< Nehemia 12 >
1 Hawa ndio makuhani na Walawi waliokuja pamoja na Zerubabeli mwana wa Shealueli, pamoja na Yoshua Seraya, Yeremia, Ezra,
This is a list of the priests and Levites who came back with Zerubbabel, son of Shealtiel, and Jeshua, the high priest: Seraiah, Jeremiah, Ezra,
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
Amariah, Malluch, Hattush,
3 Shekania, Harimu na Meremothi.
Shecaniah, Rehum, Meremoth,
4 Kulikuwa na Iddo, Ginethoni, Abiya,
Iddo, Ginnethon, Abijah,
5 Miyamini, Maazia, Bilgai,
Miniamin, Maadiah, Bilgah,
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
Shemaiah, Joiarib, Jedaiah,
7 Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hawa walikuwa wakuu wa makuhani na washirika wao katika siku za Yoshua.
Sallu, Amok, Hilkiah, and Jedaiah. These were the leaders of the priests and their relatives in Jeshua's time.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na Matania, aliyekuwa akiongoza nyimbo za shukrani, pamoja na washirika wake.
The Levites were Jeshua, Binnui, Kadmiel, Sherebiah, Judah, and Mattaniah, who with his fellow Levites was in charge of the songs of praise.
9 Bakbukia na Uno, washirika wao, walisimama pembeni yao wakati wa huduma.
Two other Levites, Bakbukiah and Unni, stood opposite them in the service.
10 Yoshua alikuwa babaye Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa babaye Yoyada,
Jeshua the high priest was the father of Joiakim, who was the father of Eliashib, who was the father of Joiada,
11 Yoyada alimzaa Yonathani, Yonathani akamzaa Yadua.
who was the father of Jonathan, who was the father of Jaddua.
12 Katika siku za Yoyakimu hawa walikuwa makuhani, wakuu wa jamaa; Meraya alikuwa mkuu wa Seraya, Hanania alikuwa kiongozi wa Yeremia,
In Joiakim's time, these were the family leaders of the priests: of the family of Seraiah, Meraiah; of Jeremiah, Hananiah;
13 Meshulam alikuwa kiongozi wa Ezra, Yehohanani alikuwa kiongozi wa Amaria,
of Ezra, Meshullam; of Amariah, Jehohanan;
14 Yonathani alikuwa kiongozi wa Maluki, na Yusufu alikuwa kiongozi wa Shekania.
of Malluchi, Jonathan; of Shebaniah, Joseph;
15 Ili kuendelea, Adna alikuwa kiongozi wa Harimu, Helkai kiongozi wa Meremothi,
of Harim, Adna; of Meraioth, Helkai;
16 Zekaria alikuwa kiongozi wa Ido, Meshulamu alikuwa kiongozi wa Ginethoni, na
of Iddo, Zechariah; of Ginnethon, Meshullam;
17 Zikri alikuwa kiongozi wa Abia wa Miyaamini. Piltai alikuwa kiongozi wa Maazia.
of Abijah, Zichri; of Miniamin and of Moadiah, Piltai;
18 Shamua alikuwa kiongozi wa Bilgai, Yehonathani alikuwa kiongozi wa Shemaya,
of Bilgah, Shammua; of Shemaiah, Jehonathan;
19 Matenai alikuwa kiongozi wa Yoyaribu, Uzi alikuwa kiongozi wa Yedaya,
of Joiarib, Mattenai; of Jedaiah, Uzzi;
20 Kalai alikuwa kiongozi wa Salu, Eberi alikuwa kiongozi wa Amok,
of Sallai, Kallai; of Amok, Eber;
21 Hashabia alikuwa kiongozi wa Hilkia, na Nethanel alikuwa kiongozi wa Yedaya.
of Hilkiah, Hashabiah; of Jedaiah, Nethanel.
22 Katika siku za Eliashibu, Walawi Eliashibu, Yoyada, Yohana, na Yadua waliandikwa kama vichwa vya familia, na makuhani waliandikwa wakati wa utawala wa Dariyo wa Persia.
The family leaders of the Levites in the time of Eliashib, Joiada, Johanan, and Jaddua, in addition to those of the priests, were recorded during the reign of Darius the Persian.
23 Wana wa Lawi na viongozi wao wa familia waliandikwa katika Kitabu cha tarehe hadi siku za Yohana mwana wa Eliashibu.
As for the genealogy of the sons of Levi, the family leaders up to the time of Johanan, son of Eliashib, were listed in the Book of the Records.
24 Wakuu wa Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua mwana wa Kadmieli, pamoja na washirika wao, waliokuwa wamesimama mbele yao kumtukuza na kumshukuru, akijibu sehemu kwa sehemu, kwa kutii amri ya Daudi, mtu wa Mungu.
The Levite leaders were Hashabiah, Sherebiah, and Jeshua, son of Kadmiel, together with their fellow Levites, who stood opposite them, each section giving praise and thanks and responding to one another, as arranged by David, the man of God.
25 Matania, Bakbukia, Obadiya, Meshulamu, Talmoni na Akubu walikuwa walinzi wa malango waliokuwa wakiwa wamesimama katika vyumba vya hazina penye malango.
They were joined by Mattaniah, Bakbukiah, and Obadiah. Meshullam, Talmon, and Akkub were gatekeepers who guarded the storehouses at the gates.
26 Walitumika katika siku za Yoyakimu, mwana wa Yoshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za Nehemiya, gavana na Ezra kuhani na mwandishi.
They served in the time of Joiakim, son of Jeshua, son of Jozadak, and in the time of Nehemiah the governor and Ezra the priest and scribe.
27 Katika kujitolea kwa ukuta wa Yerusalemu, watu walitafuta Walawi popote walipokuwa wakiishi, wakawaleta Yerusalemu ili kusherehekea kujitolea kwa furaha, pamoja na shukrani na kuimba kwa ngoma, vinanda na vinubi.
In order to dedicate the wall of Jerusalem, the Levites were called from everywhere they were living to come to Jerusalem and celebrate with joy the dedication with songs of praise and thanks, accompanied by cymbals, harps, and lyres.
28 Ushirika wa waimbaji walikusanyika pamoja kutoka wilaya iliyozunguka Yerusalemu na kutoka vijiji vya Wanetofathi.
The singers were also brought in from the area around Jerusalem and from the villages of the Netophathites,
29 Walikuja kutoka Beth-gilgali na kutoka katika mashamba ya Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji karibu na Yerusalemu.
as well as from Beth-gilgal and from the area of Geba and Azmaveth, for the singers had built villages for themselves all around Jerusalem.
30 Makuhani na Walawi wakajitakasa, kisha wakawatakasa watu, milango na ukuta.
Once the priests and the Levites had purified themselves, they purified the people, the gates, and the wall.
31 Kisha nilikuwa na viongozi wa Yuda kwenda juu ya ukuta, na mimi kuteua mikutano miwili mikubwa ya hao walioshukuru. Mmoja alienda upande wa kulia juu ya ukuta kuelekea lango la jaa.
I had the leaders of Judah go up on the wall, and arranged two large choirs that to give thanks. One group went to right along the wall to the Refuse Gate.
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda walimfuata,
Hoshaiah and half the leaders of Judah followed them,
33 na baada yake akaenda Azaria, Ezra na Meshulamu,
with Azariah, Ezra, Meshullam,
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia
Judah, Benjamin, Shemaiah, and Jeremiah,
35 na wana wa makuhani waliokuwa na tarumbeta, na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Mataniya, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu.
as well as some of the priests with trumpets, and Zechariah, son of Jonathan, son of Shemaiah, son of Mattaniah, son of Micaiah, son of Zaccur, son of Asaph,
36 Na pia jamaa za Zekaria, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, Hanani, pamoja na vyombo vya muziki vya Daudi mtu wa Mungu. Ezra mwandishi alikuwa mbele yao.
and his fellow priests, Shemaiah, Azarel, Milalai, Gilalai, Maai, Nethanel, Judah, and Hanani, along with the musical instruments as required by David, the man of God. Ezra the scribe led them.
37 Na kwa Lango la Chemchemi walikwenda moja kwa moja na madaraja ya mji wa Daudi juu ya kupanda kwa ukuta, juu ya nyumba ya Daudi, kwenye lango la Maji upande wa mashariki.
At the Fountain Gate they headed straight up by the stairs of the city of David, where the wall goes uphill, above the house of David, and on to the Water Gate on the east.
38 Na waimbaji wengine ambao walishukuru wakaenda upande mwingine. Niliwafuata juu ya ukuta pamoja na nusu ya watu, juu ya mnara wa vinyago, hadi kuta kubwa,
The other choir group went in the opposite direction. I followed them, along with half the people, on the wall passing the Tower of the Ovens, on to the Broad Wall,
39 na juu ya lango la Efraimu, na mlango wa kale, na kwa lango la samaki na mnara wa Hananeli na mnara wa Hamea, kwa lango la Kondoo, na wakasimama kwenye mlango wa walinzi.
over the Ephraim Gate, the Jeshanah Gate, the Fish Gate, the Tower of Hananel, and the Tower of the Hundred, as far as the Sheep Gate, stopping at the Guard Gate.
40 Kwa hiyo, mikutano miwili ya wale waliomshukuru walipata nafasi yao katika nyumba ya Mungu, na mimi pia nikachukua nafasi yangu na nusu ya viongozi pamoja nami.
Both thanksgiving choirs then took their places in God's Temple. I followed with the group of leaders that was with me,
41 Na makuhani wakachukua nafasi zao Eliakimu, Maaseya, Miyamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania wenye tarumbeta,
along with the priests blowing their trumpets: Eliakim, Maaseiah, Miniamin, Micaiah, Elioenai, Zechariah, and Hananiah.
42 Maaseya, na Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, Ezeri. Waimbaji waliimba na Yezrahia kama wasimamizi.
Then came the singers Maaseiah, Shemaiah, Eleazar, Uzzi, Jehohanan, Malchijah, Elam, and Ezer, and the choirs sang, directed by Jezrahiah.
43 Walitoa dhabihu kubwa siku ile, wakafurahi, kwa sababu Mungu alikuwa amewafurahisha kwa furaha kubwa. Pia wanawake na watoto walifurahi. Hivyo furaha ya Yerusalemu ikasikiwa toka mbali.
Many sacrifices were offered that day, celebrating that God had brought them so much happiness, tremendous happiness. The women and children also celebrated, and the sounds of joy in Jerusalem could be heard far away.
44 Siku hiyo watu waliteuliwa juu ya nyumba ya hazina kwa ajili ya michango, matunda ya kwanza, na zaka, ili kuzikusanya ndani yao sehemu zinazohitajika katika sheria za makuhani na Walawi. Kila mmoja aliteuliwa kufanya kazi mashambani karibu na miji. Kwa maana Yuda alifurahi juu ya makuhani na Walawi waliokuwa wamesimama mbele yao.
On the same day men were put in charge over the storerooms that contained the offerings, the first part of the crops, and tithes. What was allocated by the Law for the priests and Levites was brought into these storerooms from the fields around the towns, because all the people of Judah were happy for the service of the priests and Levites.
45 Walifanya utumishi wa Mungu wao, na huduma ya utakaso, kwa mujibu wa amri ya Daudi na ya mwanawe Sulemani, na hivyo
They were responsible for the worship of their God and for the service of purification, along with the singers and gatekeepers, following the instructions of David and his son Solomon.
46 Zamani za kale, katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa na wasimamizi wa waimbaji, na kulikuwa na nyimbo za sifa na shukrani kwa Mungu.
For long ago, back in the time of David and Asaph, directors had been appointed for the singers and for the songs of praise and thanks to God.
47 Katika siku za Zerubabeli na katika siku za Nehemia, Israeli wote walitoa sehemu za kila siku kwa waimbaji na walinzi wa mlango. Wakaweka pembeni sehemu ya Walawi, na Walawi waliweka sehemu ya wana wa Haruni.
So in the time of Zerubbabel and of Nehemiah, everyone in Israel provided the daily food allowances for the singers and the gatekeepers. They also made sure to provide for the other Levites, and the Levites gave a share of this to the descendants of Aaron.