< Nehemia 3 >

1 Kisha Eliashibu, kuhani mkuu, akasimama pamoja na ndugu zake makuhani, wakajenga lango la kondoo. Walitakasa na kuweka milango yake. Waliweka wakfu hadi mnara wa Hamea na hadi mnara wa Hananeli.
And Eliashib the high priest rises, and his brothers the priests, and they build the Sheep Gate; they have sanctified it, and set up its doors, even to the Tower of Meah they have sanctified it, to the Tower of Hananeel;
2 Baada yao watu wa Yeriko walijenga, na baada yao Zakuri mwana wa Imri alijenga.
and by his hand men of Jericho have built; and by their hand Zaccur son of Imri has built;
3 Wana wa Senaa wakajenga lango la samaki. Wanaweka mihimili yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
and sons of Hassenaah have built the Fish Gate; they have walled it, and set up its doors, its locks, and its bars.
4 Meremoth aliandaa sehemu inayofuata. Yeye ni mwana wa Uria mwana wa Hakosi. Na baada yao Meshulamu akatengeneza. Yeye ni mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli. Karibu nao Sadoki akatengeneza. Yeye ni mwana wa Baana.
And by their hand Merimoth son of Urijah, son of Koz, has strengthened; and by his hand Meshullam son of Berechiah, son of Meshezabeel, has strengthened; and by his hand Zadok son of Baana has strengthened;
5 Baada yao Watekoi wakatengeneza, lakini viongozi wao walikataa kufanya kazi iliyoagizwa na wakuu wao.
and by his hand the Tekoites have strengthened, and their majestic ones have not brought in their neck to the service of their Lord.
6 Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya, walitengeneza lango la Kale. Wanaweka mihimili, na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
And Jehoiada son of Paseah and Meshullam son of Besodeiah have strengthened the Old Gate; they have walled it, and set up its doors, and its locks, and its bars.
7 Nao, Melatia Mgibeoni, na Yadoni Meronothi, watu wa Gibeoni na Mispa, walifanyia matengenezo juu ya sehemu ambapo mkuu wa mkoa wa ng'ambo ya Mto aliishi.
And by their hand Melatiah the Gibeonite has strengthened, and Jadon the Meronothite, men of Gibeon and of Mizpah, [belonging] to the throne of the governor beyond the River.
8 Na baada yake Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa wafua dhahabu, akatengeneza; na baada yake Hanania, mtengenezaji wa manukato. Wakajenga tena Yerusalemu mpaka Ukuta mpana.
By his hand Uzziel son of Harhaiah of the refiners has strengthened; and by his hand Hananiah son of [one of] the compounders has strengthened; and they leave Jerusalem to the broad wall.
9 Na baada yao Refaya mwana wa Huri akajenga. Alikuwa mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu.
And by their hand Rephaiah son of Hur, head of the half of the district of Jerusalem, has strengthened.
10 Na baada yao Yedaya mwana wa Harumafu akajenga karibu na nyumba yake. Na baada yake Hatushi mwana wa Hashabneya akajenga.
And by their hand Jedaiah son of Harumaph has strengthened, and opposite his own house; and by his hand Hattush son of Hashabniah has strengthened.
11 Malkiya mwana wa Harimu na Hashubu mwana wa Pahat Moabu, wajenga sehemu nyingine pamoja na mnara wa tanuu.
A second measure Malchijah son of Harim has strengthened, and Hashub son of Pahath-Moab, even the Tower of the Furnaces.
12 Baada yao Shalumu mwana wa Haloheshi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akajenga, pamoja na binti zake.
And by his hand Shallum son of Halohesh, head of the half of the district of Jerusalem, has strengthened, he and his daughters.
13 Hanuni na wenyeji wa Zanoa walijenga lango la bondeni. Walijenga tena na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake. Walijenga dhiraa elfu hadi lango la jaa.
Hanun has strengthened the Valley Gate, and the inhabitants of Zanoah; they have built it, and set up its doors, its locks, and its bars, and one thousand cubits in the wall to the Refuse Gate.
14 Malkiya, mwana wa Rekabu, mkuu wa wilaya ya Beth-Hakeremu, akajenga lango la jaa. Alijenga na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake.
And Malchijah son of Rechab, head of the district of Beth-Haccerem, has strengthened the Refuse Gate; he builds it, and sets up its doors, its locks, and its bars.
15 Shalumu mwana wa Kolhoze, mkuu wa wilaya ya Mispa, akajenga lango la Chemchemi. Alijenga, na kuweka kifuniko juu yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake. Alijenga upya ukuta wa Pwani wa Silowamu kwa bustani ya mfalme, hadi ngazi ya kuongoza kutoka mji wa Daudi.
And Shallum son of Col-Hozeh, head of the district of Mizpah, has strengthened the Fountain Gate: he builds it, and covers it, and sets up its doors, its locks, and its bars, and the wall of the pool of Siloah, to the garden of the king, and to the steps that are going down from the City of David.
16 Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-suri, akajenga mahali hapo, toka maburini ya Daudi, mpaka birika lililojengwa na watu, na nyumba ya watu wenye nguvu.
After him Nehemiah son of Azbuk, head of the half of the district of Beth-Zur, has strengthened to opposite the graves of David, and to the pool that is made, and to the house of the mighty ones.
17 Baada yake, Walawi walijenga, pamoja na Rehumi mwana wa Bani na baada yake, Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, kwa wilaya yake.
After him the Levites have strengthened, [and] Rehum son of Bani; by his hand Hashabiah, head of the half of the district of Keilah, has strengthened for his district.
18 Baada yake watu wa nchi zao walijenga, ikiwa ni pamoja na Binui mwana wa Henadadi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila.
After him their brothers have strengthened, [and] Bavvai son of Henadad, head of the half of the district of Keilah.
19 Baada yake alijenga Ezeri, mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alijenga sehemu nyingine kuelekea ghala ya silaha, kwenye kona ya ukuta.
And Ezer son of Jeshua, head of Mizpah, strengthens, by his hand, a second measure, from in front of the ascent of the armory at the angle.
20 Baada yake Baruki, mwana wa Zakai, akajenga kwa hiari sehemu nyingine, toka kona ya ukuta mpaka mlango wa nyumba ya Eliashibu, kuhani mkuu.
After him Baruch son of Zabbai has hurried to strengthen a second measure from the angle to the opening of the house of Eliashib the high priest.
21 Baada yake Meremothi, mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, akajenga sehemu nyingine, toka mlango wa nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.
After him Meremoth son of Urijah, son of Koz, has strengthened a second measure, from the opening of the house of Eliashib even to the completion of the house of Eliashib.
22 Kisha baada yake makuhani, watu wa eneo hilo karibu na Yerusalemu, walijenga.
And after him the priests, men of the circuit, have strengthened.
23 Baada yao Benyamini na Hashubu walijenga kuielekea nyumba yao. Baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania, alijenga karibu na nyumba yake.
After them Benjamin has strengthened, and Hashub, opposite their house; after him Azariah son of Maaseiah, son of Ananiah, has strengthened near his house.
24 Baada yake Binui mwana wa Henadadi akajenga sehemu nyingine, kutoka nyumba ya Azaria hadi kona ya ukuta.
After him Binnui son of Henadad has strengthened a second measure, from the house of Azariah to the angle, and to the corner.
25 Palali, mwana wa Uzai, akajenga juu ya kona ya ukuta na mnara unaoenea juu kutoka nyumba ya juu ya mfalme katika uwanda wa walinzi. Baada yake Pedaya mwana wa Paroshi akajenga.
Palal son of Uzai [strengthened] from opposite the angle, and the tower that is going out from the upper house of the king that [is] at the court of the prison; after him Pedaiah son of Parosh [strengthened].
26 Sasa watumishi wa hekalu waliokaa Ofeli walijenga mpaka upande wa Hifadhi ya Maji upande wa mashariki wa mnara unaojitokeza.
And the Nethinim have been dwelling in Ophel, to opposite the Water Gate at the east, and the tower that goes out.
27 Baada yake, Watekoi walijenga sehemu nyingine, kuelekea mnara mkubwa ulio nje, mpaka ukuta wa Ofeli.
After him the Tekoites have strengthened a second measure, from opposite the great tower that goes out, and to the wall of Ophel.
28 Makuhani wakajenga juu ya lango la farasi, kila mmoja kuelekea nyumba yake.
From above the Horse Gate the priests have strengthened, each opposite his house.
29 Baada yao Sadoki, mwana wa Imeri, alijenga sehemu hiyo kuelekea nyumba yake. Na baada yake Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa lango la mashariki, akajenga.
After them Zadok son of Immer has strengthened opposite his house; and after him Shemaiah son of Shechaniah, keeper of the East Gate, has strengthened.
30 Baada yake Hanania, mwana wa Shelemia, na Hanuni, mwana wa sita wa Salafu, wakajenga sehemu nyingine. Meshulamu mwana wa Berekia akajenga kuelekea kwenye vyumba vyake.
After him Hananiah son of Shelemiah has strengthened, and Hanun the sixth son of Zalaph, a second measure; after him Meshullam son of Berechiah has strengthened opposite his chamber.
31 Baada yake Malkiya, mmoja wa wafua dhahabu, akajenga mpaka nyumba ya watumishi wa hekalu na wafanyabiashara waliokuwa wakielekea lango la gereza na mpaka chumba cha juu cha pembeni.
After him Malchijah son of the refiner has strengthened, to the house of the Nethinim, and of the merchants, opposite the Miphkad Gate, and to the ascent of the corner.
32 Wafanyabiashara wa dhahabu na wafanyabiashara walijenga kati ya chumba cha juu cha kona na Lango la Kondoo.
And between the ascent of the corner and the Sheep Gate, the refiners and the merchants have strengthened.

< Nehemia 3 >