< Nehemia 5 >

1 Kisha wale wanaume na wake zao wakalia kwa nguvu dhidi ya Wayahudi wenzao.
[Later, ] many of the men and their wives protested loudly about what [some of] the [other] Jews were doing.
2 Kwa maana kulikuwa na baadhi ya watu ambao walisema, “Sisi na wana wetu na binti zetu tupo wengi. Basi hebu tupate nafaka tuweze kula na tukae tuishi.”
Some/One of them said, “We have many children. So we need a lot of grain to be able to eat and continue to live.”
3 Pia kulikuwa na baadhi ya watu ambao walisema, “Tunaweka rehani mashamba yetu, mizabibu yetu, na nyumba zetu ili tupate nafaka wakati wa njaa.”
Others said, “The fields and vineyards and houses that we own, it has been necessary for us to (mortgage them/promise to give them to someone if we do not pay back to him the money he has loaned us) in order to get money to buy grain, during this (famine/time where there is not much food).”
4 Wengine pia walisema, “Tumekopesha pesa kulipa kodi ya mfalme kwenye mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu.
Others said, “We have [needed to] borrow money to pay the taxes that the king [commanded us to pay] on our fields and our vineyards.
5 Hata hivyo sasa miili yetu na damu ni sawa na ndugu zetu, na watoto wetu ni sawa na watoto wao. Tunalazimishwa kuuza wana wetu na binti zetu kuwa watumwa. Baadhi ya binti zetu tayari wamekuwa watumwa. Lakini hatuna nguvu za kusaidia kwa sababu watu wengine sasa wana mashamba yetu na mizabibu yetu.”
We are Jews just like [IDM] they are. Our children are ([just as good as/equal with)] their children. But we have needed to sell some of our children to become slaves [in order to pay what we owe]. We have already sold some of our daughters to become slaves. Our fields and vineyards have been taken away from us, so now we do not have [the money to pay what we owe, and we are forced to sell our children to get money to pay those debts].”
6 Nilikasirika sana niliposikia kilio chao na maneno haya.
I was very angry when I heard these things that they were complaining about.
7 Kisha nikafikiri juu ya hili, na kuleta mashtaka dhidi ya wakuu na viongozi. Nikawaambia, “Ninyi mnatafuta riba, kila mmoja kutoka kwa ndugu yake mwenyewe.” Nikakutanisha kusanyiko kubwa juu yao
So I thought about what I could do about it. I told the leaders and officials [who were responsible for this work], “You are charging interest to your own relatives [when they borrow money from you]!” Then I called together a large group of people,
8 na kuwaambia, “Sisi, kwa kadiri tulivyoweza, tumewakomboa toka utumwani ndugu zetu wa Kiyahudi ambao walikuwa wameuzwa kwa mataifa, lakini hata mnawauza ndugu na dada zenu ili wauzwe tena kwetu!” Walikuwa kimya na hawakupata neno la kusema.
and I said to their [leaders], “Some of our Jewish relatives have been forced to sell themselves to become slaves of people who have come from other countries. As much as we have been able to, we have been buying them back [out of slavery]. But now you are forcing your own relatives to sell themselves to you, their fellow Jews, as slaves!” [When I said that to them, ] they were silent. There was nothing that they could say [because they knew that what I said was true].
9 Pia nikasema, 'Mnachokifanya sio kizuri. Je, hampaswi kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili kuzuia malalamiko ya mataifa ambayo ni adui zetu?
Then I said to them, “What you are doing is terrible [EUP]! You certainly ought to [RHQ] obey God and do what is right! If you did that, our enemies who do not revere Yahweh [would see that we are doing what is right and] would not ridicule us.
10 Mimi na ndugu zangu na watumishi wangu tunawapa fedha na nafaka. Lakini lazima tuache kutoza riba juu ya mikopo hii.
My fellow Jews and I and my servants have lent money and grain to people [without charging interest]. So you all should stop charging interest on these loans.
11 Warudishieni leo leo mashamba yao, mizabibu yao, mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao na asilimia ya fedha, nafaka, divai mpya, na mafuta mliyowatoza.”
Also, you must give back to them their fields, their vineyards, their olive tree orchards, and their houses that you have taken from them. You must also give back to them the interest that you charged them when they borrowed money, grain, wine, and [olive] oil from you, and you must do it today!”
12 Wakasema, “Tutarudisha kile tulichochukua kutoka kwao, wala hatutahitaji kitu kutoka kwao. Tutafanya kama unavyosema.” Ndipo nikawaita makuhani, na kuwaapisha kuwafanya kama walivyoahidi.
The leaders replied, “We will do what you have said. We will return to them everything that we forced them to give to us, and we will not require that they give us anything more.” Then I summoned the priests, and I forced the leaders to vow in front of them that they would do what they had promised to do.
13 Nikakung'uta vazi langu, nikasema, “Basi Mungu aondoe nyumba na mali ya kila mtu asiyetimiza ahadi yake. Kwa hiyo akung'utwe na kuwa hana kitu. Kusanyiko lote likasema “Amina,” na wakamsifu Bwana. Na watu wakafanya kama walivyoahidi.
I shook out the folds of my robe and said to them, “If you do not do what you have just now promised to do, I hope/desire that God will shake you like I am shaking my robe. He will take away your homes and everything else that you own.” They all replied, “Amen/May it be so!” And they praised Yahweh. Then they did what they had promised to do.
14 Kwa hiyo tangu wakati niliowekwa kuwa mkuu wao katika nchi ya Yuda, tangu mwaka wa ishirini mpaka mwaka wa thelathini na pili wa mfalme Artashasta, miaka kumi na miwili, mimi na ndugu zangu hatukula chakula kilichotolewa kwa gavana.
I was appointed to be the governor of Judea in the twentieth year that Artaxerxes was the king [of Persia]. For the next twelve years, until he had been ruling for almost 32 years, neither I nor my officials accepted [the money that we were allowed/entitled to receive to buy] food because of my being the governor.
15 Lakini wakuu wa zamani waliokuwa kabla yangu waliwaweka watu mizigo mizito, na wakachukua kwao shekeli arobaini za fedha kwa ajili ya chakula na divai yao ya kila siku. Hata watumishi wao waliwadhulumu watu. Lakini sikufanya hivyo kwa sababu ya hofu ya Mungu.
The men who were governors before I became the governor had burdened the people by requiring them to pay a lot of taxes. They had forced each person to pay to them 40 silver coins every day, in addition to giving food and wine to them. Even their servants/officials oppressed the people. But I did not do that, because I revered God.
16 Niliendelea kufanya kazi kwenye ukuta, na hatukununua ardhi. Na watumishi wangu wote walikusanyika huko kwa ajili ya kazi hiyo.
I also continued to work on the wall, and I did not take land from people [who were unable to pay back the money that they had borrowed from me]. All those who worked for me joined me to work on the wall.
17 Katika meza yangu walikuwa Wayahudi na maafisa, watu 150, isipokuwa wale waliokuja kwetu kutoka kwa mataifa waliokuwa wakituzunguka.
Also, every day I was responsible to feed 150 Jewish officials, and also [official] visitors who came from nearby countries.
18 Kila kitu kilichoandaliwa kila siku kilikuwa ng'ombe moja, kondoo sita waliochaguliwa, na ndege, na kila siku kumi aina zote za divai nyingi. Na hata kwa haya yote sikuhitaji mahitaji ya chakula cha gavana, kwa sababu madai yalikuwa mazito sana juu ya watu.
Each day I [told my servants to] serve [us the meat from] one ox, six very good sheep, and chickens. And every ten days I gave them a large new supply of wine. But I knew that the people were burdened [by paying lots of taxes], so I did not accept [the money that I was entitled/allowed to receive to buy all this] food because of my being the governor.
19 Nikumbuke, Ee Mungu wangu, kwa wema, kwa sababu ya yote niliyoyafanya kwa watu hawa.
My God, do not forget me, and reward me because of all that I have done for these people.

< Nehemia 5 >