< Nehemia 4 >
1 Sanbalati alipoposikia tulikuwa tukijenga ukuta, akaghadhabika ndani yake, naye akakasirika sana, akawacheka Wayahudi.
Lorsque Sanballat apprit que nous étions en train de rebâtir le mur, il en fut contrarié et entra dans une grande colère. II tourna en dérision les Judéens,
2 Mbele ya ndugu zake na jeshi la Samaria, akasema, “Wayahudi dhaifu hawa wanafanya nini? Je, watajifanyia mji wenyewe? Je, watatoa dhabihu? Je, wataimaliza kazi siku moja? Je! Watawaletea mawe kutoka kwenye kifusi baada ya kuchomwa moto?
et dit devant ses frères et les gens de guerre de Samarie: "Que se proposent ces misérables Judéens? Les laissera-t-on faire? Offriront-ils des sacrifices? En viendront-ils à bout aujourd’hui? Rendront-ils la vie aux pierres tirées des tas de poussière et qui ont été brûlées?"
3 Tobia Mwamoni alikuwa pamoja naye, naye akasema, 'Ikiwa tu mbweha angepanda juu ya hichi wanachokijenga, angeubomoa ukuta huo wa mawe.”
Tobia l’Ammonite, à côté de lui, ajoutait: "Qu’ils bâtissent toujours: il suffira qu’un renard monte dessus pour renverser leur muraille de pierres!"
4 Tusikilize, Mungu wetu, kwa maana sisi tunatukanwa. Rudisha malalamiko yao juu ya vichwa vyao wenyewe na kuwapa wapate kutekwa katika nchi ambapo wao ni wafungwa.
Ecoute, ô notre Dieu, comme nous sommes devenus un objet de mépris; fais retomber leurs outrages sur leur tête, et livre-les au pillage sur une terre de captivité.
5 Usiufunike uovu wao, wala usiondoe dhambi zao mbele yako; kwa sababu wamewachukiza wanaojenga.
Ne voile pas leur iniquité; que leur méfait ne s’efface point devant toi, puisqu’ils se sont déchaînés contre les travailleurs!
6 Kwa hiyo tulijenga ukuta na ukuta wote uliunganishwa kwa nusu ya urefu wake, kwa kuwa watu walikuwa na hamu ya kufanya kazi
Cependant, nous continuâmes à rebâtir le mur; et lorsque tout le mur fut bouché jusqu’à mi-hauteur, le peuple eut de nouveau du cœur à l’ouvrage.
7 Lakini Sanbalati, Tobia, Waarabu, Waamoni, na Waashdodi waliposikia kwamba kazi ya ukarabati wa kuta za Yerusalemu ilikuwa ikiendelea, na kwamba sehemu zilizovunjika katika ukuta zilikuwa zimefungwa, ghadhabu kubwa ikawaka ndani yao.
Lorsque Sanballat, Tobia, les Arabes, les Ammonites et les gens d’Asdod apprirent que la restauration des murs de Jérusalem allait bon train, que les brèches commençaient à se fermer, ils en furent très dépités.
8 Wote walifanya shauri pamoja, na walikuja kupigana dhidi ya Yerusalemu na kusababisha machafuko ndani yake.
Ils complotèrent tous ensemble d’aller attaquer Jérusalem et d’y jeter le désarroi.
9 Lakini tuliomba kwa Mungu wetu na kuweka walinzi kama ulinzi dhidi yao mchana na usiku kwa sababu ya tishio lao.
Nous implorâmes notre Dieu et, pour nous défendre contre eux, nous établîmes un service de faction chargé de les surveiller jour et nuit.
10 Kisha watu wa Yuda wakasema, “Nguvu ya wale wanaobeba mizigo inashindwa. Kuna kifusi kikubwa, na hatuwezi kujenga ukuta.”
Juda disait: "Les forces des porteurs de charges sont à bout et les décombres sont considérables; nous sommes hors d’état de rebâtir la muraille."
11 Na adui zetu wakasema,” Wala hawatajua au kuona mpaka tutakapokuja kati yao na kuwaua, na kuisimamisha kazi.”
Et nos adversaires disaient: "Ils ne se douteront ni ne s’apercevront de rien jusqu’à ce que nous pénétrions au milieu d’eux pour les massacrer, et ainsi nous mettrons fin à ce travail."
12 Wakati huo Wayahudi waliokuwa wakiishi karibu nao walitoka pande zote na kuzungumza nasi mara kumi, wakituonya juu ya mipango waliyofanya dhidi yetu.
Comme des Judéens établis parmi eux vinrent nous dire jusqu’à dix fois: "De quelque localité que vous soyez, il faut que-vous retourniez chez nous",
13 Kwa hiyo nikaweka watu katika sehemu za chini za ukuta katika sehemu zilizo wazi. Niliweka kila familia wenye upanga, mikuki, na upinde.
je plaçai en contrebas, derrière la muraille, sur des terrains secs, je plaçai, dis-je, le peuple par familles, avec leurs épées, leurs lances et leurs arcs.
14 Nikatazama, nikasimama, nikawaambia wakuu, na watawala, na watu wengine, “Msiogope. mkumbukeni Bwana, ambaye ni mkuu na wa kushangaza. Wapiganie ndugu zenu, wana zenu, binti zenu, wake zenu na nyumba zenu.
Ayant tout inspecté, je m’avançai et dis aux grands, aux chefs et au reste du peuple: "N’Ayez pas peur d’eux; pensez au Seigneur grand et redoutable et combattez pour vos frères, vos fils et vos filles, vos femmes et vos maisons."
15 Ilipokuwa wakati adui zetu waliposikia kwamba mipango yao ilikuwa inayojulikana kwetu, na Mungu alikuwa amebatilisha mipango yao, sote tulirudi ukutani, kila mmoja kwa kazi yake.
Quand nos ennemis eurent été informés que nous étions avertis et que Dieu avait ruiné leur plan, nous retournâmes tous à la muraille, chacun à son ouvrage.
16 Kwa hiyo tangu wakati huo nusu ya watumishi wangu walifanya kazi tu juu ya kujenga ukuta, na nusu yao wakaishika mikuki, ngao, pinde, na kuvaa silaha, wakati viongozi walisimama nyuma ya watu wote wa Yuda.
A partir de ce jour, la moitié de mes gens s’occupait de l’ouvrage, et l’autre moitié était munie de lances, de boucliers, d’arcs et de cuirasses; les seigneurs se tenaient derrière toute la maison de Juda.
17 Na hivyo wafanyakazi haohao ambao walikuwa wakijenga ukuta na kubeba mizigo walikuwa pia wakilinda nafasi zao. Kila mtu alifanya kazi kwa mkono mmoja, na kwa mkono mwingine alikuwa na silaha yake.
De ceux qui étaient occupés à la bâtisse, d’une part les manœuvres, porteurs de charges, faisaient leur besogne d’une main et tenaient l’épée de l’autre;
18 Kila mjenzi alivaa upanga wake ubavuni mwake na ndivyo alivyojenga. Yule aliyepiga tarumbeta akakaa karibu nami.
d’autre part, les maçons construisaient, ayant chacun son épée attachée aux reins, et celui qui sonnait de la trompette était à mes côtés.
19 Niliwaambia wakuu na viongozi na watu wengine, “Kazi ni nzuri na ya kina, na tumejitenga kwenye ukuta, mbali na mtu mwingine.
Et je dis aux nobles, aux chefs et au reste du peuple: "L’Ouvrage est considérable et s’étend sur un vaste espace, de sorte que nous sommes dispersés le long de la muraille, éloignés l’un de l’autre.
20 Lazima mkimbilie mahali ambapo mtasikia sauti ya tarumbeta na kusanyika huko. Mungu wetu atatupigania.”
A l’endroit d’où vous parviendra le son de la trompette, là vous viendrez vous rallier à nous: Dieu combattra en notre faveur."
21 Kwa hiyo tulifanya kazi hiyo. Nusu yao walikuwa wakichukua mikuki kutoka kupambazuka asubuhi hadi kutokea kwa nyota.
C’Est ainsi que nous nous occupions de l’ouvrage, la moitié des gens tenant les lances depuis le lever de l’aurore jusqu’à l’apparition des étoiles.
22 Nikawaambia watu wakati huo, “Kila mtu na mtumishi wake waende usiku katikati ya Yerusalemu, ili wawe walinzi wakati wa usiku na mfanyakazi wakati huo.”
En ce temps-là aussi, je demandai au peuple que chacun passât la nuit à Jérusalem avec son serviteur, pour nous servir de sentinelles pendant la nuit et consacrer le jour au travail.
23 Basi si mimi, wala ndugu zangu, wala watumishi wangu, wala watu wa walinzi waliokuwa wananifuata, hakuna hata mmoja wetu aliyebadili nguo zake, na kila mmoja wetu alichukua silaha yake, hata kama angeenda kwa ajili ya kuteka maji.
Quant à moi, à mes frères, à mes gens et aux hommes de garde qui me suivaient, nous ne quittions point nos vêtements: chacun gardait son épée dans la main droite.