< Nehemia 12 >
1 Hawa ndio makuhani na Walawi waliokuja pamoja na Zerubabeli mwana wa Shealueli, pamoja na Yoshua Seraya, Yeremia, Ezra,
Now these are the priests and the Levites who went up with Zerubbabel the son of Shealtiel, and Jeshua: Seraiah, Jeremiah, Ezra,
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
Amariah, Malluch, Hattush,
3 Shekania, Harimu na Meremothi.
Shecaniah, Rehum, Meremoth,
4 Kulikuwa na Iddo, Ginethoni, Abiya,
Iddo, Ginnethoi, Abijah,
5 Miyamini, Maazia, Bilgai,
Mijamin, Maadiah, Bilgah,
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
Shemaiah, Joiarib, Jedaiah,
7 Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hawa walikuwa wakuu wa makuhani na washirika wao katika siku za Yoshua.
Sallu, Amok, Hilkiah, and Jedaiah. These were the chiefs of the priests and of their brothers in the days of Jeshua.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na Matania, aliyekuwa akiongoza nyimbo za shukrani, pamoja na washirika wake.
Moreover the Levites were Jeshua, Binnui, Kadmiel, Sherebiah, Judah, and Mattaniah, who was over the thanksgiving songs, he and his brothers.
9 Bakbukia na Uno, washirika wao, walisimama pembeni yao wakati wa huduma.
Also Bakbukiah and Unno, their brothers, were close to them according to their offices.
10 Yoshua alikuwa babaye Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa babaye Yoyada,
Jeshua became the father of Joiakim, and Joiakim became the father of Eliashib, and Eliashib became the father of Joiada,
11 Yoyada alimzaa Yonathani, Yonathani akamzaa Yadua.
and Joiada became the father of Jonathan, and Jonathan became the father of Jaddua.
12 Katika siku za Yoyakimu hawa walikuwa makuhani, wakuu wa jamaa; Meraya alikuwa mkuu wa Seraya, Hanania alikuwa kiongozi wa Yeremia,
In the days of Joiakim were priests, heads of fathers’ households: of Seraiah, Meraiah; of Jeremiah, Hananiah;
13 Meshulam alikuwa kiongozi wa Ezra, Yehohanani alikuwa kiongozi wa Amaria,
of Ezra, Meshullam; of Amariah, Jehohanan;
14 Yonathani alikuwa kiongozi wa Maluki, na Yusufu alikuwa kiongozi wa Shekania.
of Malluchi, Jonathan; of Shebaniah, Joseph;
15 Ili kuendelea, Adna alikuwa kiongozi wa Harimu, Helkai kiongozi wa Meremothi,
of Harim, Adna; of Meraioth, Helkai;
16 Zekaria alikuwa kiongozi wa Ido, Meshulamu alikuwa kiongozi wa Ginethoni, na
of Iddo, Zechariah; of Ginnethon, Meshullam;
17 Zikri alikuwa kiongozi wa Abia wa Miyaamini. Piltai alikuwa kiongozi wa Maazia.
of Abijah, Zichri; of Miniamin, of Moadiah, Piltai;
18 Shamua alikuwa kiongozi wa Bilgai, Yehonathani alikuwa kiongozi wa Shemaya,
of Bilgah, Shammua; of Shemaiah, Jehonathan;
19 Matenai alikuwa kiongozi wa Yoyaribu, Uzi alikuwa kiongozi wa Yedaya,
of Joiarib, Mattenai; of Jedaiah, Uzzi;
20 Kalai alikuwa kiongozi wa Salu, Eberi alikuwa kiongozi wa Amok,
of Sallai, Kallai; of Amok, Eber;
21 Hashabia alikuwa kiongozi wa Hilkia, na Nethanel alikuwa kiongozi wa Yedaya.
of Hilkiah, Hashabiah; of Jedaiah, Nethanel.
22 Katika siku za Eliashibu, Walawi Eliashibu, Yoyada, Yohana, na Yadua waliandikwa kama vichwa vya familia, na makuhani waliandikwa wakati wa utawala wa Dariyo wa Persia.
As for the Levites, in the days of Eliashib, Joiada, Johanan, and Jaddua, there were recorded the heads of fathers’ households; also the priests, in the reign of Darius the Persian.
23 Wana wa Lawi na viongozi wao wa familia waliandikwa katika Kitabu cha tarehe hadi siku za Yohana mwana wa Eliashibu.
The sons of Levi, heads of fathers’ households, were written in the book of the chronicles, even until the days of Johanan the son of Eliashib.
24 Wakuu wa Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua mwana wa Kadmieli, pamoja na washirika wao, waliokuwa wamesimama mbele yao kumtukuza na kumshukuru, akijibu sehemu kwa sehemu, kwa kutii amri ya Daudi, mtu wa Mungu.
The chiefs of the Levites: Hashabiah, Sherebiah, and Jeshua the son of Kadmiel, with their brothers close to them, to praise and give thanks according to the commandment of David the man of God, section next to section.
25 Matania, Bakbukia, Obadiya, Meshulamu, Talmoni na Akubu walikuwa walinzi wa malango waliokuwa wakiwa wamesimama katika vyumba vya hazina penye malango.
Mattaniah, Bakbukiah, Obadiah, Meshullam, Talmon, and Akkub were gatekeepers keeping the watch at the storehouses of the gates.
26 Walitumika katika siku za Yoyakimu, mwana wa Yoshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za Nehemiya, gavana na Ezra kuhani na mwandishi.
These were in the days of Joiakim the son of Jeshua, the son of Jozadak, and in the days of Nehemiah the governor, and of Ezra the priest and scribe.
27 Katika kujitolea kwa ukuta wa Yerusalemu, watu walitafuta Walawi popote walipokuwa wakiishi, wakawaleta Yerusalemu ili kusherehekea kujitolea kwa furaha, pamoja na shukrani na kuimba kwa ngoma, vinanda na vinubi.
At the dedication of the wall of Jerusalem, they sought the Levites out of all their places, to bring them to Jerusalem to keep the dedication with gladness, both with giving thanks and with singing, with cymbals, stringed instruments, and with harps.
28 Ushirika wa waimbaji walikusanyika pamoja kutoka wilaya iliyozunguka Yerusalemu na kutoka vijiji vya Wanetofathi.
The sons of the singers gathered themselves together, both out of the plain around Jerusalem and from the villages of the Netophathites;
29 Walikuja kutoka Beth-gilgali na kutoka katika mashamba ya Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji karibu na Yerusalemu.
also from Beth Gilgal and out of the fields of Geba and Azmaveth, for the singers had built themselves villages around Jerusalem.
30 Makuhani na Walawi wakajitakasa, kisha wakawatakasa watu, milango na ukuta.
The priests and the Levites purified themselves; and they purified the people, the gates, and the wall.
31 Kisha nilikuwa na viongozi wa Yuda kwenda juu ya ukuta, na mimi kuteua mikutano miwili mikubwa ya hao walioshukuru. Mmoja alienda upande wa kulia juu ya ukuta kuelekea lango la jaa.
Then I brought the princes of Judah up on the wall, and appointed two great companies who gave thanks and went in procession. One went on the right hand on the wall toward the dung gate;
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda walimfuata,
and after them went Hoshaiah, with half of the princes of Judah,
33 na baada yake akaenda Azaria, Ezra na Meshulamu,
and Azariah, Ezra, and Meshullam,
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia
Judah, Benjamin, Shemaiah, Jeremiah,
35 na wana wa makuhani waliokuwa na tarumbeta, na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Mataniya, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu.
and some of the priests’ sons with trumpets: Zechariah the son of Jonathan, the son of Shemaiah, the son of Mattaniah, the son of Micaiah, the son of Zaccur, the son of Asaph;
36 Na pia jamaa za Zekaria, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, Hanani, pamoja na vyombo vya muziki vya Daudi mtu wa Mungu. Ezra mwandishi alikuwa mbele yao.
and his brothers, Shemaiah, Azarel, Milalai, Gilalai, Maai, Nethanel, Judah, and Hanani, with the musical instruments of David the man of God; and Ezra the scribe was before them.
37 Na kwa Lango la Chemchemi walikwenda moja kwa moja na madaraja ya mji wa Daudi juu ya kupanda kwa ukuta, juu ya nyumba ya Daudi, kwenye lango la Maji upande wa mashariki.
By the spring gate, and straight before them, they went up by the stairs of David’s city, at the ascent of the wall, above David’s house, even to the water gate eastward.
38 Na waimbaji wengine ambao walishukuru wakaenda upande mwingine. Niliwafuata juu ya ukuta pamoja na nusu ya watu, juu ya mnara wa vinyago, hadi kuta kubwa,
The other company of those who gave thanks went to meet them, and I after them, with the half of the people on the wall above the tower of the furnaces, even to the wide wall,
39 na juu ya lango la Efraimu, na mlango wa kale, na kwa lango la samaki na mnara wa Hananeli na mnara wa Hamea, kwa lango la Kondoo, na wakasimama kwenye mlango wa walinzi.
and above the gate of Ephraim, and by the old gate, and by the fish gate, the tower of Hananel, and the tower of Hammeah, even to the sheep gate; and they stood still in the gate of the guard.
40 Kwa hiyo, mikutano miwili ya wale waliomshukuru walipata nafasi yao katika nyumba ya Mungu, na mimi pia nikachukua nafasi yangu na nusu ya viongozi pamoja nami.
So the two companies of those who gave thanks in God’s house stood, and I and the half of the rulers with me;
41 Na makuhani wakachukua nafasi zao Eliakimu, Maaseya, Miyamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania wenye tarumbeta,
and the priests, Eliakim, Maaseiah, Miniamin, Micaiah, Elioenai, Zechariah, and Hananiah, with trumpets;
42 Maaseya, na Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, Ezeri. Waimbaji waliimba na Yezrahia kama wasimamizi.
and Maaseiah, Shemaiah, Eleazar, Uzzi, Jehohanan, Malchijah, Elam, and Ezer. The singers sang loud, with Jezrahiah their overseer.
43 Walitoa dhabihu kubwa siku ile, wakafurahi, kwa sababu Mungu alikuwa amewafurahisha kwa furaha kubwa. Pia wanawake na watoto walifurahi. Hivyo furaha ya Yerusalemu ikasikiwa toka mbali.
They offered great sacrifices that day, and rejoiced, for God had made them rejoice with great joy; and the women and the children also rejoiced, so that the joy of Jerusalem was heard even far away.
44 Siku hiyo watu waliteuliwa juu ya nyumba ya hazina kwa ajili ya michango, matunda ya kwanza, na zaka, ili kuzikusanya ndani yao sehemu zinazohitajika katika sheria za makuhani na Walawi. Kila mmoja aliteuliwa kufanya kazi mashambani karibu na miji. Kwa maana Yuda alifurahi juu ya makuhani na Walawi waliokuwa wamesimama mbele yao.
On that day, men were appointed over the rooms for the treasures, for the wave offerings, for the first fruits, and for the tithes, to gather into them according to the fields of the cities the portions appointed by the law for the priests and Levites; for Judah rejoiced for the priests and for the Levites who served.
45 Walifanya utumishi wa Mungu wao, na huduma ya utakaso, kwa mujibu wa amri ya Daudi na ya mwanawe Sulemani, na hivyo
They performed the duty of their God and the duty of the purification, and so did the singers and the gatekeepers, according to the commandment of David and of Solomon his son.
46 Zamani za kale, katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa na wasimamizi wa waimbaji, na kulikuwa na nyimbo za sifa na shukrani kwa Mungu.
For in the days of David and Asaph of old there was a chief of the singers, and songs of praise and thanksgiving to God.
47 Katika siku za Zerubabeli na katika siku za Nehemia, Israeli wote walitoa sehemu za kila siku kwa waimbaji na walinzi wa mlango. Wakaweka pembeni sehemu ya Walawi, na Walawi waliweka sehemu ya wana wa Haruni.
All Israel in the days of Zerubbabel and in the days of Nehemiah gave the portions of the singers and the gatekeepers, as every day required; and they set apart that which was for the Levites; and the Levites set apart that which was for the sons of Aaron.