< Nehemia 1 >
1 Maneno ya Nehemia mwana wa Hakalia Ikawa, katika mwezi wa Kisleu, katika mwaka wa ishirini, nilikuwa katika mji mkuu wa Sushani,
The words of Nehemias the son of Helchias. And it came to pass in the month of Casleu, in the twentieth year, as I was in the castle of Susa,
2 mmoja wa ndugu zangu, Hanani, alikuja pamoja na watu wengine kutoka Yuda, nami nikawauliza kuhusu Wayahudi waliopona, Wayahudi waliosalia waliokuwa huko, na kuhusu Yerusalemu.
That Hanani one of my brethren came, he and some men of Juda; and I asked them concerning the Jews, that remained and were left of the captivity, and concerning Jerusalem.
3 Wakaniambia, “Wale waliokuwa katika mkoa ule waliookoka katika kifungo wapo katika shida kubwa na aibu kwa sababu ukuta wa Yerusalemu umebomolewa na milango yake imeteketezwa kwa moto.”
And they said to me: They that have remained, and are left of the captivity there in the province, are in great affliction, and reproach: and the wall of Jerusalem is broken down, and the gates thereof are burnt with fire.
4 Na mara tu niliposikia maneno haya, nikakaa na kulia, na kwa siku niliendelea kuomboleza na kufunga na kuomba mbele ya Mungu wa mbinguni.
And when I had heard these words, I sat down, and wept, and mourned for many days: and I fasted, and prayed before the face of the God of heaven.
5 Ndipo nikasema, “Wewe ndiwe Bwana, Mungu wa mbinguni, Mungu uliye mkuu na kushangaza, unayetimiza agano na upendo wa kudumu pamoja na wale wanaokupenda na kushika amri zake.
And I said: I beseech thee, O Lord God of heaven, strong, great, and terrible, who keepest covenant and mercy with those that love thee, and keep thy commandments:
6 Sikiliza maombi yangu na fungua macho yako, ili uisikie sala ya mtumishi wako kwamba sasa nasali mbele yako mchana na usiku kwa ajili ya watu wa Israeli watumishi wako. Mimi ninakiri dhambi za watu wa Israeli, ambazo tumefanya dhidi yako. Wote mimi na nyumba ya baba yangu tumefanya dhambi.
Let thy ears be attentive, and thy eyes open, to hear the prayer of thy servant, which I pray before thee now, night and day, for the children of Israel thy servants: and I confess the sins of the children of Israel, by which they have sinned against thee: I and my father’s house have sinned.
7 Tumefanya uovu sana juu yako, na hatukuzingatia amri, sheria, na hukumu ambazo ulimwamuru mtumishi wako Musa.
We have been seduced by vanity, and have not kept thy commandments, and ceremonies and judgments, which thou hast commanded thy servant Moses.
8 Tafadhali kumbuka neno ulilomuamuru mtumishi wako Musa, 'mkitenda pasipo uaminifu, nitawatawanya kati ya mataifa,
Remember the word that thou commandedst to Moses thy servant, saying: If you shall transgress, I will scatter you abroad among the nations:
9 lakini mkirudi kwangu na kufuata amri zangu na kuzifanya, ingawa watu wako walienea chini ya mbingu za mbali, Nami nitawakusanya kutoka huko na kuwaleta mahali pale nilipopachagua ili kulifanya jina langu.'
But if you return to me, and keep my commandments, and do them, though you should be led away to the uttermost parts of the world, I will gather you from thence, and bring you back to the place which I have chosen for my name to dwell there.
10 Sasa wao ni watumishi wako na watu wako, ambao uliwaokoa kwa nguvu yako kubwa na kwa mkono wako wenye nguvu.
And these are thy servants, and thy people: whom thou hast redeemed by thy great strength, and by thy mighty hand.
11 Bwana, naomba, sikiliza sasa maombi ya watumishi wako na sala ya watumishi wako ambao hufurahia kuheshimu jina lako. Sasa unifanikishe mimi mtumishi wako leo, na unijalie rehema mbele ya mtu huyu.” Nilikuwa mnyweshaji wa mfalme.
I beseech thee, O Lord, let thy ear be attentive to the prayer of thy servant, and to the prayer of thy servants who desire to fear thy name: and direct thy servant this day, and give him mercy before this man. For I was the king’s cupbearer.