< Hesabu 10 >

1 BWANA alinena na Musa, akasema,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
2 “tengenza tarumbeta mbili za fedha. Uzitengeneze kwa kufua hizo fedha. Utazitumia hizo tarumbeta kwa kuwaita watu waje pamoja na kwa kuwaita watu wote wakati wa kuondoka kwenye kambi zao.
« Fais-toi deux trompettes d’argent; tu les feras d’argent battu. Elles te serviront pour la convocation de l’assemblée et pour la levée des camps.
3 Makuhani watapiga tarumbeta kwa ajili ya kuwaita watu wote mbele yako kwenye lango la hema ya kukutania.
Quand on en sonnera, toute l’assemblée se réunira auprès de toi, à l’entrée de la tente de réunion.
4 Kama makuhani watapiga tarumbeta moja tu, basi viongozi, vichwa koo za Israeli ndipo watakapokutana kwako.
Si l’on ne sonne que d’une trompette, les princes seulement, les chefs des milliers d’Israël, se réuniront auprès de toi.
5 Utakapopiga tarumbeta ya sauti kuu, ile kambi ya upande wa mashariki itaanza kusafiri.
Quand vous sonnerez avec éclat, ceux qui campent à l’orient se mettront en marche;
6 Nawe utakapopiga tarumeta kwa sauti kuu mara ya pili, ile kambi ya upande wa kusini wataanza kusafiri. Watapiga tarumbeta kwa sauti kuu ili kuanza safari yao.
quand vous sonnerez avec éclat pour la seconde fois, ceux qui campent au midi se mettront en marche; on sonnera avec éclat pour leur départ.
7 Watu wote watakapokutana pamoja, piga hizo tarumbeta lakini si kwa sauti kuu.
Vous sonnerez aussi pour convoquer l’assemblée, mais non avec éclat.
8 Wana wa Haruni, makuhani, watapiga hizo tarumbeta. Huu ndio utakaokuwa utaratibu wa watu wako kwa vizazi vyote.
Les fils d’Aaron, les prêtres, sonneront des trompettes: ce sera une loi perpétuelle pour vous et pour vos descendants.
9 Nanyi mtakapoenda vitani katika ardhi yenu dhidi ya maadui wenu wanaowakandamiza, ndipo mtakapotoa ishara ya sauti ya tarumbeta. Mimi, BWANA Mungu wako nitawaita kuwakumbuka na kuwaokoa kutoka kwa maadui wenu.
Quand vous irez à la guerre dans votre pays contre l’ennemi qui vous attaquera, vous sonnerez des trompettes avec éclat, et vous serez rappelés au souvenir de Yahweh, votre Dieu, et vous serez délivrés de vos ennemis.
10 Pia, wakati wa kusherehekea, sikukuu zenu za kawaida na katika miandamo ya miezi, mtapiga tarumbeta zenu kwa heshima ya sadaka zenu za kuteketezwa na kwa sadaka zenu za amani. Huu utakuwa ukumbusho wenu kwangu, Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
Dans vos jours de joie, dans vos fêtes et à vos nouvelles lunes, vous sonnerez des trompettes, en offrant vos holocaustes et vos sacrifices pacifiques, et elles seront pour vous un mémorial devant votre Dieu. Je suis Yahweh, votre Dieu. »
11 Katika siku ya ishrini, mwezi wa pili, mwaka wa pili, Lile wingu liliinuliwa toka masikani ya amri za maagano.
La seconde année, au vingtième jour du deuxième mois, la nuée s’éleva de dessus la Demeure du témoignage;
12 Wana wa Israeli wakaendelea na safari yao toka jangwa la Sinai. Lile wingu likasimama kwenye jangwa la Parani.
et les enfants d’Israël, reprenant leurs marches, partirent du désert de Sinaï, et la nuée s’arrêta dans le désert de Pharan.
13 Walifanya safari yao ya kwanza, kufuatia amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa.
Ils se mirent en marche pour la première fois, suivant le commandement de Yahweh par l’organe de Moïse.
14 Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda iliondoka ya kanza, wakiondoa majeshi yao binafsi. Nashoni mwana wa Aminadabu ndiye aliyeongoza jeshi la Yuda.
La bannière du camp des fils de Juda partit la première, selon leurs troupes, et la troupe de Juda était commandée par Nahasson, fils d’Aminadab;
15 Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
la troupe de la tribu des fils d’Issachar était commandée par Nathanaël, fils de Suar;
16 Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.
et la troupe de la tribu des fils de Zabulon était commandée par Éliab, fils de Hélon.
17 Uzao wa Gerishoni na Merari, ambao walitunza masikani, na kuanza kusafiri.
La Demeure fut démontée, et les fils de Gerson et les fils de Mérari partirent, portant la Demeure.
18 Baadaye Walifuata jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni walianza safari yao. Elizuri mwana wa Shedeuri alliongoza jeshi la Reubebni.
La bannière du camp de Ruben partit, selon leurs troupes, et la troupe de Ruben était commandée par Elisur, fils de Sédéur;
19 Shelumieli mwana wa Zurishadai aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Simeoni.
la troupe de la tribu des fils de Siméon était commandée par Salamiel, fils de Surisaddaï;
20 Eliasafu mwana Deuli aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Gadi.
et la troupe de la tribu des fils de Gad était commandée par Éliasaph, fils de Duel.
21 Kabila la Kohathi nalo lilianza safari. Wao walibebba vyombo vya mahali patakatifu. Wengine waliisimamisha masikani kabla ya Wakohathi kufika kambi inayofuata.
Les Caathites partirent portant les objets sacrés, et les autres dressaient la Demeure, en attendant leur arrivée.
22 Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu ndio waliofuata. Elishama mwana wa Amihudi ndiye aliyeongoza jeshi la Efraimu.
La bannière du camp des fils d’Éphraïm partit, selon leurs troupes et la troupe d’Éphraïm était commandée par Élisama, fils d’Ammiud;
23 Gamalieli mwana wa Pedazuri aliongoza jeshi la uzao wa Manase.
la troupe de la tribu des fils de Manassé était commandée par Gamaliel, fils de Phadassur,
24 Abidani mwana wa Gidioni aliongoza jeshi la uzao wa kabila la Benjamini.
et la troupe de la tribu de Benjamin était commandée par Abidan, fils de Gédéon.
25 Lile jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la uzao wa Dani lilikuwa la mwisho kuondoka. Ahizeri mwana wa Amishadai ndiye aliyeongoza jeshi la Dani.
La bannière du camp des fils de Dan partit, selon leurs troupes: elle formait l’arrière-garde de tous les camps. La troupe de Dan était commandée par Ahiéser, fils d’Ammisaddaï;
26 Pagieli mwana wa Okirani aliongoza jeshi la wana wa uzao wa Asheri.
la troupe de la tribu des fils d’Aser était commandée par Phégiel, fils d'Ochran,
27 Ahira mwana wa Enani aliongoza jeshi la uzao wa kabila ya Naftali.
et la troupe des fils de Nephthali était commandée par Ahira, fils d’enan.
28 Hivi ndivyo majeshi ya wana wa Israeli yalivyosafiri.
Tel était l’ordre de marche des enfants d’Israël selon leurs troupes; et ils partirent.
29 Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
Moïse dit à Hobab, fils de Raguel, le Madianite, beau-père de Moïse: « Nous partons pour le lieu dont Yahweh a dit: Je vous le donnerai. Viens avec nous, et nous te ferons du bien, car Yahweh a promis de faire du bien à Israël. »
30 Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
Hobab lui répondit: « Je n’irai point, mais je m’en irai dans mon pays et ma famille. »
31 Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
Et Moïse dit: « Ne nous quitte pas, je te prie; puisque tu connais les lieux où nous aurons à camper dans le désert, tu nous serviras d’œil.
32 Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
Si tu viens avec nous, nous te ferons partager le bien que Yahweh nous fera. »
33 Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
Étant partis de la montagne de Yahweh, ils firent trois journées de marche, et pendant ces trois journées de marche, l’arche de l’alliance de Yahweh s’avança devant eux pour leur chercher un lieu de repos.
34 Wingu la BWANA lilikuwa juu yao muda wote wa mchana walipokuwa safarini.
La nuée de Yahweh était au-dessus d’eux pendant le jour, lorsqu’ils partaient du camp.
35 Kila hilo sanduku liliposafiri kwenda mbele, Musa alisema, “Inuka BWANA, Uwatawanye maadui wako. Uwafanye wale wanaokuchukia kukukimbia.”
Quand l’arche partait, Moïse disait: « Lève-toi, Yahweh, et que tes ennemis soient dispersés! Que ceux qui te haïssent fuient devant ta face! »
36 Na kila lile sanduku liliposimama, Musa alisema, “BWANA uwarudie, hawa Waisraeli makumi elfu.”
Et quand elle s’arrêtait, il disait: « Reviens, Yahweh, vers les myriades des milliers d’Israël! »

< Hesabu 10 >