< Nehemia 5 >

1 Kisha wale wanaume na wake zao wakalia kwa nguvu dhidi ya Wayahudi wenzao.
and to be cry [the] people and woman: wife their great: large to(wards) brother: compatriot their [the] Jew
2 Kwa maana kulikuwa na baadhi ya watu ambao walisema, “Sisi na wana wetu na binti zetu tupo wengi. Basi hebu tupate nafaka tuweze kula na tukae tuishi.”
and there which to say son: child our and daughter our we many and to take: take grain and to eat and to live
3 Pia kulikuwa na baadhi ya watu ambao walisema, “Tunaweka rehani mashamba yetu, mizabibu yetu, na nyumba zetu ili tupate nafaka wakati wa njaa.”
and there which to say land: country our and vineyard our and house: home our we to pledge and to take: take grain in/on/with famine
4 Wengine pia walisema, “Tumekopesha pesa kulipa kodi ya mfalme kwenye mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu.
and there which to say to borrow silver: money to/for tribute [the] king land: country our and vineyard our
5 Hata hivyo sasa miili yetu na damu ni sawa na ndugu zetu, na watoto wetu ni sawa na watoto wao. Tunalazimishwa kuuza wana wetu na binti zetu kuwa watumwa. Baadhi ya binti zetu tayari wamekuwa watumwa. Lakini hatuna nguvu za kusaidia kwa sababu watu wengine sasa wana mashamba yetu na mizabibu yetu.”
and now like/as flesh brother: compatriot our flesh our like/as son: child their son: child our and behold we to subdue [obj] son: child our and [obj] daughter our to/for servant/slave and there from daughter our to subdue and nothing to/for god: power hand: power our and land: country our and vineyard our to/for another
6 Nilikasirika sana niliposikia kilio chao na maneno haya.
and to be incensed to/for me much like/as as which to hear: hear [obj] outcry their and [obj] [the] word [the] these
7 Kisha nikafikiri juu ya hili, na kuleta mashtaka dhidi ya wakuu na viongozi. Nikawaambia, “Ninyi mnatafuta riba, kila mmoja kutoka kwa ndugu yake mwenyewe.” Nikakutanisha kusanyiko kubwa juu yao
and to advise heart my upon me and to contend [emph?] with [the] noble and with [the] ruler and to say [emph?] to/for them interest man: anyone in/on/with brother: compatriot his you(m. p.) (to lift: aid *Q(K)*) and to give: make upon them assembly great: large
8 na kuwaambia, “Sisi, kwa kadiri tulivyoweza, tumewakomboa toka utumwani ndugu zetu wa Kiyahudi ambao walikuwa wameuzwa kwa mataifa, lakini hata mnawauza ndugu na dada zenu ili wauzwe tena kwetu!” Walikuwa kimya na hawakupata neno la kusema.
and to say [emph?] to/for them we to buy [obj] brother: compatriot our [the] Jew [the] to sell to/for nation like/as sufficiency in/on/with us and also you(m. p.) to sell [obj] brother: compatriot your and to sell to/for us and be quiet and not to find word
9 Pia nikasema, 'Mnachokifanya sio kizuri. Je, hampaswi kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili kuzuia malalamiko ya mataifa ambayo ni adui zetu?
(and to say *Q(K)*) not pleasant [the] word: thing which you(m. p.) to make: do not in/on/with fear God our to go: walk from reproach [the] nation enemy our
10 Mimi na ndugu zangu na watumishi wangu tunawapa fedha na nafaka. Lakini lazima tuache kutoza riba juu ya mikopo hii.
and also I brother: male-sibling my and youth my to lend in/on/with them silver: money and grain to leave: forsake please [obj] [the] interest [the] this
11 Warudishieni leo leo mashamba yao, mizabibu yao, mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao na asilimia ya fedha, nafaka, divai mpya, na mafuta mliyowatoza.”
to return: return please to/for them like/as [the] day land: country their vineyard their olive their and house: home their and hundred [the] silver: money and [the] grain [the] new wine and [the] oil which you(m. p.) to lend in/on/with them
12 Wakasema, “Tutarudisha kile tulichochukua kutoka kwao, wala hatutahitaji kitu kutoka kwao. Tutafanya kama unavyosema.” Ndipo nikawaita makuhani, na kuwaapisha kuwafanya kama walivyoahidi.
and to say to return: rescue and from them not to seek so to make: do like/as as which you(m. s.) to say and to call: call to [obj] [the] priest and to swear them to/for to make: do like/as Chronicles [the] this
13 Nikakung'uta vazi langu, nikasema, “Basi Mungu aondoe nyumba na mali ya kila mtu asiyetimiza ahadi yake. Kwa hiyo akung'utwe na kuwa hana kitu. Kusanyiko lote likasema “Amina,” na wakamsifu Bwana. Na watu wakafanya kama walivyoahidi.
also bosom my to shake and to say [emph?] thus to shake [the] God [obj] all [the] man which not to arise: establish [obj] [the] word: promised [the] this from house: home his and from toil his and thus to be to shake and worthless and to say all [the] assembly amen and to boast: praise [obj] LORD and to make: do [the] people like/as Chronicles [the] this
14 Kwa hiyo tangu wakati niliowekwa kuwa mkuu wao katika nchi ya Yuda, tangu mwaka wa ishirini mpaka mwaka wa thelathini na pili wa mfalme Artashasta, miaka kumi na miwili, mimi na ndugu zangu hatukula chakula kilichotolewa kwa gavana.
also from day which to command [obj] me to/for to be governor their in/on/with land: country/planet Judah from year twenty and till year thirty and two to/for Artaxerxes [the] king year two ten I and brother: male-sibling my food: allowance [the] governor not to eat
15 Lakini wakuu wa zamani waliokuwa kabla yangu waliwaweka watu mizigo mizito, na wakachukua kwao shekeli arobaini za fedha kwa ajili ya chakula na divai yao ya kila siku. Hata watumishi wao waliwadhulumu watu. Lakini sikufanya hivyo kwa sababu ya hofu ya Mungu.
and [the] governor [the] first: previous which to/for face: before my to honor: heavy upon [the] people and to take: take from them in/on/with food: allowance and wine after silver: money shekel forty also youth their to domineer upon [the] people and I not to make: do so from face: because fear God
16 Niliendelea kufanya kazi kwenye ukuta, na hatukununua ardhi. Na watumishi wangu wote walikusanyika huko kwa ajili ya kazi hiyo.
and also in/on/with work [the] wall [the] this to strengthen: persevere and land: country not to buy and all youth my to gather there upon [the] work
17 Katika meza yangu walikuwa Wayahudi na maafisa, watu 150, isipokuwa wale waliokuja kwetu kutoka kwa mataifa waliokuwa wakituzunguka.
and [the] Jew and [the] ruler hundred and fifty man and [the] to come (in): come to(wards) us from [the] nation which around us upon table my
18 Kila kitu kilichoandaliwa kila siku kilikuwa ng'ombe moja, kondoo sita waliochaguliwa, na ndege, na kila siku kumi aina zote za divai nyingi. Na hata kwa haya yote sikuhitaji mahitaji ya chakula cha gavana, kwa sababu madai yalikuwa mazito sana juu ya watu.
and which to be to make: do to/for day one cattle one flock six to purify and bird to make: do to/for me and between ten day in/on/with all wine to/for to multiply and with this food: allowance [the] governor not to seek for to honor: heavy [the] service upon [the] people [the] this
19 Nikumbuke, Ee Mungu wangu, kwa wema, kwa sababu ya yote niliyoyafanya kwa watu hawa.
to remember [emph?] to/for me God my to/for welfare all which to make: do upon [the] people [the] this

< Nehemia 5 >