellement qu’elle vous ressortira de la gorge et vous deviendra en horreur; parce que vous avez outragé l’Éternel qui est au milieu de vous, et que vous avez pleuré devant lui en disant: Pourquoi sommes-nous sortis de l’Egypte?"
21 Kisha Musa akasema, “Mimi nina watu 600, 000, na wewe umesema, “Nitawapa nyama mle kwa mwezi mmoja,'
Moïse repartit: "Six cent mille voyageurs composent le peuple dont je fais partie, et tu veux que je leur donne de la viande à manger pour un mois entier!
22 Je, tutayachinja haya makundi ya ng'ombe na kondoo ili kuwatosheleza?”
Faudra-t-il leur tuer brebis et bœufs, pour qu’ils en aient assez? Leur amasser tous les poissons de la mer, pour qu’ils en aient assez?"
23 BWANA akasema na Musa, “Je mkono wangu ni mfupi? Sasa utaona kama maneno yangu ni ya kweli ama sivyo.
Et l’Éternel dit à Moïse: "Est-ce que le bras de l’Éternel est trop court? Tu verras bientôt si ma parole s’accomplit devant toi ou non."
24 Musa alitoka nje kwenda kuwaambia watu maneno ya BWANA. Aliwakusanya wazee sabini wa watu na kuwaweka kuizunguka hema.
Moïse se retira, et rapporta au peuple les paroles de l’Éternel; puis il réunit soixante-dix hommes parmi les anciens du peuple et les rangea autour de la tente.
25 BWANA akashuka chini katika wingu akaongea na Musa. BWANA akachukua sehemu ya roho iliyokuwa kwa Musa na kuiweka kwa wale wazee sabini. Roho alipowashukia, wakaanza kutoa unabii, lakini ilitokea kwenye tukio hilo tu na haikujirudia tena.
L’Éternel descendit dans une nuée et lui parla, et, détournant une partie de l’esprit qui l’animait, la reporta sur ces soixante-dix personnages, sur les anciens. Et aussitôt que l’esprit se fut posé sur eux, ils prophétisèrent, mais ils ne le firent plus depuis.
26 Watu wawili waitwao Elidadi na Medadi walibaki kambini. Lakini Roho aliwashukia pia. Majina yao yalikuwa yameandikwa kwenye orodha lakini walikuwa hawajaenda hemani. Hata hivyo nao walitoa unabii wakiwa kambini.
Deux de ces hommes étaient restés dans le camp, l’un nommé Eldad, le second Médad. L’Esprit se posa également sur eux, car ils étaient sur la liste, mais ne s’étaient pas rendus à la tente; et ils prophétisèrent dans le camp.
27 Kijana mmoja huko kambini alikimbia akaenda kumwambia Musa, “Elidadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
Un jeune homme courut l’annoncer à Moïse, en disant: "Eldad et Médad prophétisent dans le camp."
28 Joshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Musa, ambaye ni miongoni mwa wale aliowachagua akamwambia Musa, “Bwana wangu Musa, wazuie.”
Alors Josué, fils de Noun, serviteur de Moïse depuis sa jeunesse, prit la parole et dit: "Mon maître Moïse, empêche-les!"
29 Musa akamwambia, “una wivu kwa niaba yangu? Natamani kama watu wote wa BWANA wangekuwa manabii na kwamba angeweka Roho yake juu yao wote!”
Moïse lui répondit: "Tu es bien zélé pour moi! Ah! Plût au Ciel que tout le peuple de Dieu se composât de prophètes, que l’Éternel fit reposer son esprit sur eux!"
30 Kisha Musa na wale wazee wakarudi kambini.
Et Moïse rentra dans le camp, ainsi que les anciens d’Israël.
31 Kisha upepo ukavuma kutoka kwa BWANA ukaja na kware kutokea baharini. Wakaanguka karibu na kambi, kiasi cha umbali wa safari ya siku moja upande huu na umbali wa siku moja upande mwingine. Wale kware wakaizunguka kambi kiasi cha mita moja toka uso wa dunia.
Cependant un vent s’éleva de par l’Éternel, qui suscita des cailles du côté de la mer, et les abattit sur le camp dans un rayon d’une journée de part et d’autre, autour du camp, et à la hauteur de deux coudées environ sur le sol.
32 Watu wakawakusanya hao kware kwa bidii mchana huo wote na usiku huo wote, na mchana wote uliofuatia. Hakuna aliyekusanya pungufu ya mita mbili za uajazo. Wakawaanika kweye ardhi yote hapo kambini.
Le peuple s’occupa tout ce jour-là, toute la nuit, et toute la journée du lendemain, à ramasser les cailles; celui qui en recueillit le moins en eut encore dix omer. Et ils se mirent à les étaler autour du camp.
33 Wakati ile nyama ikiwa bado iko kwenye meno yao, wakiwa bado wanatafuna, BWANA akawakasirikia. Akwapiga watu wale kwa gonjwa kubwa sana.
La chair était encore entre leurs dents, elle n’était pas encore consommée, lorsque la colère du Seigneur éclata contre le peuple, et le Seigneur frappa le peuple d’une mortalité très considérable.
34 Mahali pale paliitwa Kibroti Hataava, kwa sababu pale walizika watu waliotamani nyama.
On donna à ce lieu le nom de Kibroth-Hattaava, parce que c’est là qu’on ensevelit ce peuple pris de convoitise.
35 Kutoka Kibroti Hataava watu wakasafiri hadi Hazeroti, ambapo walipumzika.
De Kibroth-Hattaava, le peuple partit pour Hacêroth, et il s’arrêta à Hacêroth.

< Hesabu 11 >