< Nehemia 3 >
1 Kisha Eliashibu, kuhani mkuu, akasimama pamoja na ndugu zake makuhani, wakajenga lango la kondoo. Walitakasa na kuweka milango yake. Waliweka wakfu hadi mnara wa Hamea na hadi mnara wa Hananeli.
Then Eliashib the high priest rose up with his brother priests, and they built the Sheep Gate. They consecrated it and set its doors in place. They consecrated it as far as the Tower of the Hundred and as far as the Tower of Hananel.
2 Baada yao watu wa Yeriko walijenga, na baada yao Zakuri mwana wa Imri alijenga.
Next to him the men of Jericho worked, and next to them Zaccur son of Imri worked.
3 Wana wa Senaa wakajenga lango la samaki. Wanaweka mihimili yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
The sons of Hassenaah built the Fish Gate. They made beams for it, and set its doors, its bolts, and its bars.
4 Meremoth aliandaa sehemu inayofuata. Yeye ni mwana wa Uria mwana wa Hakosi. Na baada yao Meshulamu akatengeneza. Yeye ni mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli. Karibu nao Sadoki akatengeneza. Yeye ni mwana wa Baana.
Meremoth repaired the next section. He is the son of Uriah son of Hakkoz. Next to them Meshullam repaired. He is the son of Berechiah son of Meshezabel. Next to them Zadok repaired. He is the son of Baana.
5 Baada yao Watekoi wakatengeneza, lakini viongozi wao walikataa kufanya kazi iliyoagizwa na wakuu wao.
Next to them the Tekoites repaired, but their leaders refused to do the work ordered by their supervisors.
6 Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya, walitengeneza lango la Kale. Wanaweka mihimili, na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
Joiada son of Paseah and Meshullam son of Besodeiah repaired the Old Gate. They made beams for it, and set its doors, its bolts, and its bars.
7 Nao, Melatia Mgibeoni, na Yadoni Meronothi, watu wa Gibeoni na Mispa, walifanyia matengenezo juu ya sehemu ambapo mkuu wa mkoa wa ng'ambo ya Mto aliishi.
Next to them Melatiah the Gibeonite and Jadon the Meronothite, who were men from Gibeon and Mizpah, made repairs on the portion where the governor of the Province Beyond the River lived.
8 Na baada yake Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa wafua dhahabu, akatengeneza; na baada yake Hanania, mtengenezaji wa manukato. Wakajenga tena Yerusalemu mpaka Ukuta mpana.
Next to him Uzziel son of Harhaiah, one of the goldsmiths, repaired, and next to him was Hananiah, a maker of perfumes. They rebuilt Jerusalem as far as the Broad Wall.
9 Na baada yao Refaya mwana wa Huri akajenga. Alikuwa mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu.
Next to them Rephaiah son of Hur repaired. He was the ruler of half the district of Jerusalem.
10 Na baada yao Yedaya mwana wa Harumafu akajenga karibu na nyumba yake. Na baada yake Hatushi mwana wa Hashabneya akajenga.
Next to them Jedaiah son of Harumaph repaired next to his house. Next to him Hattush son of Hashabneiah repaired.
11 Malkiya mwana wa Harimu na Hashubu mwana wa Pahat Moabu, wajenga sehemu nyingine pamoja na mnara wa tanuu.
Malchijah son of Harim and Hasshub son of Pahath-Moab repaired another section along with the Tower of the Ovens.
12 Baada yao Shalumu mwana wa Haloheshi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akajenga, pamoja na binti zake.
Next to them Shallum son of Hallohesh, the ruler of half the district of Jerusalem, repaired, along with his daughters.
13 Hanuni na wenyeji wa Zanoa walijenga lango la bondeni. Walijenga tena na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake. Walijenga dhiraa elfu hadi lango la jaa.
Hanun and the inhabitants of Zanoah repaired the Valley Gate. They rebuilt it and set its doors, its bolts, and its bars. They repaired a thousand cubits as far as the Dung Gate.
14 Malkiya, mwana wa Rekabu, mkuu wa wilaya ya Beth-Hakeremu, akajenga lango la jaa. Alijenga na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake.
Malchijah son of Recab, the ruler of the district of Beth Hakkerem, repaired the Dung Gate. He built it and set its doors, its bolts, and its bars.
15 Shalumu mwana wa Kolhoze, mkuu wa wilaya ya Mispa, akajenga lango la Chemchemi. Alijenga, na kuweka kifuniko juu yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake. Alijenga upya ukuta wa Pwani wa Silowamu kwa bustani ya mfalme, hadi ngazi ya kuongoza kutoka mji wa Daudi.
Shallun son of Kol-Hozeh, the ruler of the district of Mizpah, rebuilt the Fountain Gate. He built it, and put a cover on it and set its doors, its bolts, and its bars. He also rebuilt the wall of the Pool of Siloam by the king's garden, as far as the stairs leading down from the city of David.
16 Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-suri, akajenga mahali hapo, toka maburini ya Daudi, mpaka birika lililojengwa na watu, na nyumba ya watu wenye nguvu.
Nehemiah son of Azbuk, the ruler of half the district of Beth Zur, repaired to the place across from the tombs of David, to the man-made pool, and to the house of the mighty men.
17 Baada yake, Walawi walijenga, pamoja na Rehumi mwana wa Bani na baada yake, Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, kwa wilaya yake.
After him the Levites repaired, including Rehum son of Bani and next to him, Hashabiah, the ruler of half the district of Keilah, for his district.
18 Baada yake watu wa nchi zao walijenga, ikiwa ni pamoja na Binui mwana wa Henadadi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila.
After him their countrymen repaired, including Binnui son of Henadad, the ruler of half the district of Keilah.
19 Baada yake alijenga Ezeri, mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alijenga sehemu nyingine kuelekea ghala ya silaha, kwenye kona ya ukuta.
Next to him, Ezer son of Jeshua, the ruler of Mizpah, repaired another section that faced the ascent to the armory at the corner of the wall.
20 Baada yake Baruki, mwana wa Zakai, akajenga kwa hiari sehemu nyingine, toka kona ya ukuta mpaka mlango wa nyumba ya Eliashibu, kuhani mkuu.
After him Baruch son of Zabbai devotedly repaired another section, from the corner of the wall to the door of the house of Eliashib the high priest.
21 Baada yake Meremothi, mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, akajenga sehemu nyingine, toka mlango wa nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.
After him Meremoth son of Uriah son of Hakkoz repaired another section, from the door of the house of Eliashib to the end of the house of Eliashib.
22 Kisha baada yake makuhani, watu wa eneo hilo karibu na Yerusalemu, walijenga.
Next to him the priests, the men from the area around Jerusalem, repaired.
23 Baada yao Benyamini na Hashubu walijenga kuielekea nyumba yao. Baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania, alijenga karibu na nyumba yake.
After them Benjamin and Hasshub repaired opposite their own house. After them Azariah son of Maaseiah son of Ananiah repaired next to his own house.
24 Baada yake Binui mwana wa Henadadi akajenga sehemu nyingine, kutoka nyumba ya Azaria hadi kona ya ukuta.
After him Binnui son of Henadad repaired another section, from the house of Azariah to the corner of the wall.
25 Palali, mwana wa Uzai, akajenga juu ya kona ya ukuta na mnara unaoenea juu kutoka nyumba ya juu ya mfalme katika uwanda wa walinzi. Baada yake Pedaya mwana wa Paroshi akajenga.
Palal son of Uzai repaired over against the corner of the wall and the tower that extends upward from the upper house of the king at the courtyard of the guard. After him Pedaiah son of Parosh repaired.
26 Sasa watumishi wa hekalu waliokaa Ofeli walijenga mpaka upande wa Hifadhi ya Maji upande wa mashariki wa mnara unaojitokeza.
Now the temple servants living in Ophel repaired to the point opposite the Water Gate on the east and the projecting tower.
27 Baada yake, Watekoi walijenga sehemu nyingine, kuelekea mnara mkubwa ulio nje, mpaka ukuta wa Ofeli.
After him the Tekoites repaired another section that was opposite the great projecting tower as far as the wall of Ophel.
28 Makuhani wakajenga juu ya lango la farasi, kila mmoja kuelekea nyumba yake.
The priests repaired above the Horse Gate, each opposite his own house.
29 Baada yao Sadoki, mwana wa Imeri, alijenga sehemu hiyo kuelekea nyumba yake. Na baada yake Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa lango la mashariki, akajenga.
After them Zadok son of Immer repaired the section opposite his own house. Then after him Shemaiah son of Shecaniah, the keeper of the east gate, repaired.
30 Baada yake Hanania, mwana wa Shelemia, na Hanuni, mwana wa sita wa Salafu, wakajenga sehemu nyingine. Meshulamu mwana wa Berekia akajenga kuelekea kwenye vyumba vyake.
After him Hananiah son of Shelemiah, and Hanun the sixth son of Zalaph, repaired another section. After him Meshullam son of Berechiah repaired opposite his living chambers.
31 Baada yake Malkiya, mmoja wa wafua dhahabu, akajenga mpaka nyumba ya watumishi wa hekalu na wafanyabiashara waliokuwa wakielekea lango la gereza na mpaka chumba cha juu cha pembeni.
After him Malchijah, one of the goldsmiths, repaired to the house of the temple servants and the merchants that was opposite the Appointment Gate and the upper living chambers on the corner.
32 Wafanyabiashara wa dhahabu na wafanyabiashara walijenga kati ya chumba cha juu cha kona na Lango la Kondoo.
The goldsmiths and the merchants repaired between the upper chamber of the corner and the Sheep Gate.